Ambao huwa tunaangalia tamthiliya/movies zilizotafsiriwa tukutane hapa

Ambao huwa tunaangalia tamthiliya/movies zilizotafsiriwa tukutane hapa

Haha hapa kwetu ndivyo tulivyo maa. Waaris bonge la tamthiliya ila nachukia mtoto hakui tangu alipotimiza miaka 7 haongezeki
Pale nadhani wakimfanya kama anakua patakuwa hamna mtu wa kuigiza. Hapo itakuja kuonyeshwa labda ameshakuwa mkubwa kabisa.
Ina uwongo mwingi ila saa 3 kamili lazima niwe kwenye Tv. Ikiisha naunga na wildflower japo nilishaangalia ya Novela E ila ninapenda pia ya kiswahili sana sana Sehemu za Emilia.
 
Pale nadhani wakimfanya kama anakua patakuwa hamna mtu wa kuigiza. Hapo itakuja kuonyeshwa labda ameshakuwa mkubwa kabisa.
Ina uwongo mwingi ila saa 3 kamili lazima niwe kwenye Tv. Ikiisha naunga na wildflower japo nilishaangalia ya Novela E ila ninapenda pia ya kiswahili sana sana Sehemu za Emilia.
Hahaha uongo wa mtoto wa miaka saba kuwa na akili kiasi kile loh. Wild flower mimi sikuimalizaga, hiyo sister's revenge ilikuwaga inaoneshwa saa tano usiku ikarudishwa saa moja kasoro ni fire ila inaelekea kuisha nadhani
 
Habari,
Najua mtasema huku hawapo ila naamini wenzangu na mimi wapo maana kwenye msafara wa kenge na mamba wamo.
Startimes wameturahisishia sana tusiojua kizungu, kwa sasa sisi tunaangalia
A sister's revenge (Chinese)
Waaris (Indian)
Village boy (Indian)
Wild flower (wafilipino)
Hizi zote zinaoneshwa channel ya St Swahili (kasoro Village boy)
Wewe unaipenda ipi? Nani humpendi? Nani unampenda?
Uzi tayari

Najiuliza mtu mtu unapataje muda wa kuangalia tamthiliya zote hizo, maana wengine masaa24 yanaisha haraka kama masaa10, hata taarifa ya habari tu tunaona kwa bahati kwa nadra itokee tu nimekaa sehemu na ishu nyingine halafu TV iko on.
 
Najiuliza mtu mtu unapataje muda wa kuangalia tamthiliya zote hizo, maana wengine masaa24 yanaisha haraka kama masaa10, hata taarifa ya habari tu tunaona kwa bahati kwa nadra itokee tu nimekaa sehemu na ishu nyingine halafu TV iko on.
Tunatofautiana boss, wote hatuwezi kuwa busy kama wewe
 
Aha ha Startimes raha sana aisee.
Kuna tamthiliya ya kichina ilikuwa inaitwa DUNIA YA KAWAIDA nilikuwa naipenda sana.
Umewahi kuiona?
 
Back
Top Bottom