Amekasirika. Kisa...nimemuuliza "wataondoka lini"

Amekasirika. Kisa...nimemuuliza "wataondoka lini"

huko ni kumuendekeza mke wako

unapaswa kabisa kumuuliza wataondoka lini
hata kama wamekuja na nauli yao kabisa....

wewe ndo baba mwenye nyumba lazima ujue wageni wako wataondoka lini

tena hilo swali ungeuliza siku ya kwanza kabisa....

tena ungewauliza wenyewe...bila kuogopa.......

ni vizuri kuuliza wataondoka lini?
wamekuja kusalimia tu au wana shida nyingine?
wagonjwa?
au kuna pesa wanataka kutoka kwako?
au wana safari nyingine hapo ni transit?.......

Mkuu wengi wetu hatuna ujasiri huo na ndio maana tunajikuta tunaumia ndani kwa ndani. Kimsingi huu woga na kundekeza yasiyotakiwa kuendekezwa nidko kunakotuzamisha kwenye dimbwi la umaskini!
 
Baada ya majonzi ya takriban wiki nzima ya mpendwa wetu RM, ndugu yenu mitishamba nimerudi tena.
Huwa siishiwa mikasa, na mara nyingi huwa naongelea mambo yaliyonikuta ama kuyashuhudia.

Mimi na mke wangu tumekuwa tukiishi maisha ya kawaida ya ndoa (furaha, huzuni, mikasa na kutoelewana wakati mwingine).
Nyumbani kwetu huwa tunapokea wageni mbalimbali kwa nyakati tofauti. Kuna wakati wanakuja ndugu/marafiki zake na kuna wakati wanakuja ndugu/marafiki zangu.


Mara nyingi wakija ndugu zake huwa simuulizi kuwa lini wataondoka kwani najua kwa kufanya hivyo huenda ikafikirika vibaya na sikupenda iwe hivyo. Tatizo linakuja kwamba nduguze wanapokuja huwa hawatoi taarifa siku ya kuondoka hadi inapokaribia siku chache sana kabla ya kuondoka ndo wanatoa taarifa. Hii mara nyingi huniletea matatizo makubwa kwani kama ujuavyo masuala ya kiuchumi...wakati mwingine hunipasa kukopa ili niwapatie nauli kwani huwa ni short notice.


Hivi karibuni alikuja mama yake na mdogo wake. Baada ya kukaa kwa muda fulani ilibidi nimuulize "wataondoka lini"? Nia ilikuwa ni kunipa muda wa mimi kujiandaa kwani kwa wakati huo nilikuwa pia na majukumu ya kulipia ada ya shule takriban watu wanne, hivyo ni vema nikajiandaa mapema.


Nilijuta kuuliza hilo swali....
Akakasirika, akavimba, misonyo kibao, haongei......yaani kisirani mtindo mmoja.
Hadi najuta kwa nini niliuliza swali hilo.
Hadi sasa no mawasiliano.

Mimi nadhani wewe ndiyo mwenye matatizo, kuna ulazima gani kumlipia mtua nauli anapokuja kukutembelea?
 
Pole kwa stress, shida ya hawa wenzetu ni kutumia hisia kwa kila jambo, wageni wakiondoka mweke chini umweleze kwa undani kwamba familia inatakiwa kuwa na mipango na ulivyomwuliza ilikuwa ni namna mojawapo wa kujipanga.
 
Nadhani kunatatizo zaidi ya kuulizwa swali! Yawezekana hata yeye mwenyewe hajui tatizo nini! Kaa naye chini muongee vizuri! hizi hadithi za kutegesheana sio nzuri ama kusubiri baadaye sio nzuri! Kwa kuwa yeye ndio mwenye hasira muulize "mke wangu kwanini unadhani siwapendi ndugu zako". Mwache afunguke! akinuna mletee mama yake zawadi ya khanga! upendo unalainisha hasira! halafu wazazi wake wakiondoka huko baadaye kama kuna umuhimu! mtaongea tena!
 
Sasa wewe si ungemueleza lengo lako la kuuliza vile, ili akuelewe!
 
huko ni kumuendekeza mke wako

unapaswa kabisa kumuuliza wataondoka lini
hata kama wamekuja na nauli yao kabisa....

wewe ndo baba mwenye nyumba lazima ujue wageni wako wataondoka lini

tena hilo swali ungeuliza siku ya kwanza kabisa....

tena ungewauliza wenyewe...bila kuogopa.......

ni vizuri kuuliza wataondoka lini?
wamekuja kusalimia tu au wana shida nyingine?
wagonjwa?
au kuna pesa wanataka kutoka kwako?
au wana safari nyingine hapo ni transit?.......

duu hilo wazo ni zaidi ya ufikiriavyo hasa kwa mitz
 
Ndoa yako iangalie kwa jicho la pili kiukweli mkeo ulimuonesha unampenda sana na umeoza kwake hayo ndio malipo yake hebu kuwa na mcmamo si kama anawapenda jamaa zake mpaka kufikia hatua hiyo anatikisa kibiriti
 
Inawezekana ulianza vibaya wakati wa kuuliza, maana unaweza ukakurupuka na kuuliza 'hawa wageni wanaondoka lini' tena kwa sauti ya juu na ukali. Huyo ni mkewe inabidi uongee naye kwa utulivu, utaratibu na upendo ukimkumbusha majukumu yanawakabili likiwepo hilo la kuwapatia nauli wageni wenu, baada ya hapo ukitaka kujua wageni wataondoka lini utafahamishwa bila shaka!
 
Unaendekeza mambo ambayo si matatizo kuyafanya yawe matatizo.

1. Mtu uko kwako (au si kwako?)

2.Umekarimu watu kwa kuwakaribisha , jambo zuri.

3. Apparently unawapa nauli pia , jambo ambalo linapita uzuri na linaweza kuwa baya kwa sababu una wa "enable" depending hawa ni watu wzima au watoto? Wana uwezo wa kufanya kazi au hawana? Kwa nini uwape nauli?

4. Halafu inaonekana hata wewe mwenyewe mambo yako si fresh kihivyo, ukiombwa nauli kwa kushtukizwa unaenda kukopa. Haya mambo ya "keeping up appearances" na "upendo wa mshumaa" si mazuri. Waambie tu kwamba "sina" na kama una nia ya kuwasaidia zaidiwasaidie kujua kwamba hela si maji kwamba utaenda kuchota tu kwenye bomba, hata hayo maji watu wanayapigia hesabu na kuyapangia kazi.

5.Wasaidie zaidi kwa kumueleza hata mkeo kwamba ratiba ni kitu cha kawaida katika maisha.
 
Anatingisha kiberiti aone kama kina njiti za kutosha.
 
haya mambo yanaboa,sasa kanuna ya nini?mtu inapaswa aelewe hela haiokotwi na hata kama unayo basi imeshafanyiwa mipango.kuna jamaa aliniambia yeye anawatoza kodi ndugu zake na wale wa wife kwa kisingizio cha gharama kubwa za maisha.hawakai zaidi ya siku mbili kwake

Aseeee!!!!!!.
 
Unaendekeza mambo ambayo si matatizo kuyafanya yawe matatizo.

1. Mtu uko kwako (au si kwako?)

2.Umekarimu watu kwa kuwakaribisha , jambo zuri.

3. Apparently unawapa nauli pia , jambo ambalo linapita uzuri na linaweza kuwa baya kwa sababu una wa "enable" depending hawa ni watu wzima au watoto? Wana uwezo wa kufanya kazi au hawana? Kwa nini uwape nauli?

4. Halafu inaonekana hata wewe mwenyewe mambo yako si fresh kihivyo, ukiombwa nauli kwa kushtukizwa unaenda kukopa. Haya mambo ya "keeping up appearances" na "upendo wa mshumaa" si mazuri. Waambie tu kwamba "sina" na kama una nia ya kuwasaidia zaidiwasaidie kujua kwamba hela si maji kwamba utaenda kuchota tu kwenye bomba, hata hayo maji watu wanayapigia hesabu na kuyapangia kazi.

5.Wasaidie zaidi kwa kumueleza hata mkeo kwamba ratiba ni kitu cha kawaida katika maisha.

Point nzuri sana hii.
 
mwambie mkeo mjini mipango, kuendekeza ndugu mtakufa masikini.

Kwani akinuna unapungua uzito? Mwache anune ataongea tu!
 
Unaendekeza mambo ambayo si matatizo kuyafanya yawe matatizo.

1. Mtu uko kwako (au si kwako?)

2.Umekarimu watu kwa kuwakaribisha , jambo zuri.

3. Apparently unawapa nauli pia , jambo ambalo linapita uzuri na linaweza kuwa baya kwa sababu una wa "enable" depending hawa ni watu wzima au watoto? Wana uwezo wa kufanya kazi au hawana? Kwa nini uwape nauli?

4. Halafu inaonekana hata wewe mwenyewe mambo yako si fresh kihivyo, ukiombwa nauli kwa kushtukizwa unaenda kukopa. Haya mambo ya "keeping up appearances" na "upendo wa mshumaa" si mazuri. Waambie tu kwamba "sina" na kama una nia ya kuwasaidia zaidiwasaidie kujua kwamba hela si maji kwamba utaenda kuchota tu kwenye bomba, hata hayo maji watu wanayapigia hesabu na kuyapangia kazi.

5.Wasaidie zaidi kwa kumueleza hata mkeo kwamba ratiba ni kitu cha kawaida katika maisha.

Mkuu umeeleza vizuri sana.
Lakini nilishafafanua huko nyuma kuwa kwa familia zetu na utamaduni wa makabila mengi ya kitanzania....ni vigumu sana kusema ukweli hasa katika masuala kama hayo....tunakwepa kuonekana "wabaguzi". Na hapo ndipo maumivu yanapokuja.
 
Mkuu wengi wetu hatuna ujasiri huo na ndio maana tunajikuta tunaumia ndani kwa ndani. Kimsingi huu woga na kundekeza yasiyotakiwa kuendekezwa nidko kunakotuzamisha kwenye dimbwi la umaskini!

Kwa malezi ambayo wengi tumelelewa huku tukijikita katika kile ambacho tunadhani ni upendo ni ngumu sana kwa kweli.

Mfano mdogo tu.
Ukiwa "mkomunisti" labda hutoitoi ofa za bia kwa marafiki na majirani japo wewe unakunywa kila siku, watakuita mchoyo. Kuogopa hilo wengi wanajikuta katika upendo unaozidi uwezo wao.
 
Jinsi ushauri ulivyo mwingi! Nahisi utajichanganya,kwani tamaduni za maisha ya kinyumba ziko tofauti sana tanzania hii, sie kwetu, mara nyingi wageni wa kuja kutembea tu hakuna, labda siku mbili tatu, kama wakija ni wanafunzi likizo, lazima uwe na control na watoto, kama ni wazazi au ndugu watakuwa na issue unayoijua na wataondoka itakapoisha. Nikikushauri kuwa ni lazima ujue, sijui kwenu inaruhusiwa? Usijekususwa, ukaanza shida zingine zisizo na solution
 
Back
Top Bottom