Amini, Usiamini. Nimepona Magonjwa 100+ Kwa Jina la Yesu!

Huo ukristo wenu bakini nao huko makanisani mwenu, Mkileta hizo dini zenu hapa kwenye public forum tutazikosoa.

JF si mahala pa imani.

Ukiweka imani yako hapa, Tutaichambua na kuikosoa.
 
Wanaopona bila kumwamini Mungu wanapata uzima wa sasa tu, lakini uzima wa milele wataukosa kwa sababu ya kumkataa Yesu.
Hayo ni maneno ya kiimani tu

yani ni moto wa imani kama ubaya ubwela tu .
 
Hongera sana mkuu kwa kupata matibabu ya bure kwa magonjwa zaidi ya 100.
 
Huwa mna shida kubwa sana ya akili , sijakuomba uniletee mahubiri , kama hauna jibu ungepiga kimya tu
Nitapigaje kimya kimya ndugu yangu wakati ninakuonea huruma yatakayokukuta huko mbele. Anyway one day you will remember me na utasema ningejua ningefuata ushauri wa yule jamaa aliyeniambia mambo ya Mungu but it will be too late for you. Maombi yangu Mungu akufunulie siri hii ambayo watu wengi wanaibeza lakini ukweli utasimama tu sikuzote.
 
Unionee huruma kwa lipi? Thibitisha huyo Mungu kama yupo , vitisho vyako wapelekee waumini wenzako kwangu havifanyi kazi yoyote.
 
Hata mimi nimeshagundua, lengo kuu ni kurubuni wajinga.
Tafadhali, usiwaite JF Experts wajinga. Hujasoma hasara 30 za Matusi?
 
Matusi ni nini?
 
Nimeishayataja kwa sehemu, soma replies zangu zote; ila kama wewe ni mzima, mshukuru Mungu usiseme mtu hawezi kuugua magonjwa 100. Codes za magonjwa zipo zaidi ya 55,000 hayo 100 si ni tone tu?
Pole sana nakuombea uzima.. Tena uzima tele.. Kwenye hili naomba niishie hapa japo kiuhalisia kuna mtanziko mkubwa
 
Pole sana nakuombea uzima.. Tena uzima tele.. Kwenye hili naomba niishie hapa japo kiuhalisia kuna mtanziko mkubwa
Ahadi ya uzima tele tayari ninayo tangu zamani.
 
kiuhalisia kuna mtanziko mkubwa
Kuna watu wanapingwa wakisema wamepona ukimwi baada ya kuombewa kwa Jina la Yesu. Kama mtu anataja ugonjwa mmoja tu anapingwa, sembuse mimi niliyetaja 100+?
 
Nikionacho ni kwamba ulikuwa ukiumwa viungo, maumivu ya viungo mara nyingi ni either dalili za ugonjwa fulani, au matokeo a ugonjwa au hali fulani.
Hayo magonjwa 100+ wewe umeyapataje? Kumsingixia Mungu mambo ya uongo ili asifiwe, huo siyo uzalendo wala siyo ucha Mungu.
 
Labda nikuulize kwa maajabu gani ya yesu mpaka umpe vyeo ambavyo hastaili
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…