Lucas Mwashambwa
JF-Expert Member
- Jul 28, 2022
- 28,722
- 20,610
Ndugu zangu Watanzania,
Katibu wa itikadi,uenezi na Mafunzo wa CCM Taifa Mheshimiwa CPA Amos Makala Amepokelewa kwa shangwe, nderemo na vifijo vingi sana na maelfu ya wananchi wa Karatu katika uwanja wa mazingira bora wilayani Karatu.
Ambapo ni muendelezo wa ziara yake katika kupokea ,kusikiliza na kutatua kero mbalimbali za wananchi pamoja na kukagua utekelezaji wa ilani ya CCM.ambapo imeshuhudiwa maelfu ya wananchi wakifurika na kumiminika kwa wingi kama mchanga wa baharini kumlaki mtaalamu na nguli huyu wa Mahesabu hii ni kutokana na imani kubwa sana waliyonayo wananchi kwa CCM chama ambacho kimebeba matumaini ya mamilioni ya watanzania.
Lakini vilevile Mheshimiwa CPA Amos Makala ambaye amewahi kuwa mhazina wa CCM Taifa ameweza kuzungumza pia na viongozi wa CCM pamoja na serikali kutoka Ngorongoro.
Ikumbukwe wakati viongozi mbalimbali wa CCM wakiwa ziarani maeneo mbalimbali Nchini,kama tunavyoshuhudia naibu katibu mkuu Bara naye akiwa ziarani mkoani singida ,huku naye naibu katibu mkuu Zanzibar naye akiwa ziarani,.hali imekuwa ni ya kusikitisha na kutia huzuni sana kwa CHADEMA chama kilichojikatia tamaa na kupoteza matumaini.
Hakuna mikutano wala ziara wala nini zinazofanywa na viongozi wa CHADEMA.hii ni kutokana na kushindwa na kuishiwa sera na ajenda za kuzungumza kwa wananchi.ndio sababu unaona chama kimekata pumzi na kupoteza muelekeo kabisa.
Kwa hakika CCM ndio nguzo kuu ya Taifa letu na chemchemi ya matumaini ya mamilioni ya watanzania.hakuna Tanzania yenye maendeleo na utulivu pasipo CCM madarakani.ndio sababu kwa usikivu wake CCM inaendelea kuaminika na kuaminiwa na watanzania na kuungwa mkono kila uchao.
Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
Katibu wa itikadi,uenezi na Mafunzo wa CCM Taifa Mheshimiwa CPA Amos Makala Amepokelewa kwa shangwe, nderemo na vifijo vingi sana na maelfu ya wananchi wa Karatu katika uwanja wa mazingira bora wilayani Karatu.
Ambapo ni muendelezo wa ziara yake katika kupokea ,kusikiliza na kutatua kero mbalimbali za wananchi pamoja na kukagua utekelezaji wa ilani ya CCM.ambapo imeshuhudiwa maelfu ya wananchi wakifurika na kumiminika kwa wingi kama mchanga wa baharini kumlaki mtaalamu na nguli huyu wa Mahesabu hii ni kutokana na imani kubwa sana waliyonayo wananchi kwa CCM chama ambacho kimebeba matumaini ya mamilioni ya watanzania.
Lakini vilevile Mheshimiwa CPA Amos Makala ambaye amewahi kuwa mhazina wa CCM Taifa ameweza kuzungumza pia na viongozi wa CCM pamoja na serikali kutoka Ngorongoro.
Ikumbukwe wakati viongozi mbalimbali wa CCM wakiwa ziarani maeneo mbalimbali Nchini,kama tunavyoshuhudia naibu katibu mkuu Bara naye akiwa ziarani mkoani singida ,huku naye naibu katibu mkuu Zanzibar naye akiwa ziarani,.hali imekuwa ni ya kusikitisha na kutia huzuni sana kwa CHADEMA chama kilichojikatia tamaa na kupoteza matumaini.
Hakuna mikutano wala ziara wala nini zinazofanywa na viongozi wa CHADEMA.hii ni kutokana na kushindwa na kuishiwa sera na ajenda za kuzungumza kwa wananchi.ndio sababu unaona chama kimekata pumzi na kupoteza muelekeo kabisa.
Kwa hakika CCM ndio nguzo kuu ya Taifa letu na chemchemi ya matumaini ya mamilioni ya watanzania.hakuna Tanzania yenye maendeleo na utulivu pasipo CCM madarakani.ndio sababu kwa usikivu wake CCM inaendelea kuaminika na kuaminiwa na watanzania na kuungwa mkono kila uchao.
Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.