Amos Makalla nje, Zhakia Meghji ndani!

Amos Makalla nje, Zhakia Meghji ndani!

FMES amesema kuna mkutano wa dharura tarehe 28/03/2010, tusubiri tuone.

In the meantime......

Hamna mtu ndani ya chama anaweza kukomesha haya mambo jamani?

Mtu alituhumiwa kwa MATUMIZI MABAYA YA FEDHA katika wizara aliyokuwa anaongoza halafu kabla hata uchunguzi juu yake haujakamilika (hatujaambiwa) anapewa madaraka ya fedha ya chama?

Lakini Watanzania tumelogwa? Nani aliwaambia CCM huwa inawapa vyeo watu waaminifu. Huyu mama ni fisadi ndio maana amepewa (kama ni kweli) hiki cheo. Unataka wamweke mtu mwadilifu halafu wakati wa uchaguzi wakipora fedha za kampeni (kama ilivyo kawaida yao) wazipitishe wapi? Majambazi ndio yanapangana tayari kwa action hivyo.....
 
Kuna Tetesi kuwa Mwungwana kamtema Amos Makala kutoka nafasi ya Mtunza Hazina wa Chama, na kumteua Zhakia Meghji kuchukua nafasi yake.Kama tetesi hii ina ukweli, naamini la Kuvunda halina ubani.
amemtoa kibaka akamuingiza jambazi kha.
 
Wewe Kafiribangi na Injinia it appears you are not informed at all. Hela ya EPA na matumizi hayo mabaya Waziri wa Fedha hakuwa Meghji jamani. Meghji alipewa portfolio hiyo ya Fedha baada ya JK kuwa Rais. Hivi mbona hamna jema nyinyi watu? Wakati JK is working so hard to deal na ufisadi in his own unique way within a rotten system not of his creation badala ya kumuunga mkono mko busy kumkandia. Lo shame on you!! Inaelekea nyie kama mmmeoa au kuolewa basi spouses weni watakuwa wanaumia sana. Maana mna gubu haswa.

Watch your mouth mkuu. You don't know me so don't bring personal issues and spouses into this forum.

Mrs Meghji has been accused of mismanagement. If you read my post again you will see that I did mention that hatujaambiwa matokeo ya uchunguzi.

Why was she dropped from the last cabinet reshuffle? Is it that now she has been out of office for a while she has been judged as having learnt from her punishment, so to speak?

I don't hate anybody and I for sure do not have any "gubu", whatever that means
 
Hivi ni nani anafaa kushika nafasi hiyo?Mtoe na mawazo kama kweli kuna mabadiliko hayo ndani ya ccm fulni the ata fit kwenye postion hiyo!
 
I care less about all these s**$£%%^&&**.Whos Amos Makalla btw????
 
Nafikiri watu wengi tumechoka na CCM, lakini tutoe hoja kwa vizibiti, na sio kulalamikia kila kitu bila sababu. Pia tuwe makini na watu wanaojaribu kuchafua watu bila vizibiti na kujaribu kupotosha ukweli kwa sababu wanazozijua wenyewe.

Kuna wafanyabiashara na watu ambao wanajaribu kuingiza watu wao katika system ili wafaniliwe katika mambo yao. Kwa hiyo tuwe makini, tunaweza kutumika hapa JF.


Wewe Kafiribangi na Injinia it appears you are not informed at all. Hela ya EPA na matumizi hayo mabaya Waziri wa Fedha hakuwa Meghji jamani. Meghji alipewa portfolio hiyo ya Fedha baada ya JK kuwa Rais. Hivi mbona hamna jema nyinyi watu? Wakati JK is working so hard to deal na ufisadi in his own unique way within a rotten system not of his creation badala ya kumuunga mkono mko busy kumkandia. Lo shame on you!! Inaelekea nyie kama mmmeoa au kuolewa basi spouses weni watakuwa wanaumia sana. Maana mna gubu haswa.

Ni kweli uliyoyasema, lakini hizo personal attacks ungeondoa
Watch your mouth mkuu. You don't know me so don't bring personal issues and spouses into this forum.

Mrs Meghji has been accused of mismanagement. If you read my post again you will see that I did mention that hatujaambiwa matokeo ya uchunguzi.

Why was she dropped from the last cabinet reshuffle? Is it that now she has been out of office for a while she has been judged as having learnt from her punishment, so to speak?

I don't hate anybody and I for sure do not have any "gubu", whatever that means

Ungeweza kuweka hizo mismanagement accusation ingesaidia. Ni uchunguzi upi unazunguzia?
Kwani yeye ametuhumiwa kivipi?
Kwanza angalia matumizi ya fedha za EPA yalipofanyika yeye hakuwa Waziri wa Fedha.
Pili ni kwamba kwa mfumo wa wakati ule (sina hakika kama kumetokea mabadiliko) Gavana wa BoT hawajibiki wa Waziri wa Fedha.
Aliwajibika kwa kukubali kudanganywa na Balali na sio matumizi mabaya ya fedha. Na inawezekana hata kama ungekuwepo wewe ungefanya uamuzi ule ule.

Ni kweli uliyosema, isipokua Meghji hakuwajibika ila baada ya reshuffle hakurudi kwenye cabinet.

Hivi ni nani anafaa kushika nafasi hiyo?Mtoe na mawazo kama kweli kuna mabadiliko hayo ndani ya ccm fulni the ata fit kwenye postion hiyo!

Swali zuri, maana kila mtu afai..labda atoke chadema lol
 
Hiyo nafasi ya Mweka hazina ilifaaa sana kupewa Amos Makala maana hiyo nafasi ni kama Chief Financial officer wa CCM.

Amos Makala is qualified for the job, he is CPA(T). Zakia sijui ana elimu gani.
 
Kama ni kweli, basi JK atakuwa anaruka mkojo anakanyaga mavi. Kumrudisha yule aliyeidhinisha malipo BoT yasiyokuwa na kichwa wala miguu!! Meghji anajua pale alipozipeleka hizo fedha haramu yeye na Mrhm. Balali.
Anyway, tusubiri ukweli, maana bado ni tetesi.

Usipotoshe watu, kabla haujachangia please get your facts right! yeye hakuidhinisha malipo BoT.
 
Hiyo nafasi ya Mweka hazina ilifaaa sana kupewa Amos Makala maana hiyo nafasi ni kama Chief Financial officer wa CCM.

Amos Makala is qualified for the job, he is CPA(T). Zakia sijui ana elimu gani.

hahahaha mkuu siku hizi vipi?
 
Huyo Megji aliacha lini ufisadi?
Kwanza aeleze ghorofa ya Mbezi aliipataje. Sisi tunafahamu alijengewa na mafisadi wa vitalu vya uwindaji. Yeye anasemaje?
 
Mimi naona itakuwa vizuri tu maana wapinzani wa makalla walikuwa wanalalamika kuwa jamaa anatumia pesa nyingi sana kwenye maandalizi ya ubunge na kugawa misaada kibao
 
Hiyo nafasi ya Mweka hazina ilifaaa sana kupewa Amos Makala maana hiyo nafasi ni kama Chief Financial officer wa CCM.

Amos Makala is qualified for the job, he is CPA(T). Zakia sijui ana elimu gani.

Tangu lini appointments za CCM na serikalini (esp. mawaziri) huwa zinaangalia elimu ya mtu?
 
Tangu lini appointments za CCM na serikalini (esp. mawaziri) huwa zinaangalia elimu ya mtu?

mkuu siku hizi vipi?

Keil na Mwanakijiji,

Appointment ya mweka hazina wa chama sio ya KISIASA ni ya KITENDAJI.

Mawaziri wa serikali ni WANASIASA. Makatibu wakuu wa wizara ni WATENDAJI.

kWAHIYO, vyeo vya kisiasa havihitaji ELIMU ya hicho unachofanya, Ila cheo cha KIUTENDAJI kinahitaji ELIMU ya unachotenda.

Keil, sikuongelea uwaziri. Nimeongelea cheo cha utendaji cha mweka hazina wa CCM.
 
wanapeana kula tu. Hakuna kipya hapo kama ni kweli lakini.

Hii nimeipenda sana maana hata kama huna uhakika na jambo lenyewe bado unatanguliza malalamiko du. Sijuwi inakuwaje kwa mwendo huu. Yaaani hii inaitwa "Complains in advance". ili itakapotokea uwe umeshatimiza wajibu wetu wa kulalamika safi sana.

Na hii je: Nimesikia JK atamteua RA kuwa PM akishinda uchaguzi ujao na RA amekubali kugharamia gharama za kampeni za uchaguzi ujao kwa 75%.
 
Hii nimeipenda sana maana hata kama huna uhakika na jambo lenyewe bado unatanguliza malalamiko du. Sijuwi inakuwaje kwa mwendo huu. Yaaani hii inaitwa "Complains in advance". ili itakapotokea uwe umeshatimiza wajibu wetu wa kulalamika safi sana.

Na hii je: Nimesikia JK atamteua RA kuwa PM akishinda uchaguzi ujao na RA amekubali kugharamia gharama za kampeni za uchaguzi ujao kwa 75%.

Hiyo ya uwaziri mkuu haiwezekani
 
Hiyo nafasi ya Mweka hazina ilifaaa sana kupewa Amos Makala maana hiyo nafasi ni kama Chief Financial officer wa CCM.

Amos Makala is qualified for the job, he is CPA(T). Zakia sijui ana elimu gani.

mkuu mara nyingi hizi Post za kuteuana haziangalii sana sifa za kielimu, Maslahi kwanza halafu elimu baadaye. Mtu anayeteua Anaangalia ni jinsi gani atakutumia na kufaidika na wewe, na unajua kuficha siri kiasi gani, Basi.
 
Keil na Mwanakijiji,

Appointment ya mweka hazina wa chama sio ya KISIASA ni ya KITENDAJI.

Mawaziri wa serikali ni WANASIASA. Makatibu wakuu wa wizara ni WATENDAJI.

kWAHIYO, vyeo vya kisiasa havihitaji ELIMU ya hicho unachofanya, Ila cheo cha KIUTENDAJI kinahitaji ELIMU ya unachotenda.

Keil, sikuongelea uwaziri. Nimeongelea cheo cha utendaji cha mweka hazina wa CCM.

Mkuu FP,

Ninakubaliana na nadharia yako, lakini inapowekwa kwenye utekelezaji, si CCM wala Rais ambaye hufuata hayo unayoyasema wewe.

Naomba nikuulize, kwenye orodha ya Watunza Hazina wa CCM waliopita, yupi kati yao alikuwa na utaalam wa fani ya Uhasibu?

Tuanze na Rostam Azziz ambaye alimrithi Mama Mbatia (RIP), then twende kwa Mama Mbatia mwenyewe na wengine waliowahi kushika nyadhifa hizo kabla. Je, walikuwa ni magwiji wa fani ya Uhasibu?
 
Back
Top Bottom