Dalton elijah
JF-Expert Member
- Jul 19, 2022
- 373
- 829
AMRI KIEMBA|+
🗣“Kwa mazingira na namna ambavyo hizi timu zilivyo [Simba na Wydad Casablanca] na kwa heshima ya mpira wa miguu Simba inaweza kushinda kwa Mkapa.”
🗣“Kwa takwimu sasa ndio unakuja kugundua ugumu wa mechi, ugumu unaletwa na timu ambazo zinacheza. Wydad ni bingwa mtetezi lakini ameanza kwa nguvu kuutetea ubingwa.”
🗣“Kuna timu inachukua ubingwa halafu msimu unaofata anakuwa hoi! Wydad anatetea kama ndio anautafuta ubingwa, hicho ntio kitu ambacho kinaweza kuleta tofauti.”
🗣“Ukiangalia bingwa wa Kombe la Shirikisho Afrika RS Berkane, msimu huu ipo hoi na imetolewa hatua za mapema.”
🗣“Wydad ni timu ngumu kwa Simba lakini kwa historia ya Simba uwanja wa Mkapa inaonekana ni mechi ngumu pia kwa Wydad kuzuia kile ambacho Simba imekuwa ikikifanya uwanja wa Benjamin Mkapa.”
🗣“Inawezekana kumbukumbu za Raja bado zipo kwa watu wengi, inawezekana kilichoikuta Simba mbele ya Raja tayari kimekuwa somo ambalo wakati wanakutananao hawakuwanalo.”
🗣“Nyakati ambazo Simba ilifanikiwa kushinda mbele ya Al Ahly, AS Vita na hata kutoka sare na TP Mazembe, walikuwa wanaziheshimu hizo timu na historia zao lakini kwa Raja, Simba walikuwa wazi sana kama wanacheza mechi ya Ligi Kuu!”
🗣“Sioni Simba wakifanya hivyo tena dhidi ya Wydad kufunguka bila kujua wanawazuiaje.”
🗣“Kwa hiyo Simba kushinda uwanja wa Benjamin Mkapa inawezekana lakini matokeo ya jumla yatategemea zaidi mechi ya pili.”
🗣“Kwa mazingira na namna ambavyo hizi timu zilivyo [Simba na Wydad Casablanca] na kwa heshima ya mpira wa miguu Simba inaweza kushinda kwa Mkapa.”
🗣“Kwa takwimu sasa ndio unakuja kugundua ugumu wa mechi, ugumu unaletwa na timu ambazo zinacheza. Wydad ni bingwa mtetezi lakini ameanza kwa nguvu kuutetea ubingwa.”
🗣“Kuna timu inachukua ubingwa halafu msimu unaofata anakuwa hoi! Wydad anatetea kama ndio anautafuta ubingwa, hicho ntio kitu ambacho kinaweza kuleta tofauti.”
🗣“Ukiangalia bingwa wa Kombe la Shirikisho Afrika RS Berkane, msimu huu ipo hoi na imetolewa hatua za mapema.”
🗣“Wydad ni timu ngumu kwa Simba lakini kwa historia ya Simba uwanja wa Mkapa inaonekana ni mechi ngumu pia kwa Wydad kuzuia kile ambacho Simba imekuwa ikikifanya uwanja wa Benjamin Mkapa.”
🗣“Inawezekana kumbukumbu za Raja bado zipo kwa watu wengi, inawezekana kilichoikuta Simba mbele ya Raja tayari kimekuwa somo ambalo wakati wanakutananao hawakuwanalo.”
🗣“Nyakati ambazo Simba ilifanikiwa kushinda mbele ya Al Ahly, AS Vita na hata kutoka sare na TP Mazembe, walikuwa wanaziheshimu hizo timu na historia zao lakini kwa Raja, Simba walikuwa wazi sana kama wanacheza mechi ya Ligi Kuu!”
🗣“Sioni Simba wakifanya hivyo tena dhidi ya Wydad kufunguka bila kujua wanawazuiaje.”
🗣“Kwa hiyo Simba kushinda uwanja wa Benjamin Mkapa inawezekana lakini matokeo ya jumla yatategemea zaidi mechi ya pili.”