Amuua mke wake baada ya Mganga kumwambia atamuona ndotoni

Amuua mke wake baada ya Mganga kumwambia atamuona ndotoni

BARD AI

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2018
Posts
3,591
Reaction score
8,826
Jeshi la Polisi mkoani Tabora linamshikilia Ali Idd Mkonongo, mkazi wa Kijiji cha Inala kwa tuhuma za kumuua mke wake aliyefahamika kwa jina la Mariam Yusuph kwa kumpiga na kitu kizito kichwani wakati akiwa amelala majira ya saa sita usiku, kisha kuuchukua mwili na kuutumbukiza kisimani kwa lengo la kuficha ushahidi.

Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, ACP Richard Abwao, mwanaume huyo alitekeleza mauaji hayo baada ya kutoka kupigiwa ramli kwa mganga wa kienyeji na kuelezwa kwamba atamuona mchawi wake ndotoni. Baada ya kumuota mkewe, Ali amiamua kufanya mauaji hayo akitekeleza kile alichokiota ndotoni.

Mtuhumiwa atafikishwa mahakamani mara baada ya kukamilisha taratibu za uchunguzi dhidi ya mauaji hayo.
 
Jeshi la Polisi mkoani Tabora linamshikilia Ali Idd Mkonongo, mkazi wa Kijiji cha Inala kwa tuhuma za kumuua mke wake aliyefahamika kwa jina la Mariam Yusuph kwa kumpiga na kitu kizito kichwani wakati akiwa amelala majira ya saa sita usiku, kisha kuuchukua mwili na kuutumbukiza kisimani kwa lengo la kuficha ushahidi.

Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, ACP Richard Abwao, mwanaume huyo alitekeleza mauaji hayo baada ya kutoka kupigiwa ramli kwa mganga wa kienyeji na kuelezwa kwamba atamuona mchawi wake ndotoni. Baada ya kumuota mkewe, Ali amiamua kufanya mauaji hayo akitekeleza kile alichokiota ndotoni.

Mtuhumiwa atafikishwa mahakamani mara baada ya kukamilisha taratibu za uchunguzi dhidi ya mauaji hayo.
Ndoto na marudio ya mambo tunayaexperience sana sana...kuamini mganga labda umuote mtu ambae hukuwahi kumuona na baadae akaja akatokea
 
Sasa hapa anapelekwa mahakani ili iweje wakati yeye na mganga wake watangulizwe kaburini.mahakami alafu jela .wanaenda kula tena tozo zetu kwa kulishwa mara tatu kila siku.ya nini yote haya.kaua na yeye auliwe fullstop.
 
Elimu! Elimu! Elimu!

Wazazi, tujitahid sana kuwasomesha watoto wetu ili kuepukana na hizi dhana potofu zinazowaangamiza wajinga wengi.
 
... eti hawa ndio waelewe maana ya Katiba Mpya! Never! Bad enough ndio wapiga kura sasa; hawakosagi kwenda kupiga kura kwenye uchaguzi wowote ule. In short ndio wanaolichagulia taifa viongozi.
Hao watu ndio mtaji mkubwa wa chama ukiwapa kofia na shati ndio basi tena
 
... eti hawa ndio waelewe maana ya Katiba Mpya! Never! Bad enough ndio wapiga kura sasa; hawakosagi kwenda kupiga kura kwenye uchaguzi wowote ule. In short ndio wanaolichagulia taifa viongozi.
Mwanadamu aliye mbali na Mungu ni kama mnyama tu wa kawaida. Angalia karne hii bado watu wanawaamini waganga wa kienyeji ambao kimsingi,waganga hawa ni watumishi wa ibilisi. Na ibilisi ndiye muuaji tangu mwanzo. Anaendeleza kazi zake za uuaji.

JESUS IS LORD
 
Back
Top Bottom