Anaandika mwana Simba Yericko Nyerere

Binafsi kila nikifikiria future ya Simba sc huwa napata ukakasi na Boss MO .. huyu ni mwekezaji wa hii timu ndio ila naona ana sintofahamu nyingi sana zinazoigharimu simba sc.. ukiachana na makando kando mengine ya uongozi but huyu ndio kikwazo namba moja cha simba sc kutofikia hatua za juu sana japo wanachama wengi huwa hawaelewi.. MAAMUZI YAKE YAPO SELF-CENTRED na yanaigharimu simba sc pakubwa sana.. naondoka zangu.. ila matusi ruksa
 
Rage alipowaita mbumbumbu, hata hakukosea. Kipindi hicho ukiwauliza zilipo bilioni 20 za mwekezaji, walikuwa wanajibu kimbumbumbu tu!!

Eti wanachoangalia ni timu kufanya vizuri! Wachezaji wanalipwa mishahara! Basi!! Haya sasa!! Baada ya timu kuanza kupata matokeo ya kusuasua! Wanaanza tena kukamatana uchawi.
 
Yaani hizo pesa zinatolewa nususu kama kikoba.
Timu ikipiga kambi anaandikiwa rejesho, sijui wako Dubai rejesho, sijui wasajili kwa 100m rejesho, hiyo 20B hadi itimie ni miaka 20 ijayo😂😂😂
 
Mkimaliza kuparurana, mje mtupe conclusion
CC Mbaga Jr
 
Kuna kitu inabidi mtusaidie kuelewa Sisi vichwa ngumu. Tangu msimu umeanza mwaka Jana ni lini Simba ilikuwa na timu nzuri? Kwa nini mnakubali kusifia timu inayopata matokeo ya kubahatisha kama mnavyosema? Ilikuwa sahihi Sana kama Tangu mwanzo wa msimu baada ya kuona usajili mbovu mngepiga kelele kuliko kusubiri Mambo yaharibike ndo mnakuja kuchana mabango. Mwekezaji ameshawaona mnavyoridhika kirahisi ndo maana mnaletewa hata mchezaji ambaye hajacheza mwaka mzima Kwa sababu ya majeruhi na bado mnashika mabango kumsifia.
 
Hesabu ni rahisi sana:-
1. Kuliko usajili waxchezaji 6 wa kigeni wa milioni mia mbili kila mmoja sawa na bilioni moja na milioni mia mbili halafu baada ya miezi sita unawatoa kwa mkopo kwenda sijui Ihefu huko ni bora usajili wachezaji 3 wa milioni mia nne kila mmoja sawa na shilingi bilioni moja na milioni mia mbili ile ile.
2. Ni bora kuwa na wachezaji watatu wa kigeni wenye uwezo mkubwa wanaoingia kwenye first eleven moja kwa kwa moja tangu siku ya kwanza wanasajiliwa na wakakupa matokeo kuliko kuwa na rundo la wachezaji 6 wa kigeni wenye uwezo mdogo wanaokaa benchi na hata wakicheza wanakupa matokeo mabovu.

Kwenu viongozi wa Simba, bodi nzima ya Simba na mwekezaji hesabu hizo hapo juu tafakarini kuelekea super league ya Afrika na pesa za kutosha za usajili mtapewa na maandalizi muanze mapema maana mwezi wa nane sio mbali.
 
Kombe huwa linachukuliwa na team Moja pekee hivyo Simba kupoteza si Hoja maana hata msimu ujao atapoteza sana na atakuwa na draw nyingi (8) na kupoteza game 4
Safari ya kukosa bado IPO sana
 
Matatizo ya Simba yapo ndani na nje ya uwanja, tukianza nje kwenye uongozi na mwekezaji,.
Mwekezaji badala ya kutimiza malengo yake amekuwa anatumia muda mwingi kujisia twitter na kwenye vyombo vya habari. Aliwahi kusema anawekeza pesa nyingi kwenye timu na inampa hasara ingawa wakati huohuo anasema alikataa udhamini wa bilioni 2.5 ili aunge mkono juhudi za rais kutangaza utalii. Anajitapa kuwa ametumia pesa nyingi kwenye usajili lakini hatuoni quality ya wachezaji aliosajili wengine kama Sawadogo na Quatara ni watu ambao hawafikirii hata kuwekwa benchi.
Apunguze kuongea afanye vitendo kabla ya kuingia uwekezaji tuliona akilaumu Simba kuuza wachezaji wake wazuri wlakini chini yake tumeuza wachezaji tegemeo kama Luis, Bwalya na Chama ingawa alirudi. Amelazimisha uongozi uchaguliwe utakaoendana na matakwa yake.
Uongozi wengi waliopo pale hawajui mambo ya mpira ni sehemu wamekuja kutafuta umaarufu na pesa. Timu imetoka Morocco inapangiwa mechi mbili mfululizo ndani ya wiki lakini viongozi wamekaa kimya ingekuwa upande wa pili wangeshago lakini kwa sababu tuna viongozi matutusa wanaona kila kitu sawa. Lakini wameleta Siasa na kutotaka kipa namba mbili asipangwe kisa amehusishwa na kusajiliwa Singida united ambao ni ndugu na Yanga. Wameendelea kukaa na wachezaji wazee na wasio na uwezo lakini wameshindwa kumwoji kocha pale anapoacha wachezaji wazuri na kung'ang'ania wazee.
Benchi la ufundi nalo linabeba lawama kubwa kwanza Simba ina wachezaji kama Phiri, Sackho, Banda na Okra ambao wakati ligi inaanza walitubeba sana ila kama Phiri hata benchi hawekwi. Wanachelewa kufanya sub hata pale wanapoona kuna wachezaji wamechoka ama hawapo mchezoni. Wameendelea kung'ang'ania wachezaji walewale na mbinu ileile, wameendelea kumwamini kipa no 3 pamoja na mwendelezo wa makosa yake.
Wachezaji hawawezi kukwepa lawama kipa wetu anafungwa magoli rahisi sana mabeki wetu ni waziti goli la kwanza ni Inonga peke yake aliyerudi kwa haraka wengine wote walibaki wamejisahau. Mzamiru anayecheza Simba na anayecheza timu ya taifa ni watu wawili tofauti akiwa Simba akipata mpira nanshindwa kufanya maamuzi wapi aupeleke pia amekuwa harudi kwenye eneo lake kuwasaidia mabeki pamoja na kupiga pasi zisizo na macho. Mtu kama Saido sio wa kucheza dakika 90 ila dakika 20 zinatosha pia acheze kwa ajili ya timu na sio kujifikiri yeye binafsi pia Kibu Denis pamoja na kukaba vizuri maamuzi yake mengi hayana faida kwa timu.
 
Simba ni sawa na RC na CCM ni taasisi zinazoogopa mabadiliko sana
 
Duh poleni sana. Wana thimbaaaa mlete mdhungu.sasa mnadhika au mnasafirisha? Tupo hapa nanyumbu NTWARA
 
Loosers fc
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…