Anachofanya Waziri Mkuu sio sawa, sio haki, sio Good Governance! Ni udhalilishaji na kuaibishana!

Anachofanya Waziri Mkuu sio sawa, sio haki, sio Good Governance! Ni udhalilishaji na kuaibishana!

Nafikiri taasisi ya Urais ni kubwa kuliko nyingine linapokuja suala la uongozi kwenye nchi inayofuata mfumo wa kirais...
Tuna mifano kadhaa ya Marais/Watendaji wengine wakuu ambao wameshindwa kwenye uongozi wao kwa kuchekea chekea wahalifu...sioni kwanini kuwepo tena na donge pale anapoingia mtu asiyemung'unya mambo anapotumia rungu kutokomeza ubadhirifu.
 
Pasco wewe ni mjinga sana wambie waliokutuma Hatudanganyiki Mambo yawe wazi acha upopoma kabisa...
 
Wahalifu wengi hujificha nyuma ya good governance. Nidhamu ya utumishi irejee kwanza, good governance baadaye. Mwizi anadhalilika?
 
Yupo sawa, akisema awaite pembeni watamlaghai na kuomba asamehewe na km ni kugogo mazingira ya rushwa yatazidi kujengwa.
 
Hivi Pasco sio wewe uliye mshauri Rais Magufuli afute utawala wa kisheria aongoze kwa Presidential decrees ??

Nadhani hapa anazungumziwa Kassim Majaliwa ambaye si Rais wa Tanzania.

Leave Makofuli alone!!
 
Last edited by a moderator:
Inaonekana wewe una upeo mdogo sana
hadi comments zako zingine nashindwa ku reply

Kama wewe mwananchi unapenda kinachoendelea basi ujue wapo wananchi wengine hatupendi pia kinachoendelea
hatupendi kusikia waziri mkuu kagundua makontena yamepotea kila siku
tungependa hilo tatizo liwe fixed for good....wezi wakamatwe wafungwe..system ibadilishwe
biashara ziendelee na tuzungumze mengine yenye umuhimu..

sio kila mtu ana enjoy kutazama tv na kukuta the never ending story ya makontena.....
wengine tungependa story tofauti huko bandarini ...success stories.....

sisi wengine hatumpongezi mtu kwa ku expose tatizo
tunapongeza watu kwa kuli fix tatizo for good....sio kila wiki habari ndo hiyo hiyo...
Bossman, talking of success stories...man...!
Huwezi kuongelea success stories overnight. Hilo halipo na haliwezi kuwepo, success stories have sad stories behind them, lazima kuumia na pengine kutoa damu ili kuimba 'nyimbo za haleluya'.
Tatizo wengi wetu tunapenda "easy and quick fix", PM aende bandari, atoe list ya wahujumu uchumi na wezi, wafungwe na maisha yaendelee tena tupate hizo "success stories". Hilo halipo na haliwezi tokea. Hata uchina, marekani, ujerumani nk walipitia huku mnakoita "kudhalilishana" hadi leo mnawaona superpowers. Soma history za Hitler & co. Utagundua mengi kabla ya kuimba "stories of success"
I applaud PM's approach, iwe ya kidikteta ama ya kudhalilisha, na anatuma ujumbe kwa jamii yenye virusi vya wizi, ubadhirifu, hujuma, uvivu na uzembe...that it's no longer a rollercoaster...
 
Tuwape nafasi viongozi wetu wafanye kazi na zaidi tuwaunge mkono, inchi ilishaharibika hii.
 
Pasco,

Acha Majaliwa na Dr.Magufuli wafanye hivyo hayo mambo ya good governance!Mkapa na Sumaye, Jk na Pinda wameyafanya sana hayakuwa na impact yeyote.
 
Last edited by a moderator:
Hakuna kuleana tena, nchi hii ni ya watanzania wote na haiwezekani wachache kuendelea kuiibia nchi kwa manufaaa yao binafsi. Binafsi nafarijika kuona Mhe. Majaliwa, Kasim Majaliwa akifanya kazi yake kwa uhuru. Zamani "business as usual" sasa basi.
 
Hacha umandazi wewe kipindi wanapiga hizo dili walikuwa awalidhalilishi taifa??kuna watu wamekufa kwa kukosa dawa hospitalini eti nchi haina hela ya kununua dawa kumbe hela zote zipo kwa hao wapiga dili.ndio muda wao kudhalilishwa dunia ijue wezi walio lighalimu taifa hill.
 
Ni mparaganyiko kwa kweda mbele.Ila watu tukisema tunaonekana kana kwamba hatumpendi Magufuli wakati suala si kumpenda wala kumchukia.
Huu sio muda wa kupendwa na mijitu minafki kama nyie, mpende msipende haituhusu tunataka hivihivi, mgekuwa watu wenye kujielewa na kujitambua mgepinga majizi kuwa malaika ktk li chama lenu
 
Ukweli ni kwamba hata yeye PM akishtukizwa sasa ivi na kuhojiwa mambo ya huko Tamisemi alikokuwa hatakuwa na majibu sahihi. Kuwa mkuu haimaanishi umekariri data zote za ofisini. Pia ktk ofisi kuna vitengo tofauti kwaiyo ni vema akiwa anahoji awaite wahusika kutoka kila kitengo badala ya kumuandama boss tu maana mambo mengne hufanyika kwa niaba ya.
 
Huu sio muda wa kupendwa na mijitu minafki kama nyie, mpende msipende haituhusu tunataka hivihivi, mgekuwa watu wenye kujielewa na kujitambua mgepinga majizi kuwa malaika ktk li chama lenu

Umejamba mara ngapi leo?
 
Hayo ni maoni ni kwanini unataka uyanlazimishe kqwa WatanZania wote? Hayo ya utawala bora ni kulingana na tafsiri yako wewe na jinsi unavyoongoza familia nyumbani kwako usitake kutuletea kwenye nchi yetu, tumeshatoka huko, tumeshayafanya yote hayo ya kuitana faragha, kuundiana tume, kuonyana kwamba ninawajua wala rushwa msipojirekebisha mtakona cha mtema kuni kote huko tumepita lkn matokeo yake nikwamba makontena zaidi ya 2500 hayajalipiwa kodi, yaani yamekombolewa Bandarini bila kulipiwa sasa huu ni uhujumu Uchumi na kwa nchi nyingine adhabu yake ni sawa na Uhaini kwani unalinganishwa na uuwaji watu wote waliofia mapokezi kwa kukosa dawa hospitalini wameuliwa na hawa wezi!

Hivyo tuache na Magufuli wetu tumeshamkubali jinsi alivyo na vyovyote anavyofanya ana baraka zetu, na ndio maana ya kushinda Uchaguzi na kuwa Raisi vinginevyo basi kila mtu angejiongoza?

Mwambie hajielewi huyo. Sina shaka huyo jamaaa anaslahi binafsi na hao wezi. Hatutarudi nyuma, tumechoka!
 
Nimeusikiliza kwa makini mziki huu wa Magufuli na Majaliwa na nimegundua kuwa Pinda asingeuweza hata kidogo. Huu mziki ni original tena ni wa asili ya kitanzania. Hebu angalia namba ya makontena yanayopita bandari moja tu ya Dar. Bila kulipiwa kodi, sasa kwa nchi nzima mambo ya TRA yakoje?
 
Wanabodi,

Kwanza naomba kukiri, kuwa ninaunga mkono kwa asilimia 100% juhudi za serikali awamu ya 5 kupambana na rushwa, ufisadi, uzembe na ukwepaji kodi, ili mtindo unaotumiwa na Waziri Mkuu, wetu, Mhe. Majaliwa, Kasim Majaliwa, sio!.

Baada ya kukisikia kisanga cha TRA kilichomngoa Kamishna Mkuu na maofisa kadhaa kufuatia sakata la makontena, leo amerudi tena bandarini, na nimekishuhudia kitu anachokifanya, japo anashangiliwa na umati wa watu, lakini anachokifanya ni kuviziana, kutishana, kudhalilishana na kunakwenda kinyume cha utawala bora, yaani good governance!.

Waziri Mkuu anafanya ziara za kushtukiza mahali, huki akiwa na karatasi lenye tuhuma specific, lakini amelificha!, anakwenda kumuuliza mhusika wa pale kuhusu utendaji wa mfumo fulani, anaelezwa kuwa mfumo uko perfect, kisha analiibua hilo kaatasi lenye tuhuma na kuanza kumsomea mhusika mbele ya kadamnasi ya watu, abcd!, mhusika anashindwa kujibu, atasimamishwa kazi, na kama yuko juu ya mamlaka yake, atamchongea kwa rais!.

Hata TRA siku hiyo alikwenda na nondo za makomtena, alipomuuliza Bade, akamjibu details ziko kwa maofisa wangu, ndipo akaibua nondo lake na kumsomea kwenye kadamnasi ili aonekane mjinga!, huku ni kuaibishana, kudhalilishana na kinyume cha good governance!.

Baada ya kutoka bandaini, akaenda TRL na kumuuliza mkurugenzi mkuu, mlikopa bilioni 3 TIB za kufanyia nini?!, kwa nini hamkufanya kile mlichokopea?, akaambiwa tumelipia mishahara, nani aliwapa idhini ya kukopa?!, Mkuugenzi hana jibu na naamini kesho atatangazwa hana kazi!.

Top management angekaa nao ofisini na kuulizana kistaarabu ndio good governance!. Mimi hata home, wife alikuwa na tabia ya kuwafokea ma tx home, mbele ya watoto, nikamkataza!, nikamsisitiza if things are not right, muite pembeni ndipo umseme, sio kumdhalilisha mbele ya watoto!.

Anachofanya Waziri Mkuu, wetu, Mhe. Majaliwa, Kasim Majaliwa ni kuviziana, kudhalilishana na kuabishana bila sababu za msingi!, hili la kuitana na kuanza kuhojiana mbele ya waandishi ili watu wamuone alivyo mkali, ni tabia za ma populist leaders!, Leo nimemuona Magufuli akiongea na wafanyabiashara yuko very humble even cracking some jokes!.

Kama kuna watu wako karibu na Waziri Mkuu, wetu, Mhe. Majaliwa, Kasim Majaliwa, wamwambie anavyofanya sio vizuri, Sio Sawa, Sio Haki, Sio Good Governance!, Ni Udhalilishaji na Kuaibishana tuu!. Akumbushwe kuna kitu kinatwa 'karma' kisije kumshukia!.
Au wewe unaonaje?!, toa maoni yako ni sawa au sio sawa!.
Pasco

Mwaka huu wewe FISADI UTAKOMA NA BADO RUDISHA PESA ZETU. MWIZI WEWE.
 
Back
Top Bottom