Pre GE2025 Anaetaka kumpinga Rais Samia asigombee 2025 anaweza kuja na hoja gani? Anahujumiwa?

Pre GE2025 Anaetaka kumpinga Rais Samia asigombee 2025 anaweza kuja na hoja gani? Anahujumiwa?

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Kwahiyo kimsingi unakubali vyombo vya serekali vinafanya haya ya kuteka watu na kadhalika ila isipokuwa tu hoja yako ni kusema mama hausiki sio?
Hakuna mtu anakata tawi alilolikalia. Mama kifupi anazo sifa kuu 4 muhimu: Mwanamke, Mzanzibar, mchapakazi na mwanademokrasia wa kimataifa. Anafahamu kuwa dunia inampima kama Rais mwanamke, Mzanzibar, ufanisi kazini na ustawi wa demokrasia. Kwavyovyote vile hawezi kufungulia siasa za upinzani kwa mkono wa kulia na kuzifungia kwa mkono wake wa kushoto. Kuna watu wanataka kumzunguuka, lazima awawahi mapema. Ndio maana hata Dr. Nchimbi, katibu Mkuu CCM alishangaa kuona viongozi wa chadema wanapigwa na kuzuiwa kufanya mikutano ambayo Rais kasema iendelee, hujakaa vizuri anajitokeza mtu anasema yeye kahusika na ushindi wa CCM kwa 100% hata ikibidi kwa kwenda maporini. Wasomi wa Cuba tupo wengi kaka nchini. Wanataka Tanzania igonge vichwa vya habari kitaifa na kimataifa kwa mambo machafu kuhusu demokrasia. Kwanini akina Saanane hatukuwaona hadi leo, kwanini huyu atupwe hapo anunio tu kama mtekaji ni huyohuyo mmoja na kama malengo ya utekaji ni hayohayo?
 
hata ulichoandika wewe ni uongo vilevile. Mama ndiye mtu wa kwanza kupiga marufuku watu kufungiwa biashara na kunyang'anywa mali zao na TRA, kama kuna mtu bado anafanya hivyo ni kwasababu mlipakodi ana shida nyingi nyingine na kodi lazima ilipwe.
Ullichokosa ni akili
 
Critical thinkers watajua kuwa Hakuna serikali inayoteka raia
"Critical Thinkers" hao hao watakuwa siyo halisi wakishindwa kuuliza inakuwaje serikali hiyo hiyo yenye vyombo vyote vya kuzuia hayo mabaya kwa raia isiwe na uwezo wa kuyazuia!
Ni 'critical thinker' thinker wa aina gani hao wasioweza kuhoji 'paralysis' iliyo mkumba huyu kiongozi aliye mwagiwa sifa zote hizo za kiutendaji, ashindwe hata kutumia uwezo wake wa uongozi kuwatuliza raia wake na kuwahakikishia usalama wao?

Umetaja hizo '4R'; mbona hiyo ingekuwa ndiyo ngao yake kuu kabisa wakati huu wa kuwachapia hawa mnao waita wahujumu wake? Hana uwezo wa kuitumia kinga hiyo kumlinda yeye mbele za raia wake na nje ya nchi?
 
Back
Top Bottom