Analoshindwa Putin aliliweza Magufuli kwa kutumia zawadi ya tausi watatu kwa Museveni na Kenyatta

Analoshindwa Putin aliliweza Magufuli kwa kutumia zawadi ya tausi watatu kwa Museveni na Kenyatta

Rais kama anakubalika kwa wa2 wake shida nini? Pro amerika mnamuona putin ni dikteta, ila mnajitoa ufahamu kwa marais wa marekani ndiyo madikteta wenyewe, wameshauwa wengi tuu waco na hatia, so utasemaje wao co madikteta!!!!
Huna uhakika kama mimi ni pro au against america. Putin aliangusha ndege ya Uholanzi akaua mamia ya raia wasio na hatia kisa tu ndege ilikuwa inakatiza anga la Ukraine.

Ni mshenzi anayedhani nguvu bila hekima ina msaada wowote ule. Rais wa sasa wa Ukraine ni myahudi, na nadhani unawajua hao jamaa walivyo na mtandao wa watu hao dunia nzima, hawatamuacha salama akithubutu kuigusa Ukraine.
 
Huna uhakika kama mimi ni pro au against america. Putin aliangusha ndege ya Uholanzi akaua mamia ya raia wasio na hatia kisa tu ndege ilikuwa inakatiza anga la Ukraine.

Ni mshenzi anayedhani nguvu bila hekima ina msaada wowote ule. Rais wa sasa wa Ukraine ni myahudi, na nadhani unawajua hao jamaa walivyo na mtandao wa watu hao dunia nzima, hawatamuacha salama akithubutu kuigusa Ukraine.
Kwahiyo wewe nchi yako Ina strong intelligence Kuliko KGB !? [emoji16][emoji16][emoji16]
Aisee bongo shikamoo [emoji119][emoji119][emoji119]
 
Wee jmaaa ni kiazii sna aisee Una elimu gani Kwanza tuanzie apoo Kama Una bachelor nawahurumia watoto wakona walimu waliokufundisha na wazazi wako kabisa unafananisha mgogoro WA Ukrein na Kenya na uganda useless kabisa
 
Kwahiyo wewe nchi yako Ina strong intelligence Kuliko KGB !? [emoji16][emoji16][emoji16]
Aisee bongo shikamoo [emoji119][emoji119][emoji119]
Kuwa na strong intelligence sio kitu kama nchi inaongozwa na rais mbabe kama Putin
 
Wee jmaaa ni kiazii sna aisee Una elimu gani Kwanza tuanzie apoo Kama Una bachelor nawahurumia watoto wakona walimu waliokufundisha na wazazi wako kabisa unafananisha mgogoro WA Ukrein na Kenya na uganda useless kabisa
Ukitoka kuvuta bangi tulia kwanza mpaka itulie kichwani halafu ndio uingie JF. Mgogoro wowote wa kimataifa njia zake za utatuzi hazitofautiani. Somo ni lile lile la international relations.
 
Hapana,,,sinaga tabia ya kumzarau mtu. Wewe upo kimasomo huko, utayajuwa wapia ya puttin na ukraine!!! Unadhani huko ni bongo!!!
Kuwa masomoni haikuzuii kuangalia TV kila jioni, unachanganyika na watu kila siku. Unajikuta ukiwafahamu kwa ukaribu.
 
Ujerumani na Urusi naweza kusema wana historia mbaya baina yao hususani ukiangalia WW2. Mfano battle of stalingrad. Ni moja ya pambano baya sana yenye unyama mkubwa sana lililopiganwa baina ya Urusi na Ujerumani ya Hitler kuliko pambano lolote lililopiganwa kwenye WW2.

Ujerumani ilipeleka wanajeshi millioni 1, vifaru 1700 na ndege jeshi 2000. Zote kwa uelekeo mmoja kwa wakati mmoja zilielekea Urusi kuiweka Moscow chini ya Ujerumani. Ni jeshi kubwa ambalo Mjerumani hakupeleka sehemu yoyote isipokuwa Urusi. Kwa hili, Urusi ilipoteza wanajeshi na raia waliyojitolea kupambana na Ujerumani millioni 1+.. Ni sacrifice kubwa haikutokea mahala popote duniani kwenye hii vita isipokuwa Urusi tu.

Hii ni historia, inabeba maumivu na inabeba hisia. Wakati mwengine in a we za kubeba uhasama baina ya hizo nchi ikiwa juhudi za kimakusudi zisipochukuliwa ili kusameheana kwa kujenga urafiki na kusonga mbele.

Ujerumani analifahamu hili! Hivyo hataki kuingia mgogoro wa aina yoyote utakaoleta mkwaruzano mkubwa kati ya nchi yake na Urusi. Yupo NATO lakini bado ana mahusiano ukiyaangalia ni mazuri na Urusi. Licha ya mradi mkubwa wa gesi kwa manufaa ya mataifa yote mawili lakini ukiiangalia Ujerumani kiumakini haitaki kuingia kwenye mgogoro wenye mvutano mkubwa na Urusi. Njia iliyochagua Ujerumani ni kujenga urafiki wa kiuchumi ambayo ni manufaa kwa mataifa yote mawili.

Na hili Marekani linamuuma.
Well said....
 
kumbe lengo la mada yako lilikuwa ni kumsifia marehemu jiwe.

ni bora ungefupisha mada kwa kuandika paragraph mbili tu kuliko kutuchosha kwa porojo nyingi.

haya tumekusikia mzee wa kumfsia marehemu.
Mwanzo wa mada unafanana na mwisho wake.
 
Putin hana maarifa ya diplomasia. Upo muungano mwingine unaoongozwa na Russia, humo kuna kina Kirgystan na Belorussia, mataifa ambayo kwa Russia hayana nguvu ya kupinga maamuzi yao.

Wanataka na Ukraine nao wawaheshimu na wawanyenyekee, kitu ambacho ni ngumu kutokea. Ukraine ni nchi yenye ushawishi inabidi itumike akili ya ziada kuweza kuwa na ushirikiano nayo.
Natizam CNN, Fox News, Sky News+ ya Australia, RT America, Russia Insight, Euro news n.k. Mahali pekee unapoweza kupata taarifa za Urusi kiuhakika ni RT na Russia Insight. Hizo vyombo vya habari vyengine wanakata taarifa/vipande vya video na kuviweka vile ambavyo vitakavyofit ajenda zao. Ukitaka kugundua hili fuatilia vyombo vya habari vya Urusi kisha angalia kwenye hivyo vyengine nilivyovitaja utaona mchezo wanaoufanya.

Malcolm X alisema kuwa makini na vyombo vya habari, usipokuwa makini utampenda anayeonea na utamchukia anayeonewa. Kusema Putin hana maarifa ya diplomasia aiseee! Inakubidi ufuatilie kwa umakini haya masuala.
Ukraine inamuumiza kichwa Putin kwa sababu zinapakana, ule ukaribu wa pua na mdomo halafu Russia anakosa mbinu wala ushawishi wa hoja wa kumvuta karibu. Ni masuala ya ulinzi zaidi.

Ni sawa sawa na Zanzibar inavyoshikiliwa na Tanganyika. Huwezi kuelewa wala kuona umuhimu wa visiwa vikiwa chini ya Muungano lakini vikishakuwa huru ni hatari kwa uhuru wa huku Bara.
February 9, 1990 James Baker officially announced "Washington can guarantee that NATO borders won't move an inch eastward if the USSR can help them with uniting Germany"

Kwa kuliweka wazi zaidi UK secretary for foreign affairs alisema maneno hayo hayo kwa maana the unified Germany would not end up being a threat to the USSR.

10February, 1990 the future chancellor of Germany Helmut alisema;

" We believe that NATO should not expand the sphere of its activity. We have to find a reasonable resolution. I correctly understand the security interests of the Soviet Union, and i realize that you, Mr. General secretary, and the Soviet leadership will have to clearly explain what is happening to the Soviet people".

Hizi ahadi zilidumu mwisho 1997. Czech Republic, Hungary n.k walijiunga NATO. Unafikiria Urusi ikufikirie vipi? Wao ni wajinga? Na wao (west) ni werevu? Kuwa hawajui mpango wa NATO ni upi? Ukraine na Urusi ni pua na mdomo.
 
Natizam CNN, Fox News, Sky News+ ya Australia, RT America, Russia Insight, Euro news n.k. Mahali pekee unapoweza kupata taarifa za Urusi kiuhakika ni RT na Russia Insight. Hizo vyombo vya habari vyengine wanakata taarifa/vipande vya video na kuviweka vile ambavyo vitakavyofit ajenda zao. Ukitaka kugundua hili fuatilia vyombo vya habari vya Urusi kisha angalia kwenye hivyo vyengine nilivyovitaja utaona mchezo wanaoufanya.

Malcolm X alisema kuwa makini na vyombo vya habari, usipokuwa makini utampenda anayeonea na utamchukia anayeonewa. Kusema Putin hana maarifa ya diplomasia aiseee! Inakubidi ufuatilie kwa umakini haya masuala.

February 9, 1990 James Baker officially announced "Washington can guarantee that NATO borders won't move an inc eastward if the USSR can help them with uniting Germany"

Kwa kuliweka wazi zaidi UK secretary for foreign affairs alisema maneno hayo hayo kwa maana the unified Germany would not end up being a threat to the USSR.

10February, 1990 the future chancellor of Germany Helmut alisema;

" We believe that NATO should not expand the sphere of its activity. We have to find a reasonable resolution. I correctly understand the security interests of the Soviet Union, and i realize that you, Mr. General secretary, and the Soviet leadership will have to clearly explain what is happening to the Soviet people".

Hizi ahadi zilidumu mwisho 1997. Czech Republic, Hungary n.k walijiunga NATO. Unafikiria Urusi ikufikirie vipi? Wao ni wajinga? Na wao (west) ni werevu? Kuwa hawajui mpango wa NATO ni upi? Ukraine na Urusi ni pua na mdomo.
Haya yanayoendelea sasa hayakusikika miaka ile ya Yeltsin, changamoto zilimalizwa bila ya watu kutishiana misuli.

Russia inawakosa wanasiasa wenye kuyajua mazungumzo ya kidiplomasia ambao wanajenga hoja na kueleweka bila kutumia lugha za vitisho au kulazimisha mtu akubaliane na unachofikiri.
 
Haya yanayoendelea sasa hayakusikika miaka ile ya Yeltsin, changamoto zilimalizwa bila ya watu kutishiana misuli.
Yeltsin? Rais mlevi? Ambaye analewa chakari na anatoroka kabisa mpaka Ikulu kwenda kupata mvinyo! Huyo, Gorbachev ni vituko tu. Na miaka hiyo Urusi ilikuwa ni dhaifu na ndiyo maana hizo ahadi zilivunjwa na NATO kwa muda huo. Na hao wanawekwa kwenye makundi mawili, either ni traitor or stupid.
Russia inawakosa wanasiasa wenye kuyajua mazungumzo ya kidiplomasia ambao wanajenga hoja na kueleweka bila kutumia lugha za vitisho au kulazimisha mtu akubaliane na unachofikiri.
Unamjua Sergei Lavrov? Kwa sasa ndiye anafahamika kama mwanadiplomasia kamili duniani.
 
Video ya Vladmir Putin akihojiwa na waandishi wa habari wa vyombo vya habari vya magharibi inatembea mitandaoni. Putin anajitahidi sana kujenga hoja za kujibu maswali lakini kama kawaida yake anarudia makosa yale yale ya miaka yote. Putin aidha hana team nzuri ya Diplomasia au anaogopwa na wasaidizi wake ambao ni mawaziri wa Mambo ya nje wote aliowatumia tangu awe rais kwa mara ya kwanza mwaka 1999.

Putin anatumia nguvu kutaka Ukraine iwe karibu na Russia. Anataka kulazimisha wakati majibu atakayoyapata kutoka kwa Ukraine ni mepesi tu, sisi ni nchi huru wenye kuweza kufanya maamuzi yoyote muda wowote ule. Kwenye diplomasia kawaida nchi haitakiwi kulazimisha upendo au ridhaa ya mwingine. Ni mwendo wa ushawishi na nguvu ya kujenga hoja ndio inayotakiwa.

Hayati Boris Yeltsin ndio alikuwa kinara wa mahusiano ya kimataifa. Sauti yake akiongea ya mtu mlevi iliwachekesha viongozi mbalimbali wa wakati ule,. Ulevi wake wa pombe kali ulimpatia umaarufu haswa zile video zake zikimuonyesha akiwa na uso mwekundu akiwa kalewa chakali. Lilipokuja suala la diplomasia aliweza kuitawala Ukraine pasipo kulazimika kutumia majeshi.

Yeltsin alikuwa na mtu mmoja mahiri sana katika masuala ya diplomasia akiitwa Victor Stepanovich Chernomyrdin akiwa ni waziri wa mambo ya nje wa wakati ule. Asingeweza kusikika akiichimba mkwara Ukraine. Wala Russia isingeweza hata siku moja kulazimika kupiga mizinga kule Odessa. Silaha ya uhakika iliyoiweka Ukraine karibu na Russia ilikuwa ni nyepesi sana inaitwa 'nyama ya ulimi' waingereza wanaiita convincing powers, ukipenda unaweza ukaiita nguvu ya hoja. Unamteka mtu kwa hoja tu kwa kuyapangilia maneno mazuri mpaka anatulia na anakuwa upande wako kwa kila kitu.

Tanzania imeweza kudumu na umaarufu wake kimataifa ikibebwa na uteuzi mahiri unaofanywa na marais wa mawaziri wa mambo ya nje. Kuanzia RIP Mkapa alivyomuamini Kikwete kama waziri wake wa mambo ya nje. Akaja Kikwete akamwamini Benard Membe kama waziri wake wa mambo ya nje. Akaja JPM akamwamini Profesa Kabudi. Na sasa SSH anavyomuamini na kumtumia Mama Mulamula.

Jinsi Putin anavyoishindwa hii tasnia nzima ya mahusiano ya kimataifa ananikumbusha ile mbinu ambayo RIP Magufuli aliitumia ya kuwavuta kwake marais wa Kenya na Uganda kwa kuwapa ndege aina ya tausi. Kwa mtazamo wa haraka haraka mtu anaweza asielewe maana ya wale ndege. Lakini leo unampa tausi Mzee Museveni halafu kesho anakupa mradi wa kupitisha bomba la mafuta lenye urefu wa maelfu ya kilomita litakalotoa ajira nyingi za moja kwa moja.

Leo unampa tausi Kenyatta halafu kesho likitokea tatizo la kidiplomasia anakuwa wa kwanza kusema sisi ni majirani tusiokuwa na shida yoyote katika uhusiano wetu. Hiyo ni nguvu ya kidiplomasia ambayo Tanzania siku zote tunajua kutengeneza misingi ya kuiweza lakini cha ajabu Russia na ukubwa wa taifa walionao wanaonekana kuishindwa. Putin angeweza kabisa kumvuta karibu Ukraine kama ambavyo Yeltsin aliweza lakini hana maarifa hayo. Anaishia kutungua ndege za Uholanzi zinazokatiza juu ya anga la Ukraine na kutengeneza uhasama na taifa la mbali kabisa kwa kutaka tu kumtawala jirani.

Hayati JPM ulale mahali pema peponi, umenikumbusha maana ya wale tausi. Kwa wakati ule sikuona ni ishara zipi zilizojificha katika kitendo kile, ila baada ya kutazama namna Russia wanavyoshindwa kulinda utawala wa mataifa ya jirani yake ndio naelewa ujumbe mpana wa zawadi ya tausi kwa majirani wetu wawili wa kaskazini.
Fikra zilizogandana kabisa hizi
 
Kwahiyo wewe nchi yako Ina strong intelligence Kuliko KGB !? [emoji16][emoji16][emoji16]
Aisee bongo shikamoo [emoji119][emoji119][emoji119]
Kuna mtu yupo kiteto lkn anaona putin yupo pale kwa bahati mbaya
 
Yeltsin? Rais mlevi? Ambaye analewa chakari na anatoroka kabisa mpaka Ikulu kwenda kupata mvinyo! Huyo, Gorbachev ni vituko tu. Na miaka hiyo Urusi ilikuwa ni dhaifu na ndiyo maana hizo ahadi zilivunjwa na NATO kwa muda huo. Na hao wanawekwa kwenye makundi mawili, either ni traitor or stupid.

Unamjua Sergei Lavrov? Kwa sasa ndiye anafahamika kama mwanadiplomasia kamili duniani.
Yeltsin alikuwa mlevi lakini alikuwa mjanja kuwa na wanadiplomasia wazuri wenye kujua kukaa chini na kujenga hoja.
 
Back
Top Bottom