Ananiingiza hasara duka langu!!, anatia huruma usoni, sina ujasiri wa kumfukuza, nipeni mbinu kumfukuza!!!

Ananiingiza hasara duka langu!!, anatia huruma usoni, sina ujasiri wa kumfukuza, nipeni mbinu kumfukuza!!!

sky soldier

JF-Expert Member
Joined
Mar 30, 2020
Posts
5,407
Reaction score
19,264
Asikwambie mtu nlikuwa nadhani kufukuza mtu kazi kitu simpo, nshawahi kushuhudia jamaa yangu aliifata bodaboda yake stendi akamnyanganya funguo kijana anaeiendesha mbele ya umati mkubwa nidhani rahisi, Pia nliwahi kushuhudia mjomba wangu alimfukuza kijana aliekuwa akimsaidia kuuza duka, alimfukuwa wazi wazi bila kujali kijana ataenda wapi, nikadhani rahisi.

Nikiri tu maishani sijawahi kumfukuza mtu kwasababu hii ndio biasharara yangu mpya nliyofungua baada ya kushawishika niwe na vimiradi ukiachana na kazi yangu katika shirika la serikalini,

Nimefungua kamradi ka oili za magari zile oili za sevisi na vifaa muhimu vya sevisi n.k

Kila wiki ni lazima nihesabu mzigo na kulinganisha na idadi ya mizigo iliyouzwa na hapo najua idadi inayotakiwa iwepo dukani.

Sasa wiki 3 zilizopita nlikuta utofauti wa mizigo ambayo ilikuwa haipatikani stoo ya kiasi cha elf 58 nikakaa na huyu muuzaji nikamwelewesha kwamba aandike kila kitu anachouza na akiona hela ya mauzo imezidi basi ni kwamba alisahau kuandika asifikiri ni muujiza akaenda kuipigia bata

wiki iliyopita nikaona material price variance (utofauti wa mizigo kwa gharama) ikiwa ni laki na 70, kwa kweli nlichukia sana na kwa vile mshahara wake ni laki 2 nikakata laki 1 nae asikie maumivu hio 70 nikampa onyo akirudia nakata yote.

Leo sasa nmehesabu mzigo nakuta variance imefika tena laki na 20

Nilipatwa na hasira nikawa naongea sauti ya juu kidogo bila kujijua dada akaanza kutoa machozi, nlipanga kumfukuza ila sikudhani itakuwa rahisi kiasi hiki.

Naombeni uzoefu wakuu, nlitaka nisingizie biashara ni yamjomba ili nimkodishe aje kumfukuza ila yup mbali sana
 
Nadhani angekuwa wa kiume ungeweza kumfukuza mkuu. Vile umesema ni dada endelea kumvumilia tu.

Kwani tatizo nini mkuu na una kazi nyingine nzuri serekalini kwenye shirika bwana
 
Mi msichana nliemuweka dukani alifika hatua akawa anafungua duka muda anaotaka yeye.... nikamuonya mara 1, akajirekebisha km siku 2/3 akaanza tena.... nikamuonya mara ya 2... akajirekebisha km siku 2/3 akaanza tena... alijiamini akijua mimi nina kazi yng na duka liko wilaya nyingine huko.... sintajua....

Nilichukua likizo ya dharura ya wk 1 afu nikadamka dukani, nikafungua duka saa 12.45 Asub... saa 4 nikampigia kujua kama ameshafungua duka... akanambia ndio anafungua.... saa 5 anafika... kanikuta niko busy na wateja.... alichoka! Nikamlipa chake.... tukaagana!
 
Kuna watu utawaonea huruma lakini huku wanakucheka. Huyo labda hujui mahesabu na hivyo anasababisa shot bila kujua, ama anafanya kwa makusudi chunguza ujue sio kila mwanadada anayeonekana smart anajua kuhesabu chunguza, mpe mtihani wa namba fulani utajua. Lakini kwa ujumla tafuta mwingine.
 
Angalia pia Kama hapigwi chuma ulete...kua nae dukani siku tatu tu..nawew ufungue na kufunga hesabu..ukikuta zimepungua Tena ujue Kuna mtu mnamlipa mshahara kichuma ulete...ukiona hela haipungui ujue anapiga yeye
 
mkuu kabda hujamfukuza,chukua ruhusa kazini hata ya wiki then kaa nae dukani siku zote mkiweka record sawa ya kila mauzo mnayofanya....then ukiona na wewe hesabu hazipo vzr kuna loss utulie kwa makini kuna kitu cha kurekebisha hapo dukani...ukiona hesabu zipo vzr mwachie tena week moja kama mambo ni yaleyale fukuza
 
Asikwambie mtu nlikuwa nadhani kufukuza mtu kazi kitu simpo, nshawahi kushuhudia jamaa yangu aliifata bodaboda yake stendi akamnyanganya funguo kijana anaeiendesha mbele ya umati mkubwa nidhani rahisi, Pia nliwahi kushuhudia mjomba wangu alimfukuza kijana aliekuwa akimsaidia kuuza duka, alimfukuwa wazi wazi bila kujali kijana ataenda wapi, nikadhani rahisi.

Nikiri tu maishani sijawahi kumfukuza mtu kwasababu hii ndio biasharara yangu mpya nliyofungua baada ya kushawishika niwe na vimiradi ukiachana na kazi yangu katika shirika la serikalini,

Nimefungua kamradi ka oili za magari zile oili za sevisi na vifaa muhimu vya sevisi n.k

Kila wiki ni lazima nihesabu mzigo na kulinganisha na idadi ya mizigo iliyouzwa na hapo najua idadi inayotakiwa iwepo dukani.

Sasa wiki 3 zilizopita nlikuta utofauti wa mizigo ambayo ilikuwa haipatikani stoo ya kiasi cha elf 58 nikakaa na huyu muuzaji nikamwelewesha kwamba aandike kila kitu anachouza na akiona hela ya mauzo imezidi basi ni kwamba alisahau kuandika asifikiri ni muujiza akaenda kuipigia bata

wiki iliyopita nikaona material price variance (utofauti wa mizigo kwa gharama) ikiwa ni laki na 70, kwa kweli nlichukia sana na kwa vile mshahara wake ni laki 2 nikakata laki 1 nae asikie maumivu hio 70 nikampa onyo akirudia nakata yote.

Leo sasa nmehesabu mzigo nakuta variance imefika tena laki na 20

Nilipatwa na hasira nikawa naongea sauti ya juu kidogo bila kujijua dada akaanza kutoa machozi, nlipanga kumfukuza ila sikudhani itakuwa rahisi kiasi hiki.

Naombeni uzoefu wakuu, nlitaka nisingizie biashara ni yamjomba ili nimkodishe aje kumfukuza ila yup mbali sana
Huyo mfanyakazi ni demu wako itakuwa

Mtu anakutia hasara unauwezo wa kumtoa unacheka nae. Utavuna mabua mpuuzi wewe cheka na nyani
 
m=Mkuu kabda hujamfukuza,chukua ruhusa kazini hata ya wiki then kaa nae dukani siku zote mkiweka record sawa ya kila mauzo mnayofanya....then ukiona na wewe hesabu hazipo vzr kuna loss utulie kwa makini kuna kitu cha kurekebisha hapo dukani...ukiona hesabu zipo vzr mwachie tena week moja kama mambo ni yaleyale fukuza
 
Back
Top Bottom