Anaomba nimsaidie pesa, sitampa maana kipindi cha mahusiano yetu hakuwahi kunipa penzi

Ila huyo nae, inamana hana ndugu wa karibu zaidi, majirani, workmates au wafanyabiashara wenzie wa karibu mpaka aende kwa ex?? Its possibly baada ya kila mmoja kuwa kivyake mlikuwa na mawasiliano ya karibu sana,,, inashangaza sana.
 
msaidie
 
Mwambie amwambie mumewe tafadhali [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Ukija na jibu la kumsaidia utakuwa utopolo tu, mwambia kwa sasa umekosa ila mwahidi akimaliza msiba utamsaidia kumuinua na kumsahaulisha machungu, na baby baby za kumjulia hali ziwe za kutosha kipindi hiki, muunge vifurushi vya dk,sms na data, halafu kuwa nae makini aliefiwa hawezi kuwa bize na data, fuatilia uwepo wake msibani ukiona yuko bize na data ujue hudadeee
 
mkuu ntamtumia tu hakuna namna, ili serikali ikate Kodi ya uzalendo 😎

Mkuu kuna wakati kuwa mjanja ndio huwa ujinga wenyewe - alisikika muuza korosho akisema kwa sauti

Tunaomba mrejesho umeshatuma au tuendelee kukushauri?
 
Hapana, nna hasira nae hajui tu, ni vile tu kipindi kile hela ilikuwa yakuchezea, nami umri ulikuwa wa ujana ujana, nilikuwa sijali kitu,
Ulikuwa Una mpa hela nyingi Sanaa ?
 
Kafiwa!

Tena na mama yake......!!!!

Kiubinadamu kama unayo mpe tu....


Ingekuwa anaombabya saluni au mtaji au upuuzi mwingkne sawa.


Sio kila uombwapo msaada unakimbilia kukataa kwa kuwa hakukupa kifanyio!!!!!!!!

Dunia duara ndugu!!!
 
Na ww ulikuwa boya kweli unawezaje kumlipia mtu kodi ya nyumba ukafika mbali na mwanae umlipie ada bila makubaliano yeyote?![emoji848][emoji848],hivi ni rahisi hivyo ukiambiwa tuu kitu unatimiza
 
Ujana maji ya moto mazee ujanani kuna niliimlia pesa zake na aliniamini kupita maelezo alinipenda mnooo ila ndoivo nikaolewa na mwingine kabisaaa,, ila nimemuangusha namrefundi pesa zake make aliniamini mno mnoo
Dah Smart911 wa watu nae aliliwa sana aisee
 
Wengi husema uongo kuwa wamefiwa au kuuguliwa ili waaibie hela wanaume!

Buyer beware!

Wajinga ndio waliwao!
 
Hivi mwanamke unamwombaje hela mume wa mtu?

Ndio kusema unajilengesha na kumtega akutake au ?

Halafu Mleta mada kama umeoa mkeo akiona unaombwa hela ujue hatakuelewa atajua ni hawara yako tu.
 
Acha roho za kimaskini aiaseeee elfu 80 kitu gani?
 
Ungemjibu palepale kuwa huna fedha sio kumdanganya
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…