Anapopita Magufuli hamlali njaa

Si wewe uliyesema ya kwamba wakenya ndio wengi wanomfuatilia magufuli na diamond hko youtube...

Hv una akili timamu kwel
Tatizo hamna uwezo wa kutazama video, mnaogopa "bundle" litakata, umasikini wenu msijaribu kutuambukiza, ninyi ni watu masikini sana, hata kuangalia Youtube ni shida.
 
Ni ushamba tu unamsumbua Jiwe.
 
Ndio kawaida ya madikteta. Dikteta wetu Moi aligawa bunda za hela kila sehemu alipoenda na tulipogutuka miaka 24 ilikuwa imepita na uchumi ulikuwa umeporomoka. Kwasababu ya hii noti hapa.
Hii noti ya 500 ambayo ilipewa jina la utani 'Jirongo' kwa heshima ya mwenyekiti wa vijana wa KANU, YK '92, ilichapishwa kwa wingi na Moi hadi thamani ya KES ikashuka. Cyrus Jirongo na viongozi wengine wa umoja wa vijana wa KANU walichukua noti hizi moja kwa moja kutoka benki kuu na magunia kwenye boot za gari zao. Tena usiku wa manane kama movie vile. Mungu ni mkubwa kwasababu mwishowe ulofa ulituisha sisi wakenya na tukamchinja jogoo. Majirani mnalo aisee, kama hamtajifunza kutoka kwa wenzenu. Endeleeni tu kukata viuno na kuimba nyimbo za kusifia na kukuza miungu watu.
 
Moi ilkua ukimsifia tu unamwagiwa hela, kila kijiji akitua anamwaga hela..
Tulipogutuka miaka 24 imeenda hvo..
 
Usimfananishe Magufuli na upupu.
Maana Magu kuna mageuz meng kayafanya na yanaonekana.
 
"Give a man a fish, and you'll feed him for a day. Teach a man to fish, and you've fed him for a lifetime."
 
Usimfananishe Magufuli na upupu.
Maana Magu kuna mageuz meng kayafanya na yanaonekana.
Dikteta ni dikteta tu, hata Moi pia alitangulia kwa kufanya makubwa chini ya kauli yake ya Nyayo. Mashamba ya majani ya Nyayo Tea Zones, mradi wa usafiri wa Nyayo Bus, miradi ya kuzuia mmomonyoko wa udongo na kuboresha ukulima, hadi kukawa na maziwa ya Nyayo, bure kwa wanafunzi wote nchini n.k. n.k. Ila kupenda kusifiwa na kutopenda kabisa kukashifiwa na kutupilia mbali utawala wa sheria na katiba ndio ilikuwa swag yake. Kama tu huyu mwenzake.
 
Nyimbo enzi zile tuliimba "kwekwe shambani mwa nyayo na zilimwe"
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…