Anayejua Rais Magufuli anatupeleka wapi atuambie, naona kama tumepotea

Anayejua Rais Magufuli anatupeleka wapi atuambie, naona kama tumepotea

Status
Not open for further replies.
Nimelalamika kwa maneno ugumu wa maisha hadi nimeishiwa maneno,sasa natangaza kuunga mkono maandamano yoyoye Yale as long as theme itakuwa ugumu wa maisha,nimetengua kauri yangu ya zamani kuwa siwezi kushiriki maandamo,coz sioni mwisho ya kizisoma number,Mara ya mwisho n
Tulisoma number ngapi vile ( malizia basi
Hakuna siku maisha yamewahi kua rahisi toka dunia imeumbwa,ugumu wa maisha na kubanwa kwa wapiga dili ni viwili tofauti,hujuma ya wenye pesa juu kubana pesa mtaani eti kisa rais aonekane ameshindwa zitakwishilia mbali na tutasonga mbele,naiamini mamlaka kwa sababu kama MUNGU hakuikubali isingekuwepo,wale waliosema maneno mengi mazuri ni mapritenda ambao wangekuja kuimaliza inchi,mtetezi wa wanyonge ndo anazidi kusonga mbele,na wapiga dili wanalaumu kila uchao
 
tunaisoma sie wapiga dili maana maisha ya kiyumba unambiwa mpiga dili, kweli alieshiba hamkumbuki wa njaa
 
Binafsi aliyeipa ule wimbo kama yupo anafaa kusifiwa kwani alichoimba ndicho kinachojiri. Ubunifu wake umeakisi nchi hii kwa sasa
 
Tulipenda wenyewe.....ndi ndi!
Chaguo letu wenyewe...ndi! Ndi!
Wavimbe wapasuke...ndi! Ndi!
Wataisoma nambaaaaa....ccm mbele kwa mbeleeeee! Mmeipenda wenyeweeeeeeeeeee......chaguo lenu wenyeweeee,
Acha muisomeee nambaaaaaaa......... Ccm mbele kwa mbeleeeeeeeee WAPI HAMJAISOMA? INAKUJA SOON!
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
"On behalf of myself "
Mfalme amekaa kitini upepo unampiga toka bahari ya sham kwani ofisi yake ndipo ilipo ,anajiona fahari kila akitazama ukutani mwa jumba la ufalme anaona picha zake kubwa nakuandikwa mfalme wa Alexandria basi anajiona fahari nakujihisi Mungu mtu ,Mara ananyanyuka na kuita washauri wake we mshauri wa elimu Fanya hiki futa kile nawewe wa ardhi mfanyie hiki yule na wewe wa sheria umewafuta wangapi kazi ahahaha ongeza wengine.
Mara mshauri wa elimu kwakupenda sifa; mtukufu mfalme JoJo tufute wale
Mfalme;oooh sawa Fanya hivyo na ukipata idea zaidi kama hiyo SKU nyingine we lete tufukuze tuu.
Basi wanacheeeeka utadhani hawajui hali halisi juu ya vilio vya watu wao ...kwa mbali sauti inanambia hakuna mbabe duniani hata Gaddaf ali..... be good to the people
 
Kaka wacha watu wasome tarakimu toka Lumumba hadi Kisiwandui mpaka mikoani tutapata akili tu. Habari hii ya ukondoo lazima ifikie mahali iachwe
 
Sio kosa kwa rais kukiri makosa lakini ninavyomjua Rais wetu hawezi kutoka na kukiri hatharani kwamba alifanya,anafanya na ataendelea kufanya makosa ambayo yatakuwa yakiigarimu nchi moja kwa moja.

Rais alifanya wapi makosa?

Wote tunashuhudia kunachoendelea Marekani uchaguzi wao ulifanyika tarehe 8 mwazi huu lakini Trump ajaapishwa mpaka January 20.

Anachokifanya anatengeneza cabinet yake kwa utaratibu kabisa huku akijifunza mambo mbali mbali kwa kupata semina elekezi kwake yeye na watu anaowateua huku akionekana kuwa karibu zaidi na watu Wa saikolojia na watu wa usalama.

Kosa la kwanza alilolifanya Magufuli ni baada ya kuchaguliwa hapo hapo ,Kuapishwa hapo hapo,na kwenda Ikulu hapo hapo.

Kibaya zaidi alipoingia Ikulu na kuzuia semina elekezi kwa wasaidizi wake ilo ndio kosa kubwa alilolifanya.

Semina elekezi ni muhimu sana kwa Rais mwenyewe na wasaidizi wake hasa mawaziri,kukurupuka na maamuzi ya mwendokasi ni kwa sababu Rais na wasaidizi wake hawana semina elekezi mpaka sasa.

Kiufupi Rais Magufuli alitakiwa kuapishwa January 2016.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom