Anayejua Rais Magufuli anatupeleka wapi atuambie, naona kama tumepotea

Anayejua Rais Magufuli anatupeleka wapi atuambie, naona kama tumepotea

Status
Not open for further replies.
Waambie chadema mimi naongelea taifa sio chama hata ungekuwa ni vizuri unamuuliza mbowe hayo mambo Mimi nataka kujua kwanini alifuta semina elekezi wakati anajua hawezi endesha nchi?
Hahahahahaaaaaa! Kwani wewe hi ACT?
 
Mamvi alijiunga Chadema na saa hiyo hiyo akatangazwa mgombea urais. Hayo yalikuwa makosa makubwa kuliko.

Wapi uliwahi kuona huyu mleta mada akisifia uwepo wa EL hapo cdm? Jibu hoja kwani ni aibu kujitetea kwa kutaja udhaifu wa chama kingine kama ndio ubora wako.
 
Rais Alichaguliwa Oktoba 25 na akatangazwa Mshindi Oktoba 29 na kaapishwa Novemba 5. Nini matumizi ya Hapo Hapo? By the way si kila kinachofanywa na Marekani tukiige. Mambo mengine yanakuwa hasara kwa taifa
Hakuna hasara kubwa duniani kama kupoteza muda.
Fikiria mara mbili
 
ukiona mtu anaiga maisha ya mtu ujue hana maisha yake halisi ishi kwa mfumo wako wewe mkuu ucpende kuiga iga utakua mtumwa
 
Kaka, kwani CHADEMA si chama cha siasa? Kwa nini wasirekebishe kwanza mambo ndani ya chama chao ndipo wawe na mamlaka ya kuhoji masuala ya kitaifa?
Kwani anaongelewa mwenyekiti wa chama?
 
Sio kosa kwa rais kukiri makosa lakini ninavyomjua Rais wetu hawezi kutoka na kukiri hatharani kwamba alifanya,anafanya na ataendelea kufanya makosa ambayo yatakuwa yakiigarimu nchi moja kwa moja.

Rais alifanya wapi makosa?

Wote tunashuhudia kunachoendelea Marekani uchaguzi wao ulifanyika tarehe 8 mwazi huu lakini Trump ajaapishwa mpaka January 20.

Anachokifanya anatengeneza cabinet yake kwa utaratibu kabisa huku akijifunza mambo mbali mbali kwa kupata semina elekezi kwake yeye na watu anaowateua huku akionekana kuwa karibu zaidi na watu Wa saikolojia na watu wa usalama.

Kosa la kwanza alilolifanya Magufuli ni baada ya kuchaguliwa hapo hapo ,Kuapishwa hapo hapo,na kwenda Ikulu hapo hapo.

Kibaya zaidi alipoingia Ikulu na kuzuia semina elekezi kwa wasaidizi wake ilo ndio kosa kubwa alilolifanya.

Semina elekezi ni muhimu sana kwa Rais mwenyewe na wasaidizi wake hasa mawaziri,kukurupuka na maamuzi ya mwendokasi ni kwa sababu Rais na wasaidizi wake hawana semina elekezi mpaka sasa.

Kiufupi Rais Magufuli alitakiwa kuapishwa January 2016.
La kuapishwa januari linahitaji mabadiliko ya katiba.

La semina elekezi si hata ofisini wanaweza kupewa na hata sasa linaweza fanyika.
 
Katiba inatoa muda maalumu wa kutangaza matokeo tangu siku upigaji kura ukafanyike na kama sikose inaeleza matokeo yatangazwe ndani ya siku 7 tangu tarehe ya kupiga kura na pia Katiba inatamka mshindi aapishwe ndani ya kipindi cha siku 7 tangu siku matokeo yatangazwe rasimi hivyo tatizo ni Katiba.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom