I am just thinking what if tatizo halipo kwenye gari, yani abilia tumeona namna matairi yanavyo badilishwa kila siku, mara cabreta, juzi tulimwaga oil, lakini wapi gari bado halisongi.
Kondakta na mpiga debe hawana tatizo kwakua wanafata maagizo ya dereva, tumesha badili kila kifaa tulichodhani kibovu kwenye gari lakini hatuoni mabadiliko wara hali ya gari kusonga mbele na safari.
Dereva huyu tumemuajiri mpya baada ya kudhani yule aliyepita hawezi kuliendesha gari letu, dereva wetu alikuja kwa mbwembwe sana kama kuvuta mafuta kwa kasi kama gari linataka kuondoka alipiga honi kwanguvu mpaka abiria wa mabasi mengine wakatamani kama wangejaliwa kumpata huyu dereva wetu mpya.
Lakini baada ya muda kupita tumekaa kwenye basi masaa kadhaa hatuoni dalili ya safari kuanza na wale wauza bidhaa kama pipi na maji abiria wameanza kushuka mmoja mmoja kutokana na tozo kubwa inayodaiwa na dereva huyu.
Abiria tumechoka na kuanza kukata tamaa kwa kua njaa imetawala na hatuna matumaini ya kufika tuendako leo wala kesho.
Kwa namna navyoona kuna swali nikajiuliza vipi kama tatizo sio gari letu hili, gari ni zima kabisa vip kama tatizo lipo kwa dereva.
Vipi kama dereva hana uzoefu wa kuendesha gari na hataki kusikia ushauri wa abiria?
Tatizo kama sio dereva nini chanzo cha gari kutosonga mbele?