Sio kosa kwa rais kukiri makosa lakini ninavyomjua Rais wetu hawezi kutoka na kukiri hatharani kwamba alifanya,anafanya na ataendelea kufanya makosa ambayo yatakuwa yakiigarimu nchi moja kwa moja.
Rais alifanya wapi makosa?
Wote tunashuhudia kunachoendelea Marekani uchaguzi wao ulifanyika tarehe 8 mwazi huu lakini Trump ajaapishwa mpaka January 20.
Anachokifanya anatengeneza cabinet yake kwa utaratibu kabisa huku akijifunza mambo mbali mbali kwa kupata semina elekezi kwake yeye na watu anaowateua huku akionekana kuwa karibu zaidi na watu Wa saikolojia na watu wa usalama.
Kosa la kwanza alilolifanya Magufuli ni baada ya kuchaguliwa hapo hapo ,Kuapishwa hapo hapo,na kwenda Ikulu hapo hapo.
Kibaya zaidi alipoingia Ikulu na kuzuia semina elekezi kwa wasaidizi wake ilo ndio kosa kubwa alilolifanya.
Semina elekezi ni muhimu sana kwa Rais mwenyewe na wasaidizi wake hasa mawaziri,kukurupuka na maamuzi ya mwendokasi ni kwa sababu Rais na wasaidizi wake hawana semina elekezi mpaka sasa.
Kiufupi Rais Magufuli alitakiwa kuapishwa January 2016.