Habar za asubuh wana jamvi, natumai wengi wetu tumeamka salama na kwa wale ambao siku ya leo hii hawako vizur kiafya bas naomba mwenyez mungu awafanyie wepes .
Wana jamvi, mimi ni miongon mwa wale waliokuwa wakifuatilia sana speech ya mkulu ivyo napenda tu kuwakumbushia speech yake moja ambayo kwa hakika iliweza kuwajenga watanzania wengi sana kiiman. nanukuu iyo speech yenyewe inasema " MSEMA KWELI NI MPENZI WA MUNGU" Maana halis ya speech hii ni kwamba, Mkulu ametuaminisha kwamba atakuwa mkwel siku zote na hata mung'unya maneno dhid ya tuhuma zozote zitakazo kuwa zinamkabili mtu yeyote bila kujal din, itikadi ya vyama, wadhifa wa mtu n.k. iyo ndio maana halis ya iyo SPEECH niliyonukuu apo juu.
Sasa cha kuskitisha watanzania hao hao tuliojengeka kiiman na MKULU leo hii tumekuwa na kilio kikubwa sana juu ya kinachosadikika kuwa kuna kiongozi mwenye nyadhifa kubwa ki mkoa kuwa anatumia vyeti feki na kilio iki MKULU anakisikia cha ajabu anaacha machoz ya wa tz yanaenda na maji wakati kuna watu wameshaacha kazi kwa tuhuma kama hz, na wengine wamepoteza maisha kwa sababu za tuhuma kama hz, kwa anayefaham vzr naomba anijulishe jaman, hv mkulu anafaida gan na kiongoz uyu? nimeandika uzi huu kwa uchungu sana kama mtanzania mwenye mapenzi na nchi yangu na ili tuijenge tanzania mpya , tunahitaji wasom, sasa kama tutaweka vilaza nina iman hii inchi haitasonga mbele, ninaposema vilaza nadhan mkulu ananielewe kwan ni neno ambalo hata yeye alishalitumia kwa wale wanafunzi 8000 wa mafunzo maalum aliowafukuza pale Dodoma!
Kimsingi ni haki yangu kukukumbusha mkulu maana hata mm pia nina amin kuwa msema kwel ni mpenzi wa mungu na ndio maana nimeamua kukukumbusha maana huenda ukawa umejisahau kutokana na kutingwa na majukum ya apa na pale, sasa mkulu ili kutujenga kiiman wananchi wako tuendelee kukuamin na kuunga mkono jitihada zako za kupambana na MIJIZI ya aina yote ikiwemo mijizi ya taaluma bas shughulikia mapema sana suala la DAUD, baada ya kusema ayo machache naomba kuwasilisha.