Anayejua Rais Magufuli anatupeleka wapi atuambie, naona kama tumepotea

Anayejua Rais Magufuli anatupeleka wapi atuambie, naona kama tumepotea

Status
Not open for further replies.
kuna uzi wa mange kimambi umefutwa shap nimebahatika kuusoma kwa mbali. huyu modereta mbona ivo?.umesahau motto wa hii forum? where people can talk openly imebadilishwa ulivyopelekwa kule polisi? hi haijakaa poa
 
Wabwia unga kazi mnayo....mlizoea vya kunyo ga[emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28]
Watu wengne mnaushabik wa kisenge kweli, hvi hata graduate waliokaa mtaani mwaka wa 2 bila ajira na bila matumain wanaposema imani yako ni wapiga dili au wauza unga? Yaan nyumbu kama nyny ndo mwafanya watanzania tuonekane akna Bashite wote!
 
Wabwia unga kazi mnayo....mlizoea vya kunyo ga[emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28]

Akiri yako ndogo sana Tunaokosoa serikali ndo tunaitwa wapiga diri sas hivi tunaitwa wabwia Unga Akiri za Wantazina walio wengi wapumbavu
 
Wanajukwaa.
Habari za usiku,naweka mezani juu ya hoja yangu,kua je rais wa nchi yetu huyu wa awamu ya 5 je ni rais wa wanaCCM pekee au ni rais wa WATANZANIA wote?


Huyu ni baba wa familia asiejua alifanyalo au nini tatzo,anzia matamshi yake hayasadifu kutamkwa na mkuu wa nchi,mbaguzi na pengne hajui alitendalo,binafsi sikutarajia rais huyu kua hivi,naichukia October 25 km taifa tumebebeshwa mzigo wa tope.
Kwani unakula matamko??

Shame on you mbeba ngada za mwenyekiti
 
salamu wanabodi!
ghafla nimejikuta sina furaha, sina amani na wala sifurahi tena kuitwa mtanzania.Mwanzoni alipo ingia madarakani nilimpenda sana Rais Magufuli kwakuwa mambo mengi aliyo yafanya yalikuwa yana rudisha Tanzania tuliyo itaka.Baada ya miezi michache akageuka kuwa mbinafsi, anaonesha chuki za wazi kwa watumishi wa umma, Hafuati misingi na kanuni za uendeshaji wa taasisi za serikali, hafuati matumizi sahihi ya fedha za umma, kimsingi amegeuza Nchi hii ni mali yake binafsi.

Kwanini ghafla simpendi? Fikiria Rais mwenyewe aliagiza uhakiki wa watumishi wa umma akisisitiza wasio na sifa waondolewe kwenye payroll.Zoezi lile liliwagharimu watumishi wa umma muda na fedha nyingi kufuatilia taarifa zao ili zihakikiwe.Jumla ya watu 1887 wamepoteza ajira baada ya kubainika taarifa zao za taaluma kuwa na kasoro ama mapungufu.lakini alisimamisha nyongeza za mishahara na kulipa mishahara ya madaraja mapya kwa kisingizio hiki.Leo Bashite kajulikana hana vyeti anapata kigugumizi kumtoa kwenye utumishi wa umma! kwanini? ni msukuma mwenzake!! ni mkabila.

Kwangu mimi kitendo cha Magufuli kuidhinisha ujenzi wa uwanja mkubwa wa ndege Chato ni matumizi mabaya ya fedha za umma.uwanja ule nani atatumia? Kama anawapenda watu wa Chato ni bora angewajengea chuo kikuu kwani hata mtu mojammoja angeweza kufaidika na uwepo wa chuo kikuu kuliko uwanja wa ndege.

Amevuruga taratibu serikalini.Magufuli kwa sababu za kibinafs kabisa ameajiri wakurugenzi na Ma DAS nje ya kanuni za utumishi wa umma.sasa hivi watumishi wa umma hawana ari ya kazi kabisa.

Matamko yake mengi yamenifanya nifikie uamuzi wa kuto kumsikiliza kabisa. Huwezi kuwaambia wabunge wa ccm walio panga kwenda kumjulia Lema gerezani ni usaliti wa chama. Najiuliza Lema aliwekwa ndani kwa maelekezo ya Chama? siamini. Hivi Magufuli hajui kuwa kuna wana ccm walio oa wanachadema? hivi hajui kuwa ndani ya familia moja unaweza kuona wanachama wa vyama vyote? huko ni kuwagawa watanzania.

Magufuli huwa anaomba tumuombee kwa Mungu, sawa, mbona yeye haoneshi kuwaombea watanzania wawe na amani upendo na kuvumiliana? CUF,Kwenye vikao halali wamemfukuza Lipumba, lakini fedha za ruzuku ameruhusu apewe mtu ambaye siyo mwanachama yaani Lipumba! Magufuli ni msimamizi namba moja wa fedha za umma, kwanini anaruhusu ujinga huu wa msajiri wa vyama? Aheshimu maamuzi halali ya vya vingine. kulazimisha Lipumba kuiongoza CUF iko siku itatuletea maafa makubwa sana.

Kuna manung'uniko kuwa wateule wake wengi wanatoka kanda pendwa.Jambo hili siyo la kulipuuza. teuzi lazima zifuate kanuni za kitaasisi.Lakini pia zizingatie gender balance, dini,na ziwe na mtawanyiko mzuri kikanda. watumishi wa umma wanao tumbuliwa sababu za kutumbuliwa kwao wengi ni nyepesi mno hivyo kuleta maneno kuwa ni kulipa visasi.

Siku hizi watu hawapendi kuangalia au kusikiliza taarifa ya habari ya saa mbili usiku. Ni kama wamechoka na mabadiliko yasiyo na maana.

Mapungufu ni mengi, ndio maana nasema binafsi namuombea atawale amalize muda wake hata kama ni miaka kumi,huenda Mungu anataka kutufundisha kitu, ila siku akimaliza nitafurahi sana ingawa nitakuwa na miaka 89.
 
Amekiri kuwa ni yeye ndiye alipiga marufuku Bunge live!
Lengo lilikuwa ni nini?Uwazi na Ukweli au upigaji dili wa kimya kimya?
 
ASANTE KWA KULITAMBUA HILO
KARIBU CHADEMA HUKU NDIKO KUNA MABADILIKO YA KWELI.
Huko kwingine ni kujilisha upepo tu. -Wamefuta ajira
-Wamewanyima watoto wengi mikopo
-No increment
-Hakuna kupandishwa madaraja
-Helsb 15%
~Wahalifu wa vyeti wanadunda tu mitaan
*kuzid kuichagua ccm ni kuifanya nchi ya Tanzania kurudi nyuma kimaendeleo*
 
  • Thanks
Reactions: PNC
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom