Anayejua Rais Magufuli anatupeleka wapi atuambie, naona kama tumepotea

Status
Not open for further replies.
naunga mkono hoja, ni kwel kabisa kwa sasa aman imetoweka kabisa, kinachoskitisha ni kwamba, sis watu wachin kabisa ambao hatuna sehemu ya kusemea ndio tunajaribu kupiga kelele tu mitandaon, wakati wapo watu ambao wana nafas kubwa ya kukemea huu upuuzi unaoendelea ndan ya nchi lakin wamekaa kimya! wapo viongoz waandamiz, wapo pia viongozi wa din, hao wote wana nafas lakin cha kushangaza wapo kimya tu! au na wao wanafurahishwa na aya mambo yanayoendelea ndan ya nchi hii?
 
halafu alivyo mnafiki anakwambia tudumishe amani wakati yeye ndiye wa kwanza kuvunja hiyo amani
 
Toka aingie JPM madarakani,
1. Wizi wa mabenki sijasikia,
2. Mauaji ya albino sijasikia,
3. Panya roads hawapo,
4. Etc
Amani ambayo inasemekana haipo ni propaganda za kwenye mitandao za wapinzani waliokosa hoja sasa hivi!
Panya roads hujawasikia?

Tuanzie hapa kwanza ,ww unaishi wapi?
 
Toka aingie JPM madarakani,
1. Wizi wa mabenki sijasikia,
2. Mauaji ya albino sijasikia,
3. Panya roads hawapo,
4. Etc
Amani ambayo inasemekana haipo ni propaganda za kwenye mitandao za wapinzani waliokosa hoja sasa hivi!
Ni kweli mengi mazuri amefanya ila arekebishe haya mabaya machache ili awe kiongozi bora
 
Panya roads hujawasikia?

Tuanzie hapa kwanza ,ww unaishi wapi?
Naishi Dar tena mahali ambapo zilipokuwaga moja ya kambi zao!
Huwezi linganisha na mida fulani, labda huko kwenu wapo wa kuvizia!
 
Ni kweli mengi mazuri amefanya ila arekebishe haya mabaya machache ili awe kiongozi bora
Mengi yapi hayo?

Tangu aingie madarakani ajira hamna,mishahara inakatwa kila kukicha ,vyuoni wanafunzi hawapewi mikopo

Na vipi kuhusu Tanzania ya viwanda na milion 50 kila kijiji hatujasahau bado.
 
Naishi Dar tena mahali ambapo zilipokuwaga moja ya kambi zao!
Huwezi linganisha na mida fulani, labda huko kwenu wapo wa kuvizia!
Panya road wamejaa kila kona na mbaya zaidi siku hizi wanaua kabisa hawaishii kukuibia tu

Sehemu kama ukonga moshi bar haipiti mwezi bila kusikia tukio la mauaji.
 
Inatakiwa Ifike Mahali Watanzania kuangalia zaidi ni jinsi gani anaweza kuwa part ya solutions zitokanazo na Matatizo yaleteyo na Viongozi, Otherwise tutakuwa tunalalamika kila awamu ikiwa Madarakani
 
Panya road ni makonda ujaona clouds
Anajifanya hajuwi matukio yanayotokea wakati hata tukio la kutekwa kwa roma bado bichi kabisa

Na utawala huu wa kidhalimu ambao hata mawaziri wanatishiwa maisha sembuse raia?

Huyo bashe mwenyewe amekiri anatishiwa maisha,zito kabwe na baadhi ya mawaziri kila kukicha wanalalamika wanatishiwa maisha halafu huyo jamaa anakuja kutetea bila hata aibu .
 
Acha upumbavu wewe amani imetoweka kuna vita ukilinganisha utawala uliopita ambapo mauaji ya watu yalitawala kwa magufuli nani kauawa?? Na wafuatao wameuawa na kutekwa kipindi cha utawala uliopita waliokufa kwa uchache tu ni:-
1. Marehemu Dk Mvungi (Mwenyezi Mungu amlaze mahali pema peponi)
2. Alphonce Mawazo mwenyekiti CHADEMA MKOA -GEITA
3. Mchungaji aliyechinjwa Katoro
WALIOTEKWA BILA KUUAWA
1. Dr. Ulimboka
2. Absalom Kibanda
3. Mwandishi habari wa BBC toka Zanzibar
Je, wakati haya yote yanafanyika Magufuli alikuwa Rais Acheni unafiki wenu semeni ukweli hamuwezi kufa
 
Tanzania siku zote hakuna amani bali muna uvumilivu tu
Mkuu Tanzania ya awamu hii amani imetoweka kwa kiasi kikubwa

Zamani ilikuwa raia ndio wanatishiwa maisha ila kwa sasa kuanzia waandishi wa habari,mawaziri ,wabunge nk wote wanatishiwa maisha
 
We Kaa na uendelee kupiga Kampeni humu kwenye mtandao ukidhani mtashinda urais 2020.Kuna Watu hawajui Hata mtandao ni nini.
 
Tangu Magufuli aingie madarakani..amani mtaani imeongezeka mara dufu..zilizobaki ni kelele mitandaoni tu..na njama ili kufifisha malengo yake ya kutuletea maendeleo. Wale wachache weningine wanapokosea wakikamatwa na vyombo vya dola wanapiga kelelele wametekwa..mfano Bashe..Roma tunasubiri upelelezi.
Tukio gani jingine linalotishia amani?

Maana propagada zinatia kinyaa..uzuri tushawashitukia..
 
Tukio la waziri kuoneshewa bastola mbele ya umati wa watu nalo unaliona ni la kawaida?

Na mbaya zaidi hakuna onyo lolote lililotolewa juu ya yule mhusika wa tukio lile.


Na vipi kuhusu matukio ya kupotea kwa watu kama vile ben saa nane nalo ni jambo la kawaida?

Vipi kuhusu mauaji ya wanavyuo kila kukicha nalo ni la kawaida?
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…