- Umefanya maisha yamekuwa magumu kupindukia
- Watanzania wameamua tu kukaa kimya na kupambana tu na maisha yao
- Umewakaba kila kona hawapumui bado huridhiki, ukiongea tu inabidi mtu atafute panadol ameze
- Tushakubali kwamba tumepoteza, tunavumilia tunajua yatapita lakini bado huridhiki unawarushia vijembe kwanini lakini ?
............
........
- Wamewekewa mchakato mzito na wa gharama kubwa kupata mikopo ya elimu ya juu. Wametulia
- Waliohitimu vyuo umezuia wasipate kazi, Wametulia
- Wakulima wa mbaazi wanatafuta mnunuzi hata wa kg 1 kwa Tsh 200 hawapati, wametulia
- Wafanyabiashara wanapelekewa mikodi ya ajabu, wengine wanafungwa. Wametulia
- Machinga wanapigwa na polisi. Wametulia
- Watumishi wanajuta na kuminywa haki zao. Wanasoma tu magazetini kuna watu WANALIPANA POSHO LAKI 4 PER DAY. Wametulia
- Watu wamezuiwa kusafiri kwa amri yako. Hela zote za MAKUSANYO, WATUMISHI HEWA, Unagawa kama njugu kwa uwatako. Tumetulia
- Unapiga wapinzani. Tumetulia
- TUNAHANGAIKA. Tafadhali heshimu hisia zao,
Watu wamevunjiwa nyumba kwa "amri kutoka juu" licha ya kuwa na amri za mahakama kuzuia uvunjaji huu!
Nyerere alisema kwamba, mkiruhusu kuongozwa na dikteta, mtaumia. Na yeye hata hatawahurumia, kwa sababu mtakuwa mmejitakia hilo.
Alisema ukigusa moto,utaungua, hii ni kanuni ya asili, si kanuni ya Nyerere.
Alisemahivyo, video zipo Youtube. Search "Nyerere katiba1" "Nyerere katiba2" na "Nyerere katiba3".
Alikuwa anaongelea viongozi wa nchi kuongoza kwa kuvunja katiba, alilaani sana hili Salmin Amour alipoiingiza Zanzibar OIC.
Yale maneno yake yana umuhimu sana kwa kipindi hiki cha Magufuli. Kwa sababu tunaona ujinga ule ule wa nchi kuendeshwa kwa kauli za mtu badala ya sheria na katiba.
Kwa hiyo na mimi narudia mule mule.
Shurutisheni viongozi waongoze kwa sheria na katiba, si kwa ubabe wao binafsi.
Mkishindwa hili, mkishangilia viongozi wanaovunja katiba, mkiishi kama mashetani ni stahili yenu.
Kwa sababu mmeshindwa kusimamia haki zenu za msingi za kikatiba.
Mmeamua kugusa moto, mkiungua msilalamike.