Anayejua Rais Magufuli anatupeleka wapi atuambie, naona kama tumepotea

Status
Not open for further replies.
Mi jamaa mwanzoni nilimkubali sana! Alilokosea kubwa ni kutowapa Uhuru wapinzani waikosoe serikali yake! Ukikosolewa ndo utajua wapi unakosea! Mwanadamu lazima awe na kasoro, hawezi akawa perfect! Amekuwa mungu?
Hata mimi mkuu hapo tu ndo penye shida, lasivyo angekuwa rais Bomba sana.
 
Naona kila kona,kila mitandao wananchi wamechukia na wana hasira sana kiasi ambacho hakijawahi kuonekana tangu Uhuru

Je kiakili wananchi wameasi utawala wao?
Sio wananchi tu.
Mpaka wanajeshi.

Wanajeshi ndio wananchi wenye uzalendo pengine wa hali ya juu kuliko wote. Wamekubali kuilinda nchi yao ikibidi kujitolea maisha yao vitani. Wamefundishwa utii ule wa "kamanda akisema ruka, unaruka, hamna maswali".

Lakini awamu hii tumeona mpaka waraka wa jeshi ukisambaa, wanajeshi wanailalamikia serikali, wanamlalamikia rais.

Hili ni jambo la hatari sana. Hawa watu wakiamua wanachukua nchi.

Kwa hiyo ukisema wananchi tu wanalalamika, mimi nawekea msitari zaidi, mpaka wanajeshi wanalalamika.
 
Naona kila kona,kila mitandao wananchi wamechukia na wana hasira sana kiasi ambacho hakijawahi kuonekana tangu Uhuru

Je kiakili wananchi wameasi utawala wao?
Hawa makuadi wa mafisadi na mabepari ndio wanaokufanya useme wananchi wameiasi serikali yao?Inaelekea na wewe ni kuadi wa mapepari,pole.Wananchi hatujaiasi serikali yetu,tuko pamoja na Rais wetu.
 
kila kona zipi ndugu, hii nchi ni kubwa sana. hivi vikelele vya Jf vya watanzania wasiofika hata asilimia moja ya watanzania ndo kelele za kila kona, Humu wapo wengi walizoea kuishi kwa semiba, posho na kupata tenda zisizo na kichwa wala mguu ndio wapiga kelele. Huku mtwara kwa walima korosho huwaambi kitu kuhusu awamu hii
 
Ukiwa mtandaoni ni tofauti kabisa na huku uraiani maisha yanasonga tu kama kawaida
 
Watz tu wanafiki sana unakuta watu wanaongea mbovu mbovu ila ghafla wakisikia Msafara unapita wanamwagika kama nyuki barabarani huku wakiimba nyimbo za kusifu na kushangilia ila baada ya hapo ghafla wanaanza tena kuponda....
 
Hata mimi mkuu hapo tu ndo penye shida, lasivyo angekuwa rais Bomba sana.

Siyo hilo tu bali na kwenye uchumi. Kwa kuwa watu wengi hawana uelewa na uchumi wa madini, amepata nafasi ya kuwadanganya katika mengi, nao wakaamini. Lakini ukweli ni kuwa amevuruga uchumi badala ya kuuboresha.
 
Habari huenea kwa kasi sana mkuu,Mimi hii sijawahi kuona tangu nizaliwe,hakika kabisa
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…