Anayejua Rais Magufuli anatupeleka wapi atuambie, naona kama tumepotea

Status
Not open for further replies.
Imefikia mpaka kuua watu kisa wamemkosoa asiyekosolewa! Nchi imefika mahali pabaya sana kwa sababu ya mtu mmoja tu! Anayeterrorize nchi nzima!

 
hii no shida kubwa sana anataka kutufikisha Rwanda ilipo kwa sasa no nchi tulivu yenye uchumi unaokua kwa kasi na isiyo na upinzani
 
Udikteta ukabila udini chuki ndio zake hiyo jamaa lakini tusimpe nafasi.


Swissme
 
Hakuna tena Uhuru wa kujumuika
Hakuna tena Uhuru wa TV au radio yako uliyoinunua kwa pesa zako mwenyewe wala kingamuzi unschukilipia kila mwezi upate habari za kweli na hakika.
Hakuna tena kuusema ukweli hata uliowazi sana sana utatishiwa maisha au kupigwa risasi...
Yuko wapi Tundu Lissu,Yuko wapi Ben Saanane? Yuko wapi Aliphonce mawazo na vipi kuhusu usalama wa sisi wengine ?

Muda wa kulalamika uwe mwisho na mwisho ni sasa watu tumepaliwa vya kutosha sasa ni muda we kuingia barabarani kudai haki kwa uwazi bila unafiki

nakusudia kuanzisha vuguvugu la kudai katiba mpya mpya kuanzia muda wowote sasa katiba ndio nimeona ndio nguzo pekee ya kututa hapa tulipo na kwenda mbele .

Kwanza na declare interest kuwa Mimi sio mwanachama we chama chochote Bali uwa naguswa na natamani sana siku moja nchi yetu iwe na mabadiliko ya kweli..

Kila kitu kina mwisho huu uwe ni mwisho wa ukandamizaji juu ya kizazi chetu kama ikishindikana tumekufa kwa sababu ya kudai haki basi watoto wetu waje wakute tayari tumeshawapatia katiba mpya yenye mawazo ya watanzania na so mawazo ya wezi wakubwa wa nchi hii na wauaji .

lazima ipatikane kabla ya 2020 hata kama ni kwa kujitoa sadaka kwa baadhi yetu twende barabarani.

R.I.P Alphonse Mawazo bado tunakukumbuka.
 
Anapaswa kupigwa stop sasa vijana hatupaswi kuwa legelege huyu ameanzisha genge la wahuni wauaji wapora mali za nchi wanaojilimbikizia mali wanaotaka kakikundi ndio iwe nchi hajapata kutokea raisi wa hovyo kama tuliyenaye
 
Ilimchukua kitambo kidogo kutangaza baraza lake la mawaziri, wakati akisherehesha hafla ya kulitambulisha baraza rasmi kwa wananchi akasema amachagua kwa umakini mkubwa, pia amepunguza ukubwa wa baraza la mawaziri ili kupunguza mzigo wa uendeshaji wa serikali yake.
Kupunguza ukubwa wa serikali kwa kweli ilikuwa na mantiki, wananchi wengi waliufurahia mtizamo huu.
Tuliamini anachokifanya anakijua kindakindaki.
Kwa mshangao wa wengi kile alichotuaminisha kuwa ni matope leo anatuambia kuwa eti ni dhahadu hii.
Mtu huyu huyu mwenye uzoefu wa ujumbe wa baraza la mawaziri.
Ndani ya miaka miwili tumeshuhudia panga pangua ya mawaziri zaidi ya mara mbili inatia shaka leseni ya dereva wa lorry.

Ikiwa ameshindwa kusimamia anachokiamini kuwa ni sahihi kabisa (kuunganisha baadhi ya wizara) ni nani anaweza kuweka dau kwake kuwa huyu dereva anaposema anapigana vita vya uchumi anajua anasema nini?
Ni nani anaweza kumuamini anapoutangazia umma kuwa anatupeleka kwenye uchumi wa viwanda?

Mtu hutu huyu anayepambana dhidi ya matajiri? Anatamani watu waishi kama mashetani.

Je hatuelekezwi shimoni tutumbukizwe wote kwa mpigo?
 
Aondoke ikulu basi kazi imemshinda...kama baba wa familia anashindwa kumpa dira ya maisha mwanae aanzie wapi anakoelekea ili safari yake isiwe na rabsha zitakazomkwamisha utegemee nn[emoji2] [emoji2]
 
Ukitaka kujua kuwa serikali imefilisika nenda halmashauri yoyote utajua kuwa tunaelekea kwenye kaburi, ofisi zimeishiwa pini, karatasi, Stepla, hakuna mafuta, magari yamekufa, miradi hakuna, pia wafanyabiashara wanalia bidhaa hazitembei purchasing power imepungua, ajira hakuna, serikali imepunguza wafanyakazi, makampuni nayo yameprun, zaman serikali ilikuwa inaajiri watu wengi sana na sekta muhimu kama udaktar lazima waajiriwe siku hizi MDs wapo home, serikali inatoa ajira ya watu 50 matangazo meeeengi utafikir imeajiri graduates wote, watumishi wanalia hakuna nyongeza wala marupurupu, mkuu anawivu kwa watu waliifanikiwa Mara bomoabomoa isiyo na kichwa wala miguu, fikiria hela ilivyo ngumu afu Nyumba yenu tegemewa inabomolewa, nimalize kwa kusema Benito Mussolini pia alisifiwa saana baadae waliokuwa wanamsifu ndio walimtwanga risasi ili apishe njia hata hapa tz wapo wanaomsifu jamaa lakini naamini wao ndiyo watakao kuwa na hasira kuliko hata wale tunaoona mwelekeo si mwema
 
Iwapo unasimamia ukweli daima utasimama peke yako (Lucky Dube if you stand for the truth you will always stand alone).

Katika jamii ambayo ukisimamia ukweli unahatarisha maisha yako na pengine kuyapoteza basi tusiendelee kuwa waoga tuseme ukweli lakini tukiweka ukweli huo Katika kumbukumbuku za maandishi, sauti, video nk ili kesho ukipotezwa vizazi vijavyo vikuone katika maandiko yako yaliyojaa ukweli tena ukweli wa ukombozi wa kifikra

Tutaogopa nini tena kama shule hazijengwi wala hospitali vinavyojengwa ni magereza ya kuweka wasemaji wa ukweli.

Tuogope nini tena Kama walimu na madaktari hawaajiriwi tena wanaoajiriwa ni washika bunduki.

Tutaogopa nini zaidi kama dawa hazinunuliwi kwenye hospitali zetu kinachonunuliwa ni risasi na bunduki.

Tuogope nini zaidi ya mateso tuliyonayo ya watu kufukuzwa kazi bila utaratibu, watu kutekwa, watu kupigwa risasi hadharani. Tuogope nini zaidi

Tuogope nini zaidi katika mazingira ambayo sheria na katiba haziheshimiwi anaye heshimiwa ni mtu mtu mmoja.

SIMAMIA UKWELI SIMAMA PEKE YAKO USHINDI WETU UPO KARIBU

Mwanahabari Huru

Swali la Kizushi: " WATU WASIOJULIKANA NI WATU KUTOKEA NCHI JIRANI?"
 
kuisoma namba ni pale milioni 50 kila kijiji kuota mbawa.
Kuisoma namba ni pale hakuna nyongeza ya mshahara.
Kuisoma namba ni pale hakuna ajira.
Kuisoma namba ni pale Tanzania ya viwanda inapoyeyuka.
Kuisoma namba ni thamani ya pesa inaposhuka.
Kuisoma namba ni pale hela za rambirambi na maafa zinapoishia kusikojulikana.
Kuisoma namba ni pale una njaa halaf chakula cha msaada hakuna kutoa.

Namba inaendelea kusomeka.

Mwanahabari Huru
 
.........na mbele kwa mbele ni pale waandishi wa habari wanapoambiwa wana uhuru wa kuandika habari ila not to that extent.
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…