Katika nchi hii bado kero na changamoto muhimu zenye impact kubwa katika uchumi hazijafanyiwa kazi kwa kiwango chenye kutafsiri objective kuu ya serikali hii ya awamu ya tano. Sisemi kwamba serikali hii haijafanya mambo ya maana la hasha bali inasikitisha kuona kwamba serikali imeshindwa kuwa makini katika utekelezaji wa mikakati yake ya kuelekea Tanzania ya viwanda.
Naomba Leo hii niseme ukweli, niseme ukweli usio na chembe ya woga juu ya mtu yeyote bali ukweli ulio na lengo la kuniweka huru. " The truth will set me free "
UMEME WA UHAKIKA. Ninapoandika haya Mimi nipo gizani, si kwamba naishi nyumba isiyo na umeme hapana, nyumba ina umeme , unit za luku zimejaa but unfortunately nipo gizani ,, UMEME hamna! kwa nchi ambayo inaenda kujenga uchumi wa viwanda haya hayapaswi kutamalaki, inasikitisha kuona kwamba juhudi za kujenga nchi ya viwanda hazijaanza na uwepo wa umeme wa uhakika, viwanda gani bila umeme wa uhakika? uchumi gani wa kati pasipo umeme wa uhakika? . Serikali ya awamu ya tano imechukua hatua gani za kusisimua katika kutatua kero hii ya umeme ambayo bila kimung'unya maneno ndio kero iliyopaswa kuwa kipaumbele?
Nasema hivi kwa sababu ukiweka kwenye mizania utaona kwamba uwepo wa umeme wa uhakika ni faida kubwa sana kwa nchi kuliko kuwepo kwa treni za umeme, fly overs na Uwanja wa ndege wa Chato lakini je serikali hii imewekeza nguvu zaidi katika umeme? jibu ni hapana na linakuja swali jingine tatizo hasa si lipo wazi? kwamba Rais amekuwa akifanya maamuzi katika karibia kila matumizi ya pesa za umma, kwamba hii hela ifanye hiki na ile ifanyi kile jambo lililopelekea serikali yake kutoonesha dhamira ya dhati kufikia kile inachokihubiri (Tanzania ya Viwanda)
Lakini pia kuna suala la "MFUMO WA ELIMU" Miaka nenda miaka rudi nchi yetu imekuwa ikikabiliwa na changamoto katika kuzalisha wasomi wenye fikra na uwezo wa kujiajiri. Ipo wazi duniani kote kwamba tatizo la ukosefu wa ajira limekuwa kubwa kadri siku zinavyozidi kujongea. katika muktadha huo huo nionyeshe juhudi za serikali katika kufanikisha kuondolewa kwa mfumo huu wa kuzalisha wasomi "feki" ambao hawana uwezo wa kufikiri nje ya box badala yake kuendelea kuwaza ajira za kuajiriwa.
Juhudi za serikali kutoa elimu bure na kuhakikisha upatikanaji wa madawati ni juhudi za kuungwa mkono lakini ni juhudi zenye impact ndogo sana katika kukabiliana na changamoto niliyoieleza. Serikali ilipaswa kuweka kipaumbele katika kubadili mfumo wa utoaji elimu nchini ili ikiwezekana idadi ya vijana wanaopata mafunzo ya ufundi kama uvuvi wa kitaalamu, ukulima, ufundi seremala, uashi , Uinjinia wa maana na si huu feki ambao Injinia wa electronics hawez tengeneza hata Earrphone , hawez hata kucopy tecnolojia yoyote , injinia wa Electricity hawez kutengeneza hata taa tu. Niwaulize watanzania wenzangu elimu hii inayozalisha wazungumzaji hodari badala ya watendaji hodari itaifikisha nchi hii katika ndoto ya kuwa ya Viwanda?
Lastly niwaulize wale ndugu zangu wanaotoka hadharani na kusema wanamuunga mkono Rais je wanafikiri sawa sawa kweli? haikatazwi kumuunga mkono Rais lakini si kwa upofu huu jamani,, imetokea hivi karibuni mbunge kaiingiza nchi kwenye ghrama ya kurudia uchaguzi katika jimbo lake gharama ambayo ni zaidi ya billion 5-10 , gharama ambayo ingetosha kujenga vyuo hadi vitano vya ufundi..
Inauma na inakera kuona katika karne hii bado watanzania tunaendeza vyama badala ya taifa , inashangaza kuona hadi wasomi kuamua kutumikia matumbo yao badala ya jamii ambayo inawategemea.