Anayejua Rais Magufuli anatupeleka wapi atuambie, naona kama tumepotea

Anayejua Rais Magufuli anatupeleka wapi atuambie, naona kama tumepotea

Status
Not open for further replies.
Habari wakuu! Kuna muda nikiiiangalia serikali ya JPM nahisi namwelewa hivi anacholifanya! Na kuna wakati nikianglia kwa jicho la tatu nahisi kama anatupotez hivi kama taifa! Na kuna muda mwingine nikitulia zaidi nahisi kama Hta yeye hajuwi anachokifanya vilee! Lifupi ningekuwa n uwezo niangeacha labis kumfuatilia ningenyamaza. Ila nahisi nalewa tuu hata sijuwi. Hivi wenzangu mmamwelewa JPM anachokifanya?
 
Naomba tuwe na umoja wa kumwomba MUNGU atunasue kwenye hali hii ya kuelekea tusipojua.

Mbona kama gari linaelekea bondeni?. Maombi ni muhimu sana.
 
Naomba tuwe na umoja wa kumwomba MUNGU atunasue kwenye hali hii ya kuelekea tusipojua.

Mbona kama gari linaelekea bondeni?. Maombi ni muhimu sana.
[emoji28] [emoji28] [emoji28] [emoji28] fanya kufunga kusali omba sana Hali inaogopesha
 
Watanzania tusiwe na mioyo migumu kama wale wana wa Israel,tumpe Rais wetu muda, jamani bado ni mapema, Hata hivyo tu kwa muda aliokaa madarakani amefanya observable reforms, ndugu zangu reforms ni process na reformist hupambana na changamoto mbalimbali,waathirika wa reforms hawajalala wengine wanajifanya wako nae,lakini wanafanya kila jitihada kumkwamisha ili aonekani hajafanya lolote. anawafahamu ila tu anaenda nao kiana", keep your enemy very closer"(George' Washington). Tumpe muda uvumilivu na ushirikiano ana nia njena kwa nchi hii, nikumbushe tu kuwa hakuna mafanikio bila changamoto, pengine ni vyema tukafikiria jinsi ya kuzitumia hizo changamoto kama fursa badala ya kulaumu.Hata hivyo nikuhakikishie ndugu yangu subira yavuta heri, neema yaja,it is just a matter of time trust me.
 
Mkuu sawa! Bt Nan ataongoza hayo Maombi? Coz Maaskofu na Wachungaji weng mno kwa sasa wamekuwa batili Machoni pa Mungu, kwakukubali kuhalarisha maovu kwa vibahasha
 
Naomba tuwe na umoja wa kumwomba MUNGU atunasue kwenye hali hii ya kuelekea tusipojua.

Mbona kama gari linaelekea bondeni?. Maombi ni muhimu sana.


Kwenye maisha ukuguswa maala panapokufanya uishi utalalamika sana ili uhurumiwe kwa kudhani umeonewa. Tunahitaji nini watz!? Umahiri wa kuandika na kupost vitu ambavyo hatuna ushahidi navyo. Umetumia nini kujua tuanakokwenda!?
 
Watanzania tusiwe na mioyo migumu kama wale wana wa Israel,tumpe Rais wetu muda, jamani bado ni mapema, Hata hivyo tu kwa muda aliokaa madarakani amefanya observable reforms, ndugu zangu reforms ni process na reformist hupambana na changamoto mbalimbali,waathirika wa reforms hawajalala wengine wanajifanya wako nae,lakini wanafanya kila jitihada kumkwamisha ili aonekani hajafanya lolote. anawafahamu ila tu anaenda nao kiana", keep your enemy very closer"(George' Washington). Tumpe muda uvumilivu na ushirikiano ana nia njena kwa nchi hii, nikumbushe tu kuwa hakuna mafanikio bila changamoto, pengine ni vyema tukafikiria jinsi ya kuzitumia hizo changamoto kama fursa badala ya kulaumu.Hata hivyo nikuhakikishie ndugu yangu subira yavuta heri, neema yaja,it is just a matter of time trust me.
Subira ya miaka 50+ inataka moyo maana na huyu mnatuambia sio CCM au mnatupofusha,au waliaharibu ili walekebishe ili tushangilie kidogo. Hii inanipa wakati mgumu kufikiria kama hao hao ndo waliua ndege 11 na wananunua mbili mnashangilia inanikumbusha wimbo wa Solo wa Mtazamo....... Hatua mbili mbele unarudi nyuma tano unajipongeza.
 
Watanzania tusiwe na mioyo migumu kama wale wana wa Israel,tumpe Rais wetu muda, jamani bado ni mapema, Hata hivyo tu kwa muda aliokaa madarakani amefanya observable reforms, ndugu zangu reforms ni process na reformist hupambana na changamoto mbalimbali,waathirika wa reforms hawajalala wengine wanajifanya wako nae,lakini wanafanya kila jitihada kumkwamisha ili aonekani hajafanya lolote. anawafahamu ila tu anaenda nao kiana", keep your enemy very closer"(George' Washington). Tumpe muda uvumilivu na ushirikiano ana nia njena kwa nchi hii, nikumbushe tu kuwa hakuna mafanikio bila changamoto, pengine ni vyema tukafikiria jinsi ya kuzitumia hizo changamoto kama fursa badala ya kulaumu.Hata hivyo nikuhakikishie ndugu yangu subira yavuta heri, neema yaja,it is just a matter of time trust me.
hivi tunaongozwa na sera za mtu au chama hivi hiki chama kimepewa miaka 56 ni muda gani mnatakakupewa tena?
 
siku hizi simsikii anasema "mniombeee"

yaani nchi hii ina vituko!huwa naenda makanisani lakini sijawahi kusikia padri anaweka kipengele cha kumuombea,labda akina lusekekelo
 
Kwanza haujui unapokwenda,

Pili una sema gari linaelekea bondeni (kumbe unajua tunapokwenda),

Halafu haraka ya nini subiria ufike tunapokwenda ndio unajua tulipokuwa tunaenda
 
Ni wazi kabisa kwa sasa taifa limepoteza mwelekeo, raia tunajua hivyo na hata wale wateule wanaomzunguka mkubwa wanajua hivyo japokuwa hawataki kusema hadharani kwa sababu ya woga wao.

Na ukweli mchungu ni kwamba, tunakoenda ni kubaya zaidi. Why? Hakuna mwelekeo. Hakuna anayejua wapi tunakwenda na kama kweli kuna kufika huko. Hata "mtukufu" mwenyewe ameshaanza kuingiwa na wasiwasi kuhusu hilo.
Kama bado kuna mtu hataki kuamini hilo, basi ajipe muda zaidi, na ipo siku atakuja hapa hapa JF na kutupa mrejesho.
 
Nawaomba watanzania wote wanyonge,Kwa kauli moja, Kwa kulia na kusaga meno, Kwa kufunga na kuomba, Kwa kuomboleza na kujuta, Kwa kutubu dhambi zetu zote mbele za Mungu .
Tumlilie Mungu, yeye aketie mahali pa juu palipoinuka atusaidie Kwa uwezo wake wenye nguvu za kipekee ili ccm iondoke madarakani mnamo 2020.
Mateso tuliyonayo, umaskini tulionao, shida tulizonazo sasa yatosha.
Eeeh Mungu wetu, uliye mkuu kuliko vyote tuepushe na hiki kikombe kiitwacho ccm mnamo 2020.
Nakusihi Mungu wangu, uliye mwingi wa rehema, na Mungu ambaye hujawahi kushindwa ,Baba yangu, na mfalme wa wafalme, kasimame mwenyewe Mungu maana Kwa nguvu zetu na akili zetu sisi Bwana hatuwezi.
Mungu wangu, kasimame Baba, Kama ulivyo simama na wana wa Israel dhidi ya mfalme Farao.
Mungu wangu, hujawahi kushindwa Baba.
Ulitupatia nchi nzuri mno yenye kila kitu ndani yake, lakini Mungu ni ajabu tunaishi maisha magumu kana kwamba ulitulaani, Kwa Sababu tu ya genge la watu wachache ambao wanaishi wakidhani ni wao tu ndo wenye dhamana ya haki kuliko wenzao.
Tanzania ni nchi yako Mungu wangu uliyoiumba Kwa ajili yetu sote.
Mawazo yako Mungu, njia zako, matendo yako, hayachunguziki na wala siyo ya mwanadamu.

Baba Mungu wangu, tuonee huruma watu wako, baadhi yetu tunakukufuru Kwa Sababu ya hali ngumu tuliyonayo.
Mungu kasimame wewe Bwana ili jina lako litukuzwe na kuinuliwa.
Na watu wote wakajue ya kwamba, hakika Mungu upo.
Na wote humu jamiiforums Tuseme Amen.........
 
Chakufanya ni kuitisha siku ya maombi maalumu ambayo tutasema yatosha kwa kumlilia MUNGU na kufunga
 
Ndivyo hali ilivyo. Inawezekana mwenyewe na wasaidizi wake wakaona wanapatia lakini kwangu mimi anabomoa tena sana.

Uchumi. Tunaambiwa makusanyo yamepanda hadi 1.3 Bill kwa mwezi lakini fedha haionekani na maisha yamezidi ugumu. Mizigo bandarini imepunguwa sana na hali ya uchumi hairidhishi.
Watu hawana ajira na ajira hazipo zimeyeyuka na ndio kwanza uhakiki wa wafanyakazi hewa unaendelea na ni zoezi endelevu sijui litaisha lini.

Huduma. Madawa hospitalini hayatoshi, idadadi ya wanafunzi waliokatiwa mikopo imeongezeka na malalamiko ya idara za serikali kukosa mafungu ya uendeshaji yapo japo kwa usiri mkubwa.

Hali ya Siasa. Mivutano na kuvurugwa kwa demokrasia, malalamiko ya kukiukwa katiba na haki za kisiasa yameongezeka ndani ya muda mfupi. Uvumilivu wa kisiasa unaelekea kuibuka na kupotezeana muda kwa kufanywa vitimbi vya makusudi vinavyoashiria kubomoka kwa misingi ya demokrasia iliyokwisha jengwa kwa muda wote wa siasa za vyama vingi tena sehemu zote mbili Bara na visiwani. Watu wananyimwa haki za kisiasa na uhuru wa kuzungumza . Kuna viashiria vya kidikteta kila eneo ambalo mtawala anaona ni hatari kwake. Mambo ni mengi tu.

Malalamiko ya wafanyakazi. Wafanyakazi wanatishwa na kutumbuliwa bila kufuatwa taratibu kazi iliyopo ni "Kutumbuwa, Kuteua na Kutengua" (KKK) hatuoni ufanisi. Kuna visasi na kutoaminmiana. wafanyakazi hawako huru kutumia weledi wao, wanasubiri maelekezo. Maelekezo hayana formula. Unaweza UKATUMBUWA KWA NAFASI YAKO KAMA MKUBWA WA ENEO LAKINI GHAFLA MAAMUZI YANATENGULIWA. Kumekosekana mfumo kuna maagizo tu kutoka juu.

Sera. Mimi siioni, sijui tunelekea wapi tena katika nyanja zote. Si kiuchumi ingawa tunaambiwa wa viwanda lakini siuoni msingi wake. Si kisiasa naona tunarudi nyuma sana na kupandikiza uadui na kushutumiana bure. Si kijamii nako kunaathiriwa na siasa mbaya vile vile. Sera ya mambo ya nje siijui, Tunaondowa na kuweka , Inasikitisha kwa mara ya Kwanza Tanzania Kuripotiwa Vibaya huko UNHCR na UN, tumeanza kupoteza heshima yetu na kutofautiana na rafiki zetu wa muda mrefu.


HITIMISHO. Kwa ufupi wa maneno wa makala hii fupi, ni muda wa mwaka tu tokea awamu hii ya tano iwepo lakini tumeshuka sana katika maeneo yaliyotajwa. Kwa mtazamo wangu malalamiko yamezidi, ajira hakuna, wafanyakazi wanalalamikia mengi, wanasiasa wanalia na kupaza sauti za demopkrasia, ajira hakuna na mengine mengi Hii si ishara nzuri.

Katika hali hii ,umoja wa kitaifa na amani ya nchi inakwazwa na uadui unajengeka miongoni mwa Watanzania. Kipindi hiki kifupi kimekuza nyufa kati ya WADAU wa kujenga Taifa letu na ukinzani wa mawazo kati ya Dola na watawaliwa umeanza kuibuka. Misingi ya Umoja hujengwa kwa sera madhubuti na kufuatwa KATIBA ambayo kwa sasa inasiginwa sana.

Kwa muhtasari huu Rais JPM kama kiongozi Mkuu wa Nchi hawezi kuepuka lawama na kwangu mimi anabomoa zaidi kuliko kujenga.

Kishada.
 
Ndivyo hali ilivyo. Inawezekana mwenyewe na wasaidizi wake wakaona wanapatia lakini kwangu mimi anabomoa tena sana.

Uchumi. Tunaambiwa makusanyo yamepanda hadi 1.3 Bill kwa mwezi lakini fedha haionekani na maisha yamezidi ugumu. Mizigo bandarini imepunguwa sana na hali ya uchumi hairidhishi.
Watu hawana ajira na ajira hazipo zimeyeyuka na ndio kwanza uhakiki wa wafanyakazi hewa unaendelea na ni zoezi endelevu sijui litaisha lini.

Huduma. Madawa hospitalini hayatoshi, idadadi ya wanafunzi waliokatiwa mikopo imeongezeka na malalamiko ya idara za serikali kukosa mafungu ya uendeshaji yapo japo kwa usiri mkubwa.

Hali ya Siasa. Mivutano na kuvurugwa kwa demokrasia, malalamiko ya kukiukwa katiba na haki za kisiasa yameongezeka ndani ya muda mfupi. Uvumilivu wa kisiasa unaelekea kuibuka na kupotezeana muda kwa kufanywa vitimbi vya makusudi vinavyoashiria kubomoka kwa misingi ya demokrasia iliyokwisha jengwa kwa muda wote wa siasa za vyama vingi tena sehemu zote mbili Bara na visiwani. Watu wananyimwa haki za kisiasa na uhuru wa kuzungumza . Kuna viashiria vya kidikteta kila eneo ambalo mtawala anaona ni hatari kwake. Mambo ni mengi tu.

Malalamiko ya wafanyakazi. Wafanyakazi wanatishwa na kutumbuliwa bila kufuatwa taratibu kazi iliyopo ni "Kutumbuwa, Kuteua na Kutengua" (KKK) hatuoni ufanisi. Kuna visasi na kutoaminmiana. wafanyakazi hawako huru kutumia weledi wao, wanasubiri maelekezo. Maelekezo hayana formula. Unaweza UKATUMBUWA KWA NAFASI YAKO KAMA MKUBWA WA ENEO LAKINI GHAFLA MAAMUZI YANATENGULIWA. Kumekosekana mfumo kuna maagizo tu kutoka juu.

Sera. Mimi siioni, sijui tunelekea wapi tena katika nyanja zote. Si kiuchumi ingawa tunaambiwa wa viwanda lakini siuoni msingi wake. Si kisiasa naona tunarudi nyuma sana na kupandikiza uadui na kushutumiana bure. Si kijamii nako kunaathiriwa na siasa mbaya vile vile. Sera ya mambo ya nje siijui, Tunaondowa na kuweka , Inasikitisha kwa mara ya Kwanza Tanzania Kuripotiwa Vibaya huko UNHCR na UN, tumeanza kupoteza heshima yetu na kutofautiana na rafiki zetu wa muda mrefu.


HITIMISHO. Kwa ufupi wa maneno wa makala hii fupi, ni muda wa mwaka tu tokea awamu hii ya tano iwepo lakini tumeshuka sana katika maeneo yaliyotajwa. Kwa mtazamo wangu malalamiko yamezidi, ajira hakuna, wafanyakazi wanalalamikia mengi, wanasiasa wanalia na kupaza sauti za demopkrasia, ajira hakuna na mengine mengi Hii si ishara nzuri.

Katika hali hii ,umoja wa kitaifa na amani ya nchi inakwazwa na uadui unajengeka miongoni mwa Watanzania. Kipindi hiki kifupi kimekuza nyufa kati ya WADAU wa kujenga Taifa letu na ukinzani wa mawazo kati ya Dola na watawaliwa umeanza kuibuka. Misingi ya Umoja hujengwa kwa sera madhubuti na kufuatwa KATIBA ambayo kwa sasa inasiginwa sana.

Kwa muhtasari huu Rais JPM kama kiongozi Mkuu wa Nchi hawezi kuepuka lawama na kwangu mimi anabomoa zaidi kuliko kujenga.

Kishada.

Nimekumbuka na Mgogoro wa Zanzibar. Badala ya kupungua umeongezeka na kuzidi kuvuka mipaka. hakuna jitihada zozote zaidi ya kukoleza moto.
 
Kumekuwa na lawama zinazomkabili mkuu wa nchi kuhusu mambo mbalimbali. Je shida iko wapi? Ni uelewa wetu mdogo hivyo hatujui afanyalo au uelewa wetu mkubwa zaidi tunaona anaboronga?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom