Anayemjua Mohammed Ali wa Jicho Pevu

Muro alitaka kufuata nyayo za huyu jamaa. Siku aliporusha kwenye Tv, clip ikimuonyesha askari akipokea rushwa, huo ndo ukawa mwanzo wake wa 'kuporomoshwa' mpaka kuwa 'msemaji wa Yanga'. Mikasa iliyomkuta Jerry Muro sidhani kama kuna mwingine atathubutu. Labda mpaka kizazi kilichoshuhudia kiishe.
 

Aisee kweli Muro alijaribu kilichompata anakijua mwenyewe....
 
Huyo jamaa ni noma sana mkuu. Nilimpa heshima kwenye ile issue ya West Gate
Anasema alijibanza kwenye server za cctv akawa anafuatilia yanayoendelea ndani ya jengo.

Kati ya wanajeshi, polisi, na alshabaab.

Askari watiifu walikuwa wanarusha risasi hewa,huku jamaa wanaendelea kusali kama hakuna kinachoendelea.

[emoji28] [emoji28] [emoji28] mwisho wa siku kdf wakamalizia picha kwa kukomba mazaga zaga tu maana hakukuwa na namna[emoji38] [emoji38] [emoji38] .
 
Yuko vzr, niliona clip ya tukio la kifo cha saitoti. Aiseeee kwa tz bado sana kufikia level hizo za uandishi wa habari na utangazaji
 
Na huwezi kumtaja huy Mo bila kumtaja John Allan Namo.
Hiyo kolabo mwenyewe anasema anaumwa kama akiwakosa wenzake mahiri kama Linus Kaikai, Farida Karoney, John Allan Namu, Njoroge Mwaura, Waziri Khamis

Na wengine akina Catherine Soi, Peter Moss, Sinjiri Mukoba, Kizito Namulanda... mkuu ni wengi KTN News na vituo vingine
 
Nimecheka sanaaaaaa,niliiona hiyo
 
Hivi huyo njoroge si aliwahi kupewa kesi ya ugaidi?
 
Muro ilikuwa tamaa ya pesa ndio ilimtangulia mbele, kazi akaiacha nyuma
 
namkubali sana mohamed ally,nami shahada yangu ya kwanza ni ya uandishi wa habari,ninao uwezo wa kufanya zaidi ya mohamed ally kwani nami siogopi kufa kwani ni mfu mtarajiwa,is a matter of time tu,na kizuri zaidi nina uzoefu mkubwa wa upelelezi kwani nilifanya kazi kitengo hicho kwa miaka 9,ninapenda kufanya vipindi kama vyake na nilishaandika proposal kwenda media house mbalimbali hapa bongo za kufanya investigative journalism sikujibiwa,ni tv station moja tu ndio walinijibu kwamba wanaogopa kurusha vipindi kama hivyo kwenye station yao kwani nitawagombanisha na serikali kwa kufichua maovu yao,nikaishiwa nguvu kabisa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…