Andika tabia usiyoipenda ya baadhi ya member wa JF

Andika tabia usiyoipenda ya baadhi ya member wa JF

Baada kurekebisha, wanaanza dharau na kuporomosha matusi,
Sipendi hii tabia😠😠😠😠
 
Tabia ya watu kuandika juu ya ngono zembe wakati ni dhambi
...
Wakuu nimeanzisha huu kwa lengo la kuonyana kuhusu tabia mbovu zinazoonekana kwa baadhi ya member wa jamiiforums.

Naanza mimi.
1. Sipendi kabisa tabia ya baadhi ya members kuingilia na kuvuraga mada za wenzao kwa kuanzisha majibizano yasiohusika na mada iliyopo. mfano unakuta mtu kaanzisha mada yake ya kutafuta mteja wa bidhaa yake au kutafuta kazi au kuomba ushauri juu ya suala fulani, sasa unakuta kuna member wanaanza kuleta mazungumzo ya ajabu yasiyohusika kabisa. Tabia hii ya hovyo.

2. Tabia nyingine inayokera ni kukuta watu wanapoteza muda kudharau miji au mikoa mingine ndani ya nchi kana kwamba dharau zao zinawasaidia chochote.

Je wewe umeona tabia ipi inayokukera jamvini?
 
Back
Top Bottom