Android Developers wa bank ya NMB, huu uoga mmeanza lini?

kali linux umetoa hoja za msingi unfortunately umekutana na hao arrogant developers kutoka hiyo Bank au kampuni ilo develop hiyo app.
Na industry ya technology kwa Tanzania(Katika baadhi ya makampuni) ndo ilivo yaani mtu ukileta challenge mezani au uka question design ya kitu fulani anaanza kutunisha misuli ya seniority yake na taka taka za mshahara na maeneo aliko fanya kazi ili kukutisha tu.

Hizi scenario nimekutana nazo kwenye kampuni fulani hapa mjini, yaani kuna watu hawa accept na kufanyia kazi challenges hata siku moja just because wao wamekua labbelled seniors, au with many years of experience.
 
Hapo kwenye password 123456 mbona hujibu? Anayezuia developer mode na unaye allow password 123456 nani achekiwe?
JAMANI MBNA MNABISHANA SANA, NA KUPEANA MIPASHO.

1: MADA INAHUSU NINI, #Ajibiwe mada
2: KAMA WOTE MPO FITI, MU HACK IYO APP THEN MBISHANE NANI KAIBA PESA MINGI
3: MNAJIFANYA DEV KUMBE MNA DOWNLOAD NULLED SCRIPT MNAKUJA KUJISIFIA HAPA. TUNA WACHEKI TU πŸ˜‚πŸ˜‚ ACHENI KELELE
4: KAMA MKO FITI KILA MTU A SHARE GIT/GITLAB YAKE HAPA TUONE KAZI.
5: kali linux , HDMI , PakiJinja

Mimi Termux App zangu hizo zipo playstore na app store. Link : Android Apps by Fadsel Tech Apps & Games on Google Play
 
Wapuuzi sana Developers wa NMB. Nimeshindwa kufanya transactions kisa nime enable developer options. Yani concept ya user friendliness kwao hawana kabisa.
Wewe umetengeneza kitu gani ambacho kipo public wanatu wanatumia. Tuoneshe kazi yako kwanza, akuna dev ambae afanyi makosa akuna alie kamilika
 
Inatakiwa wajuzi wajibu hoja kwa ufanisi bila kutunishiana misuli. Atupo GMY hapa. Big Up kali linux
 
Kitu muhimu kufikisha ujumbe wa shida uliokutana nayo katika APP, wausika tunaomba maelezo au usaidizi
 
Inawezekana kipindi mimi naanza kazi, wazazi wako walikuwa hata hawajajua kama watakuja kukutana na kukupata wewe, haha.
Young man, control your ego. Sehemu mimi nimefanya kazi, wewe hata kazi ya ulinzi hauwezi kupewa.
Acha majigambo ya kijinga na wewe Deleted01 Wewe ndo una EGO. Bado ujakuwa ki akili, unafanya kazi nzuri ndo utangaze kwa watu. Bado ujakuwa bado una utoto, kazi yako na maisha yako atuitaji kujuwa. Tunaitaji kuchangia hoja na kuelimishana na wengine wapate kujifunza. Kila mtu akiweka mshahara wake anao lipwa hapa si itajiona πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Hizo apps zake zinaingiza Tsh ngapi? Au zimebeba risk kiasi gani kwa watumiaji? Unafananisha draft na financial app mzee? Na wewe wale wale tu. Akasome guidelines za OWASP ndio aanze ubishi
Sio kwa kutishana uku. Mbna hii app nayo UI mbaya sana. Arafu ni nulled game App. πŸ˜…πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚ developer wa mchongo. Ujanja mwingi wa ku edit code za free basi unajiona developer. Hizo coin unawauzia wabongo. Hahaha πŸ˜…πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚, system za ku copy nbanaa ku edit zina shida sana
 

Attachments

  • Screenshot_20230710-010257.png
    28.7 KB · Views: 11
Ninachoona hapa ni swala la user Experience ndo lina shida zaidi ila upande wa security labda mpaka nami nihakiki.

Lakini mkuu ungeweza kufanya nini kwa upande wa security ikiwa unaona wanaficha kitu flani, je unaweza kukifichua kama inawezekekana we fichua tu weka adharani kwa njia hiyo wanakupa mtonyo tumia id nyingine hii wanakufahamu wazi wazi kwa sababu hata hiyo app yako inaku identify wewe ni nani!.

Ukisha expose app hapa hata mjinga anajua wewe ni nani make sure you do that mimi nafahamika wazi nisha expose software yangu hapa. so kama vipi wasagie kunguni.

si nasikia kuna white hat hacker kwani huyu naye wanamfunga kwa style yake ya kuhack naomba msaada wako
 
Ila wabongo bn hapo ukute hata kujaribu kucheza bado ila ushamuhukumu mwenzako kacopy code

Em nipe app unayoweza kucheza lastcard au albastini kibongobongo yaan Kwa sheria zetu wabongo
 
Ila wabongo bn hapo ukute hata kujaribu kucheza bado ila ushamuhukumu mwenzako kacopy code

Em nipe app unayoweza kucheza lastcard au albastini kibongobongo yaan Kwa sheria zetu wabongo
Mimi sio nikupe mm nakutengenezea ukitaka, au ni clone app yako arafu niweke katika store yangu na ww udownload πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Ni shida sana mkuu, growth is hidden in solving those challenges. Mimi nikiwa sina kazi napenda sana kwenda tu playstore kuangalia apps za wenzangu zinafanyaje kazi, user interface, user experience etc... sababu najua siko perfect, hawa challenges hawataki na kibaya zaidi bora app ingakua sio service lkn tunalipia hio service, kuna makato baadhi huwa yako associated na kutumia simbankimg
 
Inaonekana una point ila utoto wako unazidi uzito wa point zako

1)Sipo hapa kushindana, my time is limited siwezi poteza muda kwa mambo ya kitoto kama hayo. Nipo hapa kukosoa huduma ambayo tumelipia na kupoteza muda wetu kuunganishwa ili kuipata.

2)Unasema tuhack kwenye hio app, nilishatoa jibu huko juu. Kaongee na NMB wafungue bug bounty program kwenye professional site yyt ya bug bounty (na-recommend hackerone) wakikubali nitumie link ya hio bug bounty program niingie mzigoni.

3)Naona umekariri neno 'Nulled scripts' kwa sababu unazitumia sana, naweza reverse engineer apps zako zote nikakuonesha ulipotumia hizo modified scripts za watu hadi ulipozitolea ila sina hio time na huwa sijibu utoto kwa utoto. Mfano kwenye hizo apps ulizoweka playstore kuna game moja umeclone, scripts ziko wazi kabisa hio ni clone

4)Hahahahaaa unaongelea github? Una misuli? Mzee watu contributions zetu zinafahamika hadi silicon valley kwa wazungu unaow-admire wewe. Big FOSS projects kama Wordpress, Gutenberg, OWASP ZAP kuna codes zangu humo, na sina github acc moja, zipo tatu na zote zipo active (coding, cyber, web3). Anyway Back to the topic sina time ya kufanya huo utoto, nmetengenezea watu zaidi ya kumi humu jf systems ambazo hadi leo wanatumia na hizo app sikutaka hata kushare lkn users wanaojua kazi zangu ndo wameshare. Na kwa taarifa yako hio app waloshare ni apps ambazo huwa natengeneza nikiwa sina kazi ya kufanya, yaani nikiwa nataka kurefresh

Kama kazi zangu hazikufanyi kuappreciate uwezo na mchango wangu basi endelea na mashindano yako na watoto wenzio ila siku ukikua njoo tujenge hoja bila kuweka mashindano yako ya kipuuzi, BTW siko hapa kuimpress watu
 
Wewe umetengeneza kitu gani ambacho kipo public wanatu wanatumia. Tuoneshe kazi yako kwanza, akuna dev ambae afanyi makosa akuna alie kamilika
Kama unajua kwamba hakuna dev alokamilika kwa nn unataka kutumia mashindano ya kipuuzi?

Weka hoja ujibiwe, kama huna hoja baki kuwa ndugu msomaji
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…