Anga la washenzi na Joana anaona kitu usiku

*ANGA LA WASHENZI II -- 28*

*Simulizi za series*


ILIPOISHIA

Ila kabla hawajanyanyuka na kuhepa, Miranda akamtaka Marwa atulie hapohapo tuli, la sivyo wangeharibu chakula mwishoni.

"Shhhhhh!!!" Miranda akampa ishara kisha akakagua eneo zima kwa macho yake mepesi.

ENDELEA

Wakiwa wametulia hapo kwa muda kidogo, wakaona watu kwa mbali wakiwa wanasonga kuzama ndani ya uzio. Na pale getini palikuwa na hekaheka.

Basi Miranda akamtaka Marwa wabadili njia, nao hawakwenda mbele bali wakarudi nyuma na kufumbukia njia huko. Baada ya muda wa dakika nane, wakawa wamelifikia gari lao. Wakapanda na kulitia moto upesi.

Hapo Miranda akatabasamu na kucheka. Walikuwa wamekamilisha kazi yao. Hata moyo wake ukawa wa baridi sasa na Marwa akalaza kichwa chake kwenye kiti akitabasamu. Alihisi ametua mzito wa toni kadhaa kichwani. Haikuwa kazi nyepesi hata kidogo.

Ila kabla hawajaikuta barabara kuu, mara risasi tatu zikalia! Pah! - pah! - pah! Kioo cha nyuma cha gari kikapasuka na kuwa unga.

Wakawehuka. Kumbe walikuwa wanafuatiliwa! Nyuma yao kulikuwa kuna gari jeusi, Toyota Harrier, imeshusha vioo vya madirisha ya nyuma.

Miranda akamtazama Marwa. Hawakuongea kitu. Kumbe walikuwa wamekosea sana. Vita bado haikuwa imeisha. Bado refa hakuwa amepuliza kipyenga cha kuhitimisha mchezo.

Sasa hapo wakawa na zoezi la kukabili lile gari ambalo ndani yake hawakuwa wanajua wapo watu wangapi.

"Marwa," Miranda akaita. "Inabidi tuwamalize hawa watu wote. Endapo tukiwatorola ila tukawaacha salama, itakuwa rahisi kutufuatilia na kutujua. Wameshalijua gari letu."

Marwa akataka kuuliza watawamalizaje, ila akaamua tu kunyamazama. Pengine Miranda alikuwa ameshapanga namna ya kufanya. Akawaza.

Na ni kweli, mwanamke huyo alikuwa tayari ameshayapanga yake kichwani. Alihakikisha hajai kwenye macho na tageti ya adui, na baada ya muda fulani akamwambia Marwa, "shika usukani!"

Hakurudia mara mbili, akachumpa kwenda nyuma ya gari. Haraka Marwa akalazimika kuudaka usukani na kusonga hapo kwenye kiti cha dereva kwa tahadhari.

Risasi zikarushwa tena. Zikabangua gari kando na kando. Marwa akawehuka kwa uoga. Akayumbisha gari huku na huko. Ila akamudu na kuliweka sawa tena. Mwendo ulikuwa mkubwa sana.

Akatazama kwenye 'sight mirror', akamwona Miranda amelala kochini. Hakujua mwanamke huyo anafanya nini maana hakuwa na muda wa kubakiza macho kiooni.

Baada ya muda kidogo, Miranda akanyanyuka toka kitini, akachungulia kutazama gari linalowafuata. Kisha akarudi tena chini. Sauti ya kukoki bundiki ikaita. Na mara kidogo akanyanyuka na kuchomoa mikono yake nje ya gari kwa kupitia uwazi uliosababishwa na kioo kuvunjwa.

Mikononi alikuwa amebebelea bunduki fupi, kama vile 'sub-machine gun' ila hizi zilikuwa fupi zaidi, zimechomekwa risasi pomoni.

Basi akaelekezea mikono yake katika lile gari liwafuatalo na kilichofuatia hapo kikawa kufuru. Alimwaga 'njugu' kama mvua ya masika. Alichokuwa anakifanya ni kupeleka mikono kushoto, kulia. Kulia, kushoto.

Risasi zikatoka pasipo kupumzisha koo la bunduki. zikachakaza kioo cha gari lile linalowafuata. Zikachomoa uhai wa dereva na mtu aliyekaa naye mbele mara moja wasiombe hata maji!

Gari likayumba. Likayeya. Mara likapiga kona ya ghafla na kubinuka, likabiringita mara ya kwanza, ya pili, ya tatu, juu kukawa chini!

Matairi yalizunguka na kukoma. Punde ndani ya gari ikasikika sauti ya mwanaume akikohoa. Kisha akaguguma kidogo kwa maumivu aliyokuwa anayapata. Si kwamba yalikuwa madogo, la hasha, mbavu zilikuwa zimembana. Anachuruza damu. Amevunjikavunjika kuanzia kiunoni kushuka chini.

Basi mara mlango wa gari hilo ukasukumwa kwanguvu, akatoka mwanaume aliyekuwa amechafuka damu kichwani. Akajivuta na mikono kutoka ndani ya gari. Akatoa mwili mpaka kiuno, kisha akalala hapo akiwa hoi!

Alilalama sana kwa maumivu makali. Hata kuhema ilikuwa tabu. Alikuwa ndiye mtu pekee aliyesalia kwenye ajali hiyo. Wenzake wote walikuwa wameshakata kauli.

Akiwa hapo chini, anagugumia, mara akasikia kishindo cha miguu kikimsongea. Akajikakamua na kunong'ona, "nisaidieee ..."

Mara kishindo cha miguu kikakomea mbele ya kichwa chake. Kutazama akaona kiatu kirefu cha kike, rangi nyeusi. Akakazana kurusha macho yake kutazama juu. Hakuona vema, ila akapata kutambua ni mwanamke waliyekuwa wanamkimbiza. Bunduki yake bado ilikuwa inanuka moto.

"Nisa ...."

Hajamalizia kauli, akala risasi tano za kichwa! Sina haja ya kusema kuwa alikufa papo hapo maana unajua kilichotokea. Damu zikamwagika kutengeneza kadimbwi.

Miranda akachuchumaa na tazama ndani ya gari, akaona kimya. Hama dalili ya uhai. Basi akaondoka zake akirusha miguu upesi.

Ila hakuridhika. Pengine mule ndani kunaweza kukawa na watu waliopoteza fahamu tu na si maisha. Basi alipokaribia gari lake, akatema tena risasi kadhaa kulenga uvungu wa gari, mara chombo kikalipuka.

Wakayeya upesi.

Kukawa kimya ndani ya gari kwa muda wa dakika kumi na, hakuna mtu aliyemwongelesha mwenzake. Ni kama vile walikuwa wanawaza na kuchambua kilichotoka kutokea. Na kama vile bado hawakuwa wanamini kama kazi imekwisha.

Walifika kwenye makutano ya barabara, Marwa akatazama 'sight mirror' baada ya kusimamisha gari lao kupisha gari kubwa lililobebelea kontena kubwa rangi ya bluu.

Nyuma yao akaona daladala moja, costa, akashusha macho yake na kumtazama Miranda aliyekuwa amejilaza kitini. Alikuwa anatazama nje akiwaza jambo.

Hakumwongelesha. Ila baada ya kukanyaga mafuta na kuondoa chombo baada ya gari lile kubwa kukatiza, akamwita mwanamke huyo na kumwambia, "You were amazing! Really amazing! I didn't expect ... oh God!" Marwa akatikisa kichwa na kumalizia, "Nifundishe na mimi!"

Miranda akatabasamu. Akaguna puani asiseme kitu. Wakafika nyumbani. Miranda akaweka ile set ya test tube mezani.

"Vipi anaendeleaje?" Marwa akamuuliza dada wa kazi akionyeshea kichwa chake kule chumbani alazwapo Jona.

"Nahisi yupo sawa," dada akajibu.

"Hauna uhakika. Hukwenda kumtazama?" Marwa akauliza. Dada akapandisha mabega. "Nilienda kumtazama jioni. Sasa kila nikimtazama naona tu yu vilevile. Sijamtazama tena mpaka muda huu!"

Marwa akatazamana na Miranda kisha akaelekea chumbani kumwona Jona. Mwanaume huyo alikuwa amekaa vilevile kama alivyomuacha. Akamshika mkono na kumwita. Hakuitika. Ila hakujali, akamtazama kidogo alafu akatabasamu na kusema, "Nimerudi, Jona. Tumefanikiwa kupata antidote."

Akatabasamu zaidi, na kuendelea kunena kwa sauti ya chini, "haikuwa rahisi hata kidogo. Miranda alikuwa so magnificient. Siamini hata kama sasa nipo na wewe. Nilijua sitakuona tena, ila Mungu si Athumani ..." akanyamaza kidogo. Kuna kitu kilikaba koo lake. Akajaribu kumeza mate kisha akaendelea kunena, "... Mungu ana makusudi nawe. Ana makusudi na sisi. Muda si mrefu utaacha kitanda na mikono yako itafanya kazi iliyozoea."

Aliposema hayo, akamtazama tena Jona kwa muda kidogo kisha akamuaga. Ila kabla hajatoka ndani ya chumba, akasikia sauti ya Miranda huko sebuleni. Alikuwa anaongea na simu.

Basi akatoka na mpaka kufika sebuleni akamkuta mwanamke huyo ameshamalizana kuteta na simu. Akaketi na kumtazama. Alikuwa ana uso wa mafikirio. Akamuuliza, "vipi kila kifu kipo sawa?"

Miranda akashusha pumzi alafu akasema, "nimetoka kuongea na BC. Nimemwelezea kuhusu hii chemical. You know what? Amesema si yenyewe ..."

Marwa akahisi baridi la ghafla limempitia. Koo limemkauka. Na joints zote za mwili zimeishiwa nguvu.

Akatoa macho. Ila kabla hajanena, Miranda akamwambia, "ngoja kwanza ..."


***
 
asante kiongozi ,vipi ndo hii moja au nyingne usiku mnene?
 
Stive big up, kuna siku nilikuwa nacheki mov Fulani ivi ya ugaibuni, huwez amini yaani vitu vidogo vidogo tu kama vile "unajiokoa na family yako zidi ya wahalifu Mara katoto kako kanadondosha tu mdoli wa kenyewe kanalia na kuhalibu kila kitu na kufanya mjulikane na adui yenu" ndo huwa vinaifanya movie inoge na ionekane kuwa yenye ubunifu wa hali ya juu sana na enye kuvutia mno.


Kuonekana kwa antidote kuwa ndiyo siyo ,kwako ww kama mtunzi ni bonge la u creative, movie haitakiwi kuwa straightforward mpaka audience afikie hatua ya kujua inaelekea wapi.
Binafsi mm kaka mm u deserve to inspire other story makers, you know what you do.
Ur Maestro story maker ever.
 
Ahsante ndugu yangu. Predictable stories zinaboa.
 
Aise hiyo antidote ndo yenyewe sema BC ana lake jambo anataka ampe kwa mashart ili amfanyie kazi zake ila Miranda kashitukia mchezo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…