SteveMollel
JF-Expert Member
- Jul 12, 2015
- 8,797
- 25,177
- Thread starter
- #2,441
*ANGA LA WASHENZI II --34*
*Simulizi za series*
ILIPOISHIA
Habari hizi zikamfurahisha sana Marwa. Akatabasamu mpaka gegoni. Ila BC akamwonya. Akamkumbusha yale makubaliano ya awali waliyoyaweka.
Atampatia Jona antidote, ila wataandikishiana makubaliano. Na atakuwa akitoa kidogo kidogo akitazama kama makubaliano yake yataheshimiwa.
ENDELEA
Marwa angelisema nini? Hakuwa na la kusema zaidi ya kuafiki kile ambacho BC alikuwa anamwambia japo ndani ya moyo wake alijawa na hofu. Hakuwa anamwamini kabisa Jona. Alihofia anaweza kiuka vifungu hivyo na kuleta tafrani.
Misukosuko waliyopitia inatosha. Pengine Jona anaweza akalitambua hilo, alijipa moyo. Basi baada ya muda mfupi BC akaaga na wakaondoka pamoja na Marwa kwa makubaliano kwamba aende kumpatia antidote.
Walipofika nyumbani kwa BC mwanaume huyo akazama maabara na kufanya kile anachokijua zaidi. Ikamchukua kama robo saa akatoka akiwa amebebelea kemikali ndani ya chupa maalum ya kioo. Akamkabidhi Marwa na kumpa maelekezo.
Marwa hakupoteza muda, akamuaga na kwenda zake BC akimsisitizia kuwa makini na chupa hiyo iliyobebelea antidote.
Alipowasili nyumbani, akampatia Jona kiasi alichoelekezwa kisha akajikuta sebuleni pamoja na Miranda.
Aliketi akiwa ana mawazo kichwani. Miranda alimtazama na kisha kumuuliza, "Marwa, kuna tatizo?"
Marwa akatikisa kichwa akiminya lips. Hakusema kitu. Miranda akamtazama na kisha akamjongea akiachana na kutazama televisheni.
Akamwambia, "Najua unachowaza."
Marwa akamtazama. Bado hakusema kitu.
"Hata mimi kinanipa hofu kama wewe. Ila natumai kila kitu kitakuwa fresh. Usiwaze sana."
Marwa akamuuliza, "una uhakika?"
Akajibu, "Hata kama sina uhakika, ila ya nini kufikiria yajayo ambayo bado hayajafika? Don't worry ..." akamshika Marwa bega. "Kama tumepita kule kwenye bonde la mauti, tutashindwa hapa?"
Marwa akashusha pumzi. Akauliza, "ila vipi kama Jona hataridhia? BC atammaliza?"
Miranda akatulia kwanza akiwaza. Kwa kama sekunde tano, akasema, "pengine hiyo inaweza ikawa kazi kubwa kuliko zote tulizozifanya.."
Miranda akashusha pumzi. "Endapo kama Jona akikataa, tutakuwa njia panda. Tuna kazi ya kumshawishi. Na naamini inawezekana ... yah! Inawezekana."
Miranda akatabasamu. Naye Marwa akatabasamu.
"Leo jioni tutatoka out for a dinner. Angalau tukatefresh minds na kujipongeza. Au unasemaje?" Miranda alichombeza. Marwa akajibu kwa kuongeza upana wa tabasamu lake.
**
Akiwa anakula chakula cha mchana ndani ya mgahawa mdogo jijini Hongkong, mara akaona askari wawili wakiingia ndani ya mgahawa huo. Mmoja wao alikuwa mrefu, kijana, mwenye nguvu, na wa pili alikuwa mzee kidogo, kofia yake alikuwa ameishikilia mkononi hivyo mvi na uso wake uliochoka ulionekana vema.
Walinyookea kaunta, wakaskizwa na kisha wakaketi kwa mbali kidogo.
Wakiwa wanafanya yote haya, Lee alikuwa anawatazama chini ya kofia yake 'kapelo' kwa macho ya kuibiaibia.
Alikuwa anafahamu anatafutwa na hata huko kwenye vyombo vya habari wamekuwa wakimrusha akihusishwa na kifo cha Chong Pyong, mpiga gitaa maarufu jijini.
Sasa anaishi kama ndege. Na hata juhudi za kujikomboa kurudi alipotoka zinakuwa ngumu zaidi kwani huko viwanja vya ndege watamtambua na kumweka chini ya ulinzi.
Basi akaendelea kula, na kwa macho ya kuibia akaendelea kuwatazama wale askari ambao nao muda si mrefu wakaletewa chakula na kuanza kushibisha matumbo wakipiga soga za hapa na pale.
Akiwa anaelekea kumaliza chakula, mhudumu akaja. Alikuwa ni mama mtu mzima anayejitahidi kujiweka vema. Alikuwa amemletea bili yake ya chakula.
Akaipokea na kuitazama, kisha akatoa pesa mfukoni na kuiweka mezani. Hakutaka hata kumtazama yule mhudumu usoni.
Mhudumu akakusanya pesa yake na kushukuru. Akaenda zake. Ila akiwa na shaka juu ya Lee. Kwanini alikuwa ana-behave namna ile? Kwa utaratibu wa kichina, si adabu, haswa ukifanya vivyo kwa mtu mzima.
Basi yule mhudumu, pasi na kujenga hoja ya kumhisi Lee, akaenda kusema kule kaunta na jikoni namna vijana wanavyobadilika siku za karibuni. Na pasipo kujua basi akaalika macho zaidi kwa Lee. Wakamtazama. Ila hawakujali sana.
Ilipopita dakika tatu, ndipo kidogo mambo yakaanza kubadilika. Televisheni iliyokuwa imepachikwa ukutani kwa ajili ya kusogezea muda wateja na kuwavutia kwenye eneo hilo dogo, ikarusha matangazo ya kutafutwa kwa Bwana Lee!
Picha yake ambazo zilikuwa zimedakwa na CCTV nazo zikarushwa, ila napo haikujalisha sana, ni watu wawili ambao walikuwa wamekaa karibu na wale askari ndiyo waliupokea ujumbe huo wa televisheni na kuanza kuujadili.
Wale askari nao wakaungana nao, wakawa wanne. Na kwasababu eneo hili halikuwa kubwa, basi kila mtu ndani ya mgahawa alisikia vema kilichokuwa kinazungumzwa, akiwamo Lee.
Napo haikujalisha sana, ila tabu halisi ikaanzia pale ambapo yule mhudumu aliyeenda kuchukua pesa toka kwa Lee kugundua kwa namna moja yule mtu aliyetangazwa kideoni anafanana na Lee!
Si kwa sura, la! Bali vazi. Lee alikuwa amebadili mavazi yake yote isipokuwa shati lake la ndani ambalo kwa juu alilifunika na koti ambalo hakulifunga zipu.
Sasa yule mhudumu akaunga taarifa kichwani kwake. Huenda yule kijana amejifunika uso na hataki kutazama watu maana anahofia kugundulika.
Hakumwambia mwenzake yoyote, taratibu akaenda kwa wale askari, kisha akawatonya akielekezea macho kwa Lee. Lee akagundua hilo.
Askari wote walitazama upande wake, pamoja na yule mhudumu.
Akasimama upesi! Kisha akageuka kuuendea mlango kwa kasi. Huku nyuma akasikia sauti ikipaza kwanguvu, ikimwamuru asimame. Hakutii. Akazidi kunyoosha mguu. Akakimbia!
Wale askari wakatoka nje na kuangaza. Kushoto ... kulia ... kushoto ... wakamwona yule kwa mbali! Yule askari kijana akachomoa filimbi na kuipuliza kwanguvu akimkimbilia Lee.
Akipiga kelele asimame! Asimame!
Lee akakimbia kwa kasi sana. Na baada ya punde fupi, akajibana sehemu, kwenye kuta ndogo ya kauchochoro, hapo akabana mpaka na pumzi asisikike.
Baada ya dakika moja, yule askari akawa amefika eneo hilo. Alikuwa anatembea, anahema kwanguvu, macho yake yanaruka huku na kule kuangaza na kupekua watu.
Alitilia shaka kiuchochoro, akatupia macho huko, hakuona mtu. Ila kabla hajapita, mara simu ya Lee ikaita mfukoni! Askari akashtuka na kuangaza. Moja kwa moja akahisi mtuhumiwa wake atakuwapo hapo.
Akajongea akiwa ameshikilia kipochi kidogo cha ngozi kiunoni mwake kilichobebelea bunduki ndogo.
Alipopiga hatua ya nne, Lee akamuwahi! Hafla! Akampiga ngumi tatu za haraka, askari akapoteza nguvu! Akamchomolea bunduki, na kunyofoa risasi zote kisha akamwachia kasha tupu akiondoka zake kwa mwendo wa wastani.
Askari akabaki chini akilalama kwa maumivu.
Lee aliposonga kwa mbali kidogo, akatazama simu yake. Akagundua ni Sheng ndiye alikuwa anampigia. Akastaajabu imewezekanaje? Amepata wapi mawasiliano yake? - ina maana ameshafahamu yuko China?
Simu ikaita tena. Akasita kupokea. Akajiuliza kwa kama sekunde nne, akakata shauri na kupokea.
Swali la kwanza, unafanya nini China? Na la pili, kwanini umemuua Chong Pyong?
Kumbe Sheng alishafahamishwa habari za kutafutwa kwa Lee. Habari zake ambazo zimezagaa ndani ya Hongkong zilishafika mpaka makao ya Wu family, nao wakamjuza Sheng kumhusu mtu wao.
Sasa Lee akawa njia panda. Mosi, hakuaga. Pili, atasema anafanya nini huko Hongkong? Kufuatilia nyaraka ya Sheng iliyopotea??
Akajikaza na kulaghai. Akasema amekuja China kusalimia na kujizoeza na mazingira. Ila bwana Sheng hakujali sana hiyo sababu wala hakumpeleleza zaidi, akamwambia kuna kazi anataka kumpatia.
Na kwakuwa yupo huko China, anaamini ataifanya vema.
**
*Simulizi za series*
ILIPOISHIA
Habari hizi zikamfurahisha sana Marwa. Akatabasamu mpaka gegoni. Ila BC akamwonya. Akamkumbusha yale makubaliano ya awali waliyoyaweka.
Atampatia Jona antidote, ila wataandikishiana makubaliano. Na atakuwa akitoa kidogo kidogo akitazama kama makubaliano yake yataheshimiwa.
ENDELEA
Marwa angelisema nini? Hakuwa na la kusema zaidi ya kuafiki kile ambacho BC alikuwa anamwambia japo ndani ya moyo wake alijawa na hofu. Hakuwa anamwamini kabisa Jona. Alihofia anaweza kiuka vifungu hivyo na kuleta tafrani.
Misukosuko waliyopitia inatosha. Pengine Jona anaweza akalitambua hilo, alijipa moyo. Basi baada ya muda mfupi BC akaaga na wakaondoka pamoja na Marwa kwa makubaliano kwamba aende kumpatia antidote.
Walipofika nyumbani kwa BC mwanaume huyo akazama maabara na kufanya kile anachokijua zaidi. Ikamchukua kama robo saa akatoka akiwa amebebelea kemikali ndani ya chupa maalum ya kioo. Akamkabidhi Marwa na kumpa maelekezo.
Marwa hakupoteza muda, akamuaga na kwenda zake BC akimsisitizia kuwa makini na chupa hiyo iliyobebelea antidote.
Alipowasili nyumbani, akampatia Jona kiasi alichoelekezwa kisha akajikuta sebuleni pamoja na Miranda.
Aliketi akiwa ana mawazo kichwani. Miranda alimtazama na kisha kumuuliza, "Marwa, kuna tatizo?"
Marwa akatikisa kichwa akiminya lips. Hakusema kitu. Miranda akamtazama na kisha akamjongea akiachana na kutazama televisheni.
Akamwambia, "Najua unachowaza."
Marwa akamtazama. Bado hakusema kitu.
"Hata mimi kinanipa hofu kama wewe. Ila natumai kila kitu kitakuwa fresh. Usiwaze sana."
Marwa akamuuliza, "una uhakika?"
Akajibu, "Hata kama sina uhakika, ila ya nini kufikiria yajayo ambayo bado hayajafika? Don't worry ..." akamshika Marwa bega. "Kama tumepita kule kwenye bonde la mauti, tutashindwa hapa?"
Marwa akashusha pumzi. Akauliza, "ila vipi kama Jona hataridhia? BC atammaliza?"
Miranda akatulia kwanza akiwaza. Kwa kama sekunde tano, akasema, "pengine hiyo inaweza ikawa kazi kubwa kuliko zote tulizozifanya.."
Miranda akashusha pumzi. "Endapo kama Jona akikataa, tutakuwa njia panda. Tuna kazi ya kumshawishi. Na naamini inawezekana ... yah! Inawezekana."
Miranda akatabasamu. Naye Marwa akatabasamu.
"Leo jioni tutatoka out for a dinner. Angalau tukatefresh minds na kujipongeza. Au unasemaje?" Miranda alichombeza. Marwa akajibu kwa kuongeza upana wa tabasamu lake.
**
Akiwa anakula chakula cha mchana ndani ya mgahawa mdogo jijini Hongkong, mara akaona askari wawili wakiingia ndani ya mgahawa huo. Mmoja wao alikuwa mrefu, kijana, mwenye nguvu, na wa pili alikuwa mzee kidogo, kofia yake alikuwa ameishikilia mkononi hivyo mvi na uso wake uliochoka ulionekana vema.
Walinyookea kaunta, wakaskizwa na kisha wakaketi kwa mbali kidogo.
Wakiwa wanafanya yote haya, Lee alikuwa anawatazama chini ya kofia yake 'kapelo' kwa macho ya kuibiaibia.
Alikuwa anafahamu anatafutwa na hata huko kwenye vyombo vya habari wamekuwa wakimrusha akihusishwa na kifo cha Chong Pyong, mpiga gitaa maarufu jijini.
Sasa anaishi kama ndege. Na hata juhudi za kujikomboa kurudi alipotoka zinakuwa ngumu zaidi kwani huko viwanja vya ndege watamtambua na kumweka chini ya ulinzi.
Basi akaendelea kula, na kwa macho ya kuibia akaendelea kuwatazama wale askari ambao nao muda si mrefu wakaletewa chakula na kuanza kushibisha matumbo wakipiga soga za hapa na pale.
Akiwa anaelekea kumaliza chakula, mhudumu akaja. Alikuwa ni mama mtu mzima anayejitahidi kujiweka vema. Alikuwa amemletea bili yake ya chakula.
Akaipokea na kuitazama, kisha akatoa pesa mfukoni na kuiweka mezani. Hakutaka hata kumtazama yule mhudumu usoni.
Mhudumu akakusanya pesa yake na kushukuru. Akaenda zake. Ila akiwa na shaka juu ya Lee. Kwanini alikuwa ana-behave namna ile? Kwa utaratibu wa kichina, si adabu, haswa ukifanya vivyo kwa mtu mzima.
Basi yule mhudumu, pasi na kujenga hoja ya kumhisi Lee, akaenda kusema kule kaunta na jikoni namna vijana wanavyobadilika siku za karibuni. Na pasipo kujua basi akaalika macho zaidi kwa Lee. Wakamtazama. Ila hawakujali sana.
Ilipopita dakika tatu, ndipo kidogo mambo yakaanza kubadilika. Televisheni iliyokuwa imepachikwa ukutani kwa ajili ya kusogezea muda wateja na kuwavutia kwenye eneo hilo dogo, ikarusha matangazo ya kutafutwa kwa Bwana Lee!
Picha yake ambazo zilikuwa zimedakwa na CCTV nazo zikarushwa, ila napo haikujalisha sana, ni watu wawili ambao walikuwa wamekaa karibu na wale askari ndiyo waliupokea ujumbe huo wa televisheni na kuanza kuujadili.
Wale askari nao wakaungana nao, wakawa wanne. Na kwasababu eneo hili halikuwa kubwa, basi kila mtu ndani ya mgahawa alisikia vema kilichokuwa kinazungumzwa, akiwamo Lee.
Napo haikujalisha sana, ila tabu halisi ikaanzia pale ambapo yule mhudumu aliyeenda kuchukua pesa toka kwa Lee kugundua kwa namna moja yule mtu aliyetangazwa kideoni anafanana na Lee!
Si kwa sura, la! Bali vazi. Lee alikuwa amebadili mavazi yake yote isipokuwa shati lake la ndani ambalo kwa juu alilifunika na koti ambalo hakulifunga zipu.
Sasa yule mhudumu akaunga taarifa kichwani kwake. Huenda yule kijana amejifunika uso na hataki kutazama watu maana anahofia kugundulika.
Hakumwambia mwenzake yoyote, taratibu akaenda kwa wale askari, kisha akawatonya akielekezea macho kwa Lee. Lee akagundua hilo.
Askari wote walitazama upande wake, pamoja na yule mhudumu.
Akasimama upesi! Kisha akageuka kuuendea mlango kwa kasi. Huku nyuma akasikia sauti ikipaza kwanguvu, ikimwamuru asimame. Hakutii. Akazidi kunyoosha mguu. Akakimbia!
Wale askari wakatoka nje na kuangaza. Kushoto ... kulia ... kushoto ... wakamwona yule kwa mbali! Yule askari kijana akachomoa filimbi na kuipuliza kwanguvu akimkimbilia Lee.
Akipiga kelele asimame! Asimame!
Lee akakimbia kwa kasi sana. Na baada ya punde fupi, akajibana sehemu, kwenye kuta ndogo ya kauchochoro, hapo akabana mpaka na pumzi asisikike.
Baada ya dakika moja, yule askari akawa amefika eneo hilo. Alikuwa anatembea, anahema kwanguvu, macho yake yanaruka huku na kule kuangaza na kupekua watu.
Alitilia shaka kiuchochoro, akatupia macho huko, hakuona mtu. Ila kabla hajapita, mara simu ya Lee ikaita mfukoni! Askari akashtuka na kuangaza. Moja kwa moja akahisi mtuhumiwa wake atakuwapo hapo.
Akajongea akiwa ameshikilia kipochi kidogo cha ngozi kiunoni mwake kilichobebelea bunduki ndogo.
Alipopiga hatua ya nne, Lee akamuwahi! Hafla! Akampiga ngumi tatu za haraka, askari akapoteza nguvu! Akamchomolea bunduki, na kunyofoa risasi zote kisha akamwachia kasha tupu akiondoka zake kwa mwendo wa wastani.
Askari akabaki chini akilalama kwa maumivu.
Lee aliposonga kwa mbali kidogo, akatazama simu yake. Akagundua ni Sheng ndiye alikuwa anampigia. Akastaajabu imewezekanaje? Amepata wapi mawasiliano yake? - ina maana ameshafahamu yuko China?
Simu ikaita tena. Akasita kupokea. Akajiuliza kwa kama sekunde nne, akakata shauri na kupokea.
Swali la kwanza, unafanya nini China? Na la pili, kwanini umemuua Chong Pyong?
Kumbe Sheng alishafahamishwa habari za kutafutwa kwa Lee. Habari zake ambazo zimezagaa ndani ya Hongkong zilishafika mpaka makao ya Wu family, nao wakamjuza Sheng kumhusu mtu wao.
Sasa Lee akawa njia panda. Mosi, hakuaga. Pili, atasema anafanya nini huko Hongkong? Kufuatilia nyaraka ya Sheng iliyopotea??
Akajikaza na kulaghai. Akasema amekuja China kusalimia na kujizoeza na mazingira. Ila bwana Sheng hakujali sana hiyo sababu wala hakumpeleleza zaidi, akamwambia kuna kazi anataka kumpatia.
Na kwakuwa yupo huko China, anaamini ataifanya vema.
**