Anga la washenzi na Joana anaona kitu usiku

Kipngozi utalatibu wakuunganishwa whatsapp ukoje
 
*ANGA LA WASHENZI II -- 42*

*Simulizi za series*


ILIPOISHIA

Basi Kinoo akaridhia, ataenda kuonana na BC kesho asubuhi na mapema. Ila akamuuliza Miranda, vipi kuhusu bwana yule, Jona? Wapi alipo na anaendeleaje?

ENDELEA

Katika namna ya ajabu, Miranda akasita kumweleza Kinoo juu ya maswali hayo. Akamtaka aende akajiandae na yeye aende zake maana kuna eneo anapitia.

Kinoo akashuka toka garini na kisha akasimama akishuhudia gari la binti huyo likitokomea.

Ila kuna jambo lilimjia kichwani. Ni kama radi jambo hilo lilikuja upesi. Akawaza namna ambavyo Miranda amekuwa kama mtu wa 'kumtenga' siku hizi.

Amekuwa si wa kumshirikisha na wala kumhitaji kama ilivyokuwa huko nyuma. Kwa namna moja ama nyingine alipata wivu wa kiume. Aliona kama vile Jona na mwenzake Marwa wametenganisha familia yake.

Nafasi yake imezibwa na hao watu.

Akawaza.

Kama hali ipo hivyo na huyo Jona bado yupo kitandani, vipi akiamka na kurejea kwenye hali yake? Atakuwa na nafasi hata robo?

Alihofia.

Aliwaza akiwa anatembea kurejea nyumbani kwake. Alipofika ndipo mawazo hayo yakaenda zake na kuacha nafasi ya kuwaza mengine. Ya mkewe.

Hakuwa amemkuta hapo nyumbani na hakuwa anajua wapi kaenda. Akalalama yaani kutoka kidogo tu naye keshafungua mlango!

"Mwanamke huyu!" Akatikisa kichwa. Akanyakua simu na kumpigia. Nayo ikaita mara tatu pasipo majibu. Akasonya na kujiongelesha mwenyewe.

"Sijui nimfanye nini. Na hivi ana ujauzito, basi keshapata sababu haswa!"

Akalalama na kulalama. Hata kama angelitukana isingelisaidia kwani mtuhumiwa hakuwapo wala hakuwa anasikia, wala kujali.

**

"Kama nilivyokuambia, kumbe yule muuaji alikuwapo huko," alisema Sasha kisha akashushia na juisi. Akamtazama dada yake, Sarah, na kuendelea kumwambia,

"Wewe umekaa siku zote hizo, umekalia pesa dada yangu. Ina maana hujui kama donge nono lilitangazwa kwa mtu atakayetoa taarifa zitazosaidia upatikanaji wake?"

Sarah akapandisha mabega akisema hana habari kabisa. Na hata kama angelikuwa na habari asingelifanya lolote kwani hakuwa anajua kama wakina Kinoo wamemuhifadhi jamaa huyo.

Basi Sarah akaendelea kumpasha habari. Akamwambia taarifa zake zilishafika polisi na hata walipoenda kumsaka, hawakumwona, tayari wameshamuamisha!

"Sasa dada yangu, nataka tupige hela kama wehu! Najua wewe utakuwa unajua wapi alipo. Tumbua basi tupige hizo milioni kisha twende zetu Ibiza huko mbali na ulimwengu."

Sarah akatikisa kichwa. Akatazama kinywaji chake mezani, juisi ya embe, ambayo haikuwa imeguswa kabisa, kisha akasema:

"Sasha, sijui niwe nakuambia vipi? Mimi sijui kabisa. Sijuuui kwa herufi kubwa!"

Sasha akatikisa kichwa chake na kuminya mdomo.

"Yani wewe unakuwa kama sio dada yangu yani. Mbona unakuwa zoba zoba wewe bana! Unashindwaje kujua na wakati unaishi na yule mwanaume?"

"Sasha!" Sarah akaita kwa tahadhari. "Nakuapia kwa Mungu wangu, yule mwanaume muda si mrefu atahisi huu mchezo tunaoufanya. Kabisa nakwambia. Ndipo anapoelekea."

Sasha akapeleka mdomo wake pembeni. "Uoga wako tu huo! Unadhani atakufanya nini na umebeba mimba yake? ... hana ujanja wowote."

Sarah hakusema kitu. Akajaribu kunywa kinywaji chake ila hakikupanda. Alipokunywa fundo moja tu, akarejesha glasi chini. Akasema,

"Naomba niende."

"Nimekuudhi?" Sasha akajishuku.

"Hapana," Sarah akajibu. "Naona tu muda umeenda. Nahisi yule bwana atakuwa amerejea nyumbani isije kuwa nongwa bure."

"Ok!" Sasha akasema na kisha akanywa fundo za nguvu kumalizia juisi yake mezani, alafu akanyanyuka.

"Twende nikusindikize."

Akampeleka Sasha hatua kadhaa akiendelea kumshawishi afanye kazi yake ya kupeleleza alipo Jona. Sarah akaahidi kulifanyia kazi, ila si kwa haraka hivyo. Akajikweza kwenye gari na kuondoka zake.

Sasha akatoa simu yake ya mkononi na kupiga. Akaongea na huyo wa kuongea naye kwenye simu ya kwamba ameshapiga hatua moja. Wavute subira kuona matokeo yake, kisha akakata simu.

**

Kesho yake, majira ya saa nne, central ...

"Nimekuja kuonana na mfanyakazi mwenzangu," alisema Kinoo akimtazama askari machoni pasi na woga. Askari akamtazama kwa jicho la uchovu wa kebehi na kumuuliza,

"Nani huyo mfanyakazi mwenzako?"

"Yule mzungu aliy ..."

"Yule jambazi!" Askari akaropoka.

"Hapana, si jambazi," Kinoo akamtetea.

"Ni nani basi?" Askari akauliza. "Mtu anayemficha jambazi ni nani kama sio na yeye ni jambazi?"

"Afande, hakuwa amemficha yeyote. Sidhani kama mtu huyo mnayemwongelea alionekana kwenye jengo lake baada ya msako mlioufanya."

"Kijana," askari akamnyooshea kidole Kinoo. "Usitufundishe kazi, sawa?"

Kinoo kimya.

"Sawaa? ... kwanza nenda zako kabla sijakuweka ndani na wewe. Wewe mwenyewe unaonekana jambaka tu. Ebu nenda bwana! ... Nenda, husikii!?"

Kinoo akashusha pumzi na kisha akageuka aende zake. Akatwaa simu mfukoni na kumpigia Miranda.

"Wamenikatalia kuonana naye."

"Kwanini?"

"Sijajua."

"It's ok. Naona wameamua hivyo. Na itakuwa ni agizo wanatekeleza. Sasa achana nao, tutafanya njia nyingine."

"Ipi hiyo?" Kinoo akatazama nyuma yake kisha akarudisha macho mbele. "Usinambie ni kama ile tuliyofanya mara ya kwanza? Kwa sasa haitawezekana. Ulinzi umekuwa mkali kupita kiasi!"

"Hapana, si njia hiyo bali nyingine ya kidiplomasia zaidi. Anyways, tutaongea baadae."

Miranda akakata simu.

**

Simu ya mezani ya bwana Sheng iliita, akainyofoa toka kwenye kitako chake na kuiweka sikioni. Alikuwa ni kamanda akimpigia majira haya ya jioni.

"Mkuu, naomba mambo yataenda kombo," alisema Kamanda simuni.

"Una maanisha nini?" Sheng akauliza akikunja ndita.

"Naona hili swala la bwana Brown litatoka nje ya mikono yangu."

"Kivipi?"

"Mahakama imeamuru aachiliwe. Amekamatwa kinyume na taratibu!"

"You can't be serious!"

"Sure! Na si hivyo tu, hata waziri wa sekta hii amenipigia simu na kuniagiza nitende kama nilivyoambiwa maana hili swala limeanza kuvuta hisia za kimataifa, haswa Uingereza juu ya namna raia wake alivyokuwa treated offensively!"

Sheng akashusha pumzi, kisha akauliza, "na vipi kuhusu zile kemikali? Hauwezi ukapata chochote huko?"

"Hamna kitu. Hata tukipeleka mahakamani, hatutashinda. Tutashindwa kutetea hoja zetu na mwishowe itaonekana kuna dhamira binafsi katika hili!"

Sheng akakosa cha kunena. Akiwa anatetemeka mkono akapachika simu yake ya mezani kwenye kitako chake na kisha akalaza kichwa kochini akiwaza.

Alihisi kuchanganyikiwa.

**

Saa mbili usiku ...

Bwana Henry Marshall alimfikisha BC nyumbani kwake alafu akaingia ndani na kuteta kidogo kuhusu swala lake, akimtoa hofu kabisa kwani kila kitu kipo sawa mikononi mwake.

BC akamshukuru sana, na akamtakia usiku mwema akapumzike maana amefanya kazi nzito siku hiyo. Bwana huyo akaenda zake.

BC akaenda kukoga na kisha akavaa vema. Akafungua jokofu lake la kuteua chupa moja ya kinywaji. Alikuwa ana kiu nacho haswa. Akafungua na kunywa kwa mtindo wa tarumbeta mpaka pale alipobakiza robo chupa ndiyo akaenda nayo mezani.

Akanywa taratibu akitafakari. Akawaza lile tukio la yeye kukamatwa, na akakubaliana na akili yake kuwa tayari wakina Sheng watakuwa wanafahamu kuwa Jona yupo mikononi mwake.

Hii ilikuwa ni vita. Na yeye kuachiwa huru na polisi si kwamba ndiyo ilikuwa imekoma, bali ndiyo inaanza.

Amejipangaje kupambana? Alikuna kichwa chake. Lazima Sheng atakuja na njia nyingine baada ya hii. Itamgharimu kiasi gani kumsimamisha Jona asimame mwenyewe?

Alikuwa amechoka sana. Hata hakuwaza vema, akamalizia kinywaji chake na kwenda kulala. Kesho yake asubuhi na mapema akamwita Miranda aje nyumbani.

Ila alipokata simu hiyo, akapewa taarifa kuwa bwana Henry Marshall amefariki dunia.

**

Sent from my SM-J110F using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…