*ANGA LA WASHENZI II -- 43*
*Simulizi za series*
ILIPOISHIA
Ila alipokata simu hiyo, akapewa taarifa kuwa bwana Henry Marshall amefariki dunia.
ENDELEA
Jambo hili likageuza maisha yake haraka, juu chini chini juu! Hata akasimama apate kuzisikia vema. Hakuamini kabisa. Na hata huyo mtu aliyempa taarifa akamwona mwehu.
Akakata simu. Ila punde kidogo ndipo akagundua kuwa jambo hilo ni kweli baada ya kumpigia simu Henry Marshall na kuita pasipo majibu, alafu akaona mtandaoni habari za mwanasheria wake.
Ajabu iliyoje hii! Alihisi mwili mzima umekuwa wa baridiii, ila kichwa kinawaka moto haswa!
Gari la Henry lilikuwa zima kabisa, isipokuwa kioo tu cha mbele ndicho kilipasuliwa na risasi zilizomwagwa kama njugu kumpasua na kumtoboa Bwana Henry, akalala pasipo msaada.
Suti yake imefyonza damu mpaka ikashiba na kuchuruza nyinginezo. Uso wake umeshindiliwa risasi tatu hivyo kufanya ugumu kidogo kutambulika!
Hakika hizi zilikuwa habari mbaya sana kwa Bwana Brown. Hakuwahi kupata habari hizi hapa karibuni isipokuwa hii. Alijikuta anapata hasira sana. Tena sana, hata akahisi hataweza kuendesha gari.
Akamwita kijakazi wake na kumpatia funguo ampeleke eneo la tukio.
Alipofika huko akakuta gari la bwana Henry likiwa linakusanywa na gari 'breakdowns' na mwili wake ushapelekwa hospitali.
Akawasiliana na baadhi ya watu wake na wakaliongelea jambo hilo kwa kukubaliana kupeleka maiti nchini Uingereza ikazikiwe huko.
Na wakakubaliana baadae majira ya usiku wakutane wapate kuteta jambo.
**
Baadae majira ya saa nne usiku, nyumbani kwa Brown Curtis.
Wanaume watatu walikuwa wamekalia sebuleni. Wawili walikuwa ni sura ngeni machoni na mmoja wao alikuwa ni Brown Curtis (BC). Wote walikuwa wamevalia suti nyeusi, si muda mrefu walikuwa wametoka kwenye makazi ya muda ya marehemu bwana Henry Marshall.
Wanaume hawa wageni inakuwa vema na rahisi kuwatofautisha kwa rangi za nywele zao. Mmoja nywele zake zilikuwa nyeusi ti, aitwa McKnight na mwingine alikuwa na nywele 'blonde', aitwa Woodman.
Pengine majina yao si ya muhimu sana maana hatutahangaika nayo sana katika simulizi hii, ila kwa hapa wana umuhimu fulani.
Basi wakiwa wanateta hapo, BC akionekana waziwazi kuwa ana hasira na anajua fika aliyetenda jambo hilo la kidhalimu, akasema anahitaji watu kadhaa wa 'kazi'.
Na watu hao waagizwe toka Uingereza mara moja pasipo kupoteza muda hata punje!
Ila mabwana wale wakawa wastaarabu kidogo, "slow down, Brown," alisema yule mwenye nywele nyeusi. "Our government will respond on this, we don't need to rush in!"
Brown akatikisa kichwa. "No! It is enough. I am done with this and now my patience is gone! I want to end things immediately! Enough is enough!"
Hakutaka kusikia wala kungoja namna Uingereza itakavyochukua hatua. Alitaka hatua achukue mwenyewe mkononi.
Siku zote hakuwa mtu aliyekuwa amepanga wala kudhamiria kummaliza Sheng. Ila kwa sasa hilo ndilo litakuwa lengo lake la kwanza kabisa!
Sheng aende kaburini!
Basi mabwana wale wengine wawili, kwa kuona sikio hili lilikuwa la kufa, wakaafikiana naye na kumwahidi kumuunga mkono. Watatimiza kile bwana huyo anataka.
***
Kesho, saa sita mchana.
Hodi ilibishwa na kabla Sheng hajatia neno akastaajabu mlango unafunguliwa, anazama Kamanda mkuu!
Uso wake haukuwa katika pumziko. Mweusi kuliko kawaida. Alikuwa amevalia nguo za kiraia, shati ya kitenge na suruali nyeusi ya kitambaa, na kichwa chake akikihifadhi ndani ya kofia 'cowboy' rangi ya kahawia.
Akaketi na kumuuliza Sheng, "ni nini umefanya?"
Sheng akatabasamu, alafu akajisukuma na kiti kwenda mpaka ukutani. Akaweka viganja vyake tumboni na kumtazama Kamanda kana kwamba mama wa kambo anavyomtazama mtoto wa mumewe akiwa anaongopa.
Akauliza, "kwani kuna nini Kamanda?"
"Sheng!" Kamanda akatahamaki. "Ina maana hujui ulichokifanya? Kulikuwa kuna haja gani ya kummaliza yule mwanasheria?"
Kimya kidogo.
" ... na nilishakwambia Sheng. Nilishakwambia. Waziri aliniambia hili jambo linaweza kuleta utata sana na serikali ya Uingereza. Tuachane nalo tu, tuangazie namna zingine. Hujataka kunisikia kabisaaaa, ndugu!
Huoni umeiingiza serikali yetu matatani. Dunia nzima watalichukuliaje hili tukio? Si wataona Bwana Henry kauawa na serikali! Na mimi nikiambiwa nipeleleze huoni nitaingia matatizoni!"
Sheng akashusha pumzi ndefu puani kisha akarembua macho na kuyakodoa.
"Kamanda, dharau kwangu zina mipaka," akasema kwa sauti ya wastani. "Zile zilikuwa ni dharau. Kuna muda a king has to remind fools that he is a king!"
Kamanda akasikitika sana. Akakunja ndita na kumweleza bwana Sheng,
"Umekosea sana na uniweka kwenye wakati mgumu mno. Bila shaka mimi na wewe tumemalizana, hatudaiani. Kwa hivyo, naomba kila mtu sasa ashunghulike na mambo yake. Pesa zako zinanuka, Sheng!"
Kamanda akasimama kwa kiburi. Akafungua mlango na kwenda zake. Sheng akatabasamu, kisha akacheka.
Ikapita dakika tatu, mlango ukagongwa tena. Na kama ilivyokuwa awali, kabla Sheng hajasema kitu, mlango ukafunguliwa. Akajiuliza kuna nini leo?
Kutazama akamwona Shao.
Bwana huyo aliketi pasipo kusalimu. Akakunja nne akimtazama Sheng na kisha akamuuliza,
"Ni wewe ndiye uliyewaita polisi kwa bwana yule?" Aliongea kiswahili kilichonyooka. Bila shaka alifanyia mazoezi maswali haya kwa msaada wa wale watu wake.
"Unasema nini wewe?" Sheng akauliza.
"Unajua ninachokiongelea, Sheng. Unajua kila kitu, na nashangazwa nia yako ni nini?"
Wakatazamana kwa sekunde mbili.
"Shao, kama umeshindwa kazi yako, usitafute mlango wa kutokea, sawa?"
"Sijashindwa," Shao akasema kwa kujiamini. "Ila wewe unataka nishindwe. Nimeligundua hilo. Sijajua utafaidika na nini katika hili. But its ok. Kama unataka kunimaliza, nimekuja. Niue."
Sheng akatabasamu. Akatikisa kichwa chake mara mbili alafu akamtazama Shao.
"Sina shida ya kukuua. Na kama nitakuua basi ni kwa mujibu wa makubaliano tuliyoweka mimi na wewe. Si vinginevyo, Shao ... kama hutojali, naomba unipishe nina kazi nyingi za kufanya."
Kabla Shao hajaamka toka kitini akamtazama kwanza Sheng na macho yanayoongea husda, kisha akanyanyuka na kwenda zake.
**
Baadae, majira ya saa tano usiku..
Kwa umbali wa kama hatua nane hivi za mtu mzima, kuna mtu alikuwa amejificha hapo akitazama mlango wa ofisi ya Sheng.
Kuna kitu alikuwa anakingoja hapo. Na ni kama muda ulikuwa unasogea kuendea hilo tukio.
Mazingira yalikuwa kimya haswa.
Zikapita dakika tano, mara mlango wa ofisi ya Sheng ukafunguliwa akatoka mwanaume mmoja aliyekuwa amevalia nguo nyeusi.
Mwanaume huyu alikuwa ndiye yule. Bila shaka unamkumbuka. Miongoni mwa wale 'vijakazi' kumi wa bwana Shao.
Mwanaume huyo alitazama huku na kule, kule na kule kisha akashika njia kujiendea. Ila hakuwa anajua kuwa leo zilikuwa zimetimia zile arobaini zake.
Akiwa anatembea, hana hili wala lile, akajikuta amedakwa shingo. Kabla hajashangaa, akatenguliwa kuvunjwa!
Akadondoka chini mfu.
Aliyemuua akamtemea mate na kusema, "tangulia kuzimu sisi twaja."
Kisha akaenda zake.
Baada ya dakika kadhaa, maiti hiyo ikagundulikana na taarif akafikishiwa Sheng.
***
Sent from my SM-J110F using
JamiiForums mobile app