Anga la washenzi na Joana anaona kitu usiku

Anga la washenzi na Joana anaona kitu usiku

*ANGA LA WASHENZI II -- 49*

*Simulizi za series*


ILIPOISHIA

“mzigo wako nimetumwa kukuletea."

Sarah alipoupokea, mwanaume huyo hakukaa, akaenda zake. Sarah akaketi kitini na kufungua mzigo huo.

ENDELEA

Akakuta boksi kubwa jeupe. Akalifungua na ndani akakuta rundo kubwa la pesa zilizo katika mfumo wa dola za kimarekani. Akatabasamu, na mwishowe akaangua kabisa kicheko.

Alifurahi mno kuona pesa hizo. Alihisi moyo wake unamwenda mbio, haraka akanyanyuka na kuzipeleka chumbani. Akajifungia huko, na kuhesabu kibunda kimoja baada ya kingine.

Hakuwa anajua ni kiasi gani cha pesa hicho ila alifahamu ni pesa nyingi. Nyingi za kuweza kutia mtu kiburi. Ila akiwa anatazama pesa hizo, akaona na kipande cha kikaratasi.

Haraka akakichomoa na kukisoma maana kilikuwa na ujumbe.

‘Habari yako ilikuwa ya kweli, ila hatujafanikiwa kumpata mlengwa. Tunatumai utakuwa na taarifa zaidi. Kila taarifa itakuwa na thamani ya pesa hizi.' Baada ya maelezo hayo, ikaandikwa namba ya simu kwa chini. Namba mbili.

Basi Sarah akajikuta anataka pesa zaidi. Alitamani Kinoo arejee nyumbani upesi ampashe habari hizi na kumtia hamasa.

Ila wakati huu anamngoja mumewe, acha sisi tujifikirishe kidogo. Mtu huyu aliyemletea hizi pesa ametumwa na nani? Bila shaka ni Sheng. Na mwanaume huyo tayari ameshapokea taarifa za kuuawa na kutupwa kwa vijakazi wake huko mtoni.

Na hata zaidi ameshatambua kuwa taarifa hizo za Jona na Miranda zimetoka kwa nani kwa kupitia Sasha. Bwana huyu anajua atapata zaidi mambo ya Jona kwa kumtumia mwanaume huyu.

Na mara hii akipata taarifa, ataingia mwenyewe uwanjani kucheza mziki ambao vijana wamefeli.

Simu ikaita. Sarah akapokea baada ya kuitazama kiooni na kujua ni ya dada yake, Sasha.

“Hallow!"

“mambo?" Sauti ya Sasha ilisikika vizuri kwenye simu.

“fresh. Vipi wewe?"

“niko poa. Vipi upo mahali salama?"

“yah! Niko fresh."

“jamaa yupo wapi?"

“ametoka kidogo. Ila nadhani anakaribia kuja."

“vipi umepokea mzigo wowote?"

“yah! Nimepokea eenh!"

“poa. Nitakutafuta baadae au kesho. Uwe karibu na simu yako, sawa?"

“Poa!"

Simu ikakata.

**

Majira ya saa mbili kasoro usiku ... Mahali fulani tulivu ...

“Kwahiyo sasa mtafanyaje?" Aliuliza Kinoo. “maana maisha yenu yamekuwa kama swala."

Miranda akashusha pumzi ndefu, alafu akanywa kinywaji chake ndani ya glasi, juisi ya dhabibu, kisha akasema;

“Tutazama kipi cha kufanya. Jona anarejea wa kasi kwenye hali yake na nadhani njia nyepesi sasa ya kuwa salama ni kwa kum-face adui yetu badala ya kumkimbia."

Akanywa kwanza kinywaji kisha akaendelea na maneno, “kadiri tunavyokimbia ndivyo anavyozidi kutuwinda. Hakuna mahali tutakayokuwa salama. Ila kwa sasa hatutaweza kwenda kukabiliana naye.

Nadhani tunahitaji siku kama tatu au nne hivi za kujipanga na Jona kuwa sawia kabisa."

“sasa kwa muda wa hizo siku, mtakuwa mnakaa wapi?" Kinoo akauliza.

“hatuwezi tukapata mahali pa kudumu. Tutajiegesha hotelini kwa siku hizo. Ntakupa habari ni wapi tutakapokuwa punde tu ntakapopapata."

“Sawa."

Kinoo akatazama saa yake ya mkononi. Muda wa kuondoka ulikuwa umekaribia. Ila kabla hajaaga akamuuliza Miranda,

“umepata habari zozote za BC?"

“hapana," Miranda akajibu na kisha akauliza, “vipi kuna mpya yoyote?"

“hapana. Ila auhisi anaweza pia akawa amehusika kuleta hao watu kuwavamia?"

“hapana. Watu waliotumwa walikuwa ni wanaume weusi. Endapo wangekuwa ni wazungu basi ningemshuku bwana Brown moja kwa moja. Na hivi tangu wazungu hao wamekuja, sidhani kama atakuwa anatukumbuka."

Kinoo akatazama tena saa yake kisha akasimama. Sasa akaaga na kwenda zake. Baada ya dakika tatu Kinoo hakuonekana, Miranda akanyanyua simu yake na kupiga.

**

Majira ya saa nne usiku ...

“Hallow!" Bwana Sheng alipaza sauti akiongea na simu yake. Alikuwa ameketi sebuleni mwa nyumba, amekunja zake nne. Amevalia nguo nyepesi za kulalia.

“umepata ujumbe wangu? ... Ok, nakusikiliza ... Sawa, hamna shida, tukubaliane tu, nadhani unajua ninachotaka ... Sawa, basi tutafanya vilevile si ndio? ... Sawa."

Simu ilipokatika, akapiga na kusema maneno machache tu kisha akakata. Baada ya muda kidogo wakaja wanaume wawili vijakazi wa Sheng. Wakasalimu na kuketi kitini kusikiza wito.

“kesho tutakuwa kazini. Nimeshapata taarifa nyingine ya makazi ya Jona. Jiandaeni maana muda wowote nitawataka twende huko! Muwataarifu na wenzenu sita."

Baada ya kusema hayo, wale vijakazi wakaenda zao. Bwana Sheng akabakia hapo sebuleni akinywa taratibu kinywaji chake na akiwaza kwa mbali.

Punde kidogo simu yake ikaita, alipotazama akaona ni mkewe toka Beijing. Akashangaa kuona amempigia majira haya. Akapokea na kuibandika simu sikioni.

Mkewe alikuwa amemkumbuka na anamuulizia ni lini atarudi China kumwona kwani hata mtoto amekuwa akisumbua sana. Hata shule haendi anakesha akilia anataka kumwona baba.

Kwa sauti ya upole kabisa, bwana Sheng akaongea. Akamwahidi mkewe kuja kumwona pindi atakapomaliza kazi fulani kubwa mbele yake.

Japo mwanamke hakumwamini, alimsisitizia zaidi. Lazima aje kuwaona muda mfupi tu baada ya kumaliza kazi hiyo. Kisha simu ikakatwa.

**

Majira ya saa saba mchana ...

Limousine nyeusi ilingia ndani ya uwanja wa hoteli. Dereva akashuka na kufungua mlango wa nyuma akatoka mwanaume fulani mweusi aliyevalia suti rangi ya kijivu.

Mwanaume huyu alikuwa mrefu, na kichwa chake hakikuwa na nywele. Suti yake ilimkaa vema na kwa kumtazama upesi ungesema ni mtu fulani mkubwa taasisi fulani.

Mdomoni alikuwa ana sigara kubwa na kwenye mkono wake wa kushoto alivalia saa ya dhahabu.

Mwanaume huyo, akiwa anapiga hatua za kikakamavu, akaendea mapokezi na kujitambulisha anaitwa bwana Lorenzo Kagula, anahitaji mapumziko kwa muda wa siku tatu hotelini hapo.

Basi mhudumu, mdada fulani mweupe aliyevalia sare, akiitwa Lidia Kombo kwa mujibu wa kibandiko kifuani mwake, akatazama orodha ya vyumba na kisha akampatia bwana huyo chumba namba 114.

“Samahani, unaweza ukanibadilishia. Nishawahi kuja hapa na sikupenda hiko chumba. Unaweza ukanitazamia chumba namba sabini na kitu hivi?"

“usijali," akasema mhudumu kisha akatupia macho yake kwenye orodha tarakilishini, baada ya punde akasema,
“aaahm ... Kuna chumba namba 74!"


“si mbaya"

Bwana huyo akalipia na akageuka aende baada ya kukabidhiwa ufunguo. Na kwasababu alisema ni mwenyeji basi hakuhitaji kusindikizwa.

Ila upesi akarejea kwa mhudumu na kumwambia,


“samahani, dada. Kuna wageni wangu pia ningependa wafikie hapa. Vipi kuna vyumba vya kutosha?"

“pasipo shaka," akasema mhudumu kwa tabasamu. Basi bwana Lorenzo akaenda zake akipiga mluzi.

Baada ya kama dakika kumi na tano, gari aina murrano nayo ikaja hapo hotelini, wakashuka wanaume watatu waliobebelea briefcase. Waliingia ndani ya hoteli na kisha wakauliza kuhusu ujio wa bwana Lorenzo hapo hotelini.

Walipohakikisha yupo, wakaweka oda ya vyumba.

“naomba utupatie chumba namba 75 au 76 ili tuwe karibu naye. Ni mwenzetu."

Yule dada mhudumu akasikitika akiwaambia vyumba hivyo vina watu, kwa kuwasaidia akawatafutia na kuwapatia vya namba 80 na 86.

Basi wakalipia na kwenda zao wakisindikizwa na mhudumu mpaka milangoni. Mhudumu akaenda zake akiwakabidhi funguo.

Wote wakaingia chumba namba 80, na baada ya dakika chache wakatoka na kwenda kwenye kile chumba cha Lorenzo. Mmoja akasema,

“vile vyumba viina watu. Bila shaka watakuwamo humo kama tulivyopewa maelezo."


Bwana Lorenzo akatikisa kichwa kisha akasema, “ila ni vema tukahakiki, usiku tumalize zoezi. Si umekuja na vile vitu nilivyokuambia?"

“ndio."

Mmoja wa wale mabwana waliokuja ‘kumcheki' Lorenzo akafungua briefcase. Ndani kulikuwa na nguo, sare zinazofanana na za wahudumu wa hoteli.

Bwana huyo akazivaa na kufanana vilevile na wahudumu, kisha akatoka ndani kuendea mlango wa chumba namba 75.

Alipofika hapo akabisha hodi.

“mhudumuu!" Akapaza na sauti.

***
 
Kuna MTU umu ndani alitoa ahadi ya kuifuta jf ,,vip anatekeleza Lin??
[emoji1] [emoji1] [emoji1] [emoji1]
 
Back
Top Bottom