Anga la washenzi na Joana anaona kitu usiku

Anga la washenzi na Joana anaona kitu usiku

Steve mwaga sumu hizo chalii yangu....mida ndio hii....
 
*ANGA LA WASHENZI --- 36*


*Simulizi za series*


ILIPOISHIA

"Ametoka?" Bilali akastaajabu. "Mbona aliniambia atakuwepo mida hii mzee?"

"Sijui, ila hayupo. Ametoka," akasisitizia mwenyeji.

Lakini kabla wakina Mustapha hawajaondoka, ikaja gari hapo, Alphard nyeupe yenye vioo vyeusi. Wakasimama na kutazama. Kioo kikashushwa na akaonekana mchina mmoja mwanaume. Akawasalimu kwa kuwapungia mkono.

"Ndiyo huyo hapo sasa!" Balali akamwambia Mustapha. Wote wakajikuta wanatabasamu.

ENDELEA

“You are welcome!” (Karibuni!) Mchina huyo ndani ya gari akasema na kisha akazama ndani ya uzio. Nyuma Mustapha na Bilali nao wakaingia na punde wakajikuta wapo sebuleni, na yule mchina akiwa anatazama ile picha ya nyaraka iliyokuwepo ndani ya simu ya Mustapha.

Kwa umakini akaikagua kwanzia mwanzo mpaka mwisho. Akairudia tena kwa mara ya pili na kisha akauliza:

“Mmeitoa wapi?” kwa sauti ya puani.

Bilali akataka kujibu, lakini Mustapha akamuwahi na kumzuia. Akauliza:

“Kuna ujumbe gani?”

Mchina yule akashusha pumzi ndefu. Alafu akasema ile nyaraka ilikuwa ina taarifa fulani za koo iliyopo huko China. Koo yenye nguvu na ushawishi. Na kwenye hiyo nyaraka kulikuwa kina kipande kidogo tu cha taarifa yao.

Yaani kuna taarifa ambayo imekosekana ili ipate kutimia. Na inaonekana taarifa hiyo ni ya siri, na koo hiyo wanaitafuta ipate kutimiza mahesabu.

“Ona sasa! Tumejisumbua bure asee!” Bilali akalaumu.

“Hapana,” akajibu yule mchina upesi. “Hii ni mali, mali kubwa sana hii, lakini pia ni damu!”

“Damu? Kivipi?” Mustapha akauliza.

“Kwanza ni mali kwasababu kuwa nacho ni pesa. Endapo ikijulikana kama mnacho, mnaweza mkavuta pesa yoyote ile kwasababu tu ya kuifanya ikawa siri…”

“Na damu kivipi?” akauliza tena Mustapha.

“Ni damu kwasababu wanaweza kuitafuta nyaraka yao pasipo kuamua kutoa pesa. Yani kwa lazima na hapo ndipo kuna shida!”

Kukawa kimya kidogo. Kila mtu alikuwa anafikiria lake kichwani. Lakini mchina yule akawatoa hofu akisema:

“Kuna namna lakini ya kutengeneza pesa kama tukikubaliana.”

Mustapha na Balali wakatenga masikio yao.

“Huyu mwenye hii nyaraka anajua makazi yenu? Au mahali anapoweza kuwapata?” mchina akauliza.

Mustapha akatikisa kichwa chake kuafiki.

“Ndio anapajua kwangu.”

“Basi hama,” mchina akashauri. “Tafuta mahali unapojua utakuwa salama, ndipo tufanye hii njia.”

“Kwanini nihame?” Mustapha akauliza.

“Kwasababu watakutafuta,” mchina akamjibu. “Kabla hawajatoa pesa watahakikisha kama kuna njia ya kufanyika kukwepesha mfuko wao. Hawawezi wakatoa pesa kirahisi. Watatoa pesa ambapo wameona hamna namna ya ziada – hamna njia nyingine!”

Mustapha akanyamaza kwa muda. Bilali naye hakuwa na cha kusema. Kukawa kimya wakitazamana. Mchina akaendelea kuongea.

“Ni hatari lakini ni pesa kubwa sana tunaweza tukaitengeneza. Pesa ambayo kila mmoja wetu ataipata na kuifurahia. Mtanunua majumba na magari. Ila ndiyo hivyo, ina gharama yake. Inabidi tuwe radhi kuilipa.”

Mustapha akamtazama Bilali, alafu akamtazama mchina na kumwambia:

“Tupo tayari,” akipandisha kichwa.

Basi mchina yule akaanza kuwaambia namna ambayo wanaweza wakatengeneza pesa kwa kupitia nyaraka ile. Kwanza wahakikishe wanaipata katika nyaraka ngumu, yani waiprint na kuihifadhi. Alafu wataituma mtandaoni moja kwa moja kwenye tovuti ya watu wao na kuwataka walipie pesa wakiwa wameshaainisha na akaunti yao ya benki.

“Hakuna kukutana nao bali kuwasiliana tu mtandaoni. Kila kitu kitafanywa mtandaoni na watainunua nyaraka yao mtandaoni. Ni kama vile unavyofanya manunuzi mtandao wa ebay ama amazon.”

Mustapha na Bilali wakakubaliana na hilo, ila sasa wakawa na kazi ya kwenda kufungua akaunti ya benki na wapate master card. Wakamshukuru mwenyeji wao kwa kuwafungua macho, wakaaga waende.

Ila kabla hawajenda, mchina yule akawaomba:

“Mnaweza mkanitumia nyaraka hiyo kwenye simu?”

Mustapha akakataa. Bado hawakuwa wanamwamini mchina huyo kiasi hicho. Vipi kama akiwazunguka?

“Its ok, hamna shida. Naelewa,” akasema mchina kwa kutabasamu. akawasindikiza wageni wake mpaka nje ya nyumba, akawaomba awabebe kuwapeleka nyumbani maana hana kazi ya kufanya kwa sasa na angependa kuwasaidia.

Mustapha na mwenzake wakaona hamna shida katika hilo, wakajipaki ndani ya Alphard na safari ikashika hatamu.

Wakadumu kwenye gari kwa kama dakika arobaini na tano kabla hawajafika kwa Mustapha ambapo wote walishukia.

“Nashukuru sana,”

“Msijali, tutawasiliana,” mchina akasema na kisha akaondoka zake.

Hili ndilo lilikuwa kosa kubwa alilolifanya Mustapha. Aliweza kuruka viunzi kote huko ila hichi akakisahau. Mchina huyu hakuwa mjinga kuchoma mafuta yake kuwaleta hapa. Kuna kitu alikuwa amekipanga na kukitaka, na alishakipata!

Akiwa ndani ya gari yake, anawasiliana na mwanaume fulani wakiteta kwa lugha yao ya nyumbani. Mchongo ukawekwa bayana wa kumuua Mustapha pamoja na mwenzake na kisha nyaraka ile ndani ya simu iwe mali yao.

Kumbuka huna rafiki wa kweli ndani ya dunia hii ya washenzi! Anamalizia kwa kusema kwa Kiswahili:

“Usibakize hata tone la ushahidi.”


***


Saa nne usiku…


Akiwa anatengeneza juice, simu yake inaita. Jona anaitazama na kuona jina la ‘Beka’ kwenye kioo. Anaguna na kuivuta simu, kisha anapokea.

Beka ni nani? Ni mwanaume jirani na fremu na ya Jona huko Mwenge. Sehemu yake ya biashara inafuatia baada ya pale kwa Jona. Kabla Jona hajapokea simu hiyo, anajiuliza kutakuwa kuna nini. Na akili yake inamwambia si salama.

Si mara kwa mara Beka humpigia.

“Niambie Beka.”

Pasipo kupoteza muda Beka anamwambia juu ya kifo cha Jumanne. Wamemkuta amejifia ndani ya fremu wasijue nani anahusika. Wametambua hilo muda si mrefu wakiwa wanafunga maeneo ya kazi, wakastaajabu kuona Jumanne hafungi na muda ushaenda.

Walipoenda kutazama, wakakutana na kisanga hicho.

“Beka, ni utani au?” Jona akauliza kwa kuchanganyikiwa.

“Si utani, brother. Tupo hapa pamoja na mwili.”

Haraka Jona akajiveka shati na kukimbilia eneo la tukio. Kichwa chake hakikuwa salama kabisa kwa mawazo. Kuna muda akajiuliza kama siku hiyo ilikuwa ya wajinga, ama? La hasha haikuwa!

Aliona dereva bodaboda anabembeleza pikipiki akamhasa aongeze mwendokasi. Alipofika, akajitupa toka kwenye bodaboda akimkabidhi dereva pesa yake. Moja kwa moja akenda eneo la tukio.

Hapo akakuta wanaume wanne wakiwa wamejikusanya na kuteta. Akawasalimu akizama ndani alipoonyeshewa mkono na Beka. Akaukuta mwili wa Jumanne ukiwa umejilaza.

Akatazama mapigo ya moyo, hayakuwa yanapiga. Akahakikisha na pumzi pia, kote hola! Akaamini sasa ni kweli Jumanne alikuwa ameenda. Alikuwa amekufa!

“Hatujui alikufa muda gani, na nani amemuua. Sijui ni nini kilichotokea!” Alisema Beka. “Lakini Chaz anasema ….” Beka akamtazama Chaz, mwanaume mrefu mwenye mwili, akampatia kijiti cha kutia neno.

“Mida ya asubuhi asubuhi hivi nilimwona njemba fulani akitoka ndani huku. Alikuwa amevalia suti, mara nikamwona anatembea fasta fasta, akadandia boda na kusepa! … nahisi anaweza akawa anahusika.”

Jona akaulizia rangi ya suti na mwonekano wa mwanaume huyo, Chaz akamjibu. Akameza taarifa hizo, na kwasababu ule ulikuwa ni mzigo wake, siku hiyo hakulala akaimaliza kwa kuhangaika huku na kule kwa ajili ya marehemu Jumanne.

Akaenda polisi kutoa taarifa na kisha kufanya utaratibu wa kusafirisha maiti mpaka mochwari, kuwasiliana na familia ya Jumanne na kadhalika.

Mpaka kwenye majira ya saa sita usiku ndiyo akawa ametulia, tena akiwa kibarazani mwa nyumba ya Jumanne. Alikuwa pamoja na mke wa marehemu aliyekuwa analia pasipo kupumzika.

Muda si mrefu, majirani wawili nao wakafika hapo kujumuika nao.

Japokuwa kulikuwa kuna maongezi kadhaa na kilio, Jona hakuwa mwenye habari. Kichwa chake alikuwa amekiegemesha ukutani akielemewa na mawazo mazito sana. Ni nani amemuua Jumanne na amefanya hivyo kwasababu gani?

Huyo mwanaume ndani ya suti, ni nani? Hakupata usingizi kabisa wala kujihisi njaa. Alishiba mawazo.

Uwanda wake wa mawazo ukapanuka zaidi, na kuna jambo alipolifikiri likamuwashia taa za hatari kichwani.

Nini kinafuata baada ya kifo cha Jumanne? Kufunga biashara … ndio … maana hataweza kukaa hapo na huku zile msheni zake zinamtaka asionekane. Hii itakuwa ni biashara ya ngapi anafunga sasa?

Kwa namna moja kubwa, Jona akajikuta anatilia mashaka ile kauli ya Kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Dar es salaam:

“Jona, maisha yako kamwe hayatakuwa sawa ukiwa nje ya jeshi. Huu ndiyo wito wako na hauwezi kuukwepa. Na sisi tutakukumbusha hilo kila uchwao.”

Alikumbuka maneno yote hayo kana kwamba ametoka kuambiwa muda si mrefu. Akawaza je yatakuwa yanahusika na kifo cha Jumanne? Na hapo tena akajiuliza, je kauli ile itakuwa ina mahusiano na kufa kwa biashara yake?

Jona akajikuta anapata mawazo ambayo hakuwahi kuyawaza hapo kabla.

Je kauli ile ya kamanda itakuwa ina mahusiano na kifo cha utata cha familia yake?

Ya kwamba maisha yake hayatakuwa salama wala ya amani akiwa nje ya jeshi?

Akaona ana haja ya kunywa. Akanyanyuka na kuondoka zake akienda kutafuta bar. Alipopata akanunua mvinyo na kunywa kwa pupa. Akanywa kwa pupa … akanywa kwa pupa.

Aliomba pombe imsaidie kupumzika japo kwa muda. Impeleke mahali ambapo atakuwa salama na mbali na uhalisia.


***


Saa nne asubuhi…


“Amesemaje ulipochonga naye?” aliuliza mwanaume fulani mweupe. Mrefu na mwenye mwili wa mazoezi. Swali hili akilielekezea kwa Nyokaa aliyekuwa ameketi kwenye kochi akivuta sigara.

“Atajua mwenyewe atakavyosema, ila najua atamleta tu yule manzi.”

“Una uhakika?”

“Asilimia mia nane, nina uhakika. Inaonekana anamzimia sana huyu malaya wake. Atajileta tu.”

Kukawa kimya kidogo.

“Ila unajua nini Nyokaa, tukimpata tena yule manzi, tujitahidi kumaliza ile ishu mazee. Unajua yule manzi anaweza akawa ametoboa gunia letu la mchele huko kama alivyotoboa la yule boya?”

“Sidhani asee. Namwamini sana yule manzi.”

“Hapo ndipo unapofeli sasa, unamwanijie manzi kiasi hicho Arif?”
.
.
.
.
***
 
*ANGA LA WASHENZI --- 37*
*Simulizi za series*

ILIPOISHIA
“Asilimia mia nane, nina uhakika. Inaonekana anamzimia sana huyu malaya wake. Atajileta tu.”
Kukawa kimya kidogo.
“Ila unajua nini Nyokaa, tukimpata tena yule manzi, tujitahidi kumaliza ile ishu mazee. Unajua yule manzi anaweza akawa ametoboa gunia letu la mchele huko kama alivyotoboa la yule boya?”
“Sidhani asee. Namwamini sana yule manzi.”
“Hapo ndipo unapofeli sasa, unamwanijie manzi kiasi hicho Arif?”
ENDELEA
“Najua Miriam ananipenda na yupo radhi kufanya jambo lolote kwa ajili yangu. We unajua ni mangapi yule manzi amefanya kwa ajili yangu?” akauliza Nyokaa. Kabla hajangoja majibu, akaendelea kumwaga sera:
“Amenifanyia mbishe mingi sana asee kabla haya mafyoko hayajatokea hapa kati. Unadhani angekuwa manzi mwingine akithubutu?”
Mwanaume yule mweupe, kwa jina Roba, akatikisa kichwa alafu akashusha pumzi yake akitazama kando. Kuna jambo alikuwa analifikiria, na punde akamshirikisha Nyokaa.
“Unajua mishe zetu, mwanangu. Za hatari kinoma, inabidi tuwe macho sana kuangaza kama kuna snitch, la sivyo tutaharibu kila kitu.”
“Najua,” akajibu Nyokaa kwa ufupi. Na hakutia tena neno lingine kukiwa kimya kwa muda wa kama dakika tatu.
“Umeshandaa kila kitu lakini?” Nyokaa akauliza.
“Kila kitu kipo tayari yani, ni huyo mgeni tu aje.”
Baada ya hapo kimya kikawa kingi.

***

Saa sita mchana.
Chumba SPACE BUTTON

“Naweza nikapata kikombe cha kahawa?” alisema Panky akimtazama Moderator.
“Cha ngapi sasa?” Moderator akauliza kwa lafudhi yake ya kichina.
“Sijui idadi,” akajibu Panky. “Naomba tu uniletee kama hutojali.”
Moderator akasita kwanza na kumtazama Panky. Panky akatabasamu kabla hajageukia tarakilishi yake na kuendelea na kazi aliyokuwa anafanya. Moderator akatoka nje.
Basi haraka Panky akamtazama Marwa. Mwanaume huyo alikuwa yupo mbali naye sana, kitu ambacho kilikuwa kinamkera si kidogo. Alinyanyuka upesi akamfuata na kumsabahi, na pasipo kupoteza muda akamwambia asome jumbe zake ambazo amemtumia kwenye mashine.
Kuepusha kukutwa na Moderator, upesi akarejea kwenye kiti na kuendelea na kazi yake. Na kweli, punde Moderator akatokea akiwa amebebelea chupa kubwa rangi ya bluu. Akaiweka mezani mwa Panky.
“Hiyo hapo, hautasumbua tena sasa!”
Panky akashukuru kwa tabasamu, akajimiminia kinywaji na kunywa akiendelea na kazi. lakini akili yake ikiwa inamuwaza Marwa kama kweli ameelewa kile alichomwambia.
“Kile kichwa kigumu nacho,” alisemea kifuani. Akavizia pale Moderator aliposogea kando, akashusha kazi zake zote chini, alafu akafungua application fulani iliyokuwa na kialama chenye rangi nyekundu, akaandika:
“Unanipata?” alafu akatuma kwenye tarakilishi aliyoitunza kwa jina la M-Spy.
Alipotuma ujumbe huo, akamtazama Marwa kwa wizi, punde naye Marwa akamtazama. Alafu akabofya keyboard.
“Ndio, nakupata. Unataka nini Panky?” Ujumbe ukaingia kwenye tarakilishi ya Panky. Panky akatabasamu kwanza kabla ya kujibu. Alifurahi sasa maana alikuwa amepata ‘chobingo’ ya kuteta na mtu wake. Nafasi adhimu hii.
Panky: sina ishu mpya, ni kuhusu tu ile picha.
M-Spy: Imefanyaje? Kwani hukunielewa?
Panky: Unajua nini Marwa, niliipenda sana ile picha. na nilivyoenda kufanya ile misheni niliyoagizwa, nikajikuta nakumbana nayo. Sidhani kama ni vibaya nikajua maana yake.
M-Spy: Panky, acha ujinga.
Panky: Kivipi? Nataka kuuondoa huo ujinga kwa kujua.
M-Spy: Nikukumbushe mara ngapi kwamba hatutakiwi kushirikiana kwa vyovyote tukiwa kazini mpaka pale Mode atakapokuwa anajua?
Panky: Marwa, acha kujifanya bingwa wa kufuata sheria. Ni mara ngapi huwa nakusaidia mambo yako? Huwa unamuita Mode?
Kimya.
Panky akatazama upande aliopo Marwa, akamwona Moderator akiwa amesimama kandokando ya mwanaume huyo. Moyo ukamlipuka kwa kudhani huenda pamebumburuka. Lakini alivyotazama vema akagundua, Marwa alikuwa tayari ameshatoa yale maongezi yao na yupo bize kufanya kazi.
Basi naye kwa muda akazama kazini mpaka baada ya dakika kama tano alipopata ujumbe toka kwa Marwa.
M-Spy: Tukutane wakati wa chakula!
Panky: Poa.
Kazi zikadumu mpaka majira ya saa nane, watu wakafunga kila kitu kwa ajili ya kwenda kutia kitu tumboni. Huko Marwa na Panky wakakutana na kuteta mambo kadhaa kuhusu ile picha. Cha kushangaza ni kwamba, hata Marwa mwenyewe hakuwa anajua nini kimo pichani!
Lakini data alizokuwa amepewa kuzitumia kufuma ile picha zilikuwa ni za kushangaza na zenye kuhitaji mafikira kung’amua.
“Nashukuru sana, Marwa. Nadhani ingekuwa vema kama ungelinitumia picha hiyo kwenye tarakilishi yangu,” alisema Panky akijua wazi pale hawana muda mrefu wa kujadili.
Marwa akatabasamu.
“Unajua hilo jambo haliwezekani, Panky.”
“Inawezekana.” Panky akamkatiza. “Nimetengeneza code ya kuniwezesha kuwasiliana na kila tarakilishi mule ndani. Nina application za kuniwezesha kutengua security na kupokea ama kutuma faili kwa yeyote ndani ya chumba.”
Marwa akastaajabu.
“Umewezaje kufanya hivyo?”
Panky akatabasamu.
“Huu si muda wa kujadiliana, Marwa. Unajua muda wetu hapa.”
“Sawa, ila unajua tarakilishi yangu haina uwezo huo kama wako. Sasa natumaje?”
“Ngoja n’takuonyesha. Wewe kuwa karibu na messenger tu, sawa?”
Wakamaliza kula na kuondoka. Wakafanya kama vile walivyoelekezana, na Panky akafanikiwa kupata picha na maelekezo yote ambayo Marwa aliyatumia kufuma picha hiyo. Basi tabasamu likajaa usoni.
Ila muda si mrefu, akashikwa bega na Moderator, akatazamwa na uso mgumu na kisha akaamriwa:
“Simama!”
Utumbo ukamtetemeka na kichwa kikaanza kumgonga! Watu wote ndani ya chumba wakamtazama. Ila Marwa akiwa anatamazama kwa woga zaidi!
Bila shaka alijua sasa kila kitu kimeanikwa wazi! Mwisho wao ulikuwa umewasili, kifo kinawaita. Marwa akajuta kwanini alifanya ujinga ule.
Moderator akakaa kwenye kiti cha Panky na kuanza kupekua tarakilishi hiyo. akachukua muda wa dakika tano kabla hajanyanyuka na kumtaka Panky aketi chini. Hakuna alichokigundua!
“Unaweza ukaendelea na kazi yako!” akasema Moderator.
Panky akaketi akiwa haamini.
Lakini baadae akajiona ‘jembe’ kwa namna alivyotengeneza mfumo wake madhubuti kiasi cha kumfanya mtaalamu asipate chochote ndani ya mashine yake.
Akajikuta anatabasamu akipekua pekua tena tarakilishi yake. Kila jambo lilikuwapo kama alivyoyaweka.
----
Saa kumi jioni:

Panky anachomoa simu yake mfukoni na kumtafuta Jona. Simu ikaita mara tatu pasipo majibu. Akasonya na kujiuliza atakuwa wapi.
Alikuwa ameshatoka kazini na akiwa tayari amebebelea flashi ambayo ina faili nyeti la ile picha.
Alikuwa ameketi nyumbani kwake, sebuleni, akitafakari. Mkewe akaja akitokea dukani.
"Vipi mbona una mawazo hivyo?" Akauliza mwanamke huyu mweupe mwembamba aliyevalia kofia ya kuziba nywele pamoja na dera la njano lenye maua mekundu mekundu.
Panky akamlaghai mkewe kwamba yupo sawa na angependa apate muda kidogo wa kutafakari peke yake.
"Unataka nikuache, sio?" Mke akauliza kwa shari. "Yani hapa nyuma uliniacha peke yangu, sikujua wapi ulipo na unafanya nini, leo upo hapa nakaa na wewe unataka nikuache?!"
"Si hivyo mpenzi!"
"Ni vipi? - haya kaa basi mwenyewe!" Mwanamke akanyanyuka na kwenda zake. Panky akabakia kumtazama.
Ila mara na simu ikaita, kutazama alikuwa ni Jona.
"Nimekutafuta sana mzee vipi? ... ishu gani hiyo? ... serious? ... pole sana kaka, sasa inakuaje? ... yah! Nimepata ile kitu sasa ndo nikawa nataka tukutane uione kama vipi ... poa, basi utanshtua au sio? ... haya baadae!"
Simu ikakata. Panky akachomoa flash mfukoni mwake na kuitazama. Akanyanyuka na kwendaze chumbani.

***

Saa moja jioni.

Ngo! Ngo! Ngo!
"Naona ameshafika, acha nikachonge naye!" Glady aliwaambia wenzake wawili aliokuwa nao chumbani kabla hajanyanyuka na kwenda mlangoni.
Alikuwa amevalia gauni fupi la njano lililoacha miguu yake uchi. Nywele zake alikuwa amezikusanyia ndani ya kiremba cheusi cha kulalia.
Alitoka nje akamkuta Mustapha. Alikuwa amevalia shati la buluu, suruali ya kaki na raba nyeupe. Mwanaume huyo akamtaka wakaongelee ndani.
"Kuna watu, tuongelee tu hapa hapa!" Glady akasisitiza. Mustapha akatazama kushoto na kulia kwake kama kuna usalama. Uso wake ulikuwa una mashaka.
"Mustapha, kuna nini?" Glady akauliza. Alihisi kuna mambo hayapo sawia.
"Naomba niingie ndani!" Akasisitiza Mustapha. "Tafadhali!"
Kabla hata Glady hajajibu, Mustapha akazama ndani na akaurudishia mlango yeye mwenyewe. Akashika kiuno na kushusha pumzi. Glady akamtazama na kumuuliza nini shida mbona anamtia woga!
Mustapha akamwambia hayupo salama, kuna mtu anataka kummaliza!
"Nani huyo?" Glady akawahi kuuliza. "Yule mchina?"
Mustapha akatikisa kichwa. Akasema muuaji huyu hamjui, amemkosa kosa na risasi akijaribu kujiepusha kwa kupitia mlango wa nyuma!
"Mustapha, upo serious?"
"Kabisa! Na hapa ninavyoongea na wewe, Bilali ameuawa tayari!"
Glady akatoa macho ya mshangao. Na hapo akawa amevaa hofu nyeusi kiasi kwamba akamshangaa Mustapha kuja hapo ilhali ana songombingo la kumwaga damu!
Vipi kama akiwaambukiza tatizo?
"Sikuwa na kwengine pa kwenda, Glady. Naomba unisaidie hifadhi," alisema Mustapha kwa huruma. Haraka Glady akaenda dirishani na kutazama huko nje.
Akateta na wenzake wakiwa katika hali ya taharuki.
"Mustapha, utakuwa umefanya nini saa hii?"
"Sijafanya kitu, ila nahisi atakuwa ni yule mchina tuliyempelekea ile nyaraka atutafsrie. Anatuzunguka, anataka kuichukua!" Alisema Mustapha. Jasho lilikuwa linamtiririka.
Akamweleza Glady kinaga ubaga walivyoenda kuomba msaada kwa yule mchina ambaye aliwapa lifti kuwarejesha nyumbani.
Wakiwa taharukini, wanasikia mlango unagongwa! Glady anamtazama Mustapha, kisha anawatazama wenzake waliokuwa kitandani.







****


Ati ni nani?
 
[emoji15] [emoji15] [emoji15] Mie mke wa mtu bana
Tutafanya siri kwani mmeo yupo humu humu jf?
Ndio yuko humu

AnaitwA shululu na tena wana watoto mapacha
Dah Shululu namfahamu sema nimepotea sana pande za makapuku forum ndio maana nimesahau kama ni wapenzi ila ahsante kwa kunikumbusha mkuu

Tumosa mama wacha nitulie tuendelee kuwa shemela shemela
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Asee leo nimekuja hapa mkoani kabisa sanawari ili ukitupia kitu niwe wa kwanza kukitusua [emoji1][emoji846]
 
Back
Top Bottom