SteveMollel
JF-Expert Member
- Jul 12, 2015
- 8,797
- 25,177
- Thread starter
-
- #1,361
*ANGA LA WASHENZI -- 60*
*Simulizi za series*
ILIPOISHIA
Huwa anawakumbuka, lakini leo hii ilikuwa ni kana kwamba ametoka kushuhudia jengo lake likiwa linateketea. Alphonce alimkumbusha kwa kina. Alikitifua kidonda kilichojenga gamba.
Akashindwa hata kupekua mafaili yale, akabaki anakunywa tu. Baada ya kuongeza mafundo matatu tu ya Bacardi, kichwa kikashindwa kuendeleza kazi, fahamu zikakata, akajimwagia kochini!
Jinamizi lililokuwa linamtesa, leo likarudi kwa nguvu zote.
ENDELEA
Saa tatu asubuhi, SPACE BUTTON.
Kulikuwa bize kama ilivyo ada. Watu walikuwa wanatazama vioo vya tarakilishi zao huku vidole vikitwangatwanga 'keyboard'. Watu hawa kwa idadi walikuwa nane, hakukuwa na mwanamke hata mmoja.
Mazingira yalikuwa tulivu ukiachana na sauti za keyboard. Hakukuonekana kama kuna shida yoyote, wala kama inaweza kubashiriwa kwa hapo mbeleni.
Hali ya hewa ilikuwa baridi, viyoyozi vilikuwa moto. Kuna baadhi yao wakawa wanavuta vikamasi na huku pua zao zikiwa nyekundu kwa kuzifikichafikicha mara kwa mara.
Pengine baridi lilikuwa kali kuliko siku zingine. Mmoja akapaza sauti kumuita Moderator na kumtaka apunguze kasi ya viyoyozi hivyo la sivyo watakufa.
Kidogo zogo likatokea hapa watu wakiunga mkono hoja hiyo. Ni kama vile walikuwa wanamngojea 'shujaa' ajitokeze kusemea hilo jambo wapate kum 'mback-up'. Kinyume kabisa na taratibu ndani ya chumba cha SPACE BUTTON watu wakaruruma na kuzoza. Haikuwa inaruhusiwa kufanya hivi.
Moderator alitii haja yao akapunguza kasi ya viyoyozi, kazi zikaendelea tena kwa ukimya. Lakini miongoni mwa watu hao waliopaza sauti zao kuhusu ukali wa viyoyozi, si Marwa wala Panky aliyekuwapo.
Wao walikuwa kimya. Wao walikuwa wakiendelea na kazi zao kana kwamba hakuna kilichojiri, hakuna walichosikia.
Zikapita dakika tano watu wakiendelea na kazi. Kama ilivyo ada ndani ya SPACE BUTTON ni keyboard tu ndiyo zikawa zinasikika. Ilipohitimu dakika ya sita, mara taratibu viyoyozi vikaanza kurudi kwa kasi.
Baridi likawa jingi, watu wakaanza kupata shida. Ni kana kwamba walipelekwa kwenye kilele cha mlima mrefu mno.
Wakaanza kulalamika tena, mada hii Moderator alikuwa ametoka kidogo. Wakazoza na kuzoza, Moderator aliporudi akastaajabishwa na hali hiyo ya 'soko'. Kabla hajafoka kukemea na kutoa vitisho, akatambua baridi lilikuwa limeongezeka maradufu.
Haraka akatazama tarakilishi yake. Akabofya keyboard mara kadhaa. Akapiga ngumi mezani kisha akatoka ndani. Bila shaka alikuwa anaenda kuangazia mitambo kama ina hitilafu.
Kiwizi, Marwa akamtazama Panky, akatabasamu, alafu akarudisha uso wake kwenye tarakilishi.
"Nimefanikisha!" Ujumbe ukaingia kwenye tarakilishi ya Panky kwa kutumia jina la M-spy.
Panky akatabasamu. Akamtazama Marwa kiwizi, alafu akachapa haraka kumjibu.
PANKY: Sure? (Hakika?)
M-SPY: Yah sure. (Ndio hakika).
PANKY: How did you do that man? (Umewezaje jamaa?)
M-SPY: Aaanh! Maswali gani hayo? Nataka nitazame kama naweza pata chochote kwenye mashine yake. Nipe muda kidogo.
Marwa akaanza kuitembelea tarakilishi ya Moderator kwa kutumia ya kwake. Alikuwa anafanya hayo kwa wepesi kwani hakuwa na muda wa kutosha, na usalama ulikuwa finyu mno.
Alijua endapo Moderator angepata muda wa kutulia kwenye mashine yake, angezijua njama zake. Kwahiyo alitakiwa kutumia fursa hiyo upesi kabla mwanaume huyo hajarejea kitini.
Dakika mbili tu, Moderator akawasili. Tayari hali ya hewa ilikuwa imetulia. Akatazama wafanyakazi wake akikagua tarakilishi zao kwa macho, kisha akaketi. Akashusha pumzi ndefu.
Akakagua tarakilishi yake akijiuliza nini shida. Akakagua kila kitu, hakuona tabu. Akakagua na tarakilishi za wafanyakazi wake kwa kutumia ya kwake, kote akaona wakifanya kazi zao.
Akajilazimsha kuamini tatizo lile la viyoyozi litakuwa ni la mitambo.
PANKY: Umefanikiwa?
M-SPY: Kiasi chake. Bado nahitaji kuingia tena kwenye mashine yake kuna kitu sijamalizia.
PANKY: Utaingiaje? Amesharejea. Ataongeza uangalifu sasa hivi kuliko mwanzoni.
M-SPY: Najua. Natazamia namna nitakavyofanya jambo hili kwa usalama.
PANKY: Be careful. (Kuwa makini)
Kukawa kimya kidogo kwa dakika nne, Ujumbe wa Marwa uka 'pop-up' kwenye kioo cha tarakilishi ya Panky.
M-SPY: Nimepata wazo.
Akamshirikisha wazo hilo Panky, naye akalikubali. Ikapita dakika moja, mara Panky akadondoka chini akihangaika kuhema kana kwamba koo lake la hewa limesiliba! Mbavu zikamsimama. Mishipa ikamchomoza. Macho akayatoa huku shingo ikishupaa.
Watu wakapigwa na butwaa. Wakaamini Panky atakuwa ameathiriwa na mabadiliko yale ya hewa yaliyokuwa yanatokea ndani ya chumba hicho hapo nyuma.
Haraka wanaume watatu wakafanya kumsaidia wakiwa pamoja na Moderator. Wakampeleka kupata huduma huko nje. Sasa Marwa akatimiza adhma yake upesi.
Baadae wakati wa kupata chakula cha mchana, wakaketi meza moja na Panky kuteta. Walihakikisha hakuna mtu aliyekuwa anawasikia, na wapo salama.
"Panky, kwanini hukuwa muigizaji?" Marwa akatania. "Unajua ulintisha aisee. Nikadhani huenda kweli umepata tatizo! Ilinihitaji roho ngumu kweli kukupuuzia."
Panky akatabasamu.
"Sikujua kama nina kipaji hicho, nitalifanyia mazingatio ... anyway, umefanikisha?" Panky akauliza.
Marwa akameza tonge kwanza. Akatikisa kichwa.
"Ndio, nimefanikiwa. Nadhani nimepata kila tunachokihitaji."
Panky akatabasamu. Lakini mara kiganja kikagusa bega lake, akageuka na kukutana na uso wa Moderator.
"Njoo," Moderator akamwambia kwa lafudhi ya ki Mandarin, kisha akaenda zake. Marwa akamtazama Panky kwa hofu. Moyo wake ulikuwa unakimbia kwa kasi. Alimshika mkono Panky akamwomba awafikishie taarifa familia yake endapo hatofanikiwa kutoka hai.
Kwa haraka pia akamwambia Panky taarifa alizozipata atakazikuta chini ya keyboard karatasini, kisha akaenda zake.
Panky akabaki na mawazo. Vipi kama Marwa amegundilikana? Hakupata hamu ya kula tena. Kifua chake kilikuwa kimejawa hofu. Je, watatambua hata kuumwa kwake kulikuwa ni mpango? Akajiuliza.
Alihisi mwili wake umekuwa wa baridi.
Mara kengele ya kurejea kazini ikalia, wote wakanyanyuka toka kantini na kurejea ndani ya SPACE BUTTON. Marwa hakuwapo kwenye kiti chake. Akamtazama na pale kwa Moderator, hakumwona, si yeye wala Moderator.
Basi haraka akanyanyuka na kwenda sehemu ya Marwa, akavuta droo ya keyboard na kutazama kwa chini, akaona kikaratasi kidogo cheupe. Akakibeba na kurudi sehemu yake upesi.
Hakukitazama kikaratasi hicho, alikiweka mfukoni na kuendelea na kazi yake lakini kila saa akawa anatazama kama atamuona Marwa ama Moderator.
Baada ya kama nusu saa, Moderator akarejea ila Marwa hakuonekana. Hapo sasa Panky akapoteza matumaini. Akahisi kweli pengine Marwa ameuawa.
Hakuweza kufanya kazi vizuri kabisa. Kichwani hakukuwa na maelewano kabisa, alikuwa anamuwaza Marwa. Mpaka unafika muda wa kuondoka kazini, Marwa hakuonekana popote pale!
Panky akakosa amani.
"Kuna shida?" Moderator akamuuliza Panky aliyekuwa amebaki mwenyewe kitini. Chumba kizima cha SPACE BUTTON kilikuwa cheupe.
***
MARWA YUPO WAPI? ANAFANYA NINI? NINI MODERATOR AMEFANYA? NINI ATAGUNDUA KWA PANKY?
*Simulizi za series*
ILIPOISHIA
Huwa anawakumbuka, lakini leo hii ilikuwa ni kana kwamba ametoka kushuhudia jengo lake likiwa linateketea. Alphonce alimkumbusha kwa kina. Alikitifua kidonda kilichojenga gamba.
Akashindwa hata kupekua mafaili yale, akabaki anakunywa tu. Baada ya kuongeza mafundo matatu tu ya Bacardi, kichwa kikashindwa kuendeleza kazi, fahamu zikakata, akajimwagia kochini!
Jinamizi lililokuwa linamtesa, leo likarudi kwa nguvu zote.
ENDELEA
Saa tatu asubuhi, SPACE BUTTON.
Kulikuwa bize kama ilivyo ada. Watu walikuwa wanatazama vioo vya tarakilishi zao huku vidole vikitwangatwanga 'keyboard'. Watu hawa kwa idadi walikuwa nane, hakukuwa na mwanamke hata mmoja.
Mazingira yalikuwa tulivu ukiachana na sauti za keyboard. Hakukuonekana kama kuna shida yoyote, wala kama inaweza kubashiriwa kwa hapo mbeleni.
Hali ya hewa ilikuwa baridi, viyoyozi vilikuwa moto. Kuna baadhi yao wakawa wanavuta vikamasi na huku pua zao zikiwa nyekundu kwa kuzifikichafikicha mara kwa mara.
Pengine baridi lilikuwa kali kuliko siku zingine. Mmoja akapaza sauti kumuita Moderator na kumtaka apunguze kasi ya viyoyozi hivyo la sivyo watakufa.
Kidogo zogo likatokea hapa watu wakiunga mkono hoja hiyo. Ni kama vile walikuwa wanamngojea 'shujaa' ajitokeze kusemea hilo jambo wapate kum 'mback-up'. Kinyume kabisa na taratibu ndani ya chumba cha SPACE BUTTON watu wakaruruma na kuzoza. Haikuwa inaruhusiwa kufanya hivi.
Moderator alitii haja yao akapunguza kasi ya viyoyozi, kazi zikaendelea tena kwa ukimya. Lakini miongoni mwa watu hao waliopaza sauti zao kuhusu ukali wa viyoyozi, si Marwa wala Panky aliyekuwapo.
Wao walikuwa kimya. Wao walikuwa wakiendelea na kazi zao kana kwamba hakuna kilichojiri, hakuna walichosikia.
Zikapita dakika tano watu wakiendelea na kazi. Kama ilivyo ada ndani ya SPACE BUTTON ni keyboard tu ndiyo zikawa zinasikika. Ilipohitimu dakika ya sita, mara taratibu viyoyozi vikaanza kurudi kwa kasi.
Baridi likawa jingi, watu wakaanza kupata shida. Ni kana kwamba walipelekwa kwenye kilele cha mlima mrefu mno.
Wakaanza kulalamika tena, mada hii Moderator alikuwa ametoka kidogo. Wakazoza na kuzoza, Moderator aliporudi akastaajabishwa na hali hiyo ya 'soko'. Kabla hajafoka kukemea na kutoa vitisho, akatambua baridi lilikuwa limeongezeka maradufu.
Haraka akatazama tarakilishi yake. Akabofya keyboard mara kadhaa. Akapiga ngumi mezani kisha akatoka ndani. Bila shaka alikuwa anaenda kuangazia mitambo kama ina hitilafu.
Kiwizi, Marwa akamtazama Panky, akatabasamu, alafu akarudisha uso wake kwenye tarakilishi.
"Nimefanikisha!" Ujumbe ukaingia kwenye tarakilishi ya Panky kwa kutumia jina la M-spy.
Panky akatabasamu. Akamtazama Marwa kiwizi, alafu akachapa haraka kumjibu.
PANKY: Sure? (Hakika?)
M-SPY: Yah sure. (Ndio hakika).
PANKY: How did you do that man? (Umewezaje jamaa?)
M-SPY: Aaanh! Maswali gani hayo? Nataka nitazame kama naweza pata chochote kwenye mashine yake. Nipe muda kidogo.
Marwa akaanza kuitembelea tarakilishi ya Moderator kwa kutumia ya kwake. Alikuwa anafanya hayo kwa wepesi kwani hakuwa na muda wa kutosha, na usalama ulikuwa finyu mno.
Alijua endapo Moderator angepata muda wa kutulia kwenye mashine yake, angezijua njama zake. Kwahiyo alitakiwa kutumia fursa hiyo upesi kabla mwanaume huyo hajarejea kitini.
Dakika mbili tu, Moderator akawasili. Tayari hali ya hewa ilikuwa imetulia. Akatazama wafanyakazi wake akikagua tarakilishi zao kwa macho, kisha akaketi. Akashusha pumzi ndefu.
Akakagua tarakilishi yake akijiuliza nini shida. Akakagua kila kitu, hakuona tabu. Akakagua na tarakilishi za wafanyakazi wake kwa kutumia ya kwake, kote akaona wakifanya kazi zao.
Akajilazimsha kuamini tatizo lile la viyoyozi litakuwa ni la mitambo.
PANKY: Umefanikiwa?
M-SPY: Kiasi chake. Bado nahitaji kuingia tena kwenye mashine yake kuna kitu sijamalizia.
PANKY: Utaingiaje? Amesharejea. Ataongeza uangalifu sasa hivi kuliko mwanzoni.
M-SPY: Najua. Natazamia namna nitakavyofanya jambo hili kwa usalama.
PANKY: Be careful. (Kuwa makini)
Kukawa kimya kidogo kwa dakika nne, Ujumbe wa Marwa uka 'pop-up' kwenye kioo cha tarakilishi ya Panky.
M-SPY: Nimepata wazo.
Akamshirikisha wazo hilo Panky, naye akalikubali. Ikapita dakika moja, mara Panky akadondoka chini akihangaika kuhema kana kwamba koo lake la hewa limesiliba! Mbavu zikamsimama. Mishipa ikamchomoza. Macho akayatoa huku shingo ikishupaa.
Watu wakapigwa na butwaa. Wakaamini Panky atakuwa ameathiriwa na mabadiliko yale ya hewa yaliyokuwa yanatokea ndani ya chumba hicho hapo nyuma.
Haraka wanaume watatu wakafanya kumsaidia wakiwa pamoja na Moderator. Wakampeleka kupata huduma huko nje. Sasa Marwa akatimiza adhma yake upesi.
Baadae wakati wa kupata chakula cha mchana, wakaketi meza moja na Panky kuteta. Walihakikisha hakuna mtu aliyekuwa anawasikia, na wapo salama.
"Panky, kwanini hukuwa muigizaji?" Marwa akatania. "Unajua ulintisha aisee. Nikadhani huenda kweli umepata tatizo! Ilinihitaji roho ngumu kweli kukupuuzia."
Panky akatabasamu.
"Sikujua kama nina kipaji hicho, nitalifanyia mazingatio ... anyway, umefanikisha?" Panky akauliza.
Marwa akameza tonge kwanza. Akatikisa kichwa.
"Ndio, nimefanikiwa. Nadhani nimepata kila tunachokihitaji."
Panky akatabasamu. Lakini mara kiganja kikagusa bega lake, akageuka na kukutana na uso wa Moderator.
"Njoo," Moderator akamwambia kwa lafudhi ya ki Mandarin, kisha akaenda zake. Marwa akamtazama Panky kwa hofu. Moyo wake ulikuwa unakimbia kwa kasi. Alimshika mkono Panky akamwomba awafikishie taarifa familia yake endapo hatofanikiwa kutoka hai.
Kwa haraka pia akamwambia Panky taarifa alizozipata atakazikuta chini ya keyboard karatasini, kisha akaenda zake.
Panky akabaki na mawazo. Vipi kama Marwa amegundilikana? Hakupata hamu ya kula tena. Kifua chake kilikuwa kimejawa hofu. Je, watatambua hata kuumwa kwake kulikuwa ni mpango? Akajiuliza.
Alihisi mwili wake umekuwa wa baridi.
Mara kengele ya kurejea kazini ikalia, wote wakanyanyuka toka kantini na kurejea ndani ya SPACE BUTTON. Marwa hakuwapo kwenye kiti chake. Akamtazama na pale kwa Moderator, hakumwona, si yeye wala Moderator.
Basi haraka akanyanyuka na kwenda sehemu ya Marwa, akavuta droo ya keyboard na kutazama kwa chini, akaona kikaratasi kidogo cheupe. Akakibeba na kurudi sehemu yake upesi.
Hakukitazama kikaratasi hicho, alikiweka mfukoni na kuendelea na kazi yake lakini kila saa akawa anatazama kama atamuona Marwa ama Moderator.
Baada ya kama nusu saa, Moderator akarejea ila Marwa hakuonekana. Hapo sasa Panky akapoteza matumaini. Akahisi kweli pengine Marwa ameuawa.
Hakuweza kufanya kazi vizuri kabisa. Kichwani hakukuwa na maelewano kabisa, alikuwa anamuwaza Marwa. Mpaka unafika muda wa kuondoka kazini, Marwa hakuonekana popote pale!
Panky akakosa amani.
"Kuna shida?" Moderator akamuuliza Panky aliyekuwa amebaki mwenyewe kitini. Chumba kizima cha SPACE BUTTON kilikuwa cheupe.
***
MARWA YUPO WAPI? ANAFANYA NINI? NINI MODERATOR AMEFANYA? NINI ATAGUNDUA KWA PANKY?