Anga la washenzi na Joana anaona kitu usiku

*ANGA LA WASHENZI -- 69*

*Simulizi za series*

ILIPOISHIA

"Ndio, Jona hapa, nina shida na wewe haraka iwezekanavyo."

"Nini shida Jona? Mbona upesi hivyo? Ni mambo ya ile picha?"

"Hapana! Ni kuhusu ajali ya mke wa mheshimiwa!"

"Ooh! My God. Jona, I didn't do it. Honestly!" (Ooh! Mungu wangu. Jona, sijalifanya hilo. Ukweli kabisa!)

ENDELEA

Jona akamtaka waonane kesho kwa ajili ya maongezi zaidi. Akakata simu na kuendelea kuwaza. Kuna yeyote zaidi Miranda?

Aliamini hata kama kuna yeyote zaidi ya Miranda basi njia ya kumpata mtu huyo ni kwa kupitia Miranda tu. Atampatia namna ya kupiga hatua hiyo.

Akatulia baada ya muda kidogo, akampigia simu Marwa. Simu ikaita pasipo matokeo. Akagundua Marwa atakuwa yupo kazini kwa muda huo, hivyo ni ngumu kupokea!

Akaachana naye avute subira mpaka majira ya mchana, aotee muda mwanaume huyo atakuwa akipata chakula cha mchana.

Muda ukasonga.

Kwenye majira ya mchana, saa saba na robo, Marwa akawa kantini akipata chakula. Alikuwa ameketi mwenyewe akijitenga kidogo na wenzake. Na kwakuwa Marwa hakuwa amezoeana na yeyote, basi hakuna aliyemuwazia.

Lakini mwanaume huyo alikuwa anamngoja Panky. Alitegemea atakuja kula na hivyo basi waketi pamoja kwa hapo pembeni.

Muda ukasonga kidogo mpaka majira ya saa saba na dakika ishirini na tano, Panky akaonekana akichukua chakula. Akatazama huku na kule pa kukaa, Marwa akanyoosha mkono amwone, Panky akaenda huko.

"Nilikuwa nakungoja muda wote huo."

"Aanh! Kuna kazi kidogo nilikuwa nazimalizia. Yani huko waliponipeleka ni kama mwehu, kazi kazi kila saa simu tu!"

"Wamekupeleka wapi kwani?"

"Uhasibu na mawasiliano."

Vile vile kama Marwa alivyokuwa anawaza. Ni ngumu sana kwa Sheng kuajiri mtu mpya kwani inakuwa ngumu sana kwa mtu huyo kujua na kuufuata utaratibu wa kazi chini yake hivyo hupendelea kutoa mtu huku na kumweka pale, kama haitaathiri.

"Ila huko hamna kiyoyozi," Marwa akatania. Wakacheka. Wakawa kimya kidogo wakitafuna.

"Sasa kuna kazi ya kufanya," Marwa akaingizia. Kabla hajaendelea simu ikaita, alikuwa ni Jona.

"Yah! Ndo nipo naye ... poa, baadae."

Akaweka simu mezani, na kumwambia Panky maagizo toka kwa Jona. Nini anatakiwa kufanya akirejea ofisini kwake.

"Hope tumeelewana!" Marwa akamalizia.

"Usijali, nitalifanyia kazi. Na nadhani hao watu watakuwa wameshaondoka. Taarifa zao zitakuwepo kule kimalipo. Nitatazama."

Wakamalizia kula, wakarejea kazini. Panky akaanza kukagua nyaraka za risiti na taarifa kadhaa kwenye tarakilishi, pesa zilizotoka hivi karibuni.

Akanoti pembeni na kumtumia ujumbe Marwa kwa kuhofu baadae anaweza akakawia kutoka hivyo hatokutana naye. Alipotuma ujumbe huo, akaendelea na kazi yake kama kawaida.

Lakini baada ya muda kidogo, akaja kuitwa.

"Unahitajika ofisini kwa mkuu," alisema mwanaume mmoja akisimama mbele ya Panky.

"Mimi?"

Japo hakujua anaitiwa nini, moyo wake ukaanza kumtwanga. Alipaliwa na hofu. Kuitwa na mkuu halikuwa jambo dogo hata kidogo.

"Ndio, wewe!" Akasema mleta wito.

"Sawa, nakuja," Panky akajibu.

"Nakungoja twende," mleta wito akamsihi.

"Kwani lazima twende wote?"

"Ndio! Nimeambiwa nikupeleke."

Hapa Panky akazidi kupata hofu. Ina maana wanahisi anaweza kukimbia? Akaacha kazi zake na kuongozana na mwanaume huyo mpaka ofisini mwa Sheng. Alipofika, yule aliyemsindikiza akaagizwa angoje nje.

"Panky," Sheng akaita huku akitazama karatasi kadhaa juu ya kashelf kake kadogo ka kioo juu ya meza.

"Naam, mkuu!" Sheng akaitikia. Mikono yake ilikuwa inatetemeka na kujawa jasho.

Sheng akamuuliza juu ya kazi aliyompatia hapo kitambo ya kummaliza Jona. Panky kusikia hivyo akaishiwa nguvu! Sasa akajua mwisho wake umewadia.

Sheng akiongea kwa lafudh yake ya kimandarin, akamwambia Panky kwamba siri yake isingeweza kudumu kwa muda. Alimpatia kazi na kwa kumdharau hakuitenda, akaja kumlaghai.

Na kwa asili ya uongo wake, inaonyesha ana mahusiano na Jona kwani mwanaume huyo alihama mara moja baada ya yeye kuja kusema amemmaliza.

Panky akalia kuomba msamaha. Hakuwa na lingine sasa la kufanya zaidi ya hilo. Akalia abakiziwe uhai wake. Atakuwa mtiifu kwa Sheng na hatorudia tena kufanya kosa.

Lakini kwa Sheng hayo yote yalikuwa makelele. Hakumwelewa Panky hata kidogo. Akafungua droo yake na kuchomoa binduki ndogo, akaitazama ina risasi ngapi.

Nne.

Akaikoki na kumwonyeshea Panky mdomo wa bunduki kwenye paji lake la uso.

"Nina mke na watoto wananitegemea. Pia wazazi huko kijijini. Tafadhali bakiza uhai wangu!" Panky akawaga machozi.

Sheng akabofya kitufe cha bunduki mara nne! Chuma zikatoboa kichwa cha Panky na kumlaza chini akiwa mfu!

Baada ya risasi hizo, yule mwanaume aliyeambiwa angoje nje, akaingia ndani na kubeba mwili wa Panky.


**


"Sasa? Si naweza nikatoka?" Akauliza Miriam. Sasa alikuwa ameboreka zaidi kiafya. Alikuwa anawasiliana na mama aliyempokea ambaye alikuwa mlangoni akitazama huko nje.

Ni majira ya jioni sasa. Jua lilikuwa linaelekea kuzama. Na siku hii Miriam aliona inafaa kwake kutoroka.

Tayari mtoto alishaenda kukagua huko nje mpaka barabarani. Akarejesha taarifa kwamba kupo salama.

"Ndio, njoo," mama akamruhusu, Miriam akatoka mpaka huko nje, akamkumbatia mwenyeji wake kumuaga akimshukuru sana. Na akamuahidi atarudi kuja kumshukuru siku moja.

"Bado hutaki nikusindikize?" Akauliza mama mwenyeji.

"Hapana, hatari niliyokuweka kwa muda wote huo inatosha. Acha hili nipambane mwenyewe."

Miriam akaanza kutembea akitazama chini. Kulikuwa na kaumbali kutoka hapo mpaka kituoni. Alikazana kutembea mkononi akiwa amebebelea kamfuko. Na mwili wake ukiwa umehifadhiwa ndani ya dira chakavu alilopewa na mwenyeji wake.

Akiwa amekaribia kituoni, kuna mtu mmoja akamuita.

"We mwanamke!"

Hakugeuka. Akakazana kutembea. Sauti ikamuita tena, we mwanamke we mwanamke. Ila hakugeuka abadani.

Akahisi anafuatwa. Watu walikuwa wengi kiasi chake hivyo kidogo akawa hana woga. Akatembea kwa kasi mpaka akafika kituoni kungoja basi.

"Napanda hilo linalokuja!" Akajisema kifuani. "Hata kama limejaa vipi."

Akatazama kushoto na kulia kwake, watu wote walikuwa wametulia, lakini akamwona mwanaume aliyemtilia shaka. Mwanaume huyu alikuwa amevalia shati jeusi, mweupe kwa rangi mwenye macho mekundu.

Naye huyu mwanaume akamtazama Miriam, wakakutana macho kwa macho. Moyo wa Miriam ukadunda kwa kasi.

Akatazama barabara. Gari alilokuwa analingojea lilikuwa limekaribia kufika. Akaendelea kuapia moyoni kwamba lazima alipande gari hilo, hata iweje.

Gari likasimama, yalikuwa ni yale mabasi ya zamani sana. Lilikuwa linamwaga moshi mzito mweusi ambao ukiujumlisha na vumbi la barabara, basi kupata mafua ama matatizo ya kifua ilikuwa haiepukiki.

"Arusha town hiyo!" Konda akapaza sauti. Lakini gari lilikuwa limejaa mno. Hakukuwa hata na pa kukanyaga sembuse pa kusimama.

Lakini wanaume wawili wakaliwahi, ikiwemo na Miriam watatu, wakang'ang'ana kulidandia. Wanaume wakafanikiwa, Miriam akaambiwa na konda angoje lijalo, hataweza.

Hakuwa namna akangoja. Akatazama mahali alipomuona mwanaume yule aliyekuwa anamtilia shaka, hakumwona!

Akajiuliza kaenda wapi? Akaangaza macho huku na kule lakini kabla hajamaliza msako wake wa macho, ghafla akasikia sauti ya gari lingine laja.

Akajiweka sawia kung'ang'ana. Sasa gari liliposimama akawa wa kwanza kufika mlangoni, akazama ndani!

Japo alikuwa amebanwa haswa, hakujali. Alichotaka ni kutoka tu eneo hilo. Lakini kuna jambo.

Kuna jambo ambalo hakuwa analifahamu.

Nyuma yake alikuwa amesimama mwanaume yule aliyekuwa anamtilia hofu. Kumbe naye aligombania gari hilo na kuzama humo ndani.

Miriam alikuja kufahamu hilo baadae baada ya kukaribia Arusha town! Lakini ajabu ni kwamba, hakuelewa kuna nini ama nini kilifanyika, akajikuta anapoteza fahamu.

"Ni dada yangu, anaumwa!" Miriam alisikia sauti ya mwanaume ikisema huku yeye akipotelea kwa kudhoofu.

Alihisi kabisa sauti hii itakuwa ni ya mwanaume yule aliyemtilia mashaka, lakini hakuweza hata kupayuka wala kujikomboa.

Pap! Akawa gizani kamili asijue kinachoendelea.

**
 
*ANGA LA WASHENZI -- 70*

*Simulizi za series*

ILIPOISHIA

Alihisi kabisa sauti hii itakuwa ni ya mwanaume yule aliyemtilia mashaka, lakini hakuweza hata kupayuka wala kujikomboa.

Pap! Akawa gizani kamili asijue kinachoendelea.

ENDELEA

Akaja kupata fahamu baada ya muda asioujua. Alikuwa begani mwa mwanaume aliyekuwa anatembea kwa miguu akipiga hatua kubwakubwa.

Alipoangaza kumtazama mwanaume huyo akagundua ndiye yule aliyekuwa anamtilia mashaka. Sasa afanyaje?

Akaangaza kushoto na kulia, akayaona mazingira batili. Haya hayakuwa mazingira ya Arusha town. Palikuwa pakavu mno, majani yaliyokauka, barabara ngumu iliyojawa vumbi na mawe.

Oh my God! Sasa akatambua alikuwa anarejeshwa kwa Nyokaa.

Hapana! Akasema nafsini. Kamwe sirudi huko nikiwa hai, labda mfu. Lakini atajinasuaje? Ni wazi asingeweza kupimana ubavu na yule jibaba!

Akaazimia kutafuta namna. Kweli, penye nia pana njia, muda mfupi akaipata ya kwake. Aliona alama ya bunduki kiunoni mwa mwanaume aliyembeba. Ilikuwa ni bunduki ndogo iliyofunikwa na shati alilolivaa.

Akawaza kuikwapua imuokoe. Japo hakuwa anajua namna ya kuitumia, itamtisha adui yake mwishowe akapata upenyo.

Ndio, hiyo ilikuwa ni njia yake sahihi kwani njia ya kwanza aliyoifikiria ya kupiga yowe kali isingemsaidia kwa muda huo. Mahali walipokuwa wanapita hapakuwa na ishara ya mtu kabisa.

Angejichomesha.

Sasa, moyo wake ukiwa unaenda mbio, akaanza kuhesabu. Akifika tatu, anasita. Akifika tatu, anasita kwa woga.

'I have to do this! Miriam you have to!' (Inanibidi nifanye hivi! Miriam inakubidi!) akajisemea kifuani.

Akafunga macho kwanguvu, akahesabu, ilipofika tatu akavuta shati la yule mwanaume upesi na kuchomoa bunduki. Akamwekea kichwani.

"Nishushe haraka kabla sijakumaliza!" Akaamuru. Yule mwanaume akamshusha akasimama mwenyewe.

"Ulidhani utanipeleka huko nilipotoka?" Akauliza kwa kiburi. "Umekosea sana. Utaenda mwenyewe."

Akamwamuru mwanaume huyo ageuke nyuma na akimbie kwa nguvu zake zote. Akihesabu mpaka tatu asimwone, la sivyo atamfyatulia risasi.

Miriam hakuwahi kuua maisha yake yote. Tukio la kumuua binadamu mwenzake lilikuwa ni zaidi ya mtihani. Yeye mwenyewe kifuani mwake alikuwa anafahamu hawezi kulifanya.

Lakini katika namna ya ajabu, mwanaume yule akiwa amenyooshewa mdomo wa bunduki, hakutii agizo alilopewa. Badala yake hata mikono aliyokuwa ameiweka juu akaishusha na kisha akatabasamu.

"Nimesema geuka ukimbie kuokoa uhai wako. Umechoka maisha unh?" Miriam akafoka.

Yule mwanaume akacheka. Kisha akamsogelea.

"Simama hapo hapo! ... nimesema simama!" Miriam alifoka lakini mwanaume yule hakutii, akafyatua bunduki, ajabu hakikutoka kitu. Akafyatua tena na tena, hola!

Mwanaume yule akampokonya bunduki hiyo.

"Ukitaka kushoot, unakoki kwanza bunduki, sawa?" Akamwambia Miriam huku akikoki bunduki kisha akamwamuru: "Haya sasa geuka twende!"

Miriam akanyong'onyea. Akapoteza matumaini ya kutoroka. Lakini akaapia moyoni mwake hatokuwa radhi kurejeshwa tena kule alipotokea.

Labda tu awe maiti.

"Nimekwambia geuka twende!" Akarudia mwanaume akitoa macho ya kutisha lakini Miriam akaendelea kusimama kana kwamba hajasikia.

Kuonyesha hana mchezo, mwanaume akapiga risasi kandokando ya Miriam kisha akarudia sentensi yake akimtaka Miriam waende.

"Siendi, niue!" Miriam akamwambia pasi na hofu. Kabla mwanaume huyo hajafanya kitu akasikia sauti nyuma yake, kilikuwa ni kishindo cha mtu kwa mbali.

Haraka akageuka kutazama. Kweli alikuwa ni mama aliyekuwa amebebelea ndoo ya maji kichwani. Mama huyo alikuwa ametoa macho ya mshangao akiwatazama.

Mwanaume akamgeuzia bunduki na kufyatua risasi moja, heri ikamkosa, mama akadondosha ndoo na kukimbia kama mwehu akipiga ukunga.

Mwanaume huyo alimpogeukia Miriam akakutana na jiwe la uso! Akadondoka chini akiacha bunduki. Akamwaga damu za kutosha akilalama kwa maumivu makali.

Miriam akaokota bunduki.

"Tatizo nikikuacha, bado utanisumbua!"

Akafyatua bunduki pasipo kumtazama mlengwa wake. Hata alipomaliza kumfyatulia hakumtazama akaondoka zake. Alikuwa anaogopa. Alijua ameshamuua mwanaume huyo.

Kumbe hizo risasi zote zilipiga chini!

***

"Honestly I thank God, kwanza shukrani ziende kwake. Na pia kwa huyo malaika aliyemtuma kuniokoa," alinguruma bwana Kamau Githeri kwenye televisheni ya KTN wasaa wa taarifa ya habari.

"Unaweza kutuambia ilikuwaje hasa?" Akauliza ripota. Kwa wakati huo maandishi yaliyokuwepo chini ya video yakisomeka kama ifuatavyo:

'MHESHIMIWA K. GITHERI APONA CHUPUCHUPU YA KUCHUNGULIA KABURI'

"Ni ujhumbe tu nilipongeaga kwa email," akaeleza mheshimiwa Githeri. "ukinitell kwamba nipo about kuwa ambushed na wauajhi. I didn't ignore it, nikatake steps along with my family immediately!"

Wakaonyesha walinzi wa nyumba ya bwana Githeri, wawili, wote walikuwa wameuawa pamoja na mbwa wao.

"Unadhani ni kwanini walitaka kukuua?" Akauliza ripota.

"I think ni haya tu issues za politics, nothing more," akajibu mheshimiwa. "Furthermore, nisingependa kuongea sana. Shauri yangu iko kwa polisi hands as we talk."

Baada ya hapo KTN wakaonyesha na upande wa pili wa mheshimiwa Otieno. Hapa kichwa cha habari kikabadilika na kusomeka ifuatavyo:

'HON. OTIENO AMIMINIWA RISASI KUUAWA'

Wakahojiwa baadhi ya mashahidi wa tukio hilo na mhusika mmoja wa familia akieleza namna walivyoguswa na msiba huo kwa ndani.

Hata mhusika huyo wa familia hakuweza kueleza kwa muda mrefu, akakabwa na kilio, mahojiano yakakatishwa.

Habari ikaendelea kurushwa. Sasa wakihamia kwa viongozi wa bunge wameupokeaje msiba huo na mashambulizi hayo ya ghafla ndani ya siku moja huku mojawapo likizaa matunda.

Spika akanena kulaani tukio hilo akisema linatishia uhuru wa bunge kama mhimili muhimu wa serikali kufanya kazi yake. Lakini zaidi akatupa lawama za waziwazi kwa karani wa bunge ambaye alipuuzia ujumbe aliotumiwa na msamaria mwema kuhusu shambulizi hilo.

"Somehow, he is responsible for such act!" (Kwa namna fulani, anawajibika na tukio hilo!)

Baada ya hapo ripota akasema uchunguzi wa kipolisi unaendelea, habari hiyo ikapita zikiendelea zingine.

"Shit!" Sheng akasaga meno. "How is this possible?" (Linawezekanaje hili?)

Alikuwa ameketi sebuleni akikodolea televisheni yake kubwa iliyomeza ukuta. Akatetemeka kwa hasira.

Ni nani aliyetuma taarifa za kutaka kuuawa viongozi hao? Ni swali lililomnyima raha. Hakuweza kukaa nalo kifuani akanyanyua simu yake ya mkononi akapiga.

Akaagiza watu wote wa vitengo vya mawasiliano pamoja na heads wa WAVES zote wafike ofisini kwake kesho asubuhi na mapema.

Wanapokuja wahakikishe wana maelezo yanayojitosheleza. La sivyo wataingia hai na kutoka wafu!

**

"Dada, una mgeni," mfanyakazi alimtaarifu Miranda.

"Nani huyo?" Miranda akauliza kwa hasira. Alikuwa ameketi kitandani kwake akiperuzi kwa kutumia tarakilishi yake mpakato. Mwilini ana gauni la kulalia.

Majira ni saa nne usiku.

"Simjui mimi. Ni mzungu!" Akajibu dada wa kazi. Miranda akashtuka. Moja kwa moja akawaza atakuwa ni BC.

Lakini mbona hakunipa taarifa?

Akanyanyuka upesi na kwenda sebuleni. Kweli akamkuta BC ndani ya suti kama ilivyo ada. Akamkaribisha na kusalimiana.

Pasipo kupoteza muda BC akamuuliza:

"Are you the one who did it?" (Wewe ndiye uliyelifanya?)

Miranda akatikisa kichwa.

"I didn't do it," (sijalifanya) akajibu kwa msisitizo.


***
 
Ooo my god !!! Panky...!!! He has gone too soon[emoji134] [emoji134] [emoji134]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…