Anga la washenzi na Joana anaona kitu usiku

*ANGA LA WASHENZI -- 71*

*Simulizi za series*

ILIPOISHIA

"Are you the one who did it?" (Wewe ndiye uliyelifanya?)

Miranda akatikisa kichwa.

"I didn't do it," (sijalifanya) akajibu kwa msisitizo.

ENDELEA

BC akashusha pumzi ndefu maana sasa alikuwa amechanganyikiwa. Kama si Miranda aliyetekeleza lile agizo, basi ni nani mwingine?

Hofu ilimuingia ukute wamezamishwa mtegoni na 'wajanja' kisha waumie huku wakiwanufaisha wengine. Lakini hao 'wajanja' ni wakina nani?

BC akamuuliza Miranda yeye alikuwa amepangaje kummaliza yule mwanamke. Miranda akasema hakuwazia njia ya ajali kabisa kwani ni risk sana. Aliwazia kumtwanga tu risasi akiigiza jambazi ili kufinya ulimwengu wa kipepelezi.

Sasa sio tu kwamba walikuwa kwenye rada za polisi, kama vile Miranda alivyosema kuwa anatafutwa na inspekta Jona, bali pia walikuwa na kazi ya kumng'amua mtu aliyewazidi hatua na kulifanya hilo akilenga kuwa 'frame' wakamatwe.

BC akamuaga Miranda na kisha akaenda zake. Alimwachia Miranda kazi ya kufanya, ashirikiane na Jona hatua kwa hatua kumjua mtu huyo. Lakini kwa wakati huo akijiweka safi, mwenye mikono isiyo na hatia.

Usiku huo kwa Miranda ukawa mgumu haswa. Alijaribu kuchambua kila mazingira aliyoyapitia kuangaza kama kuna mahali alifanya kauzembe, hakupata!

Huu mtihani ulikuwa mgumu sana.

Lakini mwanamke huyu alisahau jambo moja. Jambo moja lililomtia kwenye mtego wa ngiri. Hakufahamu, aidha tuseme alisahau kuwa ni yeye aliyefanya akajazwa kwenye rada ya adui.

Adui huyu ni mwerevu mno. Hakurupuki na hubonyeza kitufe pale anapoona anatakiwa sasa kufanya hivyo.

Unakumbuka kipindi kile Miranda alipojionyesha runingani akiwa na mke wa Boka akitambulishwa kama balozi wa kampuni hiyo ya urembo na vipodozi na akinadi bidhaa za kampuni hiyo?

Basi kama wakumbuka, mipango miwili ilianzia hapo, mosi ya kumsaka Miranda, pili, kuimaliza kabisa kampuni ya mama huyu.

Lakini yote hayo yatekelezwe katika njia 'laini'. Mama afe, Miranda afe pia ama akafie jela.

Kila Miranda alipokutana na Boka, hakujua anatazamwa na kufuatiliwa. Na ijapokuwa wanaomfuatilia hawakujua nini Boka na Miranda walikuwa wanaongea, kiutuzima, ukubwa dawa, wakang'amua watu hao wapo kwenye mahusiano.

Sasa kuna nini tena hapo?

Miranda akawa anatafutwa ajae kiganjani. Kwenda kuonana na mke wa Boka hotelini na kugombana huko, kote kulikuwa kunatazamwa.

Sasa je kuna sehemu gani ya kumaliza mchezo kama hii? Endapo tukimmaliza mke wa Boka, polisi watamalizana na Miranda. As simple as that!

Hakikisha mke anakufa, shoga yake anabaki kutoa ushahidi. Shoga huyu lazima atamtuhumu Miranda kwani alikuwapo wakati zogo latukia.

Unadhani atamhisi nani mwingine? Ni Miranda anataka kumuua mke ili abakie na mume wa mtu!

Miranda alikuwa ana fumbo hili kubwa kulifumbua. Yeye pamoja na Jona.

**

Majira ya saa nne asubuhi.

"Uliona wakati akiitwa?" Jona akamuuliza Marwa. Mezani kulikuwa kuna vikombe viwili vya chai. Vikombe hivi vilikuwa vimejaa lakini chai ikiwa imeshapoa. Tangu viwekwe hapo mezani havikuguswa.

"Sikuona akiitwa," alijibu Marwa. "Tuliachana vizuri tu kila mtu akaenda kufanya kazi yake. Baadae tulipotoka, sikumwona. Nikajua atakuwa ametingwa kwani aliniambia anaweza akawa yupo tight. Kumbe ndo' alikuwa ashauawa!"

Hizi habari zilikuwa ngumu sana kwa Jona. Alijaribu kujilazimisha aziamini lakini kichwa chake kikagoma kabisa. Kwanini Panky ameuawa?

"Marwa, inabidi uwe makini sana," Jona akashauri. "Hatuwezi jua pengine Panky ameuawa kwasababu za kipelelezi ambao unaweza ukakuweka hatarini nawe pia."

Marwa akanyamaza. Alikuwa anatazama chini uso wake ukimezwa na hofu. Aliogopa sana. Kifo cha Panky kilimshtua na kumkumbusha kuwa hayupo salama abadani.

Aliwaza mtu atakayefuata kuuawa atakuwa ni yeye. Si mwingne. Mawazo hayo yakamfanya asimsikilize kabisa Jona alichokuwa anaongea.

Jona akamtikisa.

"Marwa, tupo pamoja!" Marwa akashusha pumzi ndefu alafu akanyaka simu yake mezani na kumkabidhi Jona.

"Alinitumia ujumbe muda mfupi baada ha kuachana toka kula. Akiniambia hao ndo' watu waliotumiwa pesa muda si mrefu kwa ajili ya malazi, chakula na makazi nchini Kenya."

Jona akatazama majina hayo, akamuuliza Marwa kama anawafahamu hao watu, anaweza kumsaidia angalau kwa picha.

Marwa akazama ndani ya tarakilishi yake, punde akapata picha na kumwonyesha. Jona akatumia simu yake kudaka picha hizo na kuzitunza.

Watu hao walikuwa ni Lee na wenzake watatu: Devi, Nigaa na Mombo.

"Ahsante sana," Jona akashukuru. Marwa akamtazama mwanaume huyo na kumwambia pasi na chembe ya masikhara.

"Hapo ndiyo utakuwa mwisho wa kukusaidia. I am out!"

Jona akaduwaa.

"Una maanisha nini Marwa?"

Marwa pasipo kupepesa macho akamwambia hataki tena ushirika. Mpaka hapo alichokifanya inatosha. Anaomba asihusishwe kwa njia yoyote ile tena!

"It is enough. I cant take this risk anymore!" (Inatosha. Siwezi kubeba hii hatari zaidi!)

Haikujalisha Jona aliongea nini, Marwa hakutaka sikia. Alimtaka aende na amwache na maisha yake kama alivyomkuta.

Ni bora maisha yake ya awali kuliko haya ya sasa ambayo anaweza akakosa vyote. Kheri sasa anapata kimoja, wazazi wake kuwa hai. Inatosha!

Marwa alikuwa ame 'panik'. Alikuwa pia na hasira ndaniye ambayo ilizidi kujionyesha kadiri alivyokuwa anaongea.

Jona akaona huo si wasaa wa busara kwake kukaa hapo, akaondoka zake.

**

Aliegemea kiti cha taksi akiendelea kuwaza. Alifahamu fika kwa mawazo haya kama angelipanda daladala angepitishwa kituo. Application yake ya UBER ikamsaidia kupata usafiri chap!

Alimfikiria Panky na kisha Marwa. Marwa na kisha Panky. Akaja kubanduliwa toka kwenye mawazo hayo na mlio wa simu. Alikuwa ni Kamanda.

"Umefikia wapi?"

"Bado naendelea na upepelezi, mkuu. Nitakufahamisha, sipo maeneo mazuri."

Simu ikakata. Sasa Jona akatazama mandhari ya nje ya gari. Akapata kuwaza kidogo kuhusu kesi ya mke wake Boka, akapata wazo.

Alikuwa anaelekea hospitali kuonana na rafiki wa mke wa Boka kisha aende kwa Miranda. Lakini akaona ni vema apite kwa Boka kisha aende mawasiliano.

Akapita huko, akachukua simu na namba ya simu ya marehemu kisha akaelekea mawasiliano ambapo alifanya utaratibu wa kupata mawasiliano ya mwisho na marehemu, akaenda kumalizia utaratibu wake huo TIGO.

Akachapiwa jumbe zote na hata akapata 'access' ya 'recorded calls' za mwisho. Yote hayo yaliwezekana pasipo kuchukua muda sana kwa kujieleza anayahitaji kiupelelezi.

Napo kwa wakati huo ...

Mlio wa risasi ukasikika mara mbili toka ofisini mwa Sheng.

Tah! - tah!

Mlango ukafunguliwa ikatolewa maiti ya mtu mwenye asili ya China! Wanaume wawili walimbebelea wakielekea upande wa kushoto mwa jengo.

Marehemu huyu alikuwa ni Moderator! Moderator wa SPACE BUTTON. Tayari roho yake ilishanyofolewa na mkono wa Sheng baada ya kubainika ni yeye ndiye alifanya uzembe.

"I want that traitor alive!" (Namtaka huyo msaliti akiwa hai!) Sheng alisikika akifoka ndani ya ofisi kisha akabamiza meza.

Mara wanaume kadhaa wakatoka ndani. Wakaendelea kuteta kadiri walivyokuwa wanasonga mbali na ofisi ya mkuu.

Sasa wazi, Marwa alikuwa hatiani!

Hati ya hatiani. Uzembe mdogo hauruhusiwi ndani ya ANGA LA WASHENZI - ANGA LA WAUAJI. Ndani ya dakika chache tu kipindi cha usiku, Marwa baada ya kufanya kazi ya udukuzi, akasahau ku 'log-out'.

Hakujua alisahau na maisha yake hapo, haraka akatambuliwa. Uangalizi ulikuwa mkubwa sana haswa baada ya kubainika kuwa mawasiliano yao yalidukuliwa na kupelekea zoezi la kuokolewa kwa walengwa.

Haraka alipojulikana, akajazwa kwenye GPS na haraka tena akajulikana makazi yake yalipo. Haya makazi yalikuwa ya nani? - Marwa! Toka SPACE BUTTON - BIRD ONE.

Moderator angeachwaje hai?

**

"Miranda, kila kitu kinakuonyeshea ni wewe," Jona alisema baada ya kunywa maji mafundo kadhaa.

Miranda akasonya akitikisa kichwa.

"Jona, I swear to God. Sijafanya hicho kitu kabisa kabisa!"

"Sasa tatizo ni kwamba inabidi uthibitishe hilo. Si kwa maneno tu," Jona akasema akimtazama Miranda kana kwamba mwalimu amtazamavyo mwanafunzi mtoro.

Miranda akashika kichwa chake na kukikuna kwanguvu.

"Pengine ni maadui zangu," Miranda akajitetea kidhaifu. "Huwezi jua?"

Hata mwenyewe alijiona anaongea kitu ambacho haki 'make sense'. Jona alikunywa maji tena alafu akamtazama. Akamuuliza ni lini walianza ile projekti ya kupeleka bidhaa zao Kenya.

Miranda baada ya kufikiria kidogo, akasema anakumbuka ilikuwa ni punde tu baada ya majadiliano na makubaliano yaliyofanyika nchini Kenya kuwa bidhaa toka nchi za Afrika Mashariki zipewe kipaumbele sokoni, zipunguziwe makato na kufanyiwa wepesi.

Mke wa Boka akaona hiyo ni fursa adhimu kwake kulivamia soko hilo la vipodozi na urembo.

Baada ya maelezo hayo, Jona akamuaga Miranda aende zake lakini akimuahidi atakuwa anamtembelea mara kwa mara.

"Naamini hautaufanya uhuni wako," alimwonya akiwa ameushikilia mlango.

**

Saa saba usiku ...

Gari jeusi lilisimama kwa mbali hivyo halikuonekana vema ni la aina gani. Wakashuka wanaume wawili waliovalia suti nyeusi, tai nyekundu na vinyago vyeusi.

Wanaume hawa walikuwa wakakamavu wakitembea kwa haraka, wazi wakienda kutenda tukio.

Kutokana na giza lililokuwepo na pia mavazi yao, ilikuwa ngumu kuwatambua. Waliufikia ukuta mmoja akatumika kama ngazi mwenzake kukwea mpaka juu, alafu naye aliye juu akamvuta mwenzake wakaingia ndani.

Hakuna hata chembe ya kelele iliyotokea hapa. Na yote haya yalifanyika ndani ya sekunde tu, wala si dakika, kuthibitisha kwamba wanaume hawa walikuwa wana mafunzo.

Walitumia waya kufungulia kufuli za milango, na kwa upande wa magrili, kabla hawajafungua walimiminia mafuta viungoni, basi yakafunguka pasi na tone la makelele!

Mpaka wanafika kitandani mwa Marwa, walikuwa wametumia dakika mbili tu tangu walipotoka kwenye usafiri wao!

Wakamwamsha Marwa kwa kumpiga na kitako cha bunduki kisha wakamtaka aongozane nao kimya kimya!

"Sasa jifanye mjanja uone kilichomfanya fisi awe na miguu mifupi!

Marwa akatetemeka sana. Jasho likamiminika kama nusu ndoo. Alihisi kila aina ya haja. Aliona roho inamtoka mbele yake na hana cha kufanya!

Akasimama na kuswagwa alekee nje.

Kufika huko kabla hawajatoka, wakasikia sauti ya mluzi! Wanaume watekaji wakaangaza kushoto na kulia, hawakuona mtu!

Wakatazamana.

Sauti ya mluzi ikalia tena, mara hii ikifuatisha melodi za muziki.

***





Sent from my SM-J110F using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…