Anga la washenzi na Joana anaona kitu usiku

Anga la washenzi na Joana anaona kitu usiku

Tusubir night kali au tukamwage mate mkuu mollel??
 
*ANGA LA WASHENZI - MWISHO WA MSIMU WA KWANZA*

*Simulizi za series*

ILIPOISHIA

Kufika huko kabla hawajatoka, wakasikia sauti ya mluzi! Wanaume watekaji wakaangaza kushoto na kulia, hawakuona mtu!

Wakatazamana.

Sauti ya mluzi ikalia tena, mara hii ikifuatisha melodi za muziki.

ENDELEA

Watekaji wakachanganyikiwa. Ni nani huyo anawafanyia mchezo? Wakaangaza tena wasifanikiwe. Wakawa wamepigwa na bumbuwazi.

Wakatishia kumuua Marwa endapo huyo apigaye mluzi hatajitokeza mwenyewe. Lakini kinyume na matarajio, mpiga mluzi hakujitokeza!

Na sasa hivi badala ya kupiga mluzi akaongea:

"Najua hamuwezi kumuua. Kama mngelikuwa mmepanga hivyo, msingelikuwa na haja ya kumtoa nje."

Kisha kukawa kimya kidogo.

Kutazama huku na kule, ghafla akatokea mwanaume hewani! Alikuwa ni Jona. Hamaki kutazama, bunduki ikapigwa teke na kisha Jona akajifichia kwenye mwili wa mwanaume mtekaji.

Risasi mbili zikatupwa! Mwanaume mtekaji alimpiga mwenzake kwa pupa na kumuua. Jona akamrusha yule mtekaji marehemu kwa mwenziwe, akamdaka, ikawa kosa.

Kabla hajafanya jambo, Jona akawa amemchapa teke zito, kinyago na bunduki zikarukia kando. Kuja kukaa sawa, tayari ashawekwa chini ya ulinzi.

"Tulia kama maji mtungini!" Jona akamwamuru. Wakamfunga mikono na miguu na kisha kinywa!

Baada ya muda mfupi wakatoka wanaume wawili nje ya uzio. Walikuwa wamevalia suti na vinyago. Wakatembea kwenda kufuata lile gari lililowaleta watekaji.

Walipolifikia wakamuweka dereva chini ya ulinzi na kumwamuru asogeze gari lake kwa nyumba ya Marwa. Naye wakamfunga miguu na mikono na kinywa, wakampakia na yule marehemu kwenye gari wakawapeleka kituoni.

"Nitakuja kuwahoji mwenyewe," Jona alitoa maelezo kwa polisi kisha wakitumia lile gari la wavamizi, wakayeya.

Marehemu akapelekwa mochwari.

Lakini bado kichwani mwa Marwa kulikuwa na maswali. Jona aliwezaje kufika pale nyumbani kwake kumuokoa? Alijuaje kama wavamizi watakuja kummaliza usiku huo?

Kusema ukweli alimwona Jona kama malaika kwani alishajua amekwisha usiku huo. Kitendo cha mwanaume huyo kutokea na kumwokoa, kulikuwa ni muujiza. Bado hakuamini!

"Ahsante sana, Jona," akashukuru.

"Usijali," Jona akamjibu akitazama mbele. "Ni kazi yangu."

Kukawa kimya kidogo.

"Najua una maswali kichwani," Jona akasema akili ya Marwa. " unawaza nilifikaje pale kwako kwa muda muafaka kiasi kile. Ila tambua nilikuwa nakuwaza. Sikuweza kulala nyumbani kwangu kwa amani kabisa. Na akili yangu iliniaminisha haupo salama. Kama Panky ameuawa, basi nawe lazima utakuwa kwenye rada zao."

Baada ya kusema hayo, Marwa akaomba msamaha kwa Jona. Alitenda kosa kumfukuza kiasi kile na hata amemsaliti kwenye mapambano.

Jona akamwambia asijali, sasa watazame ya mbele. Amelenga kumfundisha mwanaume huyo sanaa ya mapambano, martial arts, ikapate kumsadia kujilinda kwani atahitaji sana mafunzo hayo kwa kipindi hicho.

Marwa akaridhia. Wakaenda nyumbani kwa Jona na kupumzika. Lakini Marwa hakulala kabisa kwa woga. Alihisi wale majamaa wanaweza kurudi tena kumuua.

Kila aliposikia sauti ya kitu akakurupuka na kuangaza. Alipomtazama Jona yeye alikuwa tayari anakoroma baada ya kunywa vinywaji vyake vikali.

Kama haitoshi Marwa alikuwa anawafikiria na wazazi wake. Yeye amenusurika kifo lakini vipi wazazi wake ambao wanategemea kupata antidote toka kwa Sheng? Wataishije?

Ina maana atawaona baba na mama yake wakifa huku hana cha kufanya? Akakosa amani.

Akajigeuza huku na huko. Akajibaraguza kitandani lakini hakupata usingizi kabisa. Akaona kuna haja ya kupumbaza kichwa.

Akanyanyuka na kumalizia kinywaji alichobakiza Jona chupani. Kilikuwa ni kinywaji kikali mno na yeye hakuwa mzoefu wa hayo mambo kabisa.

Sasa hakuchukua dakika akalala usingizi ambao hajawahi kuupata tangu azaliwe. Kama mfu!

Alikuja kuamka saa tatu asubuhi kichwa kikiwa kinamgonga haswa. Kumtazama Jona, hakuwepo! Alishaondoka akimwachia maelekezo kwa njia ya maandishi,

Aikute supu jikoni.

***

Saa ya ukutani ilikuwa inasema ni saa tano asubuhi hivi sasa. Jona hakuwa mtu wa kukaa ofisini mara kwa mara, ila leo hii huu muda ulimkuta akiwa kwenye kiti nyuma ya meza iliyobebelea tarakilishi.

Kuna mambo kadhaa alikuwa anayapitia haswa kuhusu kesi ya ajali ya mke wake Boka. Alikuwa anachambua maelezo ya Miranda akaona kuna kitu mule ndani yake.

Kuna jambo la kulifuatilia!

Mojawapo ya kanuni ya upelelezi ni kwamba kila kitu mbele yako ni mtuhumiwa katika namna yake. Hutakiwi kupuuza chochote kile, wala kukidharau. Kwani yeyote anaweza kufanya lolote kwasababu yoyote.

Jona akazama mtandaoni na kuangazia yale ambayo Miranda alikuwa anayasema kuwa mke wa Boka alianza kupeleka bidhaa zake nchini Kenya baada ya kuona hali ni shwari huko kisera.

Alipopekua kwenye vyanzo mbalimbali akaja gundua kuwa jambo hilo lilikuwa ni 'hot issue' huko nchini Kenya. Ambapo lilizua mjadala mkubwa miongoni mwa wachangiaji, hoja ikiwa kwamba soko la Kenya sasa limefurika bidhaa toka China.

Bidhaa za wazawa zimekuwa hafifu mno na kwasababu za ulimbukeni na unafuu mkubwa ambao unawekwa kwenye bidhaa za China, basi bidhaa za wazawa zimekosa soko, si wakulima wala wafanyabiashara wanaohema kwa unafuu.

Sasa mswada uliletwa bungeni kuangazia namna ya kukabili na kubadili hali hii, miswada hii ikiletwa na wabunge wa chama pinzani ambao kwa jina walikuwa ni waheshimiwa Kamau Githeri na W.Otieno.

Sasa haya majina yakamshangaza Jona! Yalikuwa ndio wale waheshimiwa waliolengwa kuuawa. Kumbe kulengwa kwao ilikuwa ni kwasababu ha hili jambo! Sasa akajua.

Kwa kupitia mswada wao waliouleta bungeni, sheria sasa ikatungwa kuweka mipaka kwa bidhaa za nchini China na huku zikiongezewa kodi na makato ili wazawa na hata wale wafanyabiashara toka nchi Afrika Mashariki wapate ahueni.

Alarm ikaita kichwani mwa Jona! Sasa hapa kulikuwa na harufu ya jambo.

"Hata ukitazama vema, most of Chinese products zimekuwa zikiwaharibu wanawake zetu. Sasa wabadilika rangi kama chameleons hata their shapes zimekuwa awkward. Why cant we allow our natural products to take over and ban these Chinese takataka?" Hii ilikuwa mojawapo ya kauli aliyoitoa marehemu W. Otieno punde baada ya kutoka kwenye mzozo mkali bungeni.

Sasa Jona akapata picha kamili. Hivi vitu vilikuwa vina mahusiano, tena ya kindakindaki! Kilichomuua mke wa Boka, hakuwa Miranda bali wachina ambao walimchukulia kama tishio kwa bishara yao ya vipodozi nchini Kenya!

Jona akatafuta clips za video ndani ya mtandao wa YOU TUBE zikionyesha hotuba za waheshimiwa Kamau Githeri na W. Otieno kupinga udhalimu wa China kwenye kudhoofisha uchumi wao wa ndani, baada ya hapo akazipakua pia na video za marehemu mke wa Boka.

Kama haitoshi akapakua na vielelezo kadhaa toka mtandaoni na kuviprint akiviweka kwenye faili. Sasa akijumuisha na vile alivyovipata kwa link kwa msaada wa Marwa, alikuwa kwenye hatua njema kabisa.

Rrrrrrrrnnng! Simu ikaita. Akaipokea na kuiweka sikioni. Kamanda.

"Nakuja, mkuu," akasema kwa ufupi simu ikakata. Akanyanyuka na kwenda kuonana na Kamanda ofisini kwake.

"Umefikia wapi?" Lilikuwa swali la kwanza la Kamanda.

Jona akamweleza namna gani anavyowashuku wachina kuhusika na kifo cha mke wa Boka, haswa kwasababu za kibiashara huko nchini Kenya. Watu hao wakilenga kummaliza mwanamke huyo ili kuendelea kutawala soko la bidhaa zao za urembo na vipodozi.

Kamanda akashusha pumzi ndefu. Alielewa kila ambacho Jona alieleza lakini ugumu unakuja hapa, kwa kesi hiyo kutimia, wanahitaji msaada toka jeshi la polisi la Kenya kwenye upelelezi na 'confirmation'. Mahusiano baina ya nchi hizi mbili kwa hapa karibuni yamedidimia, itawawia vigumu kutekeleza hilo.

"Lakini Jona, bado hii simulizi yako inahitaji ushahidi zaidi," akasema Kamanda. "Utathibitisha vipi muuaji huyo alitumwa na Wachina? pili, mauaji ya viongozi hao wa Kenya hatuwezi kuyatolea tamko bali mamlaka zao za ndani, tutawasemeaje wameuawa na wachina?"

Jona akamwomba Kamanda ampatie muda zaidi, atatafutia ufumbuzi kila swala lililopo mezani. Kwa muda huo akaomba aende ubalozi wa China kwa ajili ya mahojiano.

"Utaenda kuwauliza nini huko? Huoni utateteresha mahusiano baina yetu na wao?" Kamanda akapata hofu.

"Usijali, Kamanda," akasema Jona. "Najua namna ya kuenenda."

Jona akatoka ofisini.

Sasa ilikuwa ni majira ya saa saba ya mchana. Akaona ni kheri kama angelipata kitu tumboni. Akasonga kantini na kujipatia chakula.

Akiwa hapo mara ujumbe ukaingia ndani ya simu yake toka kwa namba mpya. Akaufungua:

'Habari, Jona. Ni Miriam hapa. Tafadhali naweza kuonana na wewe?"

"Miriam?" Jona akatahamaki. Badala ya kujibu ujumbe huo akaamua kupiga simu. Ikapokelewa na sauti ya kike, akajitambulisha ni Miriam, mke wa marehemu Eliakimu.

"Upo wapi?" Jona akauliza.

"Nipo kwa shangazi yangu Kimara," akajibu Miriam.

"Sawa, basi nitafanya mpango tuonane jioni."

Simu ikakatwa.

"Miriam!" Jona akajisemea wenyewe. Alikiri ana maswali kadhaa ya kumuuliza mwanamke huyo, kwa upande wa Eliakimu na hata pia wakina Nyokaa.

Aliamini atapata taarifa za maana toka kwa mwanamke huyo akawatie nguvuni wadhalimu.

Alipomaliza kula akalipia na kunyookea ubalozi wa China. Humo ndani hakumkuta balozi bali msaidizi wake. Wakateta kwa lisaa limoja kabla Jona hajatoka ndani ya jengo hilo.

Kitendo cha kutoka tu, ikachukua dakika mbili, Sheng akaarifiwa juu ya ujio wa Jona. Na shuku zake zote alizozileta ubalozini!

***

- JE SHENG ATAMFANYA NINI JONA?

- MARWA ATAPATA MBADALA WA TIBA YA WAZAZI WAKE?

- MIRIAM ANAMTAKIA NINI JONA?

- JONA ATAWEZA VITA HII MWENYEWE?

- MAJIBU YAPO MSIMU WA PILI!




***




Sent from my SM-J110F using JamiiForums mobile app
 
Uwa sina mazoea ya kutoa maoni mara nyingi ila umejitahidi kuendana na wakenya wanavyoongea[emoji23][emoji23][emoji119]....




Season ya pili ni hapa hapa au? Na ni lini?
 
Back
Top Bottom