Anga la washenzi na Joana anaona kitu usiku

Pamoja sana kiongozi. Langu moja tu boss, naomba usimuue Marwa asee..thanks kwa kazi nzuri, God bless!
 
Nimetuma tatu kwakuwa leo ndo tunaanza msimu wa pili ila ratiba ni mbili mbili tu. Na ntakuja kila baada ya siku moja.


Pamoja wakuu.
Yaani hiii simulizi ni kama naanagalia series fulani hivi na hapa ilipoishia naona kuna mtu kachezea waya huko Tanesko umeme umekata.
Hahha hongera sana kwa kipaji hiki.[emoji120] [emoji120]
 
*ANGA LA WASHENZI (MSIMU WA PILI) -- 04*

*Simulizi za series*

ILIPOISHIA

Pembeni ya chupa hizo zilizopasuka, kwa chini ya meza za sementi zilizokuwa zimejengwa humo, alikuwa amelala Marwa.

Alikuwa ameubana mdomo wake kwa nguvu akijitahidi kutulia lakini alikuwa anasikia maumivu makali sana. Chupa zile zilizoanguka zilimrushia kemikali usoni na alikuwa anahisi kuungua!

ENDELEA

Yule mtu wa miraba akafika eneo hilo lililopasukia chupa, akaangaza akisukuma sukuma vyupa kwa buti lake jeusi akiwa amebinua mdomo. Akatazama kushoto na kulia. Akasonya lakini kabla hajapoga hatua akauona mguu wa Marwa. Akashtuka kana kwamba ameona nyoka kwenye majani.

Akaamuru upesi Marwa atoke kwa uhai wake kabla hajamwaga ubongo.

Kwa uoga Marwa akaanza kujisogeza akiomba asiuawe. Akatoka akiwa ameshikilia uso wake alioukunja kwa kuhisi maumivu makali.

"Wewe nani?" Akauliza mtu mnene. Bwana, hakukaa sawa akala jiwe la kichwa!

Si jiwe unalolijua wewe bali ngumi. Akadondokea chini kama kiroba cha tani. Kuangaza akamwona mwanaume akiwa amesimama mbele yake hatua kadhaa.

Akaguna kwa kebehi. Akatazamia bunduki yake, akatahamaki Marwa ameshaikomba na kuijaza kiganjani.

Akacheka. Akapangusa eneo alilopigwa kisha akasimama!

Kwa mtu wa kawaida kwa ile ngumi aliyopewa, asingeamka abadani. Kwa unafuu angezirai, ila kawaida ni kufa tu.

"Najua hamuwezi nipiga risasi!" Jamaa akagamba. "Mkipiga risasi mtashtua jengo zima hili, na ndani ya sekunde tu mtageuzwa bucha. Kama nyie ni wanaume kweli, kunja!" Akatapa akitoa macho yake makubwa mithili ya bundi.

Kwakweli alikuwa anaogopesha. Mwili wake ulijawa na misuli na kwa kumtazama tu ungetambua amekomaa haswa. Nguo zilikuwa zimembana.

Jona akamtaka Marwa ashushe bunduki, na asogee kando. Wakatengeneza ka uwanja kadogo kwa ajili ya pambano.

"Utatambua kwanini nilipewa jina la Baba!" Akatapa jamaa akijitambulisha. Akanyoosha shingo yake kisha mabega, ka!-ka!-ka! Akanyoosha vidole ka!-ka!-ka!

Alafu kama fuso akamfuata Jona. Akatupa mawe ya maana. Ngumi nzito haswa. Jona akazikwepa akisogea nyuma na pembeni.

Baba akaendelea kurusha ngumi za mfululizo, mwishowe Jona katika kukwepa miwani yake ikadondoka chini. Kosa! Akala ngumi tatu zenye uzito wa tani! Akadondoka chini akiachama kwa maumivu makali! Kinyago kilipasuka. Akavuja damu mdomoni na puani kidogo.

Baba akatabasamu kiushindi.

"Amka!"

Jona akapapasapapasa chini kuitafuta miwani yake, Baba akaisukumizia kando kwa mguu, kisha akamnyanyua Jona kama unyoya na kumsogeza karibu na uso wake.

"We ni mtoto kwangu. Mimi ni Baba! Mimi ni nani?"

Jona alikuwa anona maruweruwe kana kwamba mtu anayetazama akiwa chini ya maji ama ameingiliwa na maji machoni. Alikuwa anahangaika kuona lakini hakufanikiwa. Macho nayo yalikuwa yanamvuta.

Baba akamrusha kwa juu alafu akamtwanga ngumi! Akabidukabiduka hewani kabla hajadondokea chini kama mzigo!

Tih!

Akahisi mwili mzima umevunjika. Akagugumia kwa maumivu akijikusanya. Mdomoni alikuwa anamwaga damu.

"Amka!" Baba akasema kwa kejeli akimtazama Jona. Haraka na kwa ukimya, Marwa akatambaa kuifuata miwani ya Jona. Haikuwa mbali sana na yeye. Alipoikamata mkononi akaificha alafu akamwita Baba.

"Hey!"

Baba akageuka kumtazama.

Marwa bado alikuwa anagugulia maumivu ya kemikali, jicho lake moja akiwa amelifunga. Akamkebehi Baba kwa makusudi. Baba akakasirika na kumfuata. Marwa kwa kulenga, akairusha miwani juu ya mwili wa Jona.

Jona akapapasa na kuikamata. Akaivaa.

Baba akamnyanyua Marwa juu kama alivyofanya kwa Jona. Lakini kabla hajafanya kitu, akaguswa begani. Kugeuka likawa kaburi lake. Akapokea ngumi nzito ya shavu, akapepesuka.

Asikae vema, Jona akampatia dabo bundle za teke. Akapepesuka akijakakamua kwa hali na mali asianguke chini.

Jona akaamua sasa kumpatia KATAUTI - Mateke mawili yanayoyofyatuliwa baada ya kiumbe kupaa hewani kwa namna ya mzungusho. Baba akashindwa kustahimili! Akadondoka chini kama tembo.

Jona akamuwahi Marwa kumjulia hali.

"Upo ok?"

"Yah! Am ok!" Marwa akajibu bado akiwa ameficha jicho lake moja.

"Sure?" (Hakika?) Jona akasisitiza.

"Yah! Niko ok!" Marwa akajibu lakini hali aliyomo ikimsaliti. Baadhi ya sehemu zake za uso zilikuwa zimeanza kubadili rangi, Jona aliliona hilo na akapata hofu.

Kabla hajasema kitu, Marwa akamshtua Baba anakuja. Jona akasaga meno na kumwambia:

"Ningoje hapa twende nyumbani."

Bwana we! Kama kuna kosa aliwahi kufanya Baba tangu azaliwe, lilikuwa ni hili. Kuamka tena. Na hatokuja kulisahau kosa hili maisha yake yote.

Kwa kasi ya ajabu, Jona alimrushia ngumi zisizo na idadi. Akajitahidi kupangua mbili tatu lakini baadae akashindwa. Jona alikuwa haraka mno. Kasi yake ilikuwa ya ajabu!

Mpaka Jona anamaliza, Baba akajikuta hawezi kusogeza kiungo chochote cha mwili. Akadondoka kama mbuyu asiamke tena!

Jona na Marwa wakatoka ndani ya maabara wakiwa wamebebelea antidote waliyoifuata. Wakatembea kwa tahadhari mpaka ukutani, wakaambaa na ukuta huo kwenda mbele, kidogo wakasikia sauti za watu wakiwa wanateta.

Jona akaangaza, akaona watu wakikatiza. Akamuagiza Marwa amngoje kidogo, akasonga na kuchungulia, akawaona wanaume kama kumi kwa idadi. Wote walikuwa weusi. Walikuwa wanatoa maboksi toka chumba fulani hivi na kuyaweka nje.

Kidogo, Jona akamwona mwanaume mwenye asili ya kichina akija hapo. Akafungua maboksi kadhaa na kuyatazama alafu akashika kiuno akiwatazama wanaume waliokuwa wanaendelea kuyaleta.

Hawakuchukua muda mrefu, wakasitisha zoezi. Mchina akayahesabu maboksi yale alafu akapiga simu. Ndani ya muda mfupi, gari aina ya Van jeusi likaja hapo maboksi yakaanza kupakiwa.

Kabla zoezi hilo halijakamilika, mara mlio wa tahadhari ukaita kwanguvu kuhabarisha hali si salama. Wanaume wale wakatazamana, kisha haraka wakaacha kupakia maboksi na kusambaa kila eneo.

Baada ya muda mfupi wakagundua maabara ilikuwa imekwapuliwa, mlinzi mmoja amefariki na mwingine yu hoi hajiwezi.

Kufuatilia nyayo za viatu na matone ya damu wakafika mpaka pale Jona alipokuwa anawachungulia. Wakagundua wameshatokomea.

Taarifa zikamfikia Sheng. Akiwa amevalia 'casual' akafika eneo la tukio na kushuhudia kila kitu. Akang'ata meno kwa hasira. Kwa akili yake yote akaamini ni Marwa wakishirikiana na Jona ndiyo wamefanya hayo.

Mosi, Marwa hawezi kupigana kuwaangusha wanaume wale, hivyo alimhitaji Jona. Pili, Jona hakuwa anajua mazingira hayo, hivyo alimhitaji Marwa.

Walikuwa wanaisaka antidote. Si kwasababu nyigine bali kuwapelekea wazazi wa Marwa.

Sheng akaagiza wazazi wa Marwa waangamizwe kabla ya jua la kesho halijazama. Na kuhusu Jona, awachiwe yeye anajua dawa yake.

**

"Inabidi twende hospitali," alisema Jona akimtazama Marwa kwa muda mfupi kabla hajarudishia macho yake mbele waendako.

Walikuwa ndani ya gari Jona akishikilia usukani.

"Nitakuwa poa tu usijali," Marwa akasema akiwa amelaza kichwa kitini.

"Hapana, lazima twende hospitali! That is chemical!"

Marwa hata kuongea hakuweza. Alikuwa anasikia maumivu makali. Alihisi kuna michanga na changarawe jichoni huku upande huo wa uso ukiwa unawaka moto.

Wakashika barabara ya kwenda hospitali, wakasonga nayo kwa kwa dakika kadhaa, kabla ya kukata kona kwa mbele kuingia hospitalini, Jona akatazama sight mirror. Akakunja ndita na kusema:

"Nahisi tunafuatwa!"

Marwa akakodoa jicho lake moja lililozima ila ghafla akaliminya kwa kuhisi maumivu. Ni kama vile alipigwa na shoka kichwani.

**
 
*ANGA LA WASHENZI (MSIMU WA PILI) -- 05*

*Simulizi za series*

ILIPOISHIA

"Nahisi tunafuatwa!"

Marwa akakodoa jicho lake moja lililozima ila ghafla akaliminya kwa kuhisi maumivu. Ni kama vile alipigwa na shoka kichwani.

ENDELEA

Wakakata kona kuzama ndani ya hospitali, na lile gari ambalo Jona alikuwa analishuku likanyoosha na barabara. Wakatambua kumbe ilikuwa hofu yao tu, hakuna anayewafuata. Ndani ya muda mfupi wakaonana na daktari na kisha kujieleza.

Marwa akaafanyiwa uchunguzi na ikabainika ameathirika na kemikali, mishipa midogo midogo ndani ya macho imeathirika na hivyo jicho lake hilo linaweza kuwa kipofu kabisa ama kufifia uwezo wake wa kuona.

"Kama msingeliwahi zaidi basi lingepasuka ama kulika kabisa akawa chongo," alieleza daktari. Jona akapata shaka kwa Marwa kuwa na hali kama ya kwake.

Baada ya muda mfupi wakaruhusiwa kutoka hospitalini wakiwa wamepatiwa dawa ya kutia jichoni na kupaka usoni.

Kwa maumivu aliyokuwa nayo na 'ka ahueni' alikokapata baada ya kufanyiwa dawa, Marwa akalala akimwacha Jona peke yake anaendesha gari.

Waliwasili nyumbani, Jona akamsaidia Marwa kushuka ndani ya gari na kumpeleka mpaka chumbani akapumzike alafu yeye akajirudisha sebuleni kana kwamba ilikuwa ni saa kumi na mbili jioni wakati muda ulikuwa umeshaenda.

Kwa sasa ilikuwa inaelekea saa tisa na nusu usiku.

Alifungua jokofu atoe kinywaji, akatahamaki hakukuwa na kitu. Vilikuwa vimekwisha. Akalaani vikali. Vimeishaje hata hakutambua? Akaketi kitini akiwa amekangangikiwa na akijilaumu kwa kutotambua hilo mapema.

Uzembe wa aina gani.

Mwili wake ulikuwa unamuuma kwa zoezi alilotoka kufanya ndani ya himaya ya Sheng. Na kichwani pia alikuwa ana mawazo. Alihitaji kinywaji apate kulala.

Awe anakunywa taratibu huku akiichambua siku yake nzima mpaka anapotelea usingizini. Kwa kufanya hivi huwa kunamsaidia kesho aamkapo ajue ni nini cha kufanya.

Akakaa hapo kochini kwa muda mrefu sana. Macho yalikuwa meupe na yenye nguvu lakini mwilo ukowa hoi. Hata akajilaumu kwanini hakuteka vidonge vya usingizi kule hospitali.

Alibadili kila mkao kitini mwishowe akaenda kitandani kujilaza. Muda mfupi akapitiwa na usingizi. Alipolala hapo kwa muda mfupi akakurupuka baada ya kuota ndoto mbaya.

Huwa hivi kila alalapo pasi na kinywaji. Anaota familia yake. Anakumbuka siku aliyowaona wakiteketea ndani ya nyumba yao iliyogeuzwa tanuru.

Akatazama saa, saa kumi na moja! Hata hivyo akashukuru ndoto hiyo kwa kumwamsha ndani ya muda. Akajiandaa kwenda kazini.

Hakutaka kumsumbua Marwa, alijua amechoka sana na kitambo kifupi tu amelala. Akamtazama tu kwa kumkagua na macho yake alafu akaondoka.

Lakini alipokuwa huko ofisini, bado akajihisi mchovu mno. Hakuweza kufanya kazi yake vema. Mwili ulikuwa mzito, alihisi pia kichwa kimeongezeka ukubwa anahangaika kukimudu.

Haikutakiwa awe hivyo siku hiyo. Siku hiyo ilikuwa muhimu mno kwani Sheng alikuwa anafika kituoni kwa ajili ya mahojiano na pia atazamie kama kuna haja ya kumtia ndani.

Alitakiwa awe mwenye nguvu, mwenye hari, lakini haikuwa hivyo.

Akatazama saa yake. Akamuwaza kidogo Sheng na kile walichokifanya jana. Akajikuta anagutuka! Macho yalimtoka kwa kukumbuka jambo. Akabamiza meza.

Shabash! Wazazi wake Marwa!

Haraka akatoka ofisini, akajipakia ndani ya gari na kutimka haraka. Alijilaumu sana kwa uzembe alioufanya. Kivipi aliwasahau wazazi hao?

Bayana hawatakuwa salama kwani Sheng atakuwa ameshagundua kwamba wameiba antidote. Moyoni akawa anasali akute kila jambo jema.

Kwa kasi kubwa akaendesha gari akili yake ikiwa bize. Alipowasili, akakimbilia ndani na kuangaza. Hakukuta mtu sebuleni. Akaita, napo kimya.

Akaenda chumbani. Akajikuta uchungu unamkaba baada ya kuona maiti mbili kitandani!

Wazazi wake Marwa walikuwa wameshauwa. Walididimiziwa risasi kwenye mapaji yao ya uso.

Jona akashindwa kuzuia machozi. Akaishiwa nguvu kabisa. Aliketi kitandani akishikilia kichwa chake kwa manung'uniko na lawama. Kazi yote waliyoifanya ilikuwa bure. Tena ikiwagharimu mara mbili yake.

Kwa muda kidogo akawa hajui cha kufanya. Alihisi kichwa kimeacha kufanya kazi. Hana hisia wala wazo lolote.

Hakufahamu ni kwasababu gani, ila baada ya muda, akajikuta anamkumbuka mkewe. Alijihisi mtupu. Mpweke rohoni. Alikumbuka tabasamu lake na namna alivyokuwa anamkumbatia kila arudipo kazini. Akimbebeleza alale na akimsihi aamke.

Pengine alikuwa anahisi anakosa hayo mambo kwa kipindi kama hiki kigumu. Haikuwa la kuficha, muda huu alikuwa anamhitaji sana mke wake kuliko kipindi kingine chochote.

Akiwa kama mtu asiyejitambua wala kuonyesha kujali akalala hapo na maiti hizo mbili.

Alikuja kushtuliwa na kurejeshwa fahamuni baada ya ujumbe kuingia ndani ya simu yake. Simu ilitetemeka mfukoni, akaichomoa na kuitazama. Ilikuwa ni ujumbe toka kwa Marwa.

'Naomba unisaidie kuwapelekea wazee antidote'

Jona akatikisa kichwa chake kwa masikitiko. Akaamka na kuidumbukiza simu mfukoni kisha akaendea gari na kujipakia.

Akiwa njiani, simu ikaita. Kamanda.

"Upo wapi na unajua leo Sheng anakuja kituoni?" Kamanda alifoka.

"Nipo njiani, mkuu," Jona akajibu alafu akakata simu.

Muda mfupi akawa ameshafika na mbele yake, ndani ya ofisi, yupo mwanaume mchina. Mfanyabiashara mkubwa nchini, bwana Sheng tayari kwa ajili ya mahojiano.

Lakini Jona hakuwa sawa. Asingeweza kufanya kazi yake inavyotakiwa. Akamwomba radhi Sheng na kumtaka aje siku nyingine atakayompa taarifa kwani kuna dharura.

Sheng akatabasamu, kisha akamuuliza:

"Unaenda msibani?"

Jona akamtazama kwa jicho kali. Alitamani amrukie mwanaume huyo na kumnyofoa macho kisha ayatafune. Lakini akadumisha hari yake.

"Ndio, naenda msibani," akajibu. "Bila shaka unaufahamu mi wa nani."

Sheng akatabasamu tena kisha akasema:

"Mlichofanya jana haikuwa good move. It was one of the most stupid step."

Jona akamtazama Sheng kwa kitambo kidogo kabla hajamsogelea mwanaume huyo na kumtazama machoni.

"Siku yako ipo karibuni. Nitakuvunjavunja kwa mkono wangu. Utalipa kila tone la damu ulilolimwaga."

"Siku yangu!" Sheng akacheka. Akatikisa kichwa chake na kupepea kwa kidole. "Yako ndiyo ipo karibuni kuliko udhanivyo. Siku hiyo nitaimark kwenye kalenda na kuisherehekea kila mwaka."

"Sheng," Jona akaita. "Mimi ni mfupa mgumu, wewe fisi huniwezi. Umeniwinda mara ngapi nikakurudishia maiti zako?"

"Mara hii haitakuwa kama hapo mwanzo," Sheng akajitapa. "Hilo nakuahidi."

Alafu akanyanyuka na kwenda zake Jona akimtazama kwa macho batili. Alifikiria kumsweka mwanaume huyo ndani mpaka atakapomaliza mchakato wa msiba, akaona hamna haja hiyo. Hajafikia hatua ya kumwogopa kiasi hiko!

**

Baada ya siku mbili.

Walikuwa wameyapa mgongo makaburi wakitembea kuondoka zao. Walikuwa wamevalia nguo nyeusi juu mpaka chini. Nyuso zao zikipambwa na miwani, Jona ya macho na Marwa ya jua.

Uso wa Marwa kwa upande wa kushoto ulikuwa mwekundu na hakuweza kustahimili jua, akauelekezea chini. Mikono yao ilikuwa ndani ya makoti marefu waliyoyavaa.

Anga lilikuwa jeusi kiasi, jua kwa wastani, na kulikuwa kuna kila ishara ilkionyesha mvua ilinyesha muda kidogo hapo nyuma.

Walipoyaacha makaburi kwa urefu mdogo wakielekea barabarani, simu ya Jona ikaita ndani ya koti. Akaichomoa na kuitazama, ilikuwa namba mpya. Akapokea na kuiweka sikioni.

"Unahitajika kituoni. Haraka," sauti ilisema simuni kisha simu ikakata.

Jona hakujua nini maana ya ujumbe huo na hakutaka kujishughulisha nao sana. Wakaendea usafiri wa daladala na kujipakia. Leo hawakuwa na gari kwani alilirudisha kituoni.

Wakiwa humo ndani ya daladala, muda mchache mbele, ndipo Jona akaukumbuka ujumbe ule aliopewa kwenye simu baada ya kusikia taarifa redioni kuwa Kamanda wa polisi mkoa, ameuawa na watu wasiojulikana, usiku wa kuamkia leo!

Akashangazwa sana na habari hizo. Akamtaka Marwa aelekee nyumbani, watakutana baadae. Akaenda moja kwa moja kituoni.

***

- UNADHANI KWANINI KAMANDA KAUAWA? KUFA HUKU KWA KAMANDA KUTAMWACHA JONA SALAMA?
 
[emoji91] [emoji91] [emoji91] [emoji91] [emoji91] [emoji91] [emoji91]
 
[emoji91] [emoji91] tivu Kesho sijui ntaelekea rehab gan kupunguza hii hali
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…