*ANGA LA WASHENZI (MSIMU WA PILI) -- 04*
*Simulizi za series*
ILIPOISHIA
Pembeni ya chupa hizo zilizopasuka, kwa chini ya meza za sementi zilizokuwa zimejengwa humo, alikuwa amelala Marwa.
Alikuwa ameubana mdomo wake kwa nguvu akijitahidi kutulia lakini alikuwa anasikia maumivu makali sana. Chupa zile zilizoanguka zilimrushia kemikali usoni na alikuwa anahisi kuungua!
ENDELEA
Yule mtu wa miraba akafika eneo hilo lililopasukia chupa, akaangaza akisukuma sukuma vyupa kwa buti lake jeusi akiwa amebinua mdomo. Akatazama kushoto na kulia. Akasonya lakini kabla hajapoga hatua akauona mguu wa Marwa. Akashtuka kana kwamba ameona nyoka kwenye majani.
Akaamuru upesi Marwa atoke kwa uhai wake kabla hajamwaga ubongo.
Kwa uoga Marwa akaanza kujisogeza akiomba asiuawe. Akatoka akiwa ameshikilia uso wake alioukunja kwa kuhisi maumivu makali.
"Wewe nani?" Akauliza mtu mnene. Bwana, hakukaa sawa akala jiwe la kichwa!
Si jiwe unalolijua wewe bali ngumi. Akadondokea chini kama kiroba cha tani. Kuangaza akamwona mwanaume akiwa amesimama mbele yake hatua kadhaa.
Akaguna kwa kebehi. Akatazamia bunduki yake, akatahamaki Marwa ameshaikomba na kuijaza kiganjani.
Akacheka. Akapangusa eneo alilopigwa kisha akasimama!
Kwa mtu wa kawaida kwa ile ngumi aliyopewa, asingeamka abadani. Kwa unafuu angezirai, ila kawaida ni kufa tu.
"Najua hamuwezi nipiga risasi!" Jamaa akagamba. "Mkipiga risasi mtashtua jengo zima hili, na ndani ya sekunde tu mtageuzwa bucha. Kama nyie ni wanaume kweli, kunja!" Akatapa akitoa macho yake makubwa mithili ya bundi.
Kwakweli alikuwa anaogopesha. Mwili wake ulijawa na misuli na kwa kumtazama tu ungetambua amekomaa haswa. Nguo zilikuwa zimembana.
Jona akamtaka Marwa ashushe bunduki, na asogee kando. Wakatengeneza ka uwanja kadogo kwa ajili ya pambano.
"Utatambua kwanini nilipewa jina la Baba!" Akatapa jamaa akijitambulisha. Akanyoosha shingo yake kisha mabega, ka!-ka!-ka! Akanyoosha vidole ka!-ka!-ka!
Alafu kama fuso akamfuata Jona. Akatupa mawe ya maana. Ngumi nzito haswa. Jona akazikwepa akisogea nyuma na pembeni.
Baba akaendelea kurusha ngumi za mfululizo, mwishowe Jona katika kukwepa miwani yake ikadondoka chini. Kosa! Akala ngumi tatu zenye uzito wa tani! Akadondoka chini akiachama kwa maumivu makali! Kinyago kilipasuka. Akavuja damu mdomoni na puani kidogo.
Baba akatabasamu kiushindi.
"Amka!"
Jona akapapasapapasa chini kuitafuta miwani yake, Baba akaisukumizia kando kwa mguu, kisha akamnyanyua Jona kama unyoya na kumsogeza karibu na uso wake.
"We ni mtoto kwangu. Mimi ni Baba! Mimi ni nani?"
Jona alikuwa anona maruweruwe kana kwamba mtu anayetazama akiwa chini ya maji ama ameingiliwa na maji machoni. Alikuwa anahangaika kuona lakini hakufanikiwa. Macho nayo yalikuwa yanamvuta.
Baba akamrusha kwa juu alafu akamtwanga ngumi! Akabidukabiduka hewani kabla hajadondokea chini kama mzigo!
Tih!
Akahisi mwili mzima umevunjika. Akagugumia kwa maumivu akijikusanya. Mdomoni alikuwa anamwaga damu.
"Amka!" Baba akasema kwa kejeli akimtazama Jona. Haraka na kwa ukimya, Marwa akatambaa kuifuata miwani ya Jona. Haikuwa mbali sana na yeye. Alipoikamata mkononi akaificha alafu akamwita Baba.
"Hey!"
Baba akageuka kumtazama.
Marwa bado alikuwa anagugulia maumivu ya kemikali, jicho lake moja akiwa amelifunga. Akamkebehi Baba kwa makusudi. Baba akakasirika na kumfuata. Marwa kwa kulenga, akairusha miwani juu ya mwili wa Jona.
Jona akapapasa na kuikamata. Akaivaa.
Baba akamnyanyua Marwa juu kama alivyofanya kwa Jona. Lakini kabla hajafanya kitu, akaguswa begani. Kugeuka likawa kaburi lake. Akapokea ngumi nzito ya shavu, akapepesuka.
Asikae vema, Jona akampatia dabo bundle za teke. Akapepesuka akijakakamua kwa hali na mali asianguke chini.
Jona akaamua sasa kumpatia KATAUTI - Mateke mawili yanayoyofyatuliwa baada ya kiumbe kupaa hewani kwa namna ya mzungusho. Baba akashindwa kustahimili! Akadondoka chini kama tembo.
Jona akamuwahi Marwa kumjulia hali.
"Upo ok?"
"Yah! Am ok!" Marwa akajibu bado akiwa ameficha jicho lake moja.
"Sure?" (Hakika?) Jona akasisitiza.
"Yah! Niko ok!" Marwa akajibu lakini hali aliyomo ikimsaliti. Baadhi ya sehemu zake za uso zilikuwa zimeanza kubadili rangi, Jona aliliona hilo na akapata hofu.
Kabla hajasema kitu, Marwa akamshtua Baba anakuja. Jona akasaga meno na kumwambia:
"Ningoje hapa twende nyumbani."
Bwana we! Kama kuna kosa aliwahi kufanya Baba tangu azaliwe, lilikuwa ni hili. Kuamka tena. Na hatokuja kulisahau kosa hili maisha yake yote.
Kwa kasi ya ajabu, Jona alimrushia ngumi zisizo na idadi. Akajitahidi kupangua mbili tatu lakini baadae akashindwa. Jona alikuwa haraka mno. Kasi yake ilikuwa ya ajabu!
Mpaka Jona anamaliza, Baba akajikuta hawezi kusogeza kiungo chochote cha mwili. Akadondoka kama mbuyu asiamke tena!
Jona na Marwa wakatoka ndani ya maabara wakiwa wamebebelea antidote waliyoifuata. Wakatembea kwa tahadhari mpaka ukutani, wakaambaa na ukuta huo kwenda mbele, kidogo wakasikia sauti za watu wakiwa wanateta.
Jona akaangaza, akaona watu wakikatiza. Akamuagiza Marwa amngoje kidogo, akasonga na kuchungulia, akawaona wanaume kama kumi kwa idadi. Wote walikuwa weusi. Walikuwa wanatoa maboksi toka chumba fulani hivi na kuyaweka nje.
Kidogo, Jona akamwona mwanaume mwenye asili ya kichina akija hapo. Akafungua maboksi kadhaa na kuyatazama alafu akashika kiuno akiwatazama wanaume waliokuwa wanaendelea kuyaleta.
Hawakuchukua muda mrefu, wakasitisha zoezi. Mchina akayahesabu maboksi yale alafu akapiga simu. Ndani ya muda mfupi, gari aina ya Van jeusi likaja hapo maboksi yakaanza kupakiwa.
Kabla zoezi hilo halijakamilika, mara mlio wa tahadhari ukaita kwanguvu kuhabarisha hali si salama. Wanaume wale wakatazamana, kisha haraka wakaacha kupakia maboksi na kusambaa kila eneo.
Baada ya muda mfupi wakagundua maabara ilikuwa imekwapuliwa, mlinzi mmoja amefariki na mwingine yu hoi hajiwezi.
Kufuatilia nyayo za viatu na matone ya damu wakafika mpaka pale Jona alipokuwa anawachungulia. Wakagundua wameshatokomea.
Taarifa zikamfikia Sheng. Akiwa amevalia 'casual' akafika eneo la tukio na kushuhudia kila kitu. Akang'ata meno kwa hasira. Kwa akili yake yote akaamini ni Marwa wakishirikiana na Jona ndiyo wamefanya hayo.
Mosi, Marwa hawezi kupigana kuwaangusha wanaume wale, hivyo alimhitaji Jona. Pili, Jona hakuwa anajua mazingira hayo, hivyo alimhitaji Marwa.
Walikuwa wanaisaka antidote. Si kwasababu nyigine bali kuwapelekea wazazi wa Marwa.
Sheng akaagiza wazazi wa Marwa waangamizwe kabla ya jua la kesho halijazama. Na kuhusu Jona, awachiwe yeye anajua dawa yake.
**
"Inabidi twende hospitali," alisema Jona akimtazama Marwa kwa muda mfupi kabla hajarudishia macho yake mbele waendako.
Walikuwa ndani ya gari Jona akishikilia usukani.
"Nitakuwa poa tu usijali," Marwa akasema akiwa amelaza kichwa kitini.
"Hapana, lazima twende hospitali! That is chemical!"
Marwa hata kuongea hakuweza. Alikuwa anasikia maumivu makali. Alihisi kuna michanga na changarawe jichoni huku upande huo wa uso ukiwa unawaka moto.
Wakashika barabara ya kwenda hospitali, wakasonga nayo kwa kwa dakika kadhaa, kabla ya kukata kona kwa mbele kuingia hospitalini, Jona akatazama sight mirror. Akakunja ndita na kusema:
"Nahisi tunafuatwa!"
Marwa akakodoa jicho lake moja lililozima ila ghafla akaliminya kwa kuhisi maumivu. Ni kama vile alipigwa na shoka kichwani.
**