*ANGA LA WASHENZI (MSIMU WA PILI) -- 07*
*Simulizi za series*
ILIPOISHIA
"Kwasababu mojawapo ya mtuhumiwa ama watuhumiwa ni watu toka jeshi letu la polisi," Kamanda akajibu. "Hivyo kufanya kazi hii kwa ufanisi zaidi, pasipo na aina yoyote ya upendeleo ama kupindisha mambo, tulihitaji mtu toka nje."
Jona akahisi hapa kuna jambo halipo sawa.
ENDELEA
Ni nani huyo mtuhumiwa toka jeshi la polisi? Mbona upelelezi wake mfupi umeonyesha tofauti? Alijiuliza maswali haya kichwani kwa haraka. Ila hakuwa na namna zaidi ya kufuata agizo alilopewa na mkuu wake.
Hakuwa katika nafasi ya kupinga agizo bali kutekeleza agizo. Akaongea na Elliot Parker mpaka alipofikia na kisha akisindikizana naye akampeleka mpaka nyumbani kwa marehemu Kamanda.
Elliot Parker akitumia vifaa vyake vya kitaalamu akachukua ushahidi kwa 'kuscan' eneo ambalo mtuhumiwa alilishika wakati anaingilia na kutokea ndani kwa lengo la kupata alama za dole gumba.
Alipomaliza hilo akatumia "magnifying glass' kupekulia njia na nyayo za mtuhumiwa. Akaandika taarifa na kisha wakaondoka na Jona kurudi kituoni.
**
"Marwa, things are not ok. Nasense kuna mchezo unafanyila nyuma ya mgongo wangu," alisema Jona akiwa ameshikilia kichwa chake amejilaza kitini.
"Ni kuhusu ile kesi?" Marwa akauliza baada ya kuvuta juisi ndani ya glasi kwa mrija wake mwembamba. Mezani kulikuwa kuna dumu la lita tano likiwa limesheheni juisi ya embe. Kila mtu alikuwa na glasi yake ya juisi ila ya Jona haikuwa imepungua hata kidogo tangu ijazwe.
Mrija ulikuwa unaeleaelea juu ukikosa mteja.
"Yah ni kuhusu hiyo kesi," Jona akajibu. Macho yalionyesha yupo mbali kifkra. "Sielewi kuna nini hapa kati, lakini ..." Jona akatikisa kichwa. "Mambo hayapo sawa kabisa kabisa."
"Nini shida haswa?" Marwa akauliza akimtazama Jona na chongo lake.
"Nimefanya uchunguzi, na kwa clue ndogo niliyoipata, muuaji ni miongoni mwa watu wa Sheng kwa mujibu wa sare za viatu. Lakini ajabu ni kwamba, baadae shahidi anakuja kunambia gari aliloliona likiwa limebeba watuhumiwa ndilo lile tulilotumia hapa karibuni.
Kama haitoshi, Kamanda naye ananiambia mmoja wa watuhumiwa ni mtu toka jeshi la polisi, nastaajabu amejuaje kama mmoja wa watuhumiwa ni polisi na huku hajafanya uchunguzi, mpaka anafikia hatua ya kumleta mtu mgeni? Na alafu ilikuaje watuhumiwa hao wa mauaji wakapata gari ambalo lipo kituoni?
"
Marwa akaguna. Akaweka glasi chini na kukiri kuna jambo.
"Hapo inabidi uwe makini sana, Jona," akashauri. "Mi nakusihi kitu kimoja, usimwachie huyo mgeni akafanya upelelezi peke yake. Kula naye sahani moja. Unajua kwanini nakuambia hivyo?"
Marwa akaweka kituo kisha akaendelea:
"Hapo lolote linaweza kutokea. Sasa lazima na wewe uwe na nafasi ya kujihami. Uwe na maelezo yenye mantiki ya kukuweka salama na kulimaliza hili."
Ujumbe huu ukapenya kwenye masikio ya Jona. Kweli ulikuwa na mashiko. Aliona ana haja ya kujua kila kitu kitakachoendelea kwenye kesi hiyo. Na si tu kujua, bali awe amemtangulia bwana Elliot Parker kwenye harakati zake.
Ajue alichokiona mzungu huyo, alichokisikia, alichokiandika na kukisoma.
Baada ya hapo, angalau Jona akapata unafuu wa mawazo. Akanyanyua juisi na kuigida mapafu kadhaa. Sasa kichwani mwake alikuwa anafikiria namna gani atahakikisha anamweka bwana Elliot Parker mgongoni mwake.
Mara simu ikaita, akaitazama, alikuwa ni Miriam
.
"Hallo ... yes, habari yako? ... safi tu. Unaendeleaje? ... niko poa, nihabarishe ... saa hii? ... serious? ..."
Jona akatazama saa yake ya mkononi, saa moja usiku.
" ... ok, nakuja. Nipe dakika chache."
Akakata simu na kumtazama Marwa.
"Nadhani nimepata kazi ya dharura."
**
"Yupo wapi?" Lilikuwa swali la kwanza Jona kuuliza baada ya kuingia ndani mwa Shangazi yake Miriam. Alitumia kama nusu saa kufika hapo. Miriam, aliyekuwa ana uso wa hofu na macho mekundu, alimpokea na kumkumbatia kwanguvu. Hakuamini kama Jona angefika.
"Ahsante sana kwa kuja, Jona," alisema kwa toni ya uoga. "Naogopa, naogopa!"
"Usijali," Jona akamtoa hofu. "Yupo wapi?" Akarudia tena swali lake. Miriam akamwonyeshea mlango wa chumba kwa kidole, Jona akakimbilia huko kutazama akimwacha Miriam sebuleni.
Baada ya muda mfupi akarejea.
"It is not that serious," Jona alisema akiketi kochini. "Itakuwa ni Malaria tu si kingine."
"Kweli?" Miriam akauliza akitoa macho.
"Yah its true."
"Tumpeleke basi hospitali!"
"Hapana. Hamna haja hiyo. She is not in that critical situation, Miriam."
"Kweli? Mimi niliogopa sana," akasema Miriam kisha akajilazimisha kutabasamu.
"Ndo' ulikuwa ukiishi hivi na wanao?" Jona akauliza. Miriam akatabasamu kabla hajajibu.
"Mimi muoga sana. Eliakimu ndiyo alikuwa akisumbuka nao sana kipindi wanaumwa. Mimi mmh mmh mwoga sana."
"Hujawamiss watoto wako?"
"Nimewamiss mno. Ila naona ni kheri kwao wakawa na mimi mbali kwa muda huu. Natumai huko kwa shangazi yao wanaishi vema japo kuna muda huwa nawakumbuka sana!"
"Pole mama. "
"Vipi kuhusu wewe?"
"Mimi sina familia."
"Haiwezekani. Serious?"
"Ndio. Walifariki kwenye ajali ya moto miaka miwili iliyopita."
"Oh my God. Pole sana," alisema Miriam akimtazama Jona kwa sura ya huruma. Jona hakutaka kuendelea na simulizi hizo, huwa zinamuumiza sana pindi anapozikumbuka, akabadili mada kwa kumtaka Miriam amwonyeshe jokofu lao apate kutengeneza dawa ya mgonjwa.
"Dawa?" Miriam akatahamaki. "Hamna dawa kwenye friji."
"Najua haipo, ndiyo maana nataka kutengeneza," Jona akamjibu na kuongezea: "Nikiona vilivyomo nitajua cha kufanya. Usiku huu haitakiwi aachwe hivi hivi."
Wakaongozana mpaka jikoni, ndani ya jokofu Jona akatoa tunda moja la chenza na kulikata robo kipande kisha akakichemsha. Maji yake akampatia Miriam ampatie shangazi anywe.
"Akimaliza atalala vema."
Baada ya muda mfupi Miriam akarejea na kikombe kitupu. Akamwambia Jona tayari Shangazi amemaliza.
"Una uhakika itamsaidia?"
"Asilimia zote. Ndani ya kinywaji alichokunywa kuna unmodified natural quinine, itamsaidia."
Miriam akamkumbatia tena Jona.
"Nashukuru sana."
"Nadhani napaswa kwenda sasa," Jona akasema akijipapasa mifuko.
**
Ngo! Ngo! Ngo!
"Ingia," Jona alirusu hodi akitazama mlangoni. Akamwona bwana Elliot Parker akiingia ndani, amevalia suti nyeusi na kwenye mkono wake wa kushoto amebebelea mkoba wa kahawia.
Wakasilimiana, Elliot akaketi na kueleza dhamira ya ujio wake. Yupo pale kwa ajili ya kumuuliza Jona maswali kadhaa juu ya kesi ya mauaji ya Kamanda.
Jona hakuona shida, akamkarimu kwa mikono yote. Akamuahidi bwana Elliot atampatia ushirikiano wote autakao.
Elliot Parker akafungua mkoba wake na kutoa karatasi kadhaa. Akazitazama kwa zamu alafu moja akaiweka mezani na zingine akazirudisha mkobani.
Akaitazama tena ile karatasi aliyoiweka mezani alafu akaanza kumuuliza Jona maswali.
"Do you know the last person Chisanza communicated with?" (Unamjua mtu wa mwisho aliyewasiliana na Chisanza?)
"No, I dont," (Hapana, simjui,) Jona akajibu kwa kujiamini.
"Are you sure?" (Una uhakika?)
"Yes, I am." (Ndio, nina uhakika.)
"The last person was you," (mtu wa mwisho alikuwa wewe,) akasema Elliot Parker. "And it happened a few minutes before Chisanza was killed. Anything to say about that?" (Na ilitokea muda mfupi kabla Chisanza hajauawa. Chochote cha kusema kuhusu hilo?)
"I dont know anything about that," (sijui lolote kuhusu hilo,) alisema Jona. "I only contacted him about the case he gave me to deal with." (Niliwasiliana naye kuhusu kesi tu aliyonipa nihangaike nayo.)
"But you know that his house troubles them with network, right? And one has to go out to talk clearly?" (Lakini unajua nyumba yao inawasumbua mtandao, sio? Na mtu inambidi aende nje aongee vizuri?)
"Yes, I do." (Ndio, najua.)
Elliot Parker akaandika karatasini. Alafu akamuuliza Jona kuhusu gari linalosadikika kutumiwa na wauaji. Lini ilikuwa mara yake ya mwisho kulitumia na kama kuna mtu yeyote anayemjua ameshawahi kutumia gari hilo tangu lije kituoni.
Jona akaeleza hakuna aliyekuwa analitumia isipokuwa yeye tu ila kwenye shughuli zake za kazi. Baada ya maelezo hayo, bwana Elliot Parker akapaki vitu vyake na kuaga.
Akamwacha Jona akiwa na maswali kichwani. Hakuelewa kinachoendelea.
Ndani ya muda mfupi, wakaja polisi watatu, wakamuweka chini ya ulinzi. Akatiwa pingu mikononi.
Alikuwa ni mtuhumiwa namba moja wa mauaji.
**