Anga la washenzi na Joana anaona kitu usiku

Anga la washenzi na Joana anaona kitu usiku

Kwa kweli mkuu
Najaribu kuwaza hivi hawa producers wa hizi so called bongo movies hawaoni vitu kama hv
Naamini ingekuwa mbele washakutafuta kukujaza mshiko ili watengeneze movie kama vile inferno na da vinci code za Dan Brown.
Kazi imesimama sana mkuu ,big up
Mimi mwenyewe nilikua nawaza hivyo
 
*ANGA LA WASHENZI (MSIMU WA PILI) -- 06*

*Simulizi za series*

ILIPOISHIA

Wakiwa humo ndani ya daladala, muda mchache mbele, ndipo Jona akaukumbuka ujumbe ule aliopewa kwenye simu baada ya kusikia taarifa redioni kuwa Kamanda wa polisi mkoa, ameuawa na watu wasiojulikana, usiku wa kuamkia leo!

Akashangazwa sana na habari hizo. Akamtaka Marwa aelekee nyumbani, watakutana baadae. Akaenda moja kwa moja kituoni.

ENDELEA

Huko inspekta Jona akapata maelezo kuwa Kamanda aliuawa usiku na mtu aliyefika nyumbani kwake na mojawapo ya gari iliyopo kituoni.

Jona akatahamaki. Kwa maelezo hayo maana yake Kamanda aliuawa na polisi? Alitaka taarifa zaidi lakini hakuna aliyempatia. Ilionekana kila mtu ana taarifa nusu nusu, na hakuna mwenye uhakika.

Akiwa amekaa ofisini kwake akitafakari, akakumbuka hata maneno ya Sheng. Je ndiye kammaliza? Hapana. Mbona Sheng alisema atammaliza yeye na si Kamanda?

Au hiyo ndiyo mojawapo ya njia ya kumtafuta? Akawaza sana. Akatamani apatiwe hii nafasi ya kufuatilia hili tukio. Akakaa humo ofisini mpaka majira fulani walipotoka kwenda kuonana na kamanda mkuu wa polisi. Alikuja kuwatembelea.

"Wewe ndiyo Jona?" Kamanda mkuu akamuuliza kana kwamba hamjui. Akampatia mkono.

"Ndiyo, ni mimi, afande," Jona akajibu kwa ukakamavu.

"Oooh! Nilikuwa nikipata taarifa zako toka kwa bwana Chisanza."

Bwana Chisanza ndilo jina la Kamanda aliyefariki dunia.

"Alikuwa anakubali kazi zako. Ameondoka ametuachia pengo kubwa sana." Kamanda mkuu aliendelea kuongea na Jona. Akamshika bega lake la kulia alafu akaenda kwa mtu mwingine afuataye kwenye mstari walioupanga kumpokea mkuu huyo.

Baada ya kusalimiana na kila mmoja, wakapata kuwa na kikao kidogo ndani ya kituo kikuu.

"Hili jambo si la kuvumilika kabisa kabisa!" Alibweka Kamanda Mkuu. "Haiwezekani tukaenda kwa namna hii, lazima jambo lifanyike tena haraka iwezekanavyo, mambo yakae hadharani upesi ili wananchi wasipoteze imani kwa jeshi lao."

Akanywa maji kupooza koo alafu akaendelea kunguruma.

"Isipite wiki moja ... isipite wiki moja huyu muuaji hajakamatwa! Haiwezekani RPC auawe alafu hili jambo likachukuliwa wepesi wepesi tu. It is a serious issue. Na watu wote, nchi nzima wajue hilo. This is a serious issue."

Baada ya maongezi hayo Kamanda Mkuu akapendekeza Jona apatiwe kesi hiyo mikononi mwake. Akamsihi aitendee haki, na ndani ya muda mfupi awe ameshaonyesha matunda.

Kwa moyo mkunjufu, Jona akabeba jukumu hilo.

**

Aliyapekua mazingira yote ya ndani baada ya kufanya mahojiano na wanafamilia, mahojiano ambayo hayakuwa na matunda mengi kwake.

Kwa ufupi akagundua muuaji alifika na gari na kulipaki nje, akazama ndani kwa kuruka ukuta kisha akamuua mlinzi kwa kumnyonga, na kutulia hapo kwa muda kidogo kabla hajarahisishiwa kazi kwa Kamanda kutoka nje akiongea na simu.

Kamanda alikuwa anaongea na nani kwa muda huo? Na kwanini alitoka nje?

Kwa haraka Jona akaelezwa na kumbukumbu yake kuwa ni yeye ndiye alikuwa anateta na Kamanda kwa muda huo. Kuhakikisha akatazama 'call log' kwenye simu yake. Na kuhusu kutoka nje, ni Kamanda alimweleza hivyo baada ya kuona mtandao unasumbuwa awapo ndani.

Kwahiyo basi kwa upesi na wepesi kabisa, muuaji akamaliza tukio lake kwa kumpiga Kamanda risasi tatu za kichwani alafu akatumia tena ukuta na kuyeya.

Sehemu za ukuta alizotumia kuingia na kutoka nazo zililuwa zimechafuka. Na kwa nje ya uzio alipokuwa anatua, aliacha alama za viatu.

Mwanaume wa makamo, kwa mujibu wa ukubwa wa kiatu, na ni mwanaume mzito, kwa mujibu wa kutitia kwa nyayo za viatu ardhini.

Ubaya hakuna aliyekuwa anajua kimo wala mjazo wake wa mwili kwani mtu ambaye angeweza kuwa shuhuda, yani mlinzi, aliuawa na wanafamilia wengine walikuwa ndani wakati wa tendo.

Yani mwanaume mmoja tu alifanya haya, Jona aliwaza akiwa anatazama nyayo za viatu. Akapata wazo. Akapiga picha nyayo hizo na kuondoka zake kwenda kwa majirani kuuliza uliza kama kuna shuhuda yeyote aliyeona jambo.

Lakini akawaza akiwa njiani. Mwanaume huyo muuaji alikuwa anategemea kumuua Kamanda hapo nje au ilitokea kama bahati ya mtende?

**

Alitazama viatu vya wale wanaume aliowakamata kule kwa Marwa akivilinganisha na picha yake ya nyayo za viatu alizozipiga nyumbani kwa Kamanda, akagundua vyafanana.

Hapo Jona akapata kutengeneza picha yake kichwani kwamba mtu huyo alikuwa pia amevalia suti na kinyago usoni kama wafanyavyo wafuasi wa Sheng pindi watakapo kufanya tukio.

Sasa angalau akawa amepata pa kuanzia. Sheng atakuwa anahusika na mauaji haya lakini kwanini amuue Kamanda?

Simu ikaita na namba ngeni. Akapokea.

"Halo ... ndio, ni mwenyewe ..."

Simu ikakata. Huenda ni salio. Jona akaamua kuipigia namba hiyo na kuendelea kumskiza.

" ... usijali, enhe ulikuwa unasema ... ndio ... una uhakika? ... ndio mida ya usiku ... sawa, nashukuru kwa taarifa."

Mtu huyo aliyekuwa anaongea naye alijitambulisha kwa jina la Deo. Alikuwa ni mwanaume mwenye sauti nzito aliyejinasibu kuwa shahidi wa tukio. Ametumia namba ambazo Jona aliziacha kwa majirani kwa maelezo kuwa wakipata cha kumshirikisha basi wasisite kumtafuta.

Bwana Deo akamwambia Jona kuwa alishuhudia gari la watu waliofanya tukio. Na alipolielezea gari hilo lipoje, Jona akajikuta anashangaa kwa kufananisha taarifa hizo na gari walilokuwa wanalitumia yeye na Marwa hapa karibuni.

Habari hizi zikamshtua. Akataka kuonana na bwana Deo lakini mwanaume huyo akamwambia hana muda huo. Amejitolea tu kama msamaria mwema.

Jona akashusha pumzi ndefu ya uchovu.

**

"Karibu," Jona alimwonyeshea Marwa chupa kubwa whisky akiiweka mezani.

"Hapana, nashukuru," Marwa akamjibu akitabasamu kwa mbali. Jicho lake la kushoto lilikuwa limefunikwa na pamba na plasta. Walikuwa 'wamejiachia' sebuleni wakipigiwa muziki laini kandokando.

"Poleni kwa msiba, wanasafirisha?" Marwa akauliza.

"Nadhani," Jona akajibu akitazama chupa yake ya kileo. "Wataupeleka Morogoro."

Kukawa kimya kidogo Jona akimiminia kinywaji kwenye glasi.

"Vipi mmebaini chochote?"

"Yah! .. " Jona akajibu pasi na uhakika ndani yake. "Kiasi chake. Natumai mengi yatakuja kwa mujibu wa muda."

Kisha hawakuongea kwa muda mrefu kidogo Marwa akiwa anachezea simu na Jona akiwa anakunywa kinywaji chake.

"Hii kesi inaonyesha dalili ya kuwa controversial sana," Jona akauvunja ukimya. Alikuwa ameshakata nusu chupa ya kileo chake. "Lakini nitaimaliza tu," akajihakikishia. "Nitashinda."

Alikuwa kana kwamba anajiongelesha mwenyewe. Marwa alimuitikia kwa tabasamu tu na kupiga kimya. Pengine kwasababu hakujua nini Jona anamaanisha.

Jona hakufunguka kwa undani.

**

"Unahitajika ofisini kwa Kamanda," alisema afande fulani mwanamke aliyechungulia mlangoni mwa ofisi ya Jona baada ya kugonga mara tatu.

Jona asijiulize sana, akanyanyuka na kwenda huko alipokutana na kaimu Kamanda, ambaye kwa sasa tunaweza kusema yeye ndiye aliyekuwa katika nafasi ya marehemu Kamanda japokuwa bado hakuapishwa na kutangazwa.

Lakini hakuwa mwenyewe, ofisini pia alikuwapo mwanaume mzungu aliyevalia suti rangi ya grey. Nywele zake zilikuwa za gold 'blonde'. Lips ya juu ya mdomowe ilifunikwa na mustachi, macho yake yakifanana na ya paka.

Jona akaketi na kutambulishwa, yule mzungu alikwa anaitwa Elliot Parker. Ni mpelelezi mashuhuri toka kwenye shirika la viwango vya juu duniani kwenye maswala ya ujasusi na upelelezi.

Akaambiwa kuanzia muda huo kesi ya mauaji ya Kamanda itakuwa mikononi mwa mzungu huyo, Elliot Parker. Ampatie ushirikiano wote.

"Utamweleza ulipofikia na kila kitu ulichokipata huko," Kamanda akatoa agizo. Jona akiwa amepigwa na butwaa akauliza:

"Kamanda, kwani kuna shida gani imetokea mpaka kufikia hatua ya kumpatia kesi mpelelezi wa kigeni?"

"Kwasababu mojawapo ya mtuhumiwa ama watuhumiwa ni watu toka jeshi letu la polisi," Kamanda akajibu. "Hivyo kufanya kazi hii kwa ufanisi zaidi, pasipo na aina yoyote ya upendeleo ama kupindisha mambo, tulihitaji mtu toka nje."

Jona akahisi hapa kuna jambo halipo sawa.

**

UNAHISI KUNA MCHEZO GANI HAPA?
 
*ANGA LA WASHENZI (MSIMU WA PILI) -- 07*

*Simulizi za series*

ILIPOISHIA

"Kwasababu mojawapo ya mtuhumiwa ama watuhumiwa ni watu toka jeshi letu la polisi," Kamanda akajibu. "Hivyo kufanya kazi hii kwa ufanisi zaidi, pasipo na aina yoyote ya upendeleo ama kupindisha mambo, tulihitaji mtu toka nje."

Jona akahisi hapa kuna jambo halipo sawa.

ENDELEA

Ni nani huyo mtuhumiwa toka jeshi la polisi? Mbona upelelezi wake mfupi umeonyesha tofauti? Alijiuliza maswali haya kichwani kwa haraka. Ila hakuwa na namna zaidi ya kufuata agizo alilopewa na mkuu wake.

Hakuwa katika nafasi ya kupinga agizo bali kutekeleza agizo. Akaongea na Elliot Parker mpaka alipofikia na kisha akisindikizana naye akampeleka mpaka nyumbani kwa marehemu Kamanda.

Elliot Parker akitumia vifaa vyake vya kitaalamu akachukua ushahidi kwa 'kuscan' eneo ambalo mtuhumiwa alilishika wakati anaingilia na kutokea ndani kwa lengo la kupata alama za dole gumba.

Alipomaliza hilo akatumia "magnifying glass' kupekulia njia na nyayo za mtuhumiwa. Akaandika taarifa na kisha wakaondoka na Jona kurudi kituoni.

**

"Marwa, things are not ok. Nasense kuna mchezo unafanyila nyuma ya mgongo wangu," alisema Jona akiwa ameshikilia kichwa chake amejilaza kitini.

"Ni kuhusu ile kesi?" Marwa akauliza baada ya kuvuta juisi ndani ya glasi kwa mrija wake mwembamba. Mezani kulikuwa kuna dumu la lita tano likiwa limesheheni juisi ya embe. Kila mtu alikuwa na glasi yake ya juisi ila ya Jona haikuwa imepungua hata kidogo tangu ijazwe.

Mrija ulikuwa unaeleaelea juu ukikosa mteja.

"Yah ni kuhusu hiyo kesi," Jona akajibu. Macho yalionyesha yupo mbali kifkra. "Sielewi kuna nini hapa kati, lakini ..." Jona akatikisa kichwa. "Mambo hayapo sawa kabisa kabisa."

"Nini shida haswa?" Marwa akauliza akimtazama Jona na chongo lake.

"Nimefanya uchunguzi, na kwa clue ndogo niliyoipata, muuaji ni miongoni mwa watu wa Sheng kwa mujibu wa sare za viatu. Lakini ajabu ni kwamba, baadae shahidi anakuja kunambia gari aliloliona likiwa limebeba watuhumiwa ndilo lile tulilotumia hapa karibuni.

Kama haitoshi, Kamanda naye ananiambia mmoja wa watuhumiwa ni mtu toka jeshi la polisi, nastaajabu amejuaje kama mmoja wa watuhumiwa ni polisi na huku hajafanya uchunguzi, mpaka anafikia hatua ya kumleta mtu mgeni? Na alafu ilikuaje watuhumiwa hao wa mauaji wakapata gari ambalo lipo kituoni?
"
Marwa akaguna. Akaweka glasi chini na kukiri kuna jambo.

"Hapo inabidi uwe makini sana, Jona," akashauri. "Mi nakusihi kitu kimoja, usimwachie huyo mgeni akafanya upelelezi peke yake. Kula naye sahani moja. Unajua kwanini nakuambia hivyo?"

Marwa akaweka kituo kisha akaendelea:

"Hapo lolote linaweza kutokea. Sasa lazima na wewe uwe na nafasi ya kujihami. Uwe na maelezo yenye mantiki ya kukuweka salama na kulimaliza hili."

Ujumbe huu ukapenya kwenye masikio ya Jona. Kweli ulikuwa na mashiko. Aliona ana haja ya kujua kila kitu kitakachoendelea kwenye kesi hiyo. Na si tu kujua, bali awe amemtangulia bwana Elliot Parker kwenye harakati zake.

Ajue alichokiona mzungu huyo, alichokisikia, alichokiandika na kukisoma.

Baada ya hapo, angalau Jona akapata unafuu wa mawazo. Akanyanyua juisi na kuigida mapafu kadhaa. Sasa kichwani mwake alikuwa anafikiria namna gani atahakikisha anamweka bwana Elliot Parker mgongoni mwake.

Mara simu ikaita, akaitazama, alikuwa ni Miriam
.
"Hallo ... yes, habari yako? ... safi tu. Unaendeleaje? ... niko poa, nihabarishe ... saa hii? ... serious? ..."

Jona akatazama saa yake ya mkononi, saa moja usiku.

" ... ok, nakuja. Nipe dakika chache."

Akakata simu na kumtazama Marwa.

"Nadhani nimepata kazi ya dharura."

**

"Yupo wapi?" Lilikuwa swali la kwanza Jona kuuliza baada ya kuingia ndani mwa Shangazi yake Miriam. Alitumia kama nusu saa kufika hapo. Miriam, aliyekuwa ana uso wa hofu na macho mekundu, alimpokea na kumkumbatia kwanguvu. Hakuamini kama Jona angefika.

"Ahsante sana kwa kuja, Jona," alisema kwa toni ya uoga. "Naogopa, naogopa!"

"Usijali," Jona akamtoa hofu. "Yupo wapi?" Akarudia tena swali lake. Miriam akamwonyeshea mlango wa chumba kwa kidole, Jona akakimbilia huko kutazama akimwacha Miriam sebuleni.

Baada ya muda mfupi akarejea.

"It is not that serious," Jona alisema akiketi kochini. "Itakuwa ni Malaria tu si kingine."

"Kweli?" Miriam akauliza akitoa macho.

"Yah its true."

"Tumpeleke basi hospitali!"

"Hapana. Hamna haja hiyo. She is not in that critical situation, Miriam."

"Kweli? Mimi niliogopa sana," akasema Miriam kisha akajilazimisha kutabasamu.

"Ndo' ulikuwa ukiishi hivi na wanao?" Jona akauliza. Miriam akatabasamu kabla hajajibu.

"Mimi muoga sana. Eliakimu ndiyo alikuwa akisumbuka nao sana kipindi wanaumwa. Mimi mmh mmh mwoga sana."

"Hujawamiss watoto wako?"

"Nimewamiss mno. Ila naona ni kheri kwao wakawa na mimi mbali kwa muda huu. Natumai huko kwa shangazi yao wanaishi vema japo kuna muda huwa nawakumbuka sana!"

"Pole mama. "

"Vipi kuhusu wewe?"

"Mimi sina familia."

"Haiwezekani. Serious?"

"Ndio. Walifariki kwenye ajali ya moto miaka miwili iliyopita."

"Oh my God. Pole sana," alisema Miriam akimtazama Jona kwa sura ya huruma. Jona hakutaka kuendelea na simulizi hizo, huwa zinamuumiza sana pindi anapozikumbuka, akabadili mada kwa kumtaka Miriam amwonyeshe jokofu lao apate kutengeneza dawa ya mgonjwa.

"Dawa?" Miriam akatahamaki. "Hamna dawa kwenye friji."

"Najua haipo, ndiyo maana nataka kutengeneza," Jona akamjibu na kuongezea: "Nikiona vilivyomo nitajua cha kufanya. Usiku huu haitakiwi aachwe hivi hivi."

Wakaongozana mpaka jikoni, ndani ya jokofu Jona akatoa tunda moja la chenza na kulikata robo kipande kisha akakichemsha. Maji yake akampatia Miriam ampatie shangazi anywe.

"Akimaliza atalala vema."

Baada ya muda mfupi Miriam akarejea na kikombe kitupu. Akamwambia Jona tayari Shangazi amemaliza.

"Una uhakika itamsaidia?"

"Asilimia zote. Ndani ya kinywaji alichokunywa kuna unmodified natural quinine, itamsaidia."

Miriam akamkumbatia tena Jona.

"Nashukuru sana."

"Nadhani napaswa kwenda sasa," Jona akasema akijipapasa mifuko.

**

Ngo! Ngo! Ngo!

"Ingia," Jona alirusu hodi akitazama mlangoni. Akamwona bwana Elliot Parker akiingia ndani, amevalia suti nyeusi na kwenye mkono wake wa kushoto amebebelea mkoba wa kahawia.

Wakasilimiana, Elliot akaketi na kueleza dhamira ya ujio wake. Yupo pale kwa ajili ya kumuuliza Jona maswali kadhaa juu ya kesi ya mauaji ya Kamanda.

Jona hakuona shida, akamkarimu kwa mikono yote. Akamuahidi bwana Elliot atampatia ushirikiano wote autakao.

Elliot Parker akafungua mkoba wake na kutoa karatasi kadhaa. Akazitazama kwa zamu alafu moja akaiweka mezani na zingine akazirudisha mkobani.

Akaitazama tena ile karatasi aliyoiweka mezani alafu akaanza kumuuliza Jona maswali.

"Do you know the last person Chisanza communicated with?" (Unamjua mtu wa mwisho aliyewasiliana na Chisanza?)

"No, I dont," (Hapana, simjui,) Jona akajibu kwa kujiamini.

"Are you sure?" (Una uhakika?)

"Yes, I am." (Ndio, nina uhakika.)

"The last person was you," (mtu wa mwisho alikuwa wewe,) akasema Elliot Parker. "And it happened a few minutes before Chisanza was killed. Anything to say about that?" (Na ilitokea muda mfupi kabla Chisanza hajauawa. Chochote cha kusema kuhusu hilo?)

"I dont know anything about that," (sijui lolote kuhusu hilo,) alisema Jona. "I only contacted him about the case he gave me to deal with." (Niliwasiliana naye kuhusu kesi tu aliyonipa nihangaike nayo.)

"But you know that his house troubles them with network, right? And one has to go out to talk clearly?" (Lakini unajua nyumba yao inawasumbua mtandao, sio? Na mtu inambidi aende nje aongee vizuri?)

"Yes, I do." (Ndio, najua.)

Elliot Parker akaandika karatasini. Alafu akamuuliza Jona kuhusu gari linalosadikika kutumiwa na wauaji. Lini ilikuwa mara yake ya mwisho kulitumia na kama kuna mtu yeyote anayemjua ameshawahi kutumia gari hilo tangu lije kituoni.

Jona akaeleza hakuna aliyekuwa analitumia isipokuwa yeye tu ila kwenye shughuli zake za kazi. Baada ya maelezo hayo, bwana Elliot Parker akapaki vitu vyake na kuaga.

Akamwacha Jona akiwa na maswali kichwani. Hakuelewa kinachoendelea.

Ndani ya muda mfupi, wakaja polisi watatu, wakamuweka chini ya ulinzi. Akatiwa pingu mikononi.

Alikuwa ni mtuhumiwa namba moja wa mauaji.

**
 
*ANGA LA WASHENZI (MSIMU WA PILI) -- 07*

*Simulizi za series*

ILIPOISHIA

"Kwasababu mojawapo ya mtuhumiwa ama watuhumiwa ni watu toka jeshi letu la polisi," Kamanda akajibu. "Hivyo kufanya kazi hii kwa ufanisi zaidi, pasipo na aina yoyote ya upendeleo ama kupindisha mambo, tulihitaji mtu toka nje."

Jona akahisi hapa kuna jambo halipo sawa.

ENDELEA

Ni nani huyo mtuhumiwa toka jeshi la polisi? Mbona upelelezi wake mfupi umeonyesha tofauti? Alijiuliza maswali haya kichwani kwa haraka. Ila hakuwa na namna zaidi ya kufuata agizo alilopewa na mkuu wake.

Hakuwa katika nafasi ya kupinga agizo bali kutekeleza agizo. Akaongea na Elliot Parker mpaka alipofikia na kisha akisindikizana naye akampeleka mpaka nyumbani kwa marehemu Kamanda.

Elliot Parker akitumia vifaa vyake vya kitaalamu akachukua ushahidi kwa 'kuscan' eneo ambalo mtuhumiwa alilishika wakati anaingilia na kutokea ndani kwa lengo la kupata alama za dole gumba.

Alipomaliza hilo akatumia "magnifying glass' kupekulia njia na nyayo za mtuhumiwa. Akaandika taarifa na kisha wakaondoka na Jona kurudi kituoni.

**

"Marwa, things are not ok. Nasense kuna mchezo unafanyila nyuma ya mgongo wangu," alisema Jona akiwa ameshikilia kichwa chake amejilaza kitini.

"Ni kuhusu ile kesi?" Marwa akauliza baada ya kuvuta juisi ndani ya glasi kwa mrija wake mwembamba. Mezani kulikuwa kuna dumu la lita tano likiwa limesheheni juisi ya embe. Kila mtu alikuwa na glasi yake ya juisi ila ya Jona haikuwa imepungua hata kidogo tangu ijazwe.

Mrija ulikuwa unaeleaelea juu ukikosa mteja.

"Yah ni kuhusu hiyo kesi," Jona akajibu. Macho yalionyesha yupo mbali kifkra. "Sielewi kuna nini hapa kati, lakini ..." Jona akatikisa kichwa. "Mambo hayapo sawa kabisa kabisa."

"Nini shida haswa?" Marwa akauliza akimtazama Jona na chongo lake.

"Nimefanya uchunguzi, na kwa clue ndogo niliyoipata, muuaji ni miongoni mwa watu wa Sheng kwa mujibu wa sare za viatu. Lakini ajabu ni kwamba, baadae shahidi anakuja kunambia gari aliloliona likiwa limebeba watuhumiwa ndilo lile tulilotumia hapa karibuni.

Kama haitoshi, Kamanda naye ananiambia mmoja wa watuhumiwa ni mtu toka jeshi la polisi, nastaajabu amejuaje kama mmoja wa watuhumiwa ni polisi na huku hajafanya uchunguzi, mpaka anafikia hatua ya kumleta mtu mgeni? Na alafu ilikuaje watuhumiwa hao wa mauaji wakapata gari ambalo lipo kituoni?
"
Marwa akaguna. Akaweka glasi chini na kukiri kuna jambo.

"Hapo inabidi uwe makini sana, Jona," akashauri. "Mi nakusihi kitu kimoja, usimwachie huyo mgeni akafanya upelelezi peke yake. Kula naye sahani moja. Unajua kwanini nakuambia hivyo?"

Marwa akaweka kituo kisha akaendelea:

"Hapo lolote linaweza kutokea. Sasa lazima na wewe uwe na nafasi ya kujihami. Uwe na maelezo yenye mantiki ya kukuweka salama na kulimaliza hili."

Ujumbe huu ukapenya kwenye masikio ya Jona. Kweli ulikuwa na mashiko. Aliona ana haja ya kujua kila kitu kitakachoendelea kwenye kesi hiyo. Na si tu kujua, bali awe amemtangulia bwana Elliot Parker kwenye harakati zake.

Ajue alichokiona mzungu huyo, alichokisikia, alichokiandika na kukisoma.

Baada ya hapo, angalau Jona akapata unafuu wa mawazo. Akanyanyua juisi na kuigida mapafu kadhaa. Sasa kichwani mwake alikuwa anafikiria namna gani atahakikisha anamweka bwana Elliot Parker mgongoni mwake.

Mara simu ikaita, akaitazama, alikuwa ni Miriam
.
"Hallo ... yes, habari yako? ... safi tu. Unaendeleaje? ... niko poa, nihabarishe ... saa hii? ... serious? ..."

Jona akatazama saa yake ya mkononi, saa moja usiku.

" ... ok, nakuja. Nipe dakika chache."

Akakata simu na kumtazama Marwa.

"Nadhani nimepata kazi ya dharura."

**

"Yupo wapi?" Lilikuwa swali la kwanza Jona kuuliza baada ya kuingia ndani mwa Shangazi yake Miriam. Alitumia kama nusu saa kufika hapo. Miriam, aliyekuwa ana uso wa hofu na macho mekundu, alimpokea na kumkumbatia kwanguvu. Hakuamini kama Jona angefika.

"Ahsante sana kwa kuja, Jona," alisema kwa toni ya uoga. "Naogopa, naogopa!"

"Usijali," Jona akamtoa hofu. "Yupo wapi?" Akarudia tena swali lake. Miriam akamwonyeshea mlango wa chumba kwa kidole, Jona akakimbilia huko kutazama akimwacha Miriam sebuleni.

Baada ya muda mfupi akarejea.

"It is not that serious," Jona alisema akiketi kochini. "Itakuwa ni Malaria tu si kingine."

"Kweli?" Miriam akauliza akitoa macho.

"Yah its true."

"Tumpeleke basi hospitali!"

"Hapana. Hamna haja hiyo. She is not in that critical situation, Miriam."

"Kweli? Mimi niliogopa sana," akasema Miriam kisha akajilazimisha kutabasamu.

"Ndo' ulikuwa ukiishi hivi na wanao?" Jona akauliza. Miriam akatabasamu kabla hajajibu.

"Mimi muoga sana. Eliakimu ndiyo alikuwa akisumbuka nao sana kipindi wanaumwa. Mimi mmh mmh mwoga sana."

"Hujawamiss watoto wako?"

"Nimewamiss mno. Ila naona ni kheri kwao wakawa na mimi mbali kwa muda huu. Natumai huko kwa shangazi yao wanaishi vema japo kuna muda huwa nawakumbuka sana!"

"Pole mama. "

"Vipi kuhusu wewe?"

"Mimi sina familia."

"Haiwezekani. Serious?"

"Ndio. Walifariki kwenye ajali ya moto miaka miwili iliyopita."

"Oh my God. Pole sana," alisema Miriam akimtazama Jona kwa sura ya huruma. Jona hakutaka kuendelea na simulizi hizo, huwa zinamuumiza sana pindi anapozikumbuka, akabadili mada kwa kumtaka Miriam amwonyeshe jokofu lao apate kutengeneza dawa ya mgonjwa.

"Dawa?" Miriam akatahamaki. "Hamna dawa kwenye friji."

"Najua haipo, ndiyo maana nataka kutengeneza," Jona akamjibu na kuongezea: "Nikiona vilivyomo nitajua cha kufanya. Usiku huu haitakiwi aachwe hivi hivi."

Wakaongozana mpaka jikoni, ndani ya jokofu Jona akatoa tunda moja la chenza na kulikata robo kipande kisha akakichemsha. Maji yake akampatia Miriam ampatie shangazi anywe.

"Akimaliza atalala vema."

Baada ya muda mfupi Miriam akarejea na kikombe kitupu. Akamwambia Jona tayari Shangazi amemaliza.

"Una uhakika itamsaidia?"

"Asilimia zote. Ndani ya kinywaji alichokunywa kuna unmodified natural quinine, itamsaidia."

Miriam akamkumbatia tena Jona.

"Nashukuru sana."

"Nadhani napaswa kwenda sasa," Jona akasema akijipapasa mifuko.

**

Ngo! Ngo! Ngo!

"Ingia," Jona alirusu hodi akitazama mlangoni. Akamwona bwana Elliot Parker akiingia ndani, amevalia suti nyeusi na kwenye mkono wake wa kushoto amebebelea mkoba wa kahawia.

Wakasilimiana, Elliot akaketi na kueleza dhamira ya ujio wake. Yupo pale kwa ajili ya kumuuliza Jona maswali kadhaa juu ya kesi ya mauaji ya Kamanda.

Jona hakuona shida, akamkarimu kwa mikono yote. Akamuahidi bwana Elliot atampatia ushirikiano wote autakao.

Elliot Parker akafungua mkoba wake na kutoa karatasi kadhaa. Akazitazama kwa zamu alafu moja akaiweka mezani na zingine akazirudisha mkobani.

Akaitazama tena ile karatasi aliyoiweka mezani alafu akaanza kumuuliza Jona maswali.

"Do you know the last person Chisanza communicated with?" (Unamjua mtu wa mwisho aliyewasiliana na Chisanza?)

"No, I dont," (Hapana, simjui,) Jona akajibu kwa kujiamini.

"Are you sure?" (Una uhakika?)

"Yes, I am." (Ndio, nina uhakika.)

"The last person was you," (mtu wa mwisho alikuwa wewe,) akasema Elliot Parker. "And it happened a few minutes before Chisanza was killed. Anything to say about that?" (Na ilitokea muda mfupi kabla Chisanza hajauawa. Chochote cha kusema kuhusu hilo?)

"I dont know anything about that," (sijui lolote kuhusu hilo,) alisema Jona. "I only contacted him about the case he gave me to deal with." (Niliwasiliana naye kuhusu kesi tu aliyonipa nihangaike nayo.)

"But you know that his house troubles them with network, right? And one has to go out to talk clearly?" (Lakini unajua nyumba yao inawasumbua mtandao, sio? Na mtu inambidi aende nje aongee vizuri?)

"Yes, I do." (Ndio, najua.)

Elliot Parker akaandika karatasini. Alafu akamuuliza Jona kuhusu gari linalosadikika kutumiwa na wauaji. Lini ilikuwa mara yake ya mwisho kulitumia na kama kuna mtu yeyote anayemjua ameshawahi kutumia gari hilo tangu lije kituoni.

Jona akaeleza hakuna aliyekuwa analitumia isipokuwa yeye tu ila kwenye shughuli zake za kazi. Baada ya maelezo hayo, bwana Elliot Parker akapaki vitu vyake na kuaga.

Akamwacha Jona akiwa na maswali kichwani. Hakuelewa kinachoendelea.

Ndani ya muda mfupi, wakaja polisi watatu, wakamuweka chini ya ulinzi. Akatiwa pingu mikononi.

Alikuwa ni mtuhumiwa namba moja wa mauaji.

**
*****, ngoma imefika patam sasa[emoji39] [emoji39] [emoji39]
 
Back
Top Bottom