*ANGA LA WASHENZI (MSIMU WA PILI) -- 12*
*Simulizi za series*
ILIPOISHIA
"Let's meet immediately and see what we can do!" (Tukutane mara moja tutazame nini tunaweza fanya!)
Akaskiza tena. Kisha akahitimisha.
"It is either we get the door or make it by ourselves" (Ni aidha tuupate mlango ama tuutengeneze wenyewe!)
ENDELEA
Akakata simu na kuirejesha mfukoni. Hamu ya kuendelea na 'shopping' ilikata. Akatoka kufuata gari lake akakwea na kuhepa.
**
"Upo sawa mzee?" Aliuliza mahabusu mmoja akimtazama Jona kwa macho ya wasi.
Jona alikuwa amelala chini akiwa ameshika kichwa kwa kuhisi maumivu makali. Pua yake ilikuwa inachuruza damu. Macho yake hayakuwa yanaona vema ingawa alivalia miwani.
Alikuwa anajihisi mdhaifu mwili mzima. Haswa kwenye maungio ya mwili. Mishipa ya damu ilikuwa inamvuta, na kwa wakati huohuo akihisi baridi kali!!
Wenzake, wanne, waliokuwepo ndani wakawa wanamtazama kwa hofu. Walikuwa wameshamtambua kama mtu asiyelala nyakati za usiku, ila hii ya leo ilikuwa mpya. Walihofu huenda amezidiwa. Haikuwa hali ya kawaida!
Alikuwa ananguruma na kugugumia kwa maumivu. Mwili unamtoka jasho jingi, alafu bado anajikunyata!!
"Muite afande," mmoja akashauri. Yule aliyekuwa karibu na langoni akapaza sauti kuita afande afande kuna mtu kazidiwa. Ndani ya muda mfupi afande fulani akafika hapo na kumtazama Jona.
Akashtuka! Haraka akaenda kaunta na kumpasha habari koplo Massawe aliyekuwa ameketi hapo.
"Afande, kuna mtu kazidiwa mahabusu. Tufanye namna!"
"Nani huyo?"
"Jona!"
"Jona?"
"Ndio. Anatokwa na damu puani. Anamiminika jasho."
Massawe akaguna na kufikiri kidogo. Akachomoa simu yake na kupiga. Baada ya muda mfupi ikapokelewa. Akaelezea hilo jambo la Jona.
"Aanh ... sawa, mkuu. Hamna shida."
Massawe akakata na kisha akaketi.
"Achana naye!" Akamwambia yule afande aliyekuja kumpasha.
"Unasema?" Afande akashangaa.
"Nimesema achana naye. Hujasikia nini hapo?" Massawe akapandisha sauti. "Achana naye atarejea kwenye hali yake mwenyewe!"
Afande yule mpasha habari akanyamaza na duku lake kifuani. Na hii ndiyo moja ya shida ya jeshi. Pale mkubwa wako anapoamuru jambo huna nafasi ya kulikosoa zaidi ya kulifuata tu. Hata kama waliona halipo sahihi!
Na kwa afande huyu alifanikiwa kulimeza duku lake akaendelea na mengine kwani alifundishwa kufanya hivi huko mafunzoni. Hata 'mkubwa' akikuagiza usukume jengo mpaka lianguke, huulizi kama inawezekana, bali unaweka mikono yako ukutani na kupoteza nguvu yako bure!
Lengo kulazimisha tu utii ustawi ndani yako. Lakini pengine pia, kwa kujua ama kutokujua, huchochea hisia za uoga na unyenyekevu zoba.
"Afandeee!" Sauti za mahabusu iliendelea kuita. "Mtu amezidiwa huku jamani!"
Massawe kama vile hakusikia hayo akaendelea na kazi zake, afande mwingine akiwa anamtazama kwa kuibiaibia, alitumai pengine Massawe angeguswa hivi karibuni.
Lakini alikosea. Massawe alitia pamba masikioni. Hakuwa anasikia wala kujali.
**
"Amekufa?" Aliuliza mwanaume aliyekuwa amesimama langoni. Macho yake yalikuwa yanamtazama Jona akiwa ametulia tuli hachezi wala hatikisiki!!
Haraka akatoka langoni na kusogea karibu kuwakuta wenzake waliokuwa wanamtazama Jona kwa macho ya maulizo.
"Amekufa nini?"
"Sijui! Mbona ametulia hivi?"
"Huyu atakuwa amekufa!" Akauliza mmoja kisha akaweka kiganja chake shavuni mwa Jona. "Wa baridi kweli!"
Mwingine akaweka sikio kifuani, "bado mzima!" Akalipuka. "Nasikia mapigo yake ya moyo kwa mbali sana!"
"Atakuwa kazirai nini?"
"Labda. Unajua mwili wa binadamu ukishindwa kuhimili maumivu, unapoteza fahamu!"
"Sasa tunafanyaje?"
"Unadhani tutafanya nini hapa? Wenzake wenyewe wamemsusa!"
"Wenzake gani?"
"Si hao mapolisi wenzake!"
"Huyu ni polisi?"
"Ndo maana yake. Inasemekana ndo kamuua RPC. Sasa naona wenzake kama vile wamemshit! Si unajua ile? ... wanamkomoa flani hivi!"
"Duh! Noma kweli mwanangu. Ila akifia humu itakuwa soo."
"Hamna soo wala nini. Mbuzi atakuwa kafia kwa muuza supu!"
Maongezi haya yote Jona alikuwa anayasikia kwa mbali sana ... mbali sana ...
Kwa mbali sauti hizi zilivuma masikioni mwake katika mfumo wa mwangwi kana kwamba zinatokea ndani ya chungu ama pango kubwa. Hakuweza hata kutambua nani aliyekuwa anaongea hapa au pale japo alikuwa anawafahamu wote waliopo mule rumande.
Alitamani kutikisa mwili wake lakini hakuwa anaweza hata kidogo. Mwili ulikuwa mzito mno! Kichwani alikuwa anasikia kana kwamba sauti ya panga ama jembe likiwa limekita kwenye mwamba mgumu!
... Kaaaaaangggg' ... kaaaaaanggggggg'
Hakujua nini kinaendelea ndani ya mwili wake. Alifahamu fika tatizo litakuwa kile chakula alichokula. Ila hakutambua hii ilikuwa sumu gani. Na lengo lake mwilini lilikuwa ni nini.
Mbona bado yupo hai? Lakini akalitilia mashaka hili. Pengine amekufa na yeye bado hajalitambua. Kama hawezi kusogeza kiungo chochote cha mwili, ni nini huko kama si kufa sasa?
"Naaammmuuuuoooonnnnaaaa ...." alisikia sauti kwa mbali ikinong'ona kwa kujivuta. Neno moja alilisikia likiwa refu mno. Sauti hii akaitambua kuwa ya kipekee tofauti na zile alizokuwa anazisikia hapo awali.
Lakini bado fahamu zake hazikuweza kumjuza ni ya nani haswa! Akakodoa macho, lakini alikuwa anaona kizakiza cha kina cha maji. Watu awaona kama vivuli kwenye kioo.
"Kwwwwiiiiiiiissssshhhaaaaaa haaaabaaaarrriiii yaaaakkkeeee!!" Aliendelea kusikia kwa mbali. "Haaaaaaappppoooo haaaattaaatuusuuumbuuaaa tenaaa. Yeyyyyeee ndooo atttaatussumbuaa sisssiiii!"
Kikafuatia kicheko. Haa haaaa haa haaaa haa!
**
"You are on time!" (Upo ndani ya muda!) Alisema BC akitazama saa yake mkononi. Alishafika nyumbani kwake, ameketi kibarazani penye viti na meza vya kupumzikia. Hakuwa amebadili nguo. Hakuingia hata ndani tokea amefika, zaidi ya kuketi hapo kumngoja mwanamke huyu,
Miranda. Ambaye alifika hapo akiwa amevalia jeans ya bluu na tisheti jeusi.
Uso wake haukuwa na furaha.
Alivuta kiti akaketi kisha pasipo kupoteza muda akaendea kilichomleta hapo.
"As I told you earlier. What should we do now?" (Kama nilivyokuambia hapo mapema. Nini tufanye sasa?)
"It is simple. We want him out, right?" (Ni rahisi. Tunamtaka atoke, sio?)
"Yes, we do! But do you think it will be that easy? He is charged of murder. Murder of a big man!" (Ndio, tunataka! Lakini unadhani itakuwa rahisi? Anashikiliwa kwa mauaji. Mauaji ya mtu mkubwa!)
"Maybe we should try to bail him out. Even if it may cost much!" (Pengine tungejaribu kumtoa kwa dhamana. Japo inaweza kugharimu mno!)
"What if that way won't work?" (Vipi kama njia hiyo haitafanikiwa?)
"Then we'll try the other one." (Basi tutajaribu nyingine.)
Miranda akachipua tabasamu. Lakini BC akampatia tahadhari.
"That other way will only be possible if Jona complies with my conditions." (Hiyo njia nyingine itawezekana kama tu Jona atakubaliana na vigezo vyangu."
**
Majira ya asubuhi ... kama saa nne hivi.
Kwa mbali kidogo Marwa anatazama kwenye lango la kituo kikuu akiwa amesimama na mfuko wake wa nailoni wenye chakula.
Alikuwa amevalia suruali pana ya kitambaa na shati lililokunjamana kwa uhaba wa pasi.
Akiwa anatazama huko akamwona afande Devi akitoka akiwa anaongozana na mwanamke fulani hivi, wakasimama langoni, na mara wakamtazama kwa pamoja, afande akamnyooshea kidole.
Punde mwanamke huyo akaanza kuchukua hatua kumfuata Marwa. Alipomfikia akamsalimu na kujitambulisha kama rafiki yake Jona. Yupo hapo kumtembelea na kumjulia hali.
Naye Marwa akajitambulisha kama ndugu na mkazi mmoja na Jona.
Lakini haikuchukua muda mrefu, Miranda akatambua Marwa hakuwa sawa. Macho yake yalikuwa mekundu, pia hakuonyesha yupo 'comfortable' kuongea naye.
Pengine alikuwa anamshuku anaweza akawa si mtu mzuri, akawaza. Kumwondoa hofu Marwa, Miranda akajipambanua kwa undani namna anavyoielewa kesi ile ya Jona kama ilivyopandikizwa mahususi kumteketeza, na mtuhumiwa wake mkubwa akiwa ni Sheng.
Ils hakusita kuonyesha imani yake.
"Naamini Jona atayashinda yote haya."
Hapa Marwa akashindwa kubana hisia zake. Machozi yakamminika.
Akasema:
"Hata atakapoyashinda haya hatakuwa Jona wa awali."
"Una maanisha nini?" Miranda akawahi kumuuliza.
"Tayari wameshamtilia virus mwilini!" Marwa akajibu machozi yakibubujika. "Hataweza kudumu muda mrefu, labda tu awe anapewa antidote! ... Antidote ambayo anayo Sheng pekee!"
Miranda akakaukiwa na mate mdomoni.
"Umejuaje wamemtilia virus? Na kwanini wafanye hivyo?" Akauliza kwa kinywa chake kikavu.
***
Sent from my SM-J110F using
JamiiForums mobile app