Anga la washenzi na Joana anaona kitu usiku

Anga la washenzi na Joana anaona kitu usiku

nakuomba kaka jona uwe hukula kile cchakula
Najua hata akitokea kula atapona tuu, pia naona Miranda akimpa boka vitu adimu na kuomba jona aachiwe afanye kazi yake haraka sana [emoji1] [emoji1] [emoji1] [emoji1] [emoji1]
 
*ANGA LA WASHENZI (MSIMU WA PILI) -- 12*

*Simulizi za series*


ILIPOISHIA

"Let's meet immediately and see what we can do!" (Tukutane mara moja tutazame nini tunaweza fanya!)

Akaskiza tena. Kisha akahitimisha.

"It is either we get the door or make it by ourselves" (Ni aidha tuupate mlango ama tuutengeneze wenyewe!)

ENDELEA

Akakata simu na kuirejesha mfukoni. Hamu ya kuendelea na 'shopping' ilikata. Akatoka kufuata gari lake akakwea na kuhepa.

**

"Upo sawa mzee?" Aliuliza mahabusu mmoja akimtazama Jona kwa macho ya wasi.

Jona alikuwa amelala chini akiwa ameshika kichwa kwa kuhisi maumivu makali. Pua yake ilikuwa inachuruza damu. Macho yake hayakuwa yanaona vema ingawa alivalia miwani.

Alikuwa anajihisi mdhaifu mwili mzima. Haswa kwenye maungio ya mwili. Mishipa ya damu ilikuwa inamvuta, na kwa wakati huohuo akihisi baridi kali!!

Wenzake, wanne, waliokuwepo ndani wakawa wanamtazama kwa hofu. Walikuwa wameshamtambua kama mtu asiyelala nyakati za usiku, ila hii ya leo ilikuwa mpya. Walihofu huenda amezidiwa. Haikuwa hali ya kawaida!

Alikuwa ananguruma na kugugumia kwa maumivu. Mwili unamtoka jasho jingi, alafu bado anajikunyata!!

"Muite afande," mmoja akashauri. Yule aliyekuwa karibu na langoni akapaza sauti kuita afande afande kuna mtu kazidiwa. Ndani ya muda mfupi afande fulani akafika hapo na kumtazama Jona.

Akashtuka! Haraka akaenda kaunta na kumpasha habari koplo Massawe aliyekuwa ameketi hapo.

"Afande, kuna mtu kazidiwa mahabusu. Tufanye namna!"

"Nani huyo?"

"Jona!"

"Jona?"

"Ndio. Anatokwa na damu puani. Anamiminika jasho."

Massawe akaguna na kufikiri kidogo. Akachomoa simu yake na kupiga. Baada ya muda mfupi ikapokelewa. Akaelezea hilo jambo la Jona.

"Aanh ... sawa, mkuu. Hamna shida."

Massawe akakata na kisha akaketi.

"Achana naye!" Akamwambia yule afande aliyekuja kumpasha.

"Unasema?" Afande akashangaa.

"Nimesema achana naye. Hujasikia nini hapo?" Massawe akapandisha sauti. "Achana naye atarejea kwenye hali yake mwenyewe!"

Afande yule mpasha habari akanyamaza na duku lake kifuani. Na hii ndiyo moja ya shida ya jeshi. Pale mkubwa wako anapoamuru jambo huna nafasi ya kulikosoa zaidi ya kulifuata tu. Hata kama waliona halipo sahihi!

Na kwa afande huyu alifanikiwa kulimeza duku lake akaendelea na mengine kwani alifundishwa kufanya hivi huko mafunzoni. Hata 'mkubwa' akikuagiza usukume jengo mpaka lianguke, huulizi kama inawezekana, bali unaweka mikono yako ukutani na kupoteza nguvu yako bure!

Lengo kulazimisha tu utii ustawi ndani yako. Lakini pengine pia, kwa kujua ama kutokujua, huchochea hisia za uoga na unyenyekevu zoba.

"Afandeee!" Sauti za mahabusu iliendelea kuita. "Mtu amezidiwa huku jamani!"

Massawe kama vile hakusikia hayo akaendelea na kazi zake, afande mwingine akiwa anamtazama kwa kuibiaibia, alitumai pengine Massawe angeguswa hivi karibuni.

Lakini alikosea. Massawe alitia pamba masikioni. Hakuwa anasikia wala kujali.

**

"Amekufa?" Aliuliza mwanaume aliyekuwa amesimama langoni. Macho yake yalikuwa yanamtazama Jona akiwa ametulia tuli hachezi wala hatikisiki!!

Haraka akatoka langoni na kusogea karibu kuwakuta wenzake waliokuwa wanamtazama Jona kwa macho ya maulizo.

"Amekufa nini?"

"Sijui! Mbona ametulia hivi?"

"Huyu atakuwa amekufa!" Akauliza mmoja kisha akaweka kiganja chake shavuni mwa Jona. "Wa baridi kweli!"

Mwingine akaweka sikio kifuani, "bado mzima!" Akalipuka. "Nasikia mapigo yake ya moyo kwa mbali sana!"

"Atakuwa kazirai nini?"

"Labda. Unajua mwili wa binadamu ukishindwa kuhimili maumivu, unapoteza fahamu!"

"Sasa tunafanyaje?"

"Unadhani tutafanya nini hapa? Wenzake wenyewe wamemsusa!"

"Wenzake gani?"

"Si hao mapolisi wenzake!"

"Huyu ni polisi?"

"Ndo maana yake. Inasemekana ndo kamuua RPC. Sasa naona wenzake kama vile wamemshit! Si unajua ile? ... wanamkomoa flani hivi!"

"Duh! Noma kweli mwanangu. Ila akifia humu itakuwa soo."

"Hamna soo wala nini. Mbuzi atakuwa kafia kwa muuza supu!"

Maongezi haya yote Jona alikuwa anayasikia kwa mbali sana ... mbali sana ...

Kwa mbali sauti hizi zilivuma masikioni mwake katika mfumo wa mwangwi kana kwamba zinatokea ndani ya chungu ama pango kubwa. Hakuweza hata kutambua nani aliyekuwa anaongea hapa au pale japo alikuwa anawafahamu wote waliopo mule rumande.

Alitamani kutikisa mwili wake lakini hakuwa anaweza hata kidogo. Mwili ulikuwa mzito mno! Kichwani alikuwa anasikia kana kwamba sauti ya panga ama jembe likiwa limekita kwenye mwamba mgumu!

... Kaaaaaangggg' ... kaaaaaanggggggg'

Hakujua nini kinaendelea ndani ya mwili wake. Alifahamu fika tatizo litakuwa kile chakula alichokula. Ila hakutambua hii ilikuwa sumu gani. Na lengo lake mwilini lilikuwa ni nini.

Mbona bado yupo hai? Lakini akalitilia mashaka hili. Pengine amekufa na yeye bado hajalitambua. Kama hawezi kusogeza kiungo chochote cha mwili, ni nini huko kama si kufa sasa?

"Naaammmuuuuoooonnnnaaaa ...." alisikia sauti kwa mbali ikinong'ona kwa kujivuta. Neno moja alilisikia likiwa refu mno. Sauti hii akaitambua kuwa ya kipekee tofauti na zile alizokuwa anazisikia hapo awali.

Lakini bado fahamu zake hazikuweza kumjuza ni ya nani haswa! Akakodoa macho, lakini alikuwa anaona kizakiza cha kina cha maji. Watu awaona kama vivuli kwenye kioo.

"Kwwwwiiiiiiiissssshhhaaaaaa haaaabaaaarrriiii yaaaakkkeeee!!" Aliendelea kusikia kwa mbali. "Haaaaaaappppoooo haaaattaaatuusuuumbuuaaa tenaaa. Yeyyyyeee ndooo atttaatussumbuaa sisssiiii!"

Kikafuatia kicheko. Haa haaaa haa haaaa haa!

**

"You are on time!" (Upo ndani ya muda!) Alisema BC akitazama saa yake mkononi. Alishafika nyumbani kwake, ameketi kibarazani penye viti na meza vya kupumzikia. Hakuwa amebadili nguo. Hakuingia hata ndani tokea amefika, zaidi ya kuketi hapo kumngoja mwanamke huyu,

Miranda. Ambaye alifika hapo akiwa amevalia jeans ya bluu na tisheti jeusi.

Uso wake haukuwa na furaha.

Alivuta kiti akaketi kisha pasipo kupoteza muda akaendea kilichomleta hapo.

"As I told you earlier. What should we do now?" (Kama nilivyokuambia hapo mapema. Nini tufanye sasa?)

"It is simple. We want him out, right?" (Ni rahisi. Tunamtaka atoke, sio?)

"Yes, we do! But do you think it will be that easy? He is charged of murder. Murder of a big man!" (Ndio, tunataka! Lakini unadhani itakuwa rahisi? Anashikiliwa kwa mauaji. Mauaji ya mtu mkubwa!)

"Maybe we should try to bail him out. Even if it may cost much!" (Pengine tungejaribu kumtoa kwa dhamana. Japo inaweza kugharimu mno!)

"What if that way won't work?" (Vipi kama njia hiyo haitafanikiwa?)

"Then we'll try the other one." (Basi tutajaribu nyingine.)

Miranda akachipua tabasamu. Lakini BC akampatia tahadhari.

"That other way will only be possible if Jona complies with my conditions." (Hiyo njia nyingine itawezekana kama tu Jona atakubaliana na vigezo vyangu."

**

Majira ya asubuhi ... kama saa nne hivi.


Kwa mbali kidogo Marwa anatazama kwenye lango la kituo kikuu akiwa amesimama na mfuko wake wa nailoni wenye chakula.

Alikuwa amevalia suruali pana ya kitambaa na shati lililokunjamana kwa uhaba wa pasi.

Akiwa anatazama huko akamwona afande Devi akitoka akiwa anaongozana na mwanamke fulani hivi, wakasimama langoni, na mara wakamtazama kwa pamoja, afande akamnyooshea kidole.

Punde mwanamke huyo akaanza kuchukua hatua kumfuata Marwa. Alipomfikia akamsalimu na kujitambulisha kama rafiki yake Jona. Yupo hapo kumtembelea na kumjulia hali.

Naye Marwa akajitambulisha kama ndugu na mkazi mmoja na Jona.

Lakini haikuchukua muda mrefu, Miranda akatambua Marwa hakuwa sawa. Macho yake yalikuwa mekundu, pia hakuonyesha yupo 'comfortable' kuongea naye.

Pengine alikuwa anamshuku anaweza akawa si mtu mzuri, akawaza. Kumwondoa hofu Marwa, Miranda akajipambanua kwa undani namna anavyoielewa kesi ile ya Jona kama ilivyopandikizwa mahususi kumteketeza, na mtuhumiwa wake mkubwa akiwa ni Sheng.

Ils hakusita kuonyesha imani yake.

"Naamini Jona atayashinda yote haya."

Hapa Marwa akashindwa kubana hisia zake. Machozi yakamminika.

Akasema:

"Hata atakapoyashinda haya hatakuwa Jona wa awali."

"Una maanisha nini?" Miranda akawahi kumuuliza.

"Tayari wameshamtilia virus mwilini!" Marwa akajibu machozi yakibubujika. "Hataweza kudumu muda mrefu, labda tu awe anapewa antidote! ... Antidote ambayo anayo Sheng pekee!"

Miranda akakaukiwa na mate mdomoni.

"Umejuaje wamemtilia virus? Na kwanini wafanye hivyo?" Akauliza kwa kinywa chake kikavu.


***

Sent from my SM-J110F using JamiiForums mobile app
 
*ANGA LA WASHENZI (MSIMU WA PILI) -- 13*

*Simulizi za series*

ILIPOISHIA

Miranda akakaukiwa na mate mdomoni.

"Umejuaje wamemtilia virus? Na kwanini wafanye hivyo?" Akauliza kwa kinywa chake kikavu.

ENDELEA

Marwa akafuta kwanza chozi lake alafu akamwambia alijua hilo punde tu alipomwona Jona. Hali yake aliyokuwa anaipitia ilikuwa ndiyo ileile ambayo wazazi wake waliipitia kwasababu ya kutiliwa virus.

"Atapata shida sana," akasema Marwa akijaribu kukumbuka namna wazazi wake walivyokuwa wanahanya. "Namwonea huruma. Na Sheng atamgeuza mtumwa!"

"Kivipi?" Miranda akawahi kuuliza.

Marwa akaeleza namna gani Sheng hutumia silaha hiyo ya virusi kumteka mtu akimfanya mtumwa wa antidote. Endapo unataka unafuu dhidi ya maumivu makali unayojisikia basi atakupatia antidote lakini kwa mabadilishano na kazi yake anayotaka utende.

Miranda akapatwa na woga. Hata akaishiwa na nguvu. Akamtaka Marwa waende kantini wakaketi na kuongea zaidi.

Wakaagiza chakula na kuendeleza soga. Miranda akamsikiliza vema Marwa akijieleza. Naye akaja kujinasibu kuwa yu mpangoni kumsaidia Jona atoke ndani, japo hajajua ni kwa namna gani.

"Afande wameniambia hawezi kupata dhamana hata kidogo, wala nisijisumbue popote pale. Nawaza namna ya kumng'amua mule."

"Dada yangu," Marwa akaita. "Naomba tu utafute namna yoyote. Na hata kama ukihitaji msaada toka kwangu, nipo radhi kukusaidia kadiri ya uwezo wangu wote ... Jona atapata shida sana mule ndani. Watamtesa haswa kwa wale virus kwa maana hata antidote tuliyonayo haitoshi hata zaidi ya siku nne!"

Miranda akakuna kichwa chake kwa ukucha. Alikuwa anawaza. Alisonya kisha akatoa simu yake mfukoni na 'kuchonga' na BC. Akampasha habari namna alivyogonga mwamba kuhusu mambo ya dhamana.

"Ok, but it should be as fast as possible!" (Sawa, lakini inabidi iwe haraka iwezekanavyo!)

Miranda akakata simu kisha akamuaga Marwa, aenda zake. Wakabadilishana namba mwanamke huyo akayeya akionekana kuwa na haraka.

Punde kidogo, Marwa akiwa bado yu kantini, akapokea ujumbe toka kwa Miranda.

'Ukifika home, nishtue!'

Akaujibu ujumbe huo kisha akarejesha simu mfukoni. Hata hakula. Hakuwa na hamu hiyo akitazama chakula alichomletea Jona hakikuguswa.

Alikuwa anawaza ni muda gani Jona atarejewa na fahamu apate kumpa chakula. Alikuwa radhi kungoja hapo mpaka usiku alimradi lengo lake litimie.

**

"Kaka, naweza nikatoa vyombo?" Sauti ilimshtua toka usingizini. Marwa akafikicha macho yake na kumtazama mhudumu, mwanamke mwembamba mweupe. Kisha akiwa na wenge lake la usingizi, akatazama mezani. Bado kulikuwa na chakula alichoagiza lisaa nyuma.

Akatikisa kichwa.

"Chukua tu, dada, hamna shida."

Mhudumu akakusanya chombo na kwenda nacho. Marwa alipotaka kugeuza shingo kumtazama mhudumu huyo ndipo alipogundua shingo yake ilikuwa inauma!

Alikuwa amelalia kiti kwa muda mrefu. Shingo ilikuwa inamvuta kana kwamba amevunjika.

Akiwa anahangaika nayo, mara akamwona afande Devi akiwa anaingia kantini. Akajikuta anataka kujua hali ya Jona. Lakini kabla hajafanya lolote lile, afande Devi akamwona mwanaume huyo, bila hiyana, akamjongea karibu.

"Bado upo?" Akaigiza kushangaa.

"Bado nipo, mkuu," Marwa akateta kinyonge akijitengenezea kitini. "Nitaenda wapi na sijampatia chakula ndugu yangu?"

Afande Devi akatikisa kichwa. Mara akanyoosha mkono wake kumuita mhudumu, upesi akaja hapo na kumwagiza amletee soda.

"Natamani sana kukusaidia ndugu yangu, sema nashindwa," alijieleza afande Devi. "Nakuonea huruma sana. Namwonea huruma pia na Jona, yupo kwenye shida kubwa sana kwakweli."

Marwa akainamisha kichwa chake chini. Akakizuia na mkono kutengeneza tama.

"Atateseka sana," akasema Marwa kwa masikitiko kisha akauliza: "Unaweza kumsaidia akapata dawa?"

"Dawa ya nini?" Afande Devi akauliza akipokea soda yake toka kwa mhudumu.

"Hamuoni anaumwa?" Marwa akastaajabu. Afande Devi akanywa kinywaji chake fundo moja alafu akatikisa kichwa.

"Ninavyokuambia siwezi kumsaidia unadhani nakutania?" Akaifunika soda yake na kizibo isijazwe inzi. "Kwanza Jona haumwi magonjwa ya hospitali. Shida ni moja tu. Akitaka kupata unafuu inabidi akiri kutenda lile tukio."

"Hata kama hajafanya!" Marwa akatahamaki.

"Ni kwa uhai wake lakini!" Afande Devi akamsabahi akikodoa macho. "Kufa na huku bado hajahusika ama kuishi kipi bora?" Akauliza Devi.

Marwa hakuwa na jibu, akakaa kimya. Devi akanywa mafundo kadhaa ya soda mpaka kuifikisha karibu na kikomo.

"Anyway, lete chakula hicho nitampatia. Wewe nenda kapumzike. Siku nzima upo hapa."

"Sure?" Marwa akahakiki.

"Yeah. Leta tu wala usijali," afande Devi akamtoa mashaka. Marwa akamkabidhi chakula.

"Nakuomba umpatie ndugu yangu. Nakuomba sana!" Marwa akasisitiza.

**

Jioni ya saa moja ...

'Nimefika nyumbani' Marwa alituma ujumbe kwa Miranda kama mwanamke huyo alivyomtaka.

Lakini kiuhalisia hakuwa bado amefika nyumbani bali karibia na maeneo ya nyumbani. Alikuwa amesimama dukani akinunua baadhi ya mahitaji yake, mojawapo likiwa hilo la vocha lililomwezesha kutuma ujumbe.

Muda si mrefu, Miranda akampigia simu. Akapokea na kuipachika sikioni.

"Ndio, nimefika ... kesho? Mida ya saa ngapi na wapi? Ooh! Unapafahamu? ... basi nakutumia ujumbe kukuelekeza ... sawa, n'tajitahidi!"

Simu ilipokata alimalizia kuchukua vitu vyake hapo dukani, mkate na majani ya chai, alafu akashika zake barabara kwendelea na safari.

Lakini kuna mtu alikuwa anamtazama!! Kuna mtu alikuwa anamfuatilia. Mwanaume huyu alikuwa amevalia kapelo nyeusi, shati jeusi na suruali ya jeans. Alikuwa ameweka mikono yake mfukoni.

Kila Marwa alipokuwa anasogea, akasogea naye na mpaka akahakikisha Marwa aingiapo. Kazi yake ikawa imekomea hapo.

**

'Nimeshapaona mkuu.' ujumbe ulitumwa toka kwenye simu ndogo aina ya Samsung.

'Safi, sasa ngoja mpaka ntakapokupa agizo' ujumbe ukaingia kwenye simu hiyo.

'Sawa' ujumbe ukajibiwa.

**

Kwa dirishani moshi wa sigara ulikuwa unafuka. Kama ungelikuwa kwa nje ungeweza dhani kwa ndani kuna kitu fulani kimeshika moto.

BC alikuwa anavuta sigara yake kubwa kwa fujo. Hufanya hivi akiwa na mawazo lukuki kichwani mwake. Pembeni alikuwa ameketi Miranda akipooza koo lake na kinywaji ghali, John Walker.

Kulikuwa kuna ukimya hapa. Kama vile shetani alikatiza. Kwa muda kidogo kila mmoja alikuwa akishughulisha mdomo wake.

"What if we kill the inspector?" (Vipi kama tukimuua inspekta?) Aliuliza BC akiwa amefunikwa na moshi wa sigara. Uso wake alikuwa ameugeuzia dirishani.

"No!' Miranda akatikisa kichwa. "You know what. Getting Jona out is our no-escape plan. Not only because Jona will save my ass, but will keep Sheng too obstracted to be comfortable. Without Jona, Sheng can even swallow us. We need him out, for me for us!" (Unajua nini. Kumtoa Jona ni mpango wetu usioepukika. Sio tu kwasababu Jona atanisaidia, lakini atamzuiza sana Sheng asiwe huru. Bila Jona, Sheng anaweza hata akatumeza. Tunamhitaji atoke, kwa ajili yangu, kwa ajili yetu!) Miranda alinguruma.

"But Jona will be police no more!" (Lakini Jona hatakuwa polisi tena!) BC akatahadhari.

"It doesn't matter!" (Haijalishi!) Miranda akatema cheche. "Jona will make Sheng pay for all he has gone through in whatever way!" (Jona atamfanya Sheng alipe kwa yote anayoyapitia kwa njia yoyote ile!)

Miranda akasafisha koo na kuongezea:

"This is the best chance to get Jona in our side!" (Hii ni nafasi yetu kubwa kumpata Jona kwenye upande wetu!)


**

Sent from my SM-J110F using JamiiForums mobile app
 
Steve kesho ungetupa offa ya sikukuu kaka, BTW ahsante kwa leo na kwa kila siku utapayo burudani
 
Back
Top Bottom