Anga la washenzi na Joana anaona kitu usiku

Anga la washenzi na Joana anaona kitu usiku

Mbona kama tumeachwa solemba? [emoji850][emoji850][emoji850][emoji24][emoji24][emoji24]
 
*ANGA LA WASHENZI -- 53*

*Simulizi za series*

ILIPOISHIA

"Kama pesa kwako si kitu. Unafanyiaje kazi maisha? Wafanya kazi kwa kuwa umezoea?"

Marwa hakujibu upesi. Alitulia kwanza. Jona hakuona haja ya kumshinikiza ajibu kwani uso wa mwanaume huyo ulimwonyesha jibu lipo karibuni. Ni vile anapanga namna ya kulitamka.

Marwa akashusha pumzi ndefu. Pasipo kumtazama Jona, akasema kwa sauti iliyotoka chini ya vungu la moyo wake.

"Output ya kazi yangu, ndiyo pumzi ya wazazi wangu."

Jona hakupata wasaa wa kuendelea kumdadisi, Panky akawasili. Sasa wakaanza kujadili kuhusu ile picha.

_Picha ya siri._

_Picha ya Bite inayotia rehani roho zao wote._

ENDELEA

Kama vile uonavyo watahiniwa wakiwa kwenye hall la mtihani, ndivyo ilivyokuwa hapa. Palikuwa tulivu, macho yote yakitazama kioo cha tarakilishi ya Marwa.

Marwa akaelezea kila anachokijua. Tangu alipopewa kazi hiyo na mpaka pale alipoikamilisha kwa Moderator wao. Akaeleza ni kwa namna gani kazi hiyo ilivyofanyika kwa siri, ustadi na mazingatio makubwa.

Kila 'detail' ilikuwa imepimwa kwa umbali wa sentimita za kuwiana. Na japokuwa hakuambiwa vitu vile vilimaanisha nini, alishatambua zitakuwa 'codes'. Na kwa wakati huo akatokea kuamini aidha ni codes za kufungulia tarakilishi tawala - yani ile 'inayomoderate' tarakilishi zote hizo ndani ya jengo.

Alipomaliza kuifanya kazi hiyo, akaikabidhi kwa moderator, lakini baada ya muda akiwa amesahau kabisa picha hiyo , Moderator akamrudishia akimwambia kuna mambo alitakiwa kurekebisha. Idadi ya mawimbi baharini!

"Kitu hichi kikanishangaza, si kwamba zilikuwa ni taarifa ndogo ndogo, lah! Bali kwa sasa aliponipatia alikuwa strict mara tatu ya awali akitazama kila nyendo za mkono wangu, macho yangu.

Nilipomaliza, akaniagiza nimrushie. Na hapo ndipo ikawa mwisho wa mimi kukutana na hiyo picha mpaka pale Panky alipoiibua na kunishtua."

"Unamfahamu Bite?" Jona akauliza.

"Bite? ... "Marwa akatengua macho kwa kufikiri. "Bite Mayanja?" Akauliza.

"Sijui jina lake la ubini, namjua kwa jina la Bite tu. Kuna mtu yeyote unayemfahamu, ama wamjua anaitwa Bite?"

Marwa akafikiri kwa dakika.

"Sidhani ... ila, ebu ngoja. Bitee? ... Bitee ... Bitee..." akameza lips zake akiendelea kuwazua. Punde akamuuliza Jona juu ya mwonekano wa mwanamke huyo, Bite. Jona akajipambanua kutumia kumbukumbu zake zote kuelezea. Hapa Marwa akapata kitu.

"Unamwongelea marehemu Bite?"

"Exactly! Atakuwa ndiye huyo. Unamjua?"

"Ndio ... ila tuseme kiasi chake ... namjua kiasi."

"Ulimjulia wapi?"

"Kazini. Bite alikuwa ni miongoni mwa wafanyakazi wachache niliowakuta. Hakuwa mwanamke muongeaji sana, wala mwepesi kumzoea. Kwa kipindi hicho alikuwa ndiye mwanamke pekee ndani ya chumba cha IT. Lakini hali hiyo haikudumu kwa muda mrefu, akaacha kazi!"

"Alikuambia ameacha? Au ulijuaje?"

"Najua tu aliacha kazi, hata kama hakuniambia. Sheng huwa hafuti mtu kazi, anafuta uhai. Unakumbuka nilivyokuambia Bite ni miongoni mwa wafanyakazi wachache niliowakuta? ... wenzake wote niliowakuta hapo, watatu kwa idadi, waliuawa."

"Umejuaje?"

"Natazama taarifa ya habari. Najua walitaka kuacha kazi, haswa baada ya Bite kufanya hivyo ila hawakufanikiwa."

"Na kwanini Bite akafanikiwa?"

"Akafanikiwa!" Marwa akastaajabu. Akatabasamu kisha akatikisa kichwa. "Bite alichofanikiwa ni kudumu kwa muda mrefu tu, tofauti na wenzake. Yeye aliweza kukaa miaka na miaka akiwa huru!"

"Lakini iliwezekaje hili?" Jona akauliza. Hapo Marwa hakuwa na majibu. Kila mtu akawa kana kwamba yupo hewani kutafuta tofali hili moja kumalizia nyumba.

Jona akatabasamu. Akatabasamu kwa upana zaidi. Na mara akacheka.

"Bite aliweza kudumu muda mrefu kwasababu ya hii picha," akajibu akionyeshea kidole kwenye kioo cha tarakilishi.

"Ni wazi Bite alikuwa anajua risk ya yeye kuacha kazi. Basi akaondoka na kitu cha thamani toka kwa Sheng. Kitu atakachokitumia kama dhamana ya uhai wake. Nacho ni hii picha!"

"Lakini mbona Sheng alimuua tu?!" Panky akauliza akistaajabu.

"Sheng alimmaliza baada ya kupata mbadala wa kile alichokuwa nacho Bite mkononi. Ukiachilia mbali bado Bite alikuwa na pandikizi la Sheng ndani ya kila shughuli aliyokuwa akiifanya. Na kwa akili tu ya kitoto, maana yake ni kwamba Sheng alikuwa anajiandaa kuzipokea shughuli hizi punde atakapomwondoa Bite duniani," Jona akadadavua.

Marwa akakunja usowe kwa kuchanganyikiwa. Akauliza:
"Umejuaje Sheng alipata mbadala wa picha aliyokuwa nayo Bite mpaka akaamua kumuua?"

Jona naye akamuuliza:
"Ilichukua muda gani kati ya wewe kubadili picha na Bite kuuawa?"

Marwa akajaribu kufikiri. Haraka akainamisha mgongo wake kutazama chini ya meza, kulikuwa kuna magazeti lukuki huko, akapekua pekua magazeti hayo na kuibuka na mojawapo.

Lilikuwa na taarifa ya mauaji ya Bite.

Akalisoma tarehe. Kisha akazama kwenye tarakilishi yake alipopekua mambo kwa muda wa dakika mbili, kisha akasema:
"Tofauti ya siku mbili tu!"

Jona akatabasam kwa mbali.

"Umeona enh?"

"Lakini," Panky akazuka. "Kama ingelikuwa ni rahisi hivyo, kubadili tu picha mchezo ukaisha, kwanini ilichukua muda mrefu Bite kuwa hai?"

"Na hapo ndipo tunaporudi pichani," Jona akamjibu. "Hizi zilizopo kwenye picha ni codes. Ni kitu kikubwa. Kuongeza tu mawimbi pichani, si tu kupendezesha mambo bali kumaanisha jambo. Jambo ambalo lilimchukua Sheng muda wote huo akichezewa sharubu na Bite!"

Sasa mambo yakaanza ku' make sense'. Kuhakiki zaidi mambo, Jona akatoa simu yake mfukoni na kutazama picha ya picha ile aliyoichora toka kwa Bite.

Kweli ilikuwa na upungufu wa idadi ya mawimbi ukiilinganisha na ile kopi ya Marwa! Upungufu wa mawimbi mawili tu! Lakini ungeliona hili endapo ungeamua kuua muda wako wa kutosha kuchunguza.

"Wamekuamini sana kukuachia hii kopi," Jona alisema akimtazama Marwa.

"Hawana hofu kuu nami," Marwa akajibu. "Maana wanajua sina janja kwao. Nikapofanya lolote lile, watakatisha dozi ya antidote kwa baba na mama yangu, nao watakufa ndani ya sekunde thelathini tu!"

Jona aliona ni namna gani Marwa anaumizwa na hilo jambo. Macho yake yalitamka namna gani anaumia kila akilikiri hilo. Hakutaka kumumiza zaidi, akakengeusha mawazo.

"Hii picha tukiikokotoa. Sheng atakuwa amejaa kiganjani."

"Hakika!" Panky akaliunga mkono hilo. Lakini kabla hawajaendelea kuumiza vichwa zaidi, Marwa akapendekeza wapate kifungua kinywa kwanza kwani tumbo limeanza kudai chake kwa fujo.

"Hli tumbo limetifuliwa na kuumiza kichwa," akasema Marwa akienenda jikoni. Pengine alikuwa sahihi kwani mara hii Jona hakumzuia.

Alihisi naye anahitaji kitu kujaza utupu wa tumbo lake.


***

Sent from my SM-J110F using JamiiForums mobile app
 
*ANGA LA WASHENZI --- 54*

*Simulizi za series*


ILIPOISHIA

Jona aliona ni namna gani Marwa anaumizwa na hilo jambo. Macho yake yalitamka namna gani anaumia kila akilikiri hilo. Hakutaka kumumiza zaidi, akakengeusha mawazo.

"Hii picha tukiikokotoa. Sheng atakuwa amejaa kiganjani."

"Hakika!" Panky akaliunga mkono hilo. Lakini kabla hawajaendelea kuumiza vichwa zaidi, Marwa akapendekeza wapate kifungua kinywa kwanza kwani tumbo limeanza kudai chake kwa fujo.

"Hli tumbo limetifuliwa na kuumiza kichwa," akasema Marwa akienenda jikoni. Pengine alikuwa sahihi kwani mara hii Jona hakumzuia.

Alihisi naye anahitaji kitu kujaza utupu wa tumbo lake.

ENDELEA

Chai na vitafunwa kadhaa vikiwa vimewekwa kwenye sinia ya plastiki, nadhifu jeupe lenye nakshi za maua maua, vikawasilishwa mezani. Vikafuatiwa na maji ya kunawa na ya kunywa pia. Marwa akawanawisha wageni wake mikono na kuwakaribisha.

"Umepika mwenyewe hivi?" Jona akauliza baada ya kung'ata kitafunwa kimoja na kukitafuna. Ladha ilikuwa tamu. Na zaidi, aliona ilikuwa ni fursa adhimu kwake kujua machache toka kwa Marwa.

"Hapana, sijapika mie ... siwezi kupika hivi!" Marwa akasema akitabasamu. "Si kwamba siwezi, hapana! Ningepika hapa mngejing'ata lakini sina huo muda. Nabanwa sana na kazi."

"Hakuna wa kukusaidia?" Jona akaendelea kudadisi akitafuna.

"Atolee wapi?" Panky akawahi kumjibu, kisha akacheka kidogo. "Unavyomuona huyu alivyo ndiyo yupo hivyo hivyo!"

Kukawa kimya kidogo. Wote walikuwa wametabasamu midomo yao ikicheza kwa kutafuna.

"Nimechagua haya maisha," Marwa akavunja barafu la ukimya. "Ni ngumu, najua ... lakini sina namna."

Jona akamtazama kwa macho ya maulizo pasipo kusema kitu. Alitumai Marwa hataishia hapo. Marwa akanywa mafundo mawili ya chai na kufuta mdomo wake kwa mgongo wa kiganja.

"Kazi yangu ya hatari sana," Marwa akasema kabla hajatia kitafunwa kingine mdomoni. "Kumpata mwanamke siyo shida. Ila nitaweka maisha yake rehani, na huenda akatumika, kama ilivyo kwa wazazi wangu, kunifanya niwe mdhaifu."

Wote wakaunga mkono hoja yake. Wakaendelea kutafuna kwa muda kidogo kabla Jona hajairudisha tena mada mezani.

"Lakini unajitahidi... indeed unajitahidi sana kukeep nyumba vizuri."

"Kiasi chake!" Marwa akapokea pongezi kwa aina yake. "Nikipatapata muda unashika hiki na kile, hapa na pale, nidumishe rangi za vitu, angalau hata mgeni akija asipate picha mbaya ya kusimulia."

Maongezi hayo yakawasha taa kichwani mwa Jona. Kuna kitu aliwaza. Kuna kitu alikipata. Alitazama sinia ile iliyobeba vitafunwa, ilikuwa ni nyeupe peh.

Kudumisha rangi ...

Rangi nyeupe ...

Rangi nyeupe huonyesha usafi.

Akilini alikuwa anaonganisha mambo ...

Ghafla, akalipuka na kuuliza:
"Vipi kama rangi za ile picha zikawa ndiyo codes zenyewe?"

"Kusema kwamba?" Panky akatahamaki. Jona akamtazama kwa macho ya uhakika.

"Kusema kwamba, rangi za vile vitu vilivyopo kwenye picha ndiyo zikawa codes!"

Hawakutaka kupinga hoja ya Jona kabla hajaithibitisha. Wakamaliza kula na kuchangia maoni yao kwenye hilo wakiwa wanatazama picha ile kwa umakini.

Lakini wakagundua walikuwa ni wadhaifu kwenye mambo ya rangi. Lakini kabla hawajakata tamaa, Marwa akataka watumie 'Techonological interpretation of colors' - yaani wazichambua zile rangi kwa kuzihusanisha na teknolojia kwani kazi hiyo ilitengenezwa na kitengo cha teknolojia tarakilishi ndani ya mtandao wa Sheng.

Basi, Marwa akafungua 'application' yake ya siri aliyoitengeneza kwa mikono yake mwenyewe, inaitwa CODAQ. Akaandika namba za siri kwa vidole vyake vyepesi juu ya keyboard. Mara zikaja namba namba nyingi. Akabofya bofya keyboard kwa haraka mno usijue hata aliandika nini, na mara kioo kikawa cheupe.

"Ni nini hii?" Jona akauliza.

"Ni app yangu ya kutengeneza Techonological logos kwa ajili ya techonological gadgets."

"Kwani wataka kutengeneza logo?"

Marwa akatabasamu. "Hapana. Nataka ku 're-assess' kila rangi na maana yake kwenye techonology field."

Akabonya bonya keyboard kwa wepesi. Jona hakusumbuka tena kutazama nini Marwa anabofya kwani macho yake hayakuweza kwenda sambamba na kasi ile.

"Unajua kila rangi ina maana yake kwenye logo ..." Alisema Marwa akiwa anaendelea kufanya mambo yake. Hakuna mtu mwingine aliyeongea, wote walikuwa wanangojea aweke mambo bayana.

Punde,

"All right!" Akasema Marwaa akitabasamu. Alikuwa amefika mahali alipokuwa anapahitaji, akashirikisha wenzake kwa kile alichokuwa nacho.

Mosi, kwenye ile picha kuna rangi ya blue - ambayo ndiyo ilitumika kupambia bahari. Pili, kuna rangi ya kijani kilichoshamiri kisiwani. Tatu, kuna rangi nyekundu na nyeupe iliyotumika kupambia ndege warukao juu.

Hizo ndo zilikuwa rangi 'dominative' pichani. Sasa wakazianisha kimaana.

- Blue = security/strength/dependable. (Ulinzi/ nguvu/cha kutegemewa)

- Kijani = life/growth/freshness. (Uhai/ukuaji/hali nzuri)

- Nyekundu = communication/energetic. (Mawasiliano/chenye nguvu)

- Nyeupe = purity/reliable (kisafi ama kitakatifu/kuaminika.)

Kwahiyo basi kwa maana hiyo, kisiwa kile (kijani) kilikuwa kinamaanisha uhai wa Sheng, ukuaji wa Sheng, hali nzuri ya Sheng. Lakini hicho kisiwa kikiwa kimezingirwa na blue (maji), kumaanisha ulinzi, nguvu na kutegemewa.

Mpaka hapo, maana yake ni kwamba hakuna ukuaji wala uhai wa Sheng kama hamna ulinzi na nguvu kuzunguka uhai huo. Na kwa tafsiri ya picha, bahari ama rangi blue ndiyo iliyochukua sehemu kubwa.

Na wale ndege waliopo juu ya kisiwa, wakimaansha utakatifu wa mawasiliano kama moja ya nguzo ya kupendezesha mandhari!

Nusu ya kazi ikawa imeisha. Sasa mkia uliobakia ukawa ni kujua maana ya idadi ya kila kilichomo ndani ya picha. Kwanini ndege watano? Mawimbi manne? Kwa maana kama yasingekuwa na maana basi Marwa asingepewa kazi ya kuyarudia kuyaongeza.

"Nguvu ya bahari ni mawimbi yake, sio?" Jona akauliza. Asisubiri majibu akaendelea kuteta: "basi haya mawimbi manne yaliyopo kwenye bahari hii, ndiyo nguvu ya ulinzi wa Sheng. Aidha ni watu ama vitengo."

"Na basi kama ni hivyo," Marwa akadakia lain. "Nguvu ya mawasiliano ya Sheng ni watu ama vitengo vitano pia!"

***

Saa kumi na mbili jioni, Whitesand Hotel.

"Nimefurahi sana sana!" Sauti ya kike ya Miranda ilivuma wakati mwanamke huyo akiagana na mheshimiwa Boka kwa kumpatia kumbatio la joto na busu mubashara shavuni.

"Usijali, nimefanya yote haya kwasababu nakupenda. Nimedhamiria haswa kuwa nawe," Mheshimiwa Boka akajivuna kabla hajatoka zake eneo hilo na kujipaki ndani ya VX yake nyeusi. Akahepa.

Miranda akarudi ndani ya hotel akiwa anatuma ujumbe simuni. Alipoketi, ndani ya muda mfupi BC akatokea nyuma yake na kuketi. Mwanaume huyo alikuwa anatabasamu usoni.

Akampongeza Miranda kwa kukamilisha kazi, kisha akamsikiliza amwambie cha ziada.

"From next month, he will be on trip in South Africa." (Kuanzia mwezi ujao, atakuwa safarini Afrika ya kusini) Miranda akajipambanua. BC akatoa macho ya mshangao.

"What a coincidence!" (Bahati iliyoje!) Akamsihi Miranda ahakikishe hiyo safari anakwenda na Boka kwani kuna baadhi ya mzigo wao utatua huko, na atakuwa na jukumu la kuuleta hapa nchini.

Kidogo Miranda akaonyesha hofu.

"Never mind, it's just small one. It will never get you in trouble," (Usijali, ni mdogo tu. Kamwe hauwezi kukuingiza matatizoni,) BC akampoza akiwa anamkanda bega kwa kiganja chake kipana.

Hawakukaa hapo sana, wakatimka zao.

***

Wivu ndiyo mapenzi. Lakini pia wivu ni kidonda, ukishiriki utakonda. Walisema waswahili. Na hakika hawakukosea kwa neno hilo, ulikuwa ni ukweli mtupu ulio uchi.

Punde baada ya mumewe kuingia bafuni, akaiteka simu ya mumewe na kuanza kuiperuzi. Boka mule bafuni asiwe na hofu yoyote, alikuwa anaimba huku akiusugua mwili wake mpana mweusi kwa ujazo wa sabuni.

Alikuwa anabadili nyimbo hii kwa hii. Wakati mwingine akiwa anagugumia kutengeneza 'beat'. Alikuwa ana furaha moyoni, ungelijua kwa kumtazama tu. Kama mwili wake ungelikuwa unamruhusu kucheza, basi angelijimwayamwaya.

Lakini laiti angelijua mkewe anaperuzi simuye, nakuhakikishia asingekumbuka hata taulo. Angekimbia upesi kwenda kumpokonya.

Alipomaliza kuoga, akatoka bafuni akiwa amejifunga taulo jeupe kiunoni. Bado akiwa anaimba, akaketi kitandani na kumtazama mkewe. Alikuwa ameigiza kulala.

Akajaribu kumuita mara mbili kwa sauti ya chini. Mama hakuitika. Basi asimsumbue, akaenda zake kabatini na kuteka nguo ya ndani apate kulala.

Bila shaka akijua usiku umeenda salama. Lakini kumbe kifuani mwa mkewe kukiwa kuna vita hatari. Vita inayomtafuna zaidi ya kirusi.

Akazima taa na kisha kujimwaga kwenye kitanda kipana, maridadi kabisa, apate kulala. Kwa 'kajoto' kalichokuwepo, hakuhitaki kujifunika shuka.

Alikuwa amechoka mno kwa 'shughuli pevu' aliyopewa na Miranda. Hakudumu macho kwa muda mrefu, akapotelea usingizini akiwa anakumbuka raha alizopewa.

Raha za karne.

Lakini mkewe hakuwa amelala. Muda huo alikuwa anatiririsha machozi bujibuji. Alikuwa akisaga meno, kichwa kinamuwaka moto. Likapita lisaa limoja. Akashindwa kuvumilia.

Akanyanyuka na kutoka ndani ya chumba. Baada ya dakika tatu, akarejea akiwa ameshikilia kisu mkononi.

***

Sent from my SM-J110F using JamiiForums mobile app
 
[emoji124][emoji124][emoji124][emoji124][emoji91][emoji91][emoji91][emoji91][emoji91][emoji125][emoji125][emoji125][emoji125][emoji125][emoji125][emoji125][emoji125][emoji125][emoji125]
 
Siku nyingine steve uwe unatushushia hata tatu au nne maana haziishi utamu hizi kitu
 
Back
Top Bottom