Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
nitafute miee[emoji1] [emoji12] [emoji2]Steve nakutafuta
Ijumaa tena
[emoji13] [emoji13] [emoji13] [emoji13] [emoji23] [emoji23] [emoji23]nitafute miee[emoji1] [emoji12] [emoji2]
Shabaash, patamu apo.*ANGA LA WASHENZI – 30*
*Simulizi za series*
ILIPOISHIA
Panky akaongezea ya kwamba pindi unapoingia ndani ya mfumo wa Sheng’, familia yako yote anakuwa anaijua. Watu wako wa karibu na marafiki zako. Ni labda ajue umekufa, na si hai akakukosa!
“Watu kadhaa walishawahi kutoroka, wengine wakitaka kuacha kazi kwa hiyari. Hakuna aliyebakiziwa uhai hata mmoja! Kwa Sheng’ kuna kuingia tu, mlango wa kutokea haupo. Na utakapoulazimisha kuujenga ukutani, basi utalipia gharama zake.”
ENDELEA
Jona hakuona haja ya kuendelea kumweka Panky mule stoo kwa ushirikiano wake alioutoa. Akamfungua kamba na kwenda naye ndani alipomkabidhia nguo kavu na nadhifu. Wakaendelea kuongea kwa muda kidogo Jona akipeleleza baadhi ya taarifa.
Panky pasipo kumficha akampatia Jona zile azijuazo. Namna gani alikuwa anatenda na kumsaidia Sheng’ kukamata Tanzania nzima, Afriika Mashariki, na hatimaye Afrika nzima. Namna gani wanavyokusanya data toka sehemu nyeti mbali mbali na kumkabidhi Sheng’ kwa ajili ya kazi zake binafsi atakazogawia vitengo vingine.
Kwa maelezo hayo, Jona akapata uelewa namna gani Panky alivyokuwa na uwezo wa kucheza na tarakilishi kwenye kila kona. Namna gani ujuzi wake ulivyokuwa mkubwa kwenye kunyambulisha taarifa, kutengeneza na kuzipoteza.
“Kama kuna taarifa ama data hatari kwa Sheng’, na taarifa hiyo ipo kwenye mashine ama tarakilishi ya mtu yeyote yule, basi ni jukumu letu kuipoteza. Tunatengeneza virusi na kuvituma kwa mtandao kama mashine ipo mbali. Virusi hao watakula mafaili yote watakayokuta humo na kiacha mashine tupu!”
Kitengo hicho hicho cha Space Button ndicho kinahusika na ukusanyaji wa taarifa popote pale ilipo kwa njia za kisasa aidha mwenye taarifa anataka ama hataki. Kama kuna mkataba ambao Sheng’ anautaka, na upo mtandaoni ama kwenye tarakilishi ya mhusika yeyote ule. Wakimtambua wataupata!
“Sheng’ ana mikataba yote ya ujenzi, madini, ardhi na kila kitu. Ana taarifa za mawaziri, na wabunge. Ana taarifa za taasisi kubwa kubwa, yote hayo yakiwezekana kwa kupitia kitengo hichi cha Space Button.”
Pia kwa kupitia mkono wa kitengo hicho, huwa wanabambikizia watu kesi kwa kuwawekea vitu ndani ya tarakilishi zao ama kwenye tovuti zao. Kutengeneza ‘application’ mbalimbali kwa ajili ya kufanyia kazi za Sheng’.
Jona akamuuliza kama kuna uwezekano wowote wa kupata data na taarifa zilizopo kwenye ‘vault’ ya Sheng’. Panky akamwambia kitu hicho hakiwezekani na hakiwezi kufanywa na mhsika yeyote yule wa Space Button kwasababu imewekwa katika usala sana.
“Kufungua Vault ya Sheng’ utahitaji alama za vidole gumba vya wahusika wote wa Space Button, na utahitaji code nne ambazo ni Sheng’ peke yake anazifahamu.”
Maelezo hayo yakamvutia sana Jona. Kichwani kwake haraka akapata wazo la kumtumia Panky katika kazi zake. Alitafakari ni kwa namna gani ujuzi wa mwanaume huyo utakavyoweza kukamilisha kazi zake kwa ufanisi zaidi.
Lakini akahofia, bado Panky hakuwa mtu wa kumwamini kiasi hicho. Bado alihitaji kumpekua na kumsoma zaidi. Na pia kama ataridhia kufanya naye kazi, maana ni jambo la hiari, si lazima.
“Unaona picha hii?” Jona alimwonyeshea Panky picha ile aliyochora kwa ajili ya Bite. Akamwambia hiyo ndiyo sababu anatafutwa na uhai wake unawindwa. Je ana ufahamu nayo?
Panky akaiteka picha hiyo kwa mikono yake na kuitazama kwa makini. Kuna jambo alikuwa analifikiria, wapi aliona picha ile. Kumbukumbu ikamjia, alishawahi iona siku moja kule ofisini kwao, mwenzake akiwa anaishughulikia.
“Sijui ina maanisha nini lakini nakumbuka siku moja niliwahi kuiona picha hii ofisini, na ndiyo ilikuwa inatengenezwa. Sikuwahi kuifuatilia wala kuiona tena.”
Jona akamuuliza kama anamfaham mtu huyo aliyekuwa anaitengeneza, Panky akasema anamfahamu mpaka na makazi yake. Jona akapanga waende kumtafuta mtu huyo ambaye alitambulishwa kwa jina la Marwa.
Lakini kabla ya kwenda huko inabidi akakutane kwanza na yule mwanaume ambaye Nade anataka kwenda kumdhibiti kwa kuhusiana na Miriam – mke wa mheshimiwa. Kazi hiyo ilikuwa ni ya kufanywa kesho yake kwenye majira ya mchana mpevu.
***
Saa tatu asubuhi…
“Huwezi amini yule mzee ameshammaliza yule jamaa!” Alisema Kinoo aliyekuwa amebebelea kikombe cheupe cha chai. Akiwa amekaa na Miranda ambaye mkononi alikuwa ameshikilia simu yake kubwa akiperuzi.
Ni ndani ya nyumba ya Miranda, Kinoo akiwa amewasili hapo muda si mwingi. Miranda alikuwa amevalia dera, nywele zake zikifungashwa na kiremba cheusi.
Kinoo alikwa hapo kumhabarisha juu ya kifo cha Mudy, mwanaume ambaye amewapatia nyaraka zile za kampuni ya umeme wa jua.
Miranda akashangazwa na taarifa hizo. Kifo cha Mudy kilikuwa ni ishara kwamba na wao, ambao wanamiliki nyaraka hizo, wanaweza wakawa ndiyo ‘tageti’ inayofuatia.
“Ni kweli,” Kinoo akamwambia. “Inabidi tuwe makini, la sivyo tutaenda na maji.”
Miranda akasonya na kubinua mdomo. Akamtazama Kinoo kwa macho ya bumbuwazi na kumwambia hawana haja ya kuishi kama digidigi sababu ya Brokoli. Kama ameanzisha vita, basi hawana budi kupambana kabla haijatoka nje ya mikono yao.
“Tuchunge ngamia huyu asije akawa mkubwa kuliko banda. Endapo tukimwacha Brokoli akaendeleza saga hili, linaweza kuwaamsha majabali yaliyolala. Akuanzae mmalize.”
Kinoo akasita kiaina. Lakini Miranda hakuona haja yay eye kufanya hivyo kwani aliamini hayo maamuzi ya yeye kumuua Mudy yametoka mikononi mwake. Na kama amemuua Mudy, sababu ya nyaraka, hatakomea hapo.
Je wapo radhi kuuawa?
“Lakini sifahamu makazi yake,” akasema Kinoo. Miranda akamuuliza:
“Umetafuta ukakosa? Mbona unakuwa kama mgeni kazini.”
Kinoo akakumbuka numbani anaishi na Sarah, pengine atakuwa anafahamu. Akaacha kuulizwa maswali ya ‘kijinga’ kama asemavyo Miranda.
“Kwahiyo kwa muda gani utakuwa umemaliza hiyo kazi?” Miranda akauliza akimtazama Kinoo na macho yake aliyoyatoa kwenye kioo cha simu.
“Nahitaji siku moja tu,” akajibu Kinoo na mjadala huo ukaisha. Miranda akamwambia Kinoo kwamba baadae jioni ana miadi ya kwenda kukutana na mke wa Boka nyumbani kwake Upanga kwa ajili ya majadiliano.
Hivyo atamtaka ampeleke huko kama atakuwa na muda. Ajabu Kinoo akakataa, akimwambia ya kwamba ana kazi ya kufanya usiku. Miranda akataka kjua kazi hiyo.
“Tangu lini ukawa na kazi usiku nisijue?”
Kinoo akatabasamu kwanza kabla hajamtaarifu Miranda ya kwamba anaishi na Sarah – aliyekuwa mfanyakazi wa Bite kwasababu za usalama. Miranda akastaajabu. Alihofia juu ya usalama wao.
“Vipi kama huyo binti akakuchota taarifa?”
Kinoo akamtoa hofu. Anajua mwanamke huyo hatakuwa na lolote kmdhuru. Miranda akamtaka awe makini na macho muda wote.
“Najua umewahi kumpa hifadhi kwasababu ni mwanamke. Huna lolote!”
Kinoo akatabasamu na kukanusha pasipo kumaanisha.
***
Saa nane mchana…
Gari aina ya Harrier rangi ya fedha inapaki kwenye uwanja wa hoteli, na baada ya punde Nade anashuka. Amevalia miwani meupe ya urembo. Koti dogo jeusi linalobana mwili wake. Suruali ya jeans na raba nyeupe.
Mkono wake wa kulia umebebelea simu ya Miriam. Na kama ukimtazama vizuri nyuma ya koti lake, utaona amefichama bunduki ndogo. Ila mpaka utazame kwa makini! Kitu ambacho ni kigmu kidogo kutokana na mwanamke huyo anavyovutia, utatazama vingine.
Akatazama kushoto na kulia. Akaridhia kila kitu kipo sawa. Akanyookea mapokezi, ambapo aliteta kidogo kabla ya kuelekezwa kwenda chumba namba fulani ambacho ndipo mtu anayemhitaji yupo.
Akabisha hodi.
Hakukuwa na majibu. Akabisha tena na tena, pasipo majibu. Akatazama simu kwa malengo ya kupiga kumtaarifu ‘mwenyeji’ kuwa ameshafika, yupo nje. Inabidi amfungulie.
Kwenye simu akakuta ujumbe. Kwasababu simu ilikuwa ‘silent’ hakujua ujumbe umeingia saa ngapi. Ilikuwa ni kama dakika kumi na tano zilizopita. Ina maana akiwa njiani kuja.
Na ujumbe huu ulikuwa umetokea kwa ‘My Heart Pale’, yaani yule mwanaume mtuhumiwa wa mahusiano na Miriam.
‘Jipangeni upya. Sipatikani kwa wepesi kiasi hicho. Mnapolala ndipo mimi naamkia.’
Shabash! Amejuaje? Nade akajiuliza. Akatazama kushoto na kulia kana kwamba labda mtu huyo anamtazama. Hakuona mtu. Akatoka eneo hilo na kwenda mapokezi kuulizia.
“Sijui, labda kweli kaondoka maana mie nimeingia zamu muda si mrefu,” alijibu mdada wa mapokezi. Nade akasonya. Itakuwa mwanaume huyo amegutuka na sauti yake, akawaza.
Lakini mwanaume huyo akampatia mawazo Nade. Atakuwa ni mtu mwerevu, ama mwenye uzoefu na mambo haya. Anajihusisha na nini?
Akatoka nje ya hoteli akiendelea kutazamatazama na kuwaza kichwani. Akafungua gari na kuzama ndani. Lakini kabla hajawasha chombo, akahisi kitu cha baridi shingoni, na amri:
“Tulia hivyo hivyo!"
Ni nani huyo?
Mzee jus cope with the timetable. Unachokiona hicho kipande costs a lot in writing in case of time. Nina kazi zingine nafanya. Si kwamba naamka naandika kisha nalala. Unachoona natuma ndicho naandika.Hii story kali lkn inakataa stimu mf apa unaeka vipande viwili tu alaf tena mpaka ijumaa au bana stiv hauna story zingine kali ivi tena unaogopa hii ikiisha ndo khari yako pia imeisha? Acha izo bana mkuu tupe story iyo bana
We vipiiiiiiShabaash, patamu apo.
Fantastic slang.
Ni katika kunogewa tu shunie, nawafuatilia kwa taratibu, samahann kwa kuwarudisha nyuma kifikira.We vipiiiiii
Acha upuziShabaash, patamu apo.
Fantastic slang.
Livafan umezinguaShabaash, patamu apo.
Fantastic slang.