Anga la washenzi na Joana anaona kitu usiku

Anga la washenzi na Joana anaona kitu usiku

Mzee jus cope with the timetable. Unachokiona hicho kipande costs a lot in writing in case of time. Nina kazi zingine nafanya. Si kwamba naamka naandika kisha nalala. Unachoona natuma ndicho naandika.

Sent from my SM-J110F using JamiiForums mobile app
Respect kwako mkuu, byt watu kama hawa wasamehe na kama amesa story hii tangu mwanzo maelezo kama haya ameshayasoma ila tu kuna muda mtu anahisi ana hati miliki ya hii stori na wewe umeihifadhi tu anapoitaka umpatie wakati anaotaka yeye. TUWE WAELEWA JAMANI.
 
Respect kwako mkuu, byt watu kama hawa wasamehe na kama amesa story hii tangu mwanzo maelezo kama haya ameshayasoma ila tu kuna muda mtu anahisi ana hati miliki ya hii stori na wewe umeihifadhi tu anapoitaka umpatie wakati anaotaka yeye. TUWE WAELEWA JAMANI.
Ahsante kwa uelewa Mkuu.

Sent from my SM-J110F using JamiiForums mobile app
 
ijumaa leo, napata vipande viwili zen maisha yanakua muruwaaa..
 
*ANGA LA WASHENZI (MSIMU WA PILI) -- 10*

*Simulizi za series*

ILIPOISHIA

"Sikujua," afande Devi akajitetea. "Nilimkuta hapo nje kwa muda mrefu. Nikamuuliza akasema haja yake. Nikaona si vibaya ku-"

"Usirudie tena!" Massawe akamkatiza. "Sawa?"

"Sawa afande!"

ENDELEA

Baada ya muda kidogo koplo Massawe akaondoka zake na kumwacha afande Devi peke yake. Devi asipoteze muda akaenda kumwona Jona rumande na kumwonya kuhusu watu wanaomtembelea.

"Hawataki upatiwe chakula, Jona. Utakapoona nimewazuia wageni wako jua nimekosa namna ya kuwaruhusu."

Jona akafadhaishwa sana na hili. Kwanini wanamfanyia hivyo? Nini lilikuwa kosa lake ndani ya jeshi? - uweledi wake?

"Usijali," afande Devi akamtoa mashaka. "Nitakuwa nakusaidia kadiri ya uwezo wangu. Nitakapokuwa napata muda ntakuwa nakupenyezea hata kidogo. Lakini kwa siri sana."

"Ahsante sana Devi," Jona akachonga. "Ila nakuomba uachane na hivi vitu. Wewe bado kijana mdogo na ndiyo kwanza umeanza kazi mwaka huu. Hili linaweza kukugharimu."

"Wala usijali, Jona," Devi akamtoa mashaka. "Wewe ni miongoni mwa watu wachache sana walionipokea vema hapa kituoni wakaniheshimu japokuwa ni mdogo kwao kiumri na kicheo. Hustahili haya. Naamini hauna roho hiyo. Mimi nitakusaidia kadiri ya uwezo wangu."

Afande Devi hakukaa sana hapo, akaenda zake kurudi anapotakiwa kuwapo. Alihofia koplo Massawe anaweza akarudi asimkute ikawa taabu.

**

Kamanda mkuu akiwa anaongozana na maaskari wengine wawili, mmoja akiwa amevalia kiraia, wakakomea langoni mwa rumande ya Jona. Kamanda akamtazama Jona kwa jicho la huruma kisha akadaka vyuma vya lango.

Jona alikuwa amekaa mbali ukutani.

Kamanda akatikisa kichwa kwa masikitiko. Kwa ishara, akamtaka mwanaume Jona ajongee karibu naye. Jona akatii. Akamsogelea mkuu wake huyo na kumtazama machoni.

"Jona," Kamanda akaita. "Kwanini umekubali kuteseka kiasi hiki? Fanya yaishe. Niruhusu nikusaidie. Haustahili kabisa kuwapo humu ndani."

Jona akamtazama Kamanda kwa sekunde kadhaa kisha akamjibu akiwa anang'ata meno.

"Anayestahili kuwepo humu ndani ni wewe pamoja na wenzako. Nitakapofanikiwa kutoka humu, basi jua ni wewe ndiye utakayeingia."

Kamanda mkuu akatabasamu.

"Shida yako ipo hapo, Jona. Unashupaza sana shingo. Unajua kisa cha chui na chungu? ... chui alizamia kijijini kwa watu akiwa anatafuta chakula kwa ajili ya wanae. Hakutaka kumla mtu kabisa bali apekue majikoni aone kama atapata chochote kitu.

Huko akafanikiwa kusikia harufu nzuri kabisa ya chakula toka kwenye chungu kidogo. Kuonja ... alah! Kilikuwa kitamu sana. Akaona kinafaa kupelekea watoto wake porini.

Lakini si bahati, chui akazamisha kichwa chake ndani ya chungu hicho hata akashindwa kukitoa. Akahangaika huku na huko kujinasua asifanikiwe mpaka wanakijiji wakamsikia. Wakajaa kumzunguka.

Walitaka sana kumsaidia, lakini silka ya chui iliwaogopesha kufanya hivyo. Je, Kucha zake zingewaacha salama? Walihofia. Na je wakishatoa hiko chungu kichwani, meno yake hayatawararua?"

Kamanda akaweka kituo. Akameza mate na kumwambia Jona.

"Badili hulka yako, uruhusu kusaidiwa. Kushupaza kwako shingo hakutakupelekea popote zaidi ya shimo la tewa."

Jona akasaga meno.

"Kama ungelibadili hulka yako kwanza, nisingelikuwepo humu ndani," akasema kwa kujiamini, kisha akaita, "Kamanda, kwa makusudi ulitengeneza kidonda kwasababu una dawa mkononi Sawa dawa yako yaweza kuponya lakini vipi maumivu niliyoyapata? Na je kovu utakaloniachia?"

Akahitimisha.

"Silambi mkono unaoniadhibu. Tena pasipo na hatia. Si kwamba ni kiburi, la hasha! Bali itanifanya niwe na hatia. Kamanda, acha nitapambana mpaka tone la mwisho."

Kamanda mkuu akabinua mdomo wake kisha akamtazama mmoja wa watu alioongozana nao kuja hapo, yule aliyevalia kiraia. Akamuuliza:

"Mmempa chakula enh?"

"Hapana, mkuu. Hajala," mwanaume huyo akajitetea akitikisa kichwa.

Kamanda akamtazama Jona kisha akarudisha macho yake kwa yule mwanaume aliyemuuliza. Akampatia maagizo.

"Hakikisha hali kwa siku zote anazokaa humu ndani!"

"Ndio, mkuu!" Akajibu mwanaume huyu kwa ukakamavu.

**

Asubuhi ...

Mlango ulipofunguka, alitoka inspekta Geof akiwa amebebelea notebook yake mkononi. Nyuma yake alikuwapo mwanadada Miranda akimsindikiza.

Wakasimama kibarazani, Inspekta akampatia Miranda mkono wa kheri kisha akamkumbusha hatakiwi kuondoka nje ya mji mpaka pale upelelezi utakapokamilika, na kesho atakuja tena kumwona.

Aliposema hayo, inspekta akaondoka zake Miranda akimtazama mpaka anatoka nje ya geti. Akarudi sebuleni na kuketi akikuna kichwa chake kwa mawazo. Nywele zilikuwa timtim, na mwili wake ndani ya dira angavu ulikuwa unahangaika kuweka kila mkao.

Aliwaza. Hakuona kama una upenyo wa kuchomoka katika kesi hii. Kama upo basi ni kama ule wa tundu la sindano. Mambo yamekuwa magumu zaidi. Kwa dalili za wazi, inspekta alionekana kudhamiria kumtia ndani.

Mawazo yake yakaenda mbali. Akamuwazia Jona. Kwanini kesi hii amepewa mtu mwingine mbali na yeye? Aliamini Jona ni mwerevu kung'amua muuaji na si huyu Geof ambaye macho yake yanakomea juu ya zulia.

Akawaza afanyaje? Mawazo yake yote yakamuelekezea msaada wa pekee ni Jona. Akanyanyua simu na kupiga. Hakuwa anafahamu kuwa Jona yupo nyuma ya vyuma.

Simu ikaita pasipo mafanikio. Akaamua kumpigia Kinoo amshirikishe habari zake kwa mara ya kwanza. Hata akisikia amekamatwa basi asije akastaajabu na aje kumtembelea rumande.

Simu ikaita mara mbili kabla ya kupokelewa. Kulikuwa na makelele kuonyesha Kinoo alikuwa mjini kwenye pilika za magari na watu. Miranda asijali hilo, akatimiza adhma yake ya kumhabarisha Kinoo.

"Sidhani kama kesho akija ataniachia huru. Maswali yake yote nilikuwa nababaika kujibu. Najiona kabisa nikitenga shingo kwa mchinjaji."

"Sasa tunafanyaje?" Kinoo akauliza.

"Tumtafute Jona. Naamini anaweza akanisaidia!"

"Jona? Yule polisi?"

"Ndio! Alikuwa ndiye mpelelezi wa hii kesi, ila wamembadilisha!"

"Miranda, kwani hujasikia habari za Jona?"

"Zipi?

Kinoo akamhabarisha Miranda kwamba Jona amekamatwa anatuhumiwa kumuua RPC hivyo asitegemee kumsikia tena.

Miranda akachanganyikiwa. Tumbo likamvuruga. Alikata simu akaiweka kando na kulaza kichwa chake kwenye kiti.

Jona amekamatwa? Jona amemuua RPC? Maswali haya yakazunguka kichwani. Akajikuta anatikisa kichwa chake kama mwehu.

Hapana.

Hakuamini hata chembe.

Akanyanyuka upesi na kwenda ndani.

**

"Jona, naamini hujaua," Miranda alisema kwa sauti ya chini akimtazama Jona kwa macho ya huruma. "You have been framed. Na ubaya si tu inakuumiza wewe bali hata na sisi. I need you out. Things are not the same."

Macho ya Miranda yalibadilika rangi na kuwa mekundu.

Jona alikuwa amesimama akishikilia nondo kwa mkono wake wa kuume akitazama chini. Sijui alikuwa anawaza nini. Ila ungemtazama ungeona moyo wake unaungua. Kifuani alikuwa ana moto mkali.

Alikuwa anasikia maumivu aliyoyaonyesha kwa kung'ata meno yake.

"Jona, Miranda akaita. "We have to do something. Usikae ukaridhika na hii hali. Najua you are innocent."

"Nitafanya nini Miranda nikiwa humu rumande nimebanwa na vyuma?" Jona akauliza. Macho yake yalikuwa mekundu. "Nimedhamiria kweli kufanya kitu, lakini nafanyaje na nipo humu ndani?"

Kabla Miranda hajasema kitu, afande Devi aliwasili eneoni akiwa amebebelea chakula kwenye mfuko. Akamkabidhi Jona.

Akamtazama machoni.

Akamtazama na Miranda kisha akarudisha macho yake kwa Jona.

"Kula upesi!" Akasema kwa kunong'oneza kisha akaenda zake.

**

"Umempatia?" lilikuwa swali la kwanza kutoka kwa koplo Massawe.

"Ndio, nimempa," akajibu afande Devi. Uso wake alikuwa ameukunja. Macho yake yalionyesha mawazo. Aliketi akafungua daftari kubwa la hapo kaunta akaigiza kulitazama ila kiuhalisia alikuwa mbali sana kimawazo.

Ndani ya muda mfupi, Miranda akafika hapo kaunta akiwa anatembea kwa madaha. Mwanamke huyo aka 'sign out' na kuwaaga.

Massawe akanyanyua simu na kupiga.

"Ndio, ameshakula kile chakula ... sawa, mkuu."

***
 
*ANGA LA WASHENZI (MSIMU WA PILI) -- 11*

*Simulizi za series*


ILIPOISHIA

Ndani ya muda mfupi, Miranda akafika hapo kaunta akiwa anatembea kwa madaha. Mwanamke huyo aka 'sign out' na kuwaaga.

Massawe akanyanyua simu na kupiga.

"Ndio, ameshakula kile chakula ... sawa, mkuu."

ENDELEA

Massawe aliongea akimtazama Miranda anayeyoyoma. Punde akakata simu akiwa anasikia sauti ya kicheko.

Sasa alikuwa ameshakamilisha kazi yake. Anachongoja ni malipo tu toka katika mkono mchafu!! Akatabasamu alafu akamuagiza afande Devi aende ndani kuhakiki kama kweli Jona amekula na kumaliza kile chakula walichompatia.

Afande Devi akatii amri. Upesi akaenda huko na baada ya muda mfupi akarejea akiwa ameshikilia mfuko wa nailoni mkononi.

"Amekula ... amemamaliza!"

"Una uhakika?" Massawe akahakiki. Alikwapua mfuko wa nailoni toka mikononi mwa Devi na kuupekua kama kuna mabaki.

"Ndio, nina uhakika," Devi akajibu akitazama chini. Akaendea daftari kubwa la mapokezi, akaketi na kuanza kulipekua.

Macho yake yalionyesha yupo mbali kimawazo. Hata daftari hilo hakuwa analipekua bali analifungua tu kuigiza.

Hakudumu hapo muda, akalifunga daftari na kwenda zake kantini. Si kwamba alikuwa na njaa. Alienda kutafuta amani.

**

"Una uhakika?" Akauliza Kamanda mkuu. Macho yake yalikuwa na mabaki ya furaha katika hali hii ya kushangazwa.

Alikuwa amevalia tisheti jepesi jeupe na suruali ya traki rangi ya bluu. Mbele yake, kiti kinachotazamana, alikuwa ameketi mwanaume mchina, Sheng, akiwa ndani ya shati jeupe, tai na suruali nyeusi ya kitambaa.

Katikati yao kulikuwa kuna meza ndogo ya kioo. Juu yake kulikuwa na chupa kubwa ya wiski yenye mfumo wa kipekee ikiwa inafanana na viglasi vyake kwa kando.

Viglasi hivyo vilikuwa vimejaa pomoni lakini havikuwa vimeguswa hata kidogo. Soga za hapa na pale zilikuwa zimenoga zikiyaweka makoo yao bize.

"Uhakika kabisa," akajibu Sheng. Lafudhi yake ya kimandarin haikukoma kuonyesha asili yake. "Yani hatutohangaika hata kidogo, utakuja nambia menyewe."

Basi Kamanda mkuu akacheka.

"Yani mimi nilikuwa nimepanga kumpa mateso ya kila aina mpaka alainike. Unajua kijana yule ni mgumu sana?" Akauliza Kamanda mkuu kiretorikali. "Mgumu sana! Sasa nilikuwa nafikiria nimuingize kwenye tanuri gani asichomoke."

Akacheka kidogo kama mtu anayeumwa kifua.

"Kumbe kuna njia nyepesi bana."

"Yes!" Sheng akatikisa kichwa. "Nakupa siku mbili tu, utaona matokeo yake."

Kukawa kimya kidogo wote wakiwa na matabasamu usoni. Sasa wakapata wasaa wa kutia kinywaji mdomoni na kunywa fundo moja moja.

"Lakini kuna jambo takuomba," alisema Sheng akiweka glas yake mezani.

"Karibu, nakusikiliza," Kamanda akamkarimu akimtazama kwa macho ya umakini.

"Naomba, ufanye kila ujhualo. Huyu mtu asitoke ndani kabisa! He stopped most of my things when he was out. Sitaki kabisa arudi uraiani!"

Kamanda akatabasamu. Na kabla hajajibu akanywa kwanza fundo moja la wiski kisha akanguruma kupooza koo linaloungua.

"Yani kuhusu hilo?" Akatikisa kichwa. "Usijali kabisa. Ondoa kila aina ya shaka. Nitahakikisha anabakia nyuma ya vyuma maisha yake yote. Na hata itakaposhindikana, basi atoke akiwa mfu."

Sheng akakunwa sana na hilo jibu. Akanywa kwa pupa kimiminika kilichobakia kisha akabamiza kiglas mezani.

"Ntashukuru sana. Now I can spend my night peacefully!"

"Kabisa yani, ondoa hofu. Namfahamu vema yule kijana. Nafahamu uwezo wake vizuri sana. Akitoka mule ndani kwa njia yoyote ile, vitanda vyetu vitageuka kuwa jehanamu. Siwezi kabisa nikaliruhusu hilo."

Bas mara Sheng akaingiza mkono wake mfukoni kana kwamba anatafuta kitu. Akaingiza kushoto kisha kulia. Akatoa pochi yake na kuitazama. Ilikuwa imesheheni fedha. Haikuwa na uwezo wa kufungwa. Kamanda akaitazama pochi hiyo akiimezea na kinywaji chake.

Mara Sheng akamuuliza:

"Unahitaji fedha yoyote ile?"

Kamanda hakujibu, akabaki anajichekesha. Sheng akaiweka pochi yake mezani na kumsogezea Kamanda.

"Ya soda hiyo."

**

"Mara yako ya mwisho kuonana naye ilikuwa lini?" Aliuliza Geof aliyejiveka suti matata ya kisasa rangi kahawia. Macho yake ya kazi yalikuwa yanamwangazoa Boka machoni.

"Ni muda mrefu sasa sijaonana naye!" Boka akadanganya. Hapa walikuwa wanamwongelea Miranda na kwa akili zake tayari alifahamu wapi inspekta huyu anapoelekea na yeye hakuwa radhi kabisa kudhalilika.

Kubainika kuwa mkewe alikufa kutoka na mahusiano na 'mchepuko' hakikuwa kitu anachotaka kimtokee hata kidogo.

Ni fedheha. Aibu.

Alishapata picha namna gani magazeti yatakavyomsakama na kumchora mbele za watu. Haswa magazeti ya udaku!!

Hili kwake lilikuwa ni jinamizi alilokuwa anajitahidi kuliokoka. Japokuwa bado hakujua ni kwa namna gani jambo hilo lilivyo na kina kirefu.

Hakuwaza ni kwa namna gani hili swala la Miranda kuhusika na kifo cha mkewe linaweza kuwa kweli, bali namna ambavyo atabaki salama kulinda heshima yake kwanza.

Japo pia hakutaka Miranda ahusike na hili. Kwanza, hakuwa anaamini kama Miranda atakuwa ametia mkono kwenye mauaji ya mkewe.

Kwake Miranda ni msichana mrembo asiye na makuu. Msichana ambaye hata kushika kijiko ama uma vizuri hawezi, sembuse kuua. Hakujua alikuwa anajidanganya.

Mwanamke huyo alikuwa ni mafia haswa!!

"Lakini mnawasiliana, sio?" Inspekta aliuliza ncha ya peni ikitoboa karatasi.

"Ndio, tunawasiliana lakini ..." Boka akazimbazimba. " ... sio sana ..."

"Unajua kama alikuwa anawasiliana na mkeo?" Inspekta akatupa swali jingine.

"Sifahamu," Boka akajibu upesi. Inspekta akamtazama kwa muda kidogo machoni.

"Mheshimiwa, huyu binti alikuwa ni mfanyakazi wa mkeo, ilikuwaje ukawa na mawasiliano naye ya karibu?"

"Si karibu kihivyo," Boka akajitetea. "Unajua Miranda ni mwanamke mchangamfu sana na mwepesi kuzoea mtu. Mke wangu alinikutanisha naye, akanizoea!"

"Mkeo akakupatia na namba yake?"

"Ha ... hapana...! Niliipata namba yake sababu za kikazi, maana ndiyo alikuwa kaimu kwa company."

"Na ukawa unakutana naye pasipo mkeo kujua."

"Hapana. Unajua mke wangu ana wivu sana. Anapenda sana kuumba mambo ambayo hayapo! Mahusiano kati yangu na Miranda yalikuwa ni ya kikazi tu, si vinginevyo."

"Kwa mujibu wa maelezo ya shuhuda namba moja wa ajali, rafiki yake mkeo aliyelazwa hospitali, amesema mkeo alishuhudia jumbe kadhaa za mapenzi kwenye simu yako toka kwa huyo mwanamke. Ni kweli?"

"Kwenye simu yangu? - mimi? Mmmh mmh sidhani! ... chukua hata wewe utazame kama utaona!"

Inspekta hakuuliza tena jambo, akanyanyuka na kuaga aende zake. Akamhusia mheshimiwa asitoke nje ya mkoa ama kukaa mbali na makazi yake kwa muda wote huu wa upelelezi.

Akaenda akiwa sasa kichwani ameshamuongea mheshimiwa kama mtuhumiwa namba mbili wa mauaji. Maelezo yake yanayojikanganya na yale aliyoyatoa Miranda yalimtia hatiani.

Pengine walishirikiana na Miranda kutimiza mauaji waishi pasipo na shida, inpekta Geof aliwaza.

**

"Mi -- mi -- skuona haja ya ..." Miranda aliongelea puani. Alikuwa ameibinyia simu sikioni, yupo sebuleni akitazama kwa macho ya kukanganyikwa.

"Nisamehe, sikujua kama yangekuwa makubwa kiasi hiki. Kweli tulikuwa na ugomvi, but nilichukulia simple tu," Miranda aliruruma. Alisimama akashika kiuno chake akienda huku na huko. Mara akikuna nywele na kuminyaminya lips zake.

"I am sorry nimekuingiza kwenye a big mess ... ndio, tulishawahi kukutana ... yes ... laki ... eeenh ... I didnt do it! Yeye ndo' alikuwa anatak ..."

Simu ikakata.

Miranda akaketi chini akishusha pumzi ndefu.

"Bila Jona hapa naenda ndani huku najiona," akajisemea mwenyewe kama chizi.

Hakuwa na amani. Tumbo lilikuwa linamkoroga. Mwili mzima anauhisi umekuwa dhaifu.

**

"Yes, Miranda," BC alinguruma baada ya kuchomoa simu yake mfukoni na kuiweka sikioni. Alikuwa ndani ya Mlimani City malls ndani ya duka la simu kama kawaida akiwa amenawiri na kupendeza hali iliyomfanya aonekane kijana zaidi kinyume kabisa na namba za umri wake.

Alikuwa ametinga kaunda suti ya bluu. Kifuani amechomeka ua dogo jekundu spesheli. Chini miguu akiihifadhi ndani ya kiatu madhubuti cha ngozi.

"What problem?" (Shida gani?) BC akauliza akiangazaangaza simu. Mara kidogo akaacha zoezi zima na kuisikiliza simu yake kwa umakini zaidi. Punde akatoka nje ya duka akiwa amekunja ndita.

"That is real serious shit!" (Hilo ni jambo kubwa kweli!)

Akatulia kidogo akiskiza. Kisha akasema kwa sauti ya agizo.

"Let's meet immediately and see what we can do!" (Tukutane mara moja tutazame nini tunaweza fanya!)

Akaskiza tena. Kisha akahitimisha.

"It is either we get the door or make it by ourselves" (Ni aidha tuupate mlango ama tuutengeneze wenyewe!)

***
 
[emoji91][emoji91][emoji91][emoji91][emoji91][emoji91][emoji91][emoji91][emoji91]
 
Back
Top Bottom