Anga la washenzi na Joana anaona kitu usiku

Anga la washenzi na Joana anaona kitu usiku

*ANGA LA WASHENZI II -- 21*

*Simulizi za series*


ILIPOISHIA

"I have never seen such a virus like this before!" (Sijawahi kuona kirusi kama hiki hapo kabla!) Sauti ya BC ilinguruma simuni. Miranda akabana pumzi kwa mshangao. Moyo wake ulianza kwenda mbio.

Akauliza kwa hofu, "So what shall we do??" (Sasa tutafanya nini??)

ENDELEA

BC akaguna kidogo alafu akasema inabidi wafanye kuipata antidote hiyo kwa namna yoyote maana la sivyo Jona atakufa. Ila kwa kusogezea muda, atampatia antidote mbadala. Hiyo itampatia Jona ahueni ila si ya kudumu!

Na ubaya ni kwamba kadiri atakavyoendelea kutumia antidote hiyo basi ataishia kuwa kilema hapo baadae kwani si nzuri sana.

"Send that man to my house. I will give it to him. (Mtume huyo mwanaume nyumbani kwangu. Nitampatia.) BC alihitimisha maongezi yake kisha akakata simu.

Miranda akateta na Marwa aende kwa BC, akamkabidhi na funguo ya gari kisha maelekezo ya namna ya kufika huko.

"Usikawie," akamsihi. "Inabidi ulete hiyo antidote upesi Jona apate unafuu."

Marwa akafichama funguo kiganjani mwake.

**

"You are welcome!" BC alimkaribisha Marwa sebuleni. Mwanaume huyo akaketi kwenye sofa zenye nyama na kumtazama Bwana huyo mzungu pasipo kutia neno. Aliamini anajua kilichomleta hapo.

BC akakung'utia mabaki ya sigara kisosini, kisha akavuta pafu ndefu na kuzima kabisa sigara yake. Akapuliza moshi angani na kumtazama Marwa.

"So you are the man?" (kwahiyo wewe ndiye mwenyewe?)

Marwa akatikisa kichwa chake, akasema, "Yes, I am."

"Ok, so listen to me very carefully," (sawa, sasa niskize kwa umakini,) BC akafungua dibaji yake ya maongezi. Akajitengenezea vema kitini kisha akamtazama Marwa aliyekuwa amemwazima masikio.

"You have to follow instructions properly. Time and diet. I didn't have time to write them down so I'll just tell you orally!" (Inabidi ufuate maelekezo vema. Muda na mpango kula. Sikuwa na muda wa kuviandika kwahiyo nitakuambia kwa mdomo!)

Baada ya hapo akamwelekeza Marwa dozi, muda na chakula anachotakiwa kupewa Jona. Marwa akavi- note vyote kichwani pasipo kubakisha hata chembe. Akashukuru, na kuaga. Alikuwa ndani ya upesi. Hakutaka kupoteza hata sekunde.Lakini bwana BC akamtaka avute subira kwanza.

Kuna jambo anataka kujadili naye kwa ufupi.

"I know you dont know but I want to let you know, I spend a lot of money on him. And it is clear that I will even spend more and more to get him on his feet. The question is, will I get his loyalty?" (Najua hujui lakini nataka kukujuza, natumia fedha nyingi juu yake. Na ipo wazi kuwa nitatumia zaidi na zaidi kumfanya asimame kwa miguu yake. Swali ni, nitaupata uaminifu wake?)

Hapa Marwa akasita. Si tu kwamna hakuwa na jibu, bali alihofia kuteta. Hakuwa anajua lililopo kichwani mwa Jona, wala mwa Bwana BC. Hakutaka kutibua mambo mapema hii, akaomba muda kidogo. Itakuwa vema Jona akisema mwenyewe punde atakapopata uwezo wa kutamka.

Bwana BC akaguna akisafisha koo lake. Akalamba lips zake kavu akimtazama Marwa kwa sekunde kadhaa akiwa kimya.

"You are his friend. I hope you know him inside out. I adopted him when he was abandoned by the world. When he was no one. So he should be someone under my shadow. Deliver this message to him." (Wewe ni rafiki yake. Natumai unamjua ndani nje. Nilimuokota akiwa ametelekezwa na ulimwengu. Akiwa si mtu. Kwahiyo inabidi awe mtu chini ya kivuli changu. Fikisha huu ujumbe.)

Marawa akatikisa kichwa kwa kuridhia, alafu akaaga na kwenda zake.


**


Akiwa kwenye mataa, akapata kufikiria yale maneno ya BC. Alilaza kichwa chake akitazama 'sight mirror'. Na kwa muda kidogo akawa amesafiri kwenda ulimwengu mwingine. Ulimwengu wa mawazo na fikra.

Akaumauma midomo yake akijaribu kupembua. Akisikia sauti ya Bwana BC na kwa muda huo akiyaweka maneno yake kwenye mizani na hulka ya Jona.

Je, Jona ataridhia masharti ya BC? Hili swali lilimuumiza kichwa kidogo. Vipi kama Jona atakaidi na kuamua kufuata njia yake, BC atachukua hatua gani? Naye atakuwa upande gani?

Mawazo haya yakaonyesha kutokuwa na komo zaidi ya kujiumiza kichwa. Asingeweza kuyapatia majibu kwa muda huo, ila alishindwa kuyafukuza kichwani mwake.

Alikuja kushtuliwa na honi kali za magari yaliyo nyuma yake maana taa zilisharuhusu na alikuwa bado hajasogeza matairi ya chombo. Haraka akapangua gia na kukanyaga pedeli ya mafuta.

**

Tip! Tip! Vidole vilibonyeza vitufe kiooni, mara ujumbe ukaenda na muda si mrefu tiki ikatokea ujumbeni kuashiria ujumbe umefika.

Lee akaweka simu yake pembeni kisha akajilaza akitazama dari. Muda ulikuwa unazidi kwenda akiwamo Hongkong pasipo mafanikio. Endapo akiendelea kukaa huko, basi Sheng atafahamu hayupo na hata akarudi akawa na wasaa mgumu wa kujieleza.

Akashusha pumzi ndefu. Akafikiri kidogo na akili yake mtambuka ikamletea majibu. Kidogo akajiona mjinga. Kama kulikuwa kuna njia ya yeye kupata anachokitaka, basi ilikuwa kwa kupitia wale majamaa watatu!

Akatikisa kichwa chake kwa masikitiko. Kwa akili yake mtambuka wale majamaa watakuwa wana mahusiano na hichi anachokitafuta. Hakuamini kama wanaweza kuwa vibaka wa kawaida tu, wakimtaka akaonane na mkuu wao.

Huyo mkuu ni nani? Na amemfahamuje ingali hapa Hongkong yeye ni 'mgeni?' Hapa mawazo yakampeleka mbali sana. Hata akaanza kuwatilia mashaka wale watu aliokuwa anawakuta kule majumbani kumtafuta Chen Zi.

Je, na wao watakuwa wanahusika na wale mabwana watatu?? Akatambua hapa kutakuwa kuna kitu, na kama akipata wasaa basi ana haja ya kuzitazama nyumba zile katika namna ya kipekee. Atagundua jambo.

Akatazama kesho yake, hakuwa na muda. Alipanga kwenda mahali ambapo marehemu Chen Zi halisi, yule aliyekuwa maarufu nchini, alikuwa akifanyia mazoezi yake. Aliamini huko anaweza akapata lolote jambo likampa mwanga.

Akaendelea kuyapanga mawazo hayo kichwani mpaka akapitiwa na usingizi.

**


"Boss, tumemaliza kazi," alisema mwanaume ndani ya suti nyeusi akimtazama Sheng kitini.

"Una uhakika mmefukia kila kitu?" Sheng akauliza. Macho yake yalikuwa yanamtazama kijana huyo mjumbe kwa ukali.

"Ndio, mkuu. Kila kitu tumemiminia shimoni!" Akaapa mjumbe. Uso wake ulikuwa umepooza. Macho yake yamelegea. Na mara akaanza kukohoa kwa pupa mpaka akatoa damu. Akamuaga Sheng kwa ishara kisha akatoka zake.

Sheng akalaza kichwa chake kitini akifikiria kwa sekunde kadhaa. Punde simu yake ikaita, akainyakua na kuweka sikioni.

"Sawa, nakuja," alisema kwa ufupi kisha akaiweka simu mezani. Akaendelea kufikiria kwa muda kidogo, na kisha akanyanyua simu yake ya mezani na kulonga, "tazameni hao vijana waliozika hizo antidotes! Kama watakuwa wameanza kubadilika, wawekeni kwenye cages. Ntakuja kuwatazama kesho mapema."

Alipotoa agizo hilo akasimama na kutoka ofisini.

**

Bandarini, usiku wa saa nne ...

Meli ya kichina inayojinasibu kuja kutoa huduma za afya bure nchini, haswa jijini. Ilikuwa tayari imeshatia nanga. Ndani yake ilikuwa imebeba wafanyakazi alfu moja na mia. Miongoni mwao vikosi vya wanajeshi wa kichina takribani vitatu kila kimoja wapo kikiwa na askari hamsini.

Ilikiwa ni meli kubwa. Juu yake ikipeperusha bendera ya nchi, na ubavuni ikiwa ina chapa ya msalaba mkubwa rangi nyekundu.

Gari jeusi, Ford Ranger modeli ya 2016 ikiwa imefunikwa bodi ya nyuma, ikasimama eneoni na punde akashuka Sheng. Kisha wanaume kadhaa watatu wenye asili ya China wakiongozana naye.

Sheng akatembea kwa ukakamavu akifunga kifungo cha koti lake la suti. Alikuwa anaelekea kule ambapo Meli ilituama. Akiwa ametazama mbele aendako, mara akasikia sauti:

"Kiongozi," kutazama, akamwona Kamanda mkuu akitokea upande wa gizani. Alikuwa yu mwenyewe akiwa amevalia nguo za kiraia. Akasogea, ila wale wanaume waliokuwa wanaongozana na Sheng wakamzuia.

Sheng akawaamuru wamwachilie.

Kamanda akampatia Sheng mkono. Akasema, "nimekuwapo hapa kwa muda."

Lakini uso wake ulionyesha shaka.



***
 
Papaa,embu ongeza kidogo,ni sik mingi mong'oo haujakuwepo hapa stivie
 
nataman zishuke 2 nyingine ili kufidia those days of suffering from missing antidote.ni ombi tu mkuu Steve..
 
Kale ka meli ka sheng bandarini, ndo kale kalikopokelewa na mheshimiwa bashite nn?
Ni wazo la Leo tu stieve Mollel !!
Ngoja tusubili ukweli unaelekea kukaa bila Nguo.
 
*ANGA LA WASHENZI II -- 22*

*Simulizi za series*



ILIPOISHIA

Sheng akawaamuru wamwachilie.

Kamanda akampatia Sheng mkono. Akasema, "nimekuwapo hapa kwa muda."

Lakini uso wake ulionyesha shaka.

ENDELEA

"Lakini sikuwa nafahamu kuwa si silaha tu umeleta. Umeleta pia na watu na chemicals!" Kamanda akakunja uso akitoa macho. Sheng akasimama na kumtazama.

"Kamanda," Sheng akaita, "kwani kuna shida nikiongezea kidogo mzigo wangu?"

Kamanda akabanwa kwanza na kigugumizi. Akatafuta neno la kuongea, akasema, "Hapana bwana Sheng. Lakini nilipaswa kuwa na taarifa rasmi. Namma hii inaweza kututia hatiani!"

Sheng hakumjibu Kamanda. Akaendelea kutembea akiwa anawaza mambo yake kichwani. Alipofika getini, akasimama na kumtazama Kamanda. Akasema, "ni hatia gani hiyo waizungumzia? Kwani nakulipa kwa kazi gani?"

Kamanda akataka kujibu, ila Sheng akasimamisha kidole chake kama ishara ya kumtaka asimuingilie. Alafu akaendelea kunena, "fanya kazi yako, Kamanda."

Kisha akazama getini na ndani ya muda mfupi yakatoka magari mawili makubwa yaliyobebelea kontena rangi za kijani. Zilipotokomea eneoni, Sheng akaonana na Kamanda na kumpatia mkono wa kheri, anataka kwenda zake.

"Samahani," Kamanda akasafisha koo na kuuliza; "Mmefikia wapi kwenye swala la Jona?" Sheng akamtazama kwa sekunde mbili kisha akamwekea mkono begani.

"Kamanda, kati yangu nawe, nani wa kumuuliza mwenzake hilo swali?"

"Aahm pengine unaweza ukawa umepata jambo. Si mbaya kunishirikisha."

"Sijapata kitu. Na nilidhani hata hilo jambo wewe ndiye utakuwa wa kwanza kuling'amua maana limeshusha hadhi ya jeshi lenu."

Sheng aliposema hayo, akamwacha Kamanda pasipo kumuaga. Akatembea hatua tano, ila mara akageuka na kumtazama Kamanda. Akasema, "fom today, hilo swala la Jona, niachie mimi, sawa?"

Kabla Kamanda hajasema jambo, Sheng akageuka na kwenda zake. Kamanda akabaki akimtazama mwanaume huyo anayoyoma.

Akalaani sana. Aliona amedharaulika. Thamani yake imeshuka. Juzi tu, alikuwa akinywa na Sheng kwa furaha, leo anaongea naye kana kwamba kakijana ka mtaani!

Akang'ata meno. Punde akajikuta ndani ya gari lake, akatekenya shina la usukani na kutimka eneoni baada ya kuhakikisha kila jambo limeenda sawa.

Alijua wazi kesho yake vyombo vyote vya habari vitakuwa hapo bandarini. Na hata yeye atakuwapo hapo akiwakilisha jeshi la polisi. Ila akiwa kama mtu asiyejua kinachoendelea hapo. Akiwa ni miongoni mwa wageni rasmi!


**

Saa nane usiku ...

"Kila kitu tayari, unaweza kwenda kupumzika, boss," alisema mwanaume mrefu mweusi, kijakazi wa Sheng. Alikuwa amevalia 'ovaroli' la bluu na kichwani akiwa amejiveka kofia ngumu na usoni amevalia miwani kubwa ya kumkinga macho na mikononi ana glovu ngumu rangi ya njano.

Sheng na Shao walikuwa wamesimama pamoja wakiwa wametia mikono mifukoni. Macho yao yalikuwa yanatazama magari yale mawili makubwa yaliyotoka bandarini, na watu kadhaa wakiwa wanashughulika hapa na pale kwenye upakuaji.

Baada ya kijakazi huyo kusema hayo, wanaume hao wa kichina wakaongozana kwenda kutazama kama kila kitu kipo sawa. Wakakuta kontena limebakia tupu, na ndani ya maabara kulikuwa kumesheheni vitu kadha wa kadha.

Wakatazama maabara ile kwa kitambo kidogo, kisha Sheng akamuuliza Shao, "unadhani vitasaidia?"

Ni nadra kwao kutumia lugha ya kiswahili katika maongezi yao. Ila Sheng aliamua kufanya hivi maana alitaka kumpa Shao mazoezi zaidi ya kutumia lugha hii. Imekuwa ikimsumbua, na kwakuwa yupo ndani ya nchi itumiayo kiswahili katika maongezi ya kila siku, hakuwa na budi kukifahamu.

"Nadhani vitasaidia sana," Shao akajibu kwa sauti ya puani. Kama ungelikuwa unamsikia usingelimwelewa kabisa kwa namna anavyoongea. Ila kwa mwenzake Sheng ilikuwa haina shida maana wanashea lugha.

"Lakini, Shao," Sheng akasema akimtazama mwenzake. "Naona kuna haja ya kuagiza vijana toka China kuja kufanya kazi huku. Hawa vijana wa hapa siwaamini kabisa, haswa ukizingatia Lee sijui alipo.

Tuna haja ya kutuma maombi nyumbani watukabidhi baadhi ya vijana waliowapika huko kwa mafunzo magumu, waliojawa stadi za mapambano, waje kutusaidia."

Shao akaminya lips zake nyembamba. Akatoa mkono wake mmoja mfukoni na kufikicha pua yake kidogo kama mtu mwenye mafua.

"Sishani kama itawezekana kwa shasha," akasema Shao akitikisa kichwa. "Unajhua shasha hivi kule nyumbani kumekuwa na shiida shana. Li wameamka na kuwa ngufu kuba tofauti na mwashoni. Inasemekana wanafadhiliwa na matafa ya magaribi. Wanapambana shana kuhakksha Wu inakufa na waon ku-rise."

Li ni wakina nani?

Miaka kadhaa huko nyuma koo ya Li ilikuwa ni moja ya koo ya kawaida sana ndani ya nchi ya China. Hakuna mtu aliyekuwa anaizungumzia wala kuipa uzito kwenye maongezi yao. Ilikuwa ni koo iliyoundwa na wakulima na wafanyabiashara wadogowadogo.

Na katika kipindi chao, koo hiyo ikashuhudia koo ama familia ya Wu ikipanda kwa kasi sana mbele ya macho yao haswa baada ya kuonekana kuvutia serikali katika namna ambavyo ilikuwa ikiwasaidia kupata na kulinda mikataba ya China. Vilevile ikihakikisha dola ya China inakua kiuchumi kwa kutumia mkono wowote, aidha wa damu ama kitabu!

Na kwasababu hiyo basi, Wu wakatengewa kitengo maalum ndani ya chemba za serikali. Kitengo ambacho kiliikabidhi koo ya Wu ofisi ya ujasusi wa kiuchumi dunia nzima. Kwa hivyo basi, koo hii ikawa si siri tena ndani ya nchi ya China japo biashara zao zingine zilikuwa haramu kama vile utumwa wa kileo, madawa na utekaji.

Sasa basi kwa kuitambua hili, nchi za magharibi ambazo hazipo tayari kuona dola zao zinawekwa miguuni na China, zikaamua kufanya jambo kujinasua na kuwadhoofu wachina wajao kwa kasi. Na njia bora waliyoichagua ikiwa ni ile ile ya 'kikulacho ki nguoni'. Wakiwa wanafahamu nguvu ya China ni familia koo ya Wu, basi wao wakaungana na koo ya Li kuhakikisha wanamtokomeza na kumdhoofisha Wu!

Na basi kwasababu Li walitaka umaarufu na pesa (Fame n' money), kwao hili hawakuliona gumu. Wakalipokea wakiwa vichwani wamedhamiria kifuta kiburi cha Wu, na kuirejesha koo ya Li kama koo yenye nguvu zaidi kama ilivyokuwa kabla ya mapinduzi ya nchini China ya mnamo mwaka 1945 mpaka 1950.

Na sasa, Li wamekuwa wakiitawala Hongkong. Taratibu wakijipanga kutanuka na kwenda kuikabili Wu popote ilipo.

Je, vipi kuhusu ile nyaraka ya Lee na saga la Chen Zi huko Hongkong??

Tuurudi kwa Sheng na Shao ...

Sheng alitikisa kichwa chake. Alikuwa ameelewa nini Shao amemaanisha. Akalaani. Akalaani tena maana aliona ni uzembe umefanyika mpaka kufikia hali kama hiyo ya sasa. Hakuwa anaamini kama Li ingefikia kipindi kuwa tishio na hata sasa Wu ikashindwa kusambaza wapambanaji wake na basi wakabakizwa hukohuko China.

Akafikiria kidogo na kuona kuna haja ya kwenda huko China. Akakutane na viongozi wake juu na kujadili mambo kadhaa. Lakini Shao akampa tahadhari. Haitakuwa vema kama akienda huko akiwa hajakamilisha kwanza kazi yake ya kumtia Jona mikononi.

Toa boriti kwenye jicho lako ndipo utazame ya wengine. Sheng akakubali shauri hilo. Punde atakapomalizana tu na Jona, atasafiri kwenda China angalau kwa juma moja tu.

Na aliamini hilo la kumshughulikia Jona halitachukua muda maana ameshaleta vifaa vya kazi.

Wakatoka maabara na kwenda kwenye ghala za silaha. Napo wakatazama ingizo jipya na kufurahishwa nalo. Baada ya hapo wakatoka na kwenda kupumzika maana muda ulikuwa umeshaenda sana.


**

Asubuhi Redioni ...


" ... kwa hivyo basi, mimi kama kiongozi mkuu wa mkoa, ningependa kutoa rai kwa wananchi wangu kutumia fursa hii adhimu. Kuanzia majira ya saa mbili asubuhi kesho mpaka majira ya kumi jioni, wafike pale kwenye meli ya kichina ili wapatiwe matibabu na vipimo bure kabisa!

Hili lamaanisha na kuonyesha namna gani serikali yao inavyowajali, na kuhakikisha kuwa kila mwananchi anapata afya bora akaijenge nchi kwa kufanya kazi."


Ilikuwa sauti ya mkuu wa mkoa.


**
 
Back
Top Bottom