Anga la washenzi na Joana anaona kitu usiku

Anga la washenzi na Joana anaona kitu usiku

Mambo ya kuzingatia ..

1. Jona anarejea kwenye hali yake kwa kasi, ila BC anaagiza auawe kwakuwa amekataa kujiunga naye.

2. Jona anataka kumaliza WOTE waliompa mushkeli. Kuna atakayepona?

3. Brown Curtis ameshaleta wanaume wa kazi kumi na wawili toka Uingereza kwa ajili ya Sheng. Ila nao watamwacha Jona salama?

4. Shao na Sheng wanazungukaniani? Na nini mwisho wake? Na je vina mahusiano gani na Lee aliyepo China?

5. Sarah na Sasha? Kati ya Sarah na Kinoo nani atakuwa wa kwanza kum- time mwenzake?
 
Mambo ya kuzingatia ..

1. Jona anarejea kwenye hali yake kwa kasi, ila BC anaagiza auawe kwakuwa amekataa kujiunga naye.

2. Jona anataka kumaliza WOTE waliompa mushkeli. Kuna atakayepona?

3. Brown Curtis ameshaleta wanaume wa kazi kumi na wawili toka Uingereza kwa ajili ya Sheng. Ila nao watamwacha Jona salama?

4. Shao na Sheng wanazungukaniani? Na nini mwisho wake? Na je vina mahusiano gani na Lee aliyepo China?

5. Sarah na Sasha? Kati ya Sarah na Kinoo nani atakuwa wa kwanza kum- time mwenzake?
Hatari sana
Huyu shao asiwe ndie cheng ze alienunua nyaraka [emoji35]
 
*ANGA LA WASHENZI II -- 44*

*Simulzi za series*


ILIPOISHIA

Akadondoka chini mfu.

Aliyemuua akamtemea mate na kusema, "tangulia kuzimu sisi twaja."

Kisha akaenda zake.

Baada ya dakika kadhaa, maiti hiyo ikagundulikana na taarifa akafikishiwa Sheng.

ENDELEA

Ilikuwaje? Hilo ndilo lilikuwa swali la kwanza la Sheng. Mwanaume huyo alikuwa ametoka kumjulia hali hivi punde na sasa amekufa? Alishangazwa.

Akawaita walinzi na kuwaliza nini kilijiri. Wote hawakuwa wanajua. Swala hili likamtia hofu Sheng. Huenda mwanaume huyo kauliwa na Shao? Aliwaza. Na kama kweli anachokiwaza ndicho, ina maana Shao atakuwa anafahamu kuwa anamzunguka?

Akashusha pumzi ya mawazo. Pasipo kulifanya jambo hilo kuwa la hadhara, akamzika mtu huyo kisiri na kisha akaendelea kutafakari. Sasa hakuwa na daraja la kumfanya ajue kinachondelea kwa Shao. Hawezi kukaa hivi. Lazima afanye namna.

Akiwa anawaza hivyo, kule upande wa Shao nao wakiwa wamekutana katika usiku huu huu wakawa wanapanga mipango yao. Kuna mwanaume mmoja alikuwa amesimama mbele na ndiye huyo aliyetoka kumuua yule mwanaume aliyetoka kwa Sheng. Ungeweza kumtambua mtu huyo kwa nguo alizokuwa amevaa.

“Tuwe makini sana,” alisema Shao. “na zaidi ya kuwa makini tuwe na uahirikiano. Najua Sheng atamfuata mwinginewe ili awe anajua ninachokipaga na kukifanya. Na itakuwa ngumu kwenu kukataa, cha kufanya kubali ila utoe taarifa kwangu nami nitakuwa nakuelekeza namna ya kuenenda."

Baada ya Shao kusema hayo, akawataka waende zao na kumwacha peke yake. Vijakazi hao wakatii.

**

Ni asubuhi, katika makazi yasiyojulikana...

Marwa akamkalisha Jona kitako akitabasamu. Jona alikuwa anavuja jasho jingi na Marwa akitiririka kiasi. Wote walikuwa wamevalia nguo nyepesi chini traki rangi ya bluu zinazofanana.

“Sasa hivi inabidi uwe unafanya kila siku!" Alisema Marwa akimtazama Jona. Angalau afya yake ilikuwa imeanza kurejea. Macho yanaonekana ila bado akiwa mdhaifu kiasi.

Angalau sasa, tunaweza tukasema hivyo kwani hakuwa hivyo hapo awali. Na mtu aliyemwona ingemuwia vigumu kuamini kama mwanaume huyo angelikuja kusimamia miguu yake siku moja.

Alitabasamu na kumwambia Marwa, “Dah! Si mchezo." Akafuta jasho kwa kiganja chake. Alikuwa anahema kwanguvu.

“Ila unajitahidi sana!" Akasema Marwa. “sikutegemea leo kama ungefanya mazoezi kiasi kile. Hata Miranda akija nikamweleza hataamini!"

Jona akatabasamu. “Nataka kurudi kwenye hali yangu kwa udi na uvumba."

“Naona kwakweli," Marwa akabinua mdomo. “hautachukua hata juma moja kila kiungo kitakuwa sawa mwilini. Uanze yale mambo yako yale!"

Wakacheka.

“Ila Jona," Marwa akataka kuchokoza mada. “unamwona yule mwanamke?"

“Nani? Miranda?"

“ndio!"

“kafanyaje?"

“mwanamke hafai yule! Mamamama! Anapigana kama kazaliwa ulingoni. Yani daaah!"

Jona akacheka. Marwa akaendelea kulonga, “ila hakuzidi wewe, bana. Nakuaminia kamanda wangu. Si bure wakina Sheng wanakesha kukutafuta. Wanajua wewe jembe."

“umeanza sasa, Marwa. Mimi nimechoka hapa sina hata nguvu ya kunena. Naomba nikaoge tutaongea zaidi najua una mengi ya kunambia maana mengi yametokea kipindi sipo ulimwengu huu."

Jona akajiendea kukoga. Alipomaliza akajifuta vema na aliporejea sebuleni akamkuta Marwa akiwa pamoja na Miranda. Mwanamke huyo alikuwa amevalia shati na suruali nyeusi ya jeans. Alipomwona Jona alitabasamu toka moyoni.

“naona umepona sasa!"

Jona akatabasamu na kuketi kitini. Akatet kidogo na Miranda kuhusu hali yake na maendeleo yake yakamtia hamasa Miranda. Alifurahi sana kumwona Jona anarejea kwenye hali yake.

Walipomaliza maongezi hayo, Miranda akatazamana na Marwa katika namna fulani ya kuwasiliana kisha Marwa akasafisha koo na kusema;

“Jona, kwakuwa sasa angalau umerejea kwenye hali yako, tunaona ni muda muafaka kukushirikisha jambo."

Marwa akaweka kituo baada ya kusema hayo. Alafu akamtazama tena Miranda kabla hajaendelea.

“sidhani kama nina haja ya kusema sana juu ya namna gani Miranda na mkuu wake, bwana Brown, walivyotusadia mpaka sasa. Hilo liko wazi. Ila sasa, kuna jambo, ama naweza kusema mkataba wa maneno ambao kwa namna moja kubwa kwasababu ya kuhitaji msaada, niliuingia mimi pamoja na mr. Brown.

Bwana huyo alinisihi sana kuwa atakusaidia sana kwa kadiri ya uwezo wake, nawe unaweza ukaona. Ila akaniambia kwamba atahitaji umrudishie fadhila kiasi kidogo."

Hapa Marwa akasita kidogo. Akamtazama Miranda na kisha akaendelea.

“sasa bwana Brown anataka uwe mtumishi wake. Ni hilo tu ndi..."

“haitawezekana!" Jona akamkatisha Marwa. Akasema kuwa hilo jambo kamwe halitatokea japo anashukuru sana kwa msaada aliopatiwa.

“siwezi kufanya kazi chini ya BC. Haitakaa itokee hata siku moja hata kwa dau gani!"

Miranda akashusha pumzi ndefu alafu akatia neno, “Jona, naomba ulifikirie hili swala kwa mapana zaidi. Ni bwana Brown pekee ndiye aliyekuokota wakati wengine wakiwa wamekitekeleza. Tafadhali fikiri mara mbili."

Jona akatikisa kichwa. “Marwa, Miranda, huo ndiyo msimamo wangu na hautabadilishwa na chochote kile. Siwezi kufanya kazi na bwana Brown kwa sababu yoyote ile! Ila..."

Akanyamaza kwanza akitazama chini. Akakunja ngumi.

“lazima wale wote walionilaza chini walipe kwa gharama yoyote ile. Wamenitesa mno na kuharibu maisha yangu. Kamwe sitawaacha salama. Iwe kwa kunuka ama kunukia. Nitawasaka kama mbwa mwenye njaa na nitawaua kwa mkono wangu nwenyewe pasipo na tone la huruma.

Niliapa kwa Mungu wangu. Siku nitakayotoka kwenye mateso yale itakuwa kiama chao hakika. Sitabakiza hata mmoja. Na kila ninapokumbuka hilo, napata nguvu ya kufanya mazoezi zaidi niwe kamili."

Jona akisema haya, machozi yakamjaa machoni. Alikuwa anaongea kwa uchungu mno na kwa hisia kali. Aliminya ngumi yake mpaka akahisi maumivu.

Alisimama na kwenda zake chumbani pasipo kuaga.

“sasa tunafanyaje?" Akauliza Marwa akimtazama Miranda.

“sijui kwakweli!" Miranda akatikisa kichwa. “naona mambo yanakuwa magumu zaidi."

“kabisa! Ila hata mimi nililihisi hili jambo. Halijanishangaza kabisa. Ni asilimia ndogo sana niliihifadhi kuwa Jona ataridhia hili jambo. Kichwa chake anakijua mwenyewe."

Kukawa kimya kidogo. Miranda akanyanyuka na kumwambia Marwa,“acha nikapumzike kidogo. Baadae nitaenda kuonana na Bwana Brown "

“utamwambia nini?" Marwa akauliza upesi.

“nimwambie nini zaidi ya nilichoambiwa na Jona," akasema akienda zake. Marwa akaachwa akiwa na hofu. Aliona kabisa mambo yanapoeleka si kwema. Ila afanye nini sasa?

Alihisi tumbo linavuruga. Hakutaka kuona kazi yote ile waliyoifanya inageuka kuwa vumbi.

**

Saa mbili usiku ...

Ndege kubwa ya kampuni ya BRITISH AIRWAYS ilitua kwenye uwanja wa ndege wa Mwalimu Julius K. Nyerere. Ndege hiyo ikatema watu kadhaa ikiwemo wanaume kumi na mbili waliovalia suti nyeusi kali na wamebebelea mikoba mikononi.

Wanaume hawa waingereza kw utaifa, walikuwa wametokea jiji la London na hapa nchini walikuwa wamekuja kwa agizo la bwana Brown Curtis.

Walitoka nje ya uwanja, wakapokelewa na Bwana Brown mwenyewe ambaye alikuja na gari kubwa la kuwatosha wote, Noah nyeupe yenye vioo vyeusi. Wakajitweka humo na safari ikaanza ya kuelekea nyumbani kwa bwana Brown.

Pasipo kupoteza muda baada ya kuwasili, BC akawaeleza kuwa wamekuja nchini kwa kazi moja, kummaliza Sheng na utawala wake hapa nchini.

Lakini kwakuwa watu ha walikuwa wamechoshwa na uchovu wa safari, bwana Brown akawataka wapumzike kisha kesho itakapofika watayajenga na kuyapanga vema.

Basi wanaume hao kumi na wawili wakaenda kukoga wafanye mpango wa kupumzika. Hawakuwa watu wa soga nyingi, bali matendo. Miili yao ilikuwa imejengeka kimazoezi na macho yao yalionyesha kweli wao ni watu wa kazi.

Wakiwa wanajishughulisha huko, Miranda akafika nyumbani kwa BC. Akaelezwa juu ya ujio wa hao watu na hata wakaitwa na kutambulishwa kwa mwanamke huyo. Baada ya hapo, Miranda akasema lengo la ujio wake.

“Jona doesn't want to join with us."

BC akatabasamu. Sigara yake iliyokuwa kwenye kisosi ilikuwa haijazima, akainyakua na kuifyonza.

“ok, he's chosen death over life. He wil pay!"

Akafyonza tena sigara. “in fact I dont need him anymore. The men are already here, I know they will do the work effectively. But I won't leave Jona alive. He must die!"

Miranda hakusema kitu. Alikuwa anamtazama tu BC akivuta sigara na kunena.

“did you hear me? He must die. And you are the one who's gonna do it."

Miranda akatahamaki, “me!"

“yes, you!" BC akabweka. “kill him!" Alisema akiwa ametoa macho. Akasisitiza zaidi, Jona auawe. Na isichukue hata siku mbili awe amemletea kichwa cha mwanaume huyo mfukoni!

**
Saruti Steve mollel
 
kamoja kamoja kama Azam walivyoanza ligi. lakini yatupasa tushukuru kwa kidogo tulichopata, ahsante mtunzi wetu steve wa mollel
 
Back
Top Bottom